Beruflich Dokumente
Kultur Dokumente
Mtwara Hakiii
Ndugu wananchi,
Ni kwa sababu ya upendo wa Profesa Lipumba kwangu nilishindwa
kukataa kukubali mwaliko wake kuja hapa kujumuika nanyi katika siku
hii muhimu sana. Hakuna namna bora zaidi ya kushukuru zaidi ya
kuendelea kufanya kazi pamoja katika kuwatetea Watanzania na Tanzania
yetu. Umoja wa upinzani ndio silaha dhidi ya mabwenyenye wa kiuchumi
na kisiasa hapa nchini. Najua huko waliko inawauma sana wanapoona
wapinzani wanaungana bila kujali tofauti ndogondogo zinazojitokeza
miongoni mwao. Tutaendelea kushirikiana kwa maslahi mapana ya nchi
yetu na katika kuhakikisha kwamba utawala wa Chama cha Mapinduzi
ambacho sasa ni chama cha mabwenyenye unakoma katika nchi yetu
mapema iwezekanavyo.
Nimekuja pia Mtwara kwa sababu huu ni Mkoa wa kipekee katika historia
ya nchi yetu. Mtwara ni Mkoa ambao kwa miaka zaidi ya miaka 25 baada
ya nchi yetu kupata uhuru ulibaki kuwa ngome imara dhidi ya mabeberu
wa Kireno na waasi wa nchi jirani ya Msumbiji. Wakati mikoa mingine
ikisonga mbele katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii, Mikoa ya
Mtwara na Lindi ilibaki nyuma kwa sababu ya kulinda heshima ya mipaka
ya nchi yetu. Hii ni historia muhimu sana ambayo vijana wetu inabidi
waijue na waithamini.
Katika miaka ya hivi karibuni Mkoa wa Mtwara umechukua sura mpya
kabisa kitaifa kufuatia kugunduliwa kwa gesi. Na katika hili wananchi wa
Mtwara mmeonyesha kwamba watanzania wanaweza kupigania maslahi
ya Taifa wakiamua. Mmesimama kidete kuhakikisha kwamba utajiri huu
hauporwi na kwamba haturudii makosa yaliyofanyika Kanda ya Ziwa pale
tuliporuhusu madini kuporwa na mabeberu wa kimagharibi kwa msaada
wa mabwenyenye uchwara nchini mwetu. Nyie wananchi wa Mtwara
mmesimama kidete katika kulinda maliasiali hii iliyogunduliwa kwa niaba
ya wananchi wenzenu nchi nzima ya Tanzania.
Najua bado mnalia kuhusu Bomba la kupeleka Gesi Asili Dar es Salaam.
Machozi yenu yatafutika tu kwani tayari habari za ufisadi mkubwa katika
ujenzi wa Bomba hili zimeanza kuchomoza. Kiongozi wa Upinzani
Bungeni ametamka mara kadhaa kuwa atatoa hoja kuhusu ufisadi katika
ujenzi wa Bomba la Gesi. Sisi wengine, pale atakapohitaji msaada wetu,
tutamsaidia kwani tunaamini gharama za mradi huu zimezidishwa mara
mbili na inawezakana kabisa kuwa zaidi ya dola za Marekani 600 milioni
3
Ndugu Wananchi,
Imekuwa baraka na neema sana kufunga mwaka huu hapa Mtwara, ikiwa
ni alama ya harakati za mapambano dhidi ya mabeberu na vibaraka wao
popote walipo. Mtwara ni uwanja wa mapambano ya uwajibikaji na
demokrasia. Ndio maana nasema imekuwa neema na baraka kufungia
mwaka huu hapa. Kama Mwalimu Nyerere alivyotanagza Azimio la
Arusha mwaka 1967 katika kujenga Nchi ya kijamaa, wana mabadiliko
wote nchini wanapaswa kutangaza Azimio la Mtwara la Uwajibikaji
katika Uvunaji wa Maliasili ya Nchi yetu.
4
Mwaka huu tunaouaga leo ulianza kwa matumaini makubwa sana kwa
Taifa letu katika kupata Katiba Mpya ilitayozamiwa kuweka misingi imara
zaidi ya Uwajibikaji wa Serikali kwa Wananchi. Bahati mbaya mwaka
umemalizika kwa kubwaga chini mioyo ya Watanzania wengi sana baada
ya
kupata
Katiba
Inayopendekezwa
yenye
mambo
yale
yale
Ndugu Wananchi,
Mwaka 2014 unaisha kwa hasira. Tumeshuhudia Bunge letu likijadili moja
ya kashfa kubwa kabisa kupata kutokea katika nchi yetu. Zaidi ya shilingi
Bilioni mia tatu zimechotwa na kugawaiwa kama njugu tena na watu
wenye mamlaka na waliopewa heshima kubwa na umma. Hakuna kashfa
kubwa kama wizi uliofanyika kupitia Akaunti ya Tegeta Esrow. Ni wizi
mkubwa na tumewakamata wezi mchana kweupe kabisa. Nawakikishieni
kwamba juhudi zinazoendelea kufanywa na baadhi ya wezi wa fedha hizi
na vibaraka wao zitashindwa vibaya kwa sababu ukweli haujawahi
5
hawa
wanajua
Watanzania ni mazwazwa
na
hawafanyi
uchunguzi wa kina, yaani due diligence kwani hata kwenye EPA fedha
ziliibiwa kwa kutofanya due diligence na kwa kutumia kitu kinaitwa deed
of assignment.
Mabwana hawa wanajua kuwa Watanzania wenye ofisi za umma wana
njaa na watawahonga kidogo tu na kupitisha kila kitu. Ndivyo
ilivyofanyika.
Kama viongozi wetu wangefanya due diligence kwenye manunuzi ya
makampuni haya kama Sheria ya Kodi ya Mapato inavyowataka,
tusingekuwa na skandali ya Tegeta Escrow.
Ndugu Wananchi,
Nataka niwambie watanzania kupitia mkutano huu muhimu wa Mtwara
kwamba yaliyotokea Bungeni ni mwanzo na si mwisho. Ni mwanzo wa
safari ndefu wa kujenga utamaduni wa uwajibikaji katika nchi yetu.
Ndugu Wananchi,
Ni katika nchi ya Tanzania pekee ambapo waziri anaweza kutukana
wananchi waziwazi mchana kweupe na kuwaambia kwamba ni wajinga
na wapumbavu na akabaki katika ofisi ya Umma. Ni Tanzania tu ndipo
Katibu Mkuu wa Wizara anaweza kutukana wabunge kuwa ni washenzi
akaachwa bila kuchukuliwa hatua za kinidhamu. Huwezi kuwa na Taifa
lisiloheshimu wananchi na wawakilishi wao. Uwajibikaji ni suluhisho.
Uwajibikaji unaweka nidhamu. Uwajibikaji unatoa matumaini kwa watu
kuwa viongozi wao wanawajali.
10
Ndugu Wananchi,
Tunaingia mwaka 2015 kifua mbele katika vita dhidi ya ufisadi na katika
kusimika
uwajibikaji
nchini.
Tunataka
Watanzania
wote
wenye
Mwaka
2015
kuwa
ni mwaka
wa
kuwajibishana.
miaka
mitano
iliyopita.
Tuungane
kuhakikisha
Serikali
Hakiiii..
13