Jivutie Upako
()
About this ebook
Hii kitabu ya kipekee na Dag Heward-Mills atawafundisheni nini maana ya kupata upako na jinsi gani unaweza kuwa mafuta kwa ajili ya huduma. Kujifunza jinsi ya kukamata upako kwa ajili ya kazi ya huduma. Kitabu hiki ni lazima kwa kila mhudumu.
Dag Heward-Mills
Bishop Dag Heward-Mills is a medical doctor by profession and the founder of the United Denominations Originating from the Lighthouse Group of Churches (UD-OLGC). The UD-OLGC comprises over three thousand churches pastored by seasoned ministers, groomed and trained in-house. Bishop Dag Heward-Mills oversees this charismatic group of denominations, which operates in over 90 different countries in Africa, Asia, Europe, the Caribbean, Australia, and North and South America. With a ministry spanning over thirty years, Dag Heward-Mills has authored several books with bestsellers including ‘The Art of Leadership’, ‘Loyalty and Disloyalty’, and ‘The Mega Church’. He is considered to be the largest publishing author in Africa, having had his books translated into over 52 languages with more than 40 million copies in print.
Related to Jivutie Upako
Related ebooks
Wakristo:Mabalozi wa Ufalme wa Mungu Maagizo Kuhusu Kuishi kama Mkristo. Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKushindwa Sasa Basi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMambo ya Kufanya Saa Yako Ikifika Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwana-Adam ni Nani Naye ni Nini Mungu Amkomboe: Chuo cha Kwanza, #1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwongozi Wa Roho: Safari Maishani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSauti Ya Mungu Yenye Nguvu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJivutie Upako Rating: 4 out of 5 stars4/5Wale wanaokushitaki Rating: 5 out of 5 stars5/5Upendo wa Mungu na Msamaha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMaono Niliyoona Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHatari za Kiroho Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsRoho Mtakatifu Rating: 5 out of 5 stars5/5Mwanzo: Kitabu cha Mianzo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsAnagkazo (Nguvu ya kushurutisha!) Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsImani Kwa Wale Walioitwa na Kuchaguliwa na Mungu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNguzo za Imani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWengine... Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKusamehe Kumerahisishwa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsBinti Unaweza Kufanikiwa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWaambie Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsBadilisha Huduma yako ya kiuchungaji Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHistoria & Maisha ya Yeshua Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi ya Kusali & Kuongea na Yahweh Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsVitengo vya Ujenzi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsEneza Huduma Yako Kwa Miujiza na Udhihirishaji wa Roho Mtakatifu Rating: 4 out of 5 stars4/5Katika Eneo la Adui Kuokolewa na Silaha ya Siri: Swahili Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNguvu ya Damu Rating: 5 out of 5 stars5/5Wale Wanaojifanyisha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSiri ya Dhabihu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMrembo, Mnyama na Mchungaji Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Reviews for Jivutie Upako
0 ratings0 reviews
Book preview
Jivutie Upako - Dag Heward-Mills
Sura ya 1
Ni Lazima Upakwe Mafuta
Sikupata mafunzo rasmi katika huduma, sikupitia shule ya Biblia na nilikuwa na mawasiliano kidogo sana na mtu mkuu wa Mungu yeyote. Wakati nilipoanzisha huduma, baadhi ya watu wa Mungu niliopata kufahamiana nao, waliishia kutilia mashaka na kupambana na wito wa Mungu katika maisha yangu. Sikuwa na mbadala kunyonya kwenye upako uliokuwa kwa watu wengine wa Mungu waliokuwa mbali kupitia kanda na vitabu vyao.
Naamini kwamba nimepakwa mafuta na Roho Mtakatifu kusimama kwenye ofisi yangu ya huduma. Nina ushahidi mwingi sana unaonizunguka kutilia mashaka uhalisi wa upako katika maisha yangu. Pia naamini kwamba maendeleo ya kielekitroniki na kiteknolojia duniani ni kwa ajili ya faida ya ufalme wa Mungu na huduma. Teknolojia imefanya kuwa jambo linalowezekana kuwa karibu na watu ambao wamepakwa mafuta.
Unaouhitaji ni Upako
Wakati Mungu anapokuletea mtu wa Mungu, unapewa nafasi ya kumpokea na kujipatia upako ulioko kwenye maisha yake. Upako ni kitu kikuu ambacho wewe na mimi twakihitaji ili kufanya kazi ya Mungu. Nabii Zekaria alijua kuwa kitu muhimu zaidi kilikuwa ni upako. Ni yeye aliyesema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa Roho yangu
(Zekaria 4:6).
Elisha pia alitambua kwamba kitu kilichofanya huduma ya Eliya kuwa yenye mafanikio kilikuwa ni upako. Wakati alipopata nafasi, aliomba upako. Baadhi ya watu wangeweza kuomba fedha, elimu au sifa alizokuwa nazo Eliya. Lakini Elisha alitaka upako tu!
…Eliya akamwambia Elisha, Omba kwangu lo lote utakalo nikutendee, kabla sijaondolewa kwako. Elisha akasema, Nakuomba, sehemu mara dufu ya roho yako na iwe juu yangu.
2 Wafalme 2:9
Katika kitabu hiki, nataka nikushirikishe juu ya njia ya upako ambayo kwa kawaida huwa haiongelewi. Inaweza kuonekana mpya kwako, lakini ni halisi kabisa. Kama kuna njia yoyote ambayo unaweza kujipatia upako, tafadhali itumie! Siiwasilishi hii kama ndio njia pekee ambayo Mungu anaweza kukupaka mafuta; nakushirikisha tu kile nilichokipokea kutoka kwa Bwana. Nakushirikisha kile kilicho cha kibiblia na cha kimaandiko.
Watu wengi wamepokea upako kwa njia ya kusikiliza kanda na kusoma vitabu, lakini hawaelewi kile kilichowatokea. Wengi wa wale waliopokea upako kupitia njia hii hawawezi kuifundisha kwa sababu hawaielewi kikamilifu. Naamini kwamba ni kazi yangu kuifundisha njia hii rahisi na halisi ya kujipatia kigezo muhimu zaidi cha huduma – upako.
Sura ya 2
Kuhusiana na Watu Wakuu wa Mungu
Katika kitabu kingine ¹, nimeshirikisha juu ya umuhimu wa kuhusiana kwa ukaribu na mtu wa Mungu ili kupokea upako ulio katika maisha yake. Kwa nini huna budi kuhusiana na watu wa Mungu waliopakwa mafuta? Ni nini hasa ukipatacho kwa kupitia uhusiano? Kwa kadri uhusianapo kwa ukaribu na mtu wa Mungu, utamsikia akizungumza mara kwa mara. Maneno haya yana upako. Wakati Elisha alipohusiana kwa ukaribu na Eliya, alimsikia yeye mwenyewe akizungumza mara kwa mara.
Ikawa, walipokuwa wakiendelea mbele na kuongea…
2 Wafalme 2:11
Maneno Yana Nguvu!
Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwamba maneno yake yalikuwa na mambo mawili muhimu. Yalikuwa na uzima na Roho! Roho huyu ni yupi? Roho huyu ni upako! Maandiko husema kwamba Mungu alimpaka mafuta Yesu wa Nazareti kwa Roho Mtakatifu na kwa nguvu (Matendo 10:38). Yesu alipakwa mafuta kwa Roho Mtakatifu, na kwa hiyo Roho Mtakatifu (kitu ambacho kwacho alipakwa mafuta) ni upako.
… maneno hayo niliyowaambia ni roho tena ni uzima.
Yohana 6:63
Kwa watu wengi, uhusiano wa karibu na watu wa Mungu tunaouzungumzia hauwezekani isipokuwa kwa kutumia njia ya vitabu na kanda. Vitabu na kanda vinaweza kuwa na maneno ya watu wa Mungu walipakwa mafuta. Maneno ya watu wa Mungu waliopakwa yana Roho na uzima.
¹ Tazama The Mega Church (Kanisa Kubwa), na Bishop Heward–Mills.
Kujizamisha
kwenye vitabu vilivyoandikwa na watu waliopakwa mafuta ni njia ifaayo sana ya kuhusiana nao. Muda unaotumia kusoma kitabu unatumiwa kushirikiana na mwandishi wa kitabu. Ni upendeleo ulioje kuwasiliana na mtu mkuu kwa masaa matatu mahali pa faragha nyumbani kwako!
Wakati usomapo kitabu hiki unashirikiana nami na mimi nashirikiana nawe. Wakati niandikapo kitabu hiki, najisikia kwamba naongea na watu fulani. Nawahudumia moja kwa moja watu wengi watakaotoa muda [wao] kupokea. Kama Elisha alivyoyasikiliza maneno ya Eliya na wanafunzi walivyoyasikiliza maneno ya Yesu, unayasikiliza maneno yangu wakati usomapo kitabu hiki! Wanafunzi waliyasikiliza maneno ya Yesu; hivyo