Beruflich Dokumente
Kultur Dokumente
hii, Oktoba 25
Na January Makamba
Tarehe 25 mwezi huu Oktoba, Watanzania watapiga kura kumchagua
rais wao wa tano, wabunge na madiwani. Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu
umekuwa na msisimko mkubwa zaidi tangu kuanzishwa kwa mfumo wa
siasa za vyama vingi mwaka 1995. Mengi yamendikwa kuhusu uchaguzi
huu, hususan kutokana na hisia kwamba safari hii Upinzani una nafasi ya
kukiondoa madarakani moja ya vyama vikubwa na vyenye muundo bora
barani Afrika, chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM). Matukio
mbalimbali kuelekea uchaguzi huo yameleta shauku inayoweza
kutengeneza hadithi ya kusisimua.
Nikiwa sehemu ya Timu ya Kampeni ya CCM,na kwa manufaa ya wote
ambao wangependa kuwa na mtizamo tofauti, ninatoa sababu 9 kwanini
tunaamini kuwa CCM itaibuka mshindi na kwanini Dkt John Pombe
Magufuli atakuwa Rais ajaye wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
1. Ugombea fyongo (flawed) wa Edward Lowassa
Ilishabainika kuwa uchaguzi huu ungekuwa mgumu kwa CCM bila
kujali nani angekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Upinzani. Lakini
matokeo ya uchaguzi huu yalielemea upande wa CCM pale Upinzani
ulipomchagua Lowassa kuwa mgombea wao. Ni rahisi kwa CCM
kuchuana na Lowassa kuliko laiti mgombea wa Upinzani angekuwa
Dkt Wilbrod Slaa, ambaye ndiye aliandaliwa kuwa mgombea kabla ya
ukusukumwa kando na nafasi hiyo kupewa Lowassa. Slaa alikuwa na
uadilifu katika maeneo mengi, na aliaminika. Kwa Lowassa, ni vigumu
na inanyima raha kuchuana na mfumo aliyoshiriki kujenga na ambao
ulikuwa sehemu ya maisha yake hadi Agosti mwaka huu alipohamia
Upinzani. CCM ilikuwa na nafasi ya kumpitisha Lowassa kuwa
mgombea wake wa nafasi ya urais. Hatukufanya hivyo kwa sababu
rahisi tu kwamba ingekuwa vigumu mno kumkabidhi kwa wananchi
mgombea wa matarajio ya baadaye ambaye ni kiashirio cha yale
yasiyowaridhisha wananchi kuhusu CCM. Kuna wanaoamini kuwa
uchaguzi huu ni mgumu kwa vile Lowassa ndiye mgombea wa
1