Sie sind auf Seite 1von 260

FURAHIA MAISHA

MI L E L E !
M A S O M O YA K U J I F U N Z A B I B L I A
Anza Kusoma Biblia
Unaweza kufurahia kusoma Biblia!
Yafuatayo ni madokezo yanayoweza
kukusaidia kuanza. Chagua habari
inayokufurahisha, kisha usome
maandiko yaliyoonyeshwa.

Watu Maarufu na Hadithi


Noa na Gharika: Mwanzo 6:9–9:19
Musa kwenye Bahari Nyekundu: Kutoka 13:17–14:31
Ruthu na Naomi: Ruthu sura ya 1-4
Daudi na Goliathi: 1 Samweli sura ya 17
Abigaili: 1 Samweli 25:2-35
Danieli katika shimo la simba: Danieli sura ya 6
Elisabeti na Maria: Luka sura ya 1-2

Hekima kwa Ajili ya Maisha ya Kila Siku


Maisha ya familia: Waefeso 5:28, 29, 33; 6:1-4
Urafiki: Methali 13:20; 17:17; 27:17
Sala: Zaburi 55:22; 62:8; 1 Yohana 5:14
Mahubiri ya Mlimani: Mathayo sura ya 5-7
Kazi: Methali 14:23; Mhubiri 3:12, 13; 4:6

Unapohitaji Msaada ili Kukabiliana na . . .


Kuvunjika moyo: Zaburi 23; Isaya 41:10
Huzuni: 2 Wakorintho 1:3, 4; 1 Petro 5:7
Hatia: Zaburi 86:5; Ezekieli 18:21, 22

Mambo Ambayo Biblia Inasema Kuhusu . . .


Siku za mwisho: Mathayo 24:3-14;
2 Timotheo 3:1-5
Tumaini la wakati ujao: Zaburi 37:10, 11, 29;
Ufunuo 21:3, 4

DOKEZO: Ili kupata muktadha wa maandiko yaliyotajwa hapo juu, soma sura nzima ambazo mistari
hiyo inapatikana. Tumia chati ya “Fuatilia Usomaji Wako wa Biblia” iliyo mwishoni mwa kitabu hiki ili
kutia alama kila sura unapomaliza kuisoma. Jiwekee lengo la kusoma sehemu fulani ya Biblia kila siku.
FURAHIA MAISHA
MIL E L E !
M A S O M O YA K U J I F U N Z A B I B L I A

“Wale wanaomtafuta Yehova watamsifu. Na ufurahie maisha milele.”


—Zaburi 22:26.

Kitabu hiki ni cha

Photo Credits: Page 15: Image ˘ Homo Cosmicos/ Kitabu hiki hakiuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu
Shutterstock; page 17: NASA, ESA and the Hubble Heritage ya Biblia ya ulimwenguni pote inayotegemezwa
Team (STScI/AURA)-ESA/Hubble Collaboration. Licensed
under CC BY 4.0 (http://creativecommons.org/licenses/ kwa michango ya hiari. Ikiwa ungependa kutoa
by/4.0/). Source: https://esahubble.org/images/ mchango, tafadhali tembelea donate.jw.org.
heic0702a/; page 56: Photo by US Signal Corps/The LIFE
ˆ
Picture Collection via Getty Images; page 76: Chateau Enjoy Life Forever!
de Versailles, France/Bridgeman Images; pages 103
—An Interactive Bible Course
and 131: Based on NASA/Visible Earth imagery; page 163:
˘ SINGLECELL ANIMATION LLC/Science Source;
page 183: Daniel Osterkamp/Moment/Getty Images
Swahili (lff-SW)
Chapa ya Juni 2021
Isipokuwa iwe imeonyeshwa vingine,
Maandiko yote yamenukuliwa kutoka katika ˘ 2021 WATCH TOWER BIBLE AND TRACT
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. SOCIETY OF PENNSYLVANIA

Machapisho yote yaliyorejelewa Wachapishaji


Printed by Watch Tower Bible
yamechapishwa na Mashahidi wa Yehova. and Tract Society of South Africa NPC
1 Robert Broom Drive East, Rangeview,
Krugersdorp, 1739, R.S.A.
Made in the Republic of South Africa
Limechapishwa Katika Jamhuri ya
Afrika Kusini
SEHEMU YA KWANZA
Jinsi ya kunufaika zaidi Ili kujitayarisha kwa ajili ya kila
na masomo haya ya Biblia somo, soma sehemu ya kwanza.
Maswali yaliyoandikwa kwa wino
mzito (A) na maandiko (B) yana-
Kwanza pitia muhtasari huu, kazia mambo makuu. Soma maandi-
kisha onyesha VIDEO. ko yaliyo na neno “soma.”

01
(
Biblia Inawezaje Kukusaidia? A
Sisi sote hujiuliza maswali kuhusu maisha, ku- tutafute majibu ya maswali hayo, na watu we-
teseka, kifo, na wakati ujao. Pia tunahangaikia ngi wamepata majibu yenye kuridhisha.
shughuli za kila siku, kama vile kupata riziki na
2. Biblia inawezaje kutusaidia tufurahie
jinsi ya kuwa na familia yenye furaha. Watu
VIDEO: Karibu Kwenye Funzo wengi wametambua kwamba Biblia imewasai-
dia kupata majibu ya maswali muhimu mai-
maisha ya kila siku?
Biblia hutupatia ushauri mzuri. Kwa mfano,
shani na pia ushauri unaotegemeka kuhusu inatufundisha jinsi ya kuwa na familia yenye
Lako la Biblia (2:45) maisha ya kila siku. Je, unamjua mtu yeyo-
te ambaye anaweza kunufaika kwa kujifunza
furaha. Pia, inatoa ushauri kuhusu kukabiliana
na mikazo na jinsi ya kufurahia kazi. Utaji-
Biblia? funza yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu
mambo hayo na mengine mengi katika chapi-
1. Biblia inajibu maswali gani? sho hili. Tuna hakika utakubali kwamba “kila
Biblia inajibu maswali haya muhimu: Uhai ulia- Andiko [katika Biblia] . . . ni lenye faida.”
nzaje? Maisha yana kusudi gani? Kwa nini —2 Timotheo 3:16.
watu huteseka? Ni nini humpata mtu anapo-
kufa? Ingawa kila mtu anapenda amani, kwa
nini kuna vita ulimwenguni? Ni nini kitakachoi-
pata dunia wakati ujao? Biblia inatutia moyo

Chapisho hili si Biblia. Hata hivyo, litakusaidia kuichunguza Biblia. Kwa hiyo, tunakutia moyo
usome maandiko yaliyo kwenye masomo haya na uyalinganishe na mambo unayojifunza.

Tumia alama hii kufungua B


VIDEO hiyo, au utazame
chapisho Furahia Maisha
Milele! kwenye jw.org/sw 5

Jinsi ya kupata mistari ya Biblia



A
YOHANA 16:33—17:24 Biblia ni mkusanyo wa vitabu vidogo 66. Imegawanywa
mtapata dhiki, lakini jipeni katika sehemu mbili: Maandiko ya Kiebrania na Kiaramu
moyo! Mimi nimeushinda uli- (“Agano la Kale”) na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo

mwengu.”
B (“Agano Jipya”).
17 Yesu akasema mambo
hayo, kisha akatazama Maandiko yanaonyeshwa kwa jina la kitabu cha Biblia
mbinguni na kusema: “Baba, saa (A), kisha sura (B), na mstari au mistari (C).
imefika. Mtukuze mwana wako
ili mwana wako akutukuze, Kwa mfano, Yohana 17:3 inamaanisha kitabu
2 kama vile ulivyompa mamla- cha Yohana, sura ya 17, mstari wa 3.
ka juu ya wote wenye mwili,

ili awape uzima wa C milele
wote ambao umempa. 3 Uzi-
ma wa milele ndio huu, waku-
jue wewe, Mungu wa pekee
wa kweli, na yule uliyemtu-
ma, Yesu Kristo. 4 Nimekutu-
kuza duniani, kwa kuwa nime-
maliza kazi uliyonipa nifanye.
SEHEMU YA KATIKATI SEHEMU YA MWISHO
Maneno yaliyo mwanzoni (C) katika sehemu ya Chimba Zaidi Somo linakamilishwa kwenye sehe-
yanaeleza habari ambazo zitazungumziwa. Vichwa vidogo (D) mu ya Muhtasari na Ungejibu-
vinaonyesha mambo makuu. Ukiwa pamoja na mwalimu wako, je? (G). Andika tarehe ambayo
soma maandiko, jibu maswali, na utazame video. Chunguza somo limekamilishwa. Kwenye
picha kwa makini na maelezo ya picha (E), na ufikirie jinsi Lengo (H) kuna sehemu ya
unavyoweza kujibu swali lililo chini ya Watu Fulani mambo ambayo unaweza kufa-
Husema (F). nyia kazi. Chini ya Chunguza Zai-
di (I) kuna habari za ziada ambazo
unaweza kusoma au kutazama.

5. Unaweza kufurahia kusoma Biblia


CH I M BA ZAI DI
(

Watu wengi wanafurahia kusoma Biblia na wananufaika kwa MUHTASARI


G CH U N G U ZA ZAI DI
I
Jifunze jinsi ambavyo Biblia imewasaidia watu, jinsi unavyoweza kufurahia
kuisoma, na kwa nini unapaswa kutafuta msaada ili kuielewa.
C VIDEO: Kusoma Biblia (2:05) kufanya hivyo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Katika video hiyo, vijana hao walihisije kuhusu kusoma?
Biblia inatoa ushauri mzuri kuhusu
maisha ya kila siku, inajibu maswali Jifunze jinsi ushauri wa
˙ Kwa nini sasa wanapenda kusoma Biblia? muhimu, na inawapa watu faraja na Biblia unavyotufaa leo.
tumaini. “Mafundisho ya Biblia
Biblia inasema kwamba inaweza kutupatia mwongozo —Hekima Isiyopitwa na
unaotupatia faraja na tumaini. Soma Waroma 15:4, Wakati” (Mnara wa Mlinzi
D 3. Biblia inaweza kutuongoza kisha mzungumzie swali hili:
˙ Je, unafurahia ahadi ya Biblia ya kukupatia faraja na tumaini?
Ungejibuje? Na. 1 2018)

Biblia ni kama tochi yenye mwangaza mkali. Tunaweza kutumia ˙ Biblia inatoa ushauri wa
Biblia kujua jinsi ya kufanya maamuzi mazuri na kutambua mambo aina gani?
yatakayotokea wakati ujao. ˙ Biblia inajibu maswali gani?
( Ona jinsi Biblia ilivyomsaidia
Soma Zaburi 119:105, kisha mzungumzie maswali haya: ˙ Ungependa kujifunza nini 2:53
mwanamume aliyepambana
katika Biblia?
˙ Yule aliyeandika andiko hili alikuwa na maoni gani kuhusu Biblia? na hisia mbaya tangu utotoni.
˙ Wewe una maoni gani kuhusu Biblia? Jinsi Nilivyoanza Kufurahia
Maisha Mapya

E
Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza ushauri wa Biblia
kuhusu maisha ya familia.
“Siri 12 za Mafanikio Katika
Familia” (Amkeni! Na. 2 2018)

4. Biblia inajibu maswali tunayojiuliza 6. Watu wengine wanaweza Lengo


(

Mwanamke fulani alitambua kwamba Biblia ina majibu ya


kutusaidia kuelewa Biblia N Soma sehemu ya kwanza
ya somo linalofuata.
VIDEO: Usikate Tamaa maswali yaliyomhangaisha kwa miaka mingi. Onyesha VIDEO, Zaidi ya kusoma Biblia wakiwa peke yao, watu wengi wametambua Mwanamume Mwethiopia
Kamwe! (1:48) kisha mzungumzie maswali haya: kwamba wanaielewa vizuri zaidi wanaposaidiwa na watu wengine. alihitaji msaada ili kuelewa
N Lengo lingine:
Maandiko. Leo watu wengi
˙ Katika video hiyo, mwanamke huyo alijiuliza maswali gani? Soma Matendo 8:26-31, kisha mzungumzie swali hili: ( 3:14 Jifunze jinsi Biblia inavyofu-
wananufaika kwa kujifunza nua ukweli kuhusu yule ana-
˙ Kujifunza Biblia kulimsaidiaje? ˙ Tunawezaje kuielewa Biblia vizuri?—Ona mstari wa 30 na 31. Biblia pamoja na wengine yeutawala ulimwengu huu.
Kwa Nini Ujifunze Biblia?
Biblia inatutia moyo tuulize maswali. Soma Mathayo 7:7,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Wewe hujiuliza maswali gani ambayo yanaweza kujibiwa
H —Video Nzima

na Biblia?

WATU FULANI HUSEMA: “Kujifunza Biblia ni kupoteza wakati.” F


˙ Wewe una maoni gani? Kwa nini?
Tumia alama hii kufungua marejeo yote
ya SOMO LA 1, au utazame chapisho
7 Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw

Visanduku vilivyoandikwa VIDEO vinakuele- Yaliyomo


keza kwenye marejeo yaliyo na habari zaidi
kuhusu mambo yanayozungumziwa. Baadhi N Sehemu ya 1 — ukurasa wa 4
ya video hizo zina masimulizi ya mambo
N Sehemu ya 2 — ukurasa wa 54
halisi. Na video nyingine ni maigizo ingawa
zinaonyesha mambo yanayoweza kutokea N Sehemu ya 3 — ukurasa wa 142
kihalisi. N Sehemu ya 4 — ukurasa wa 200
Maelezo ya — ukurasa wa 255
Ziada

Tumia alama hii kupakua TOLEO


LA KIELEKTRONI la masomo
haya, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele!
kwenye jw.org/sw
SEHEMU YA 1
Wazo Kuu: Chunguza jinsi
Biblia inavyoweza kukusaidia
na jinsi unavyoweza kumjua
Mtungaji wa Biblia

MASOMO
01 Biblia Inawezaje Kukusaidia?
02 Biblia Inatupatia Tumaini
03 Je, Unaweza Kuiamini Biblia?
04 Mungu Ni Nani?
05 Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa Mungu
06 Uhai Ulianzaje?
07 Yehova Ana Sifa Gani?
08 Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova
09 Mkaribie Mungu Kupitia Sala
10 Mikutano ya Mashahidi wa Yehova
Inaweza Kukunufaishaje?
11 Jinsi Unavyoweza Kunufaika Zaidi
Unaposoma Biblia
12 Ni Nini Kitakachokusaidia Uendelee
Kujifunza Biblia?
01

Biblia Inawezaje Kukusaidia?


Sisi sote hujiuliza maswali kuhusu maisha, ku- tutafute majibu ya maswali hayo, na watu we-
teseka, kifo, na wakati ujao. Pia tunahangaikia ngi wamepata majibu yenye kuridhisha.
shughuli za kila siku, kama vile kupata riziki na
jinsi ya kuwa na familia yenye furaha. Watu 2. Biblia inawezaje kutusaidia tufurahie
wengi wametambua kwamba Biblia imewasai- maisha ya kila siku?
dia kupata majibu ya maswali muhimu mai- Biblia hutupatia ushauri mzuri. Kwa mfano,
shani na pia ushauri unaotegemeka kuhusu inatufundisha jinsi ya kuwa na familia yenye
maisha ya kila siku. Je, unamjua mtu yeyo- furaha. Pia, inatoa ushauri kuhusu kukabiliana
te ambaye anaweza kunufaika kwa kujifunza na mikazo na jinsi ya kufurahia kazi. Utaji-
Biblia? funza yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu
mambo hayo na mengine mengi katika chapi-
1. Biblia inajibu maswali gani? sho hili. Tuna hakika utakubali kwamba “kila
Biblia inajibu maswali haya muhimu: Uhai ulia- Andiko [katika Biblia] . . . ni lenye faida.”
nzaje? Maisha yana kusudi gani? Kwa nini —2 Timotheo 3:16.
watu huteseka? Ni nini humpata mtu anapo-
kufa? Ingawa kila mtu anapenda amani, kwa
nini kuna vita ulimwenguni? Ni nini kitakachoi-
pata dunia wakati ujao? Biblia inatutia moyo

Chapisho hili si Biblia. Hata hivyo, litakusaidia kuichunguza Biblia. Kwa hiyo, tunakutia moyo
usome maandiko yaliyo kwenye masomo haya na uyalinganishe na mambo unayojifunza.

5
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi ambavyo Biblia imewasaidia watu, jinsi unavyoweza kufurahia


kuisoma, na kwa nini unapaswa kutafuta msaada ili kuielewa.

3. Biblia inaweza kutuongoza


Biblia ni kama tochi yenye mwangaza mkali. Tunaweza kutumia
Biblia kujua jinsi ya kufanya maamuzi mazuri na kutambua mambo
yatakayotokea wakati ujao.
Soma Zaburi 119:105, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Yule aliyeandika andiko hili alikuwa na maoni gani kuhusu Biblia?
˙ Wewe una maoni gani kuhusu Biblia?

(
4. Biblia inajibu maswali tunayojiuliza
Mwanamke fulani alitambua kwamba Biblia ina majibu ya
VIDEO: Usikate Tamaa maswali yaliyomhangaisha kwa miaka mingi. Onyesha VIDEO,
Kamwe! (1:48) kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Katika video hiyo, mwanamke huyo alijiuliza maswali gani?
˙ Kujifunza Biblia kulimsaidiaje?

Biblia inatutia moyo tuulize maswali. Soma Mathayo 7:7,


kisha mzungumzie swali hili:
˙ Wewe hujiuliza maswali gani ambayo yanaweza kujibiwa
na Biblia?
(
5. Unaweza kufurahia kusoma Biblia
Watu wengi wanafurahia kusoma Biblia na wananufaika kwa
VIDEO: Kusoma Biblia (2:05) kufanya hivyo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Katika video hiyo, vijana hao walihisije kuhusu kusoma?
˙ Kwa nini sasa wanapenda kusoma Biblia?

Biblia inasema kwamba inaweza kutupatia mwongozo


unaotupatia faraja na tumaini. Soma Waroma 15:4,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Je, unafurahia ahadi ya Biblia ya kukupatia faraja na tumaini?

6. Watu wengine wanaweza


kutusaidia kuelewa Biblia
Zaidi ya kusoma Biblia wakiwa peke yao, watu wengi wametambua Mwanamume Mwethiopia
kwamba wanaielewa vizuri zaidi wanaposaidiwa na watu wengine. alihitaji msaada ili kuelewa
Soma Matendo 8:26-31, kisha mzungumzie swali hili: Maandiko. Leo watu wengi
wananufaika kwa kujifunza
˙ Tunawezaje kuielewa Biblia vizuri?—Ona mstari wa 30 na 31. Biblia pamoja na wengine

WATU FULANI HUSEMA: “Kujifunza Biblia ni kupoteza wakati.”


˙ Wewe una maoni gani? Kwa nini?

7
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Biblia inatoa ushauri mzuri kuhusu
maisha ya kila siku, inajibu maswali Jifunze jinsi ushauri wa
muhimu, na inawapa watu faraja na Biblia unavyotufaa leo.
tumaini. “Mafundisho ya Biblia
—Hekima Isiyopitwa na
Wakati” (Mnara wa Mlinzi
Ungejibuje? Na. 1 2018)

˙ Biblia inatoa ushauri wa


aina gani?
˙ Biblia inajibu maswali gani?
( Ona jinsi Biblia ilivyomsaidia
˙ Ungependa kujifunza nini 2:53
mwanamume aliyepambana
katika Biblia?
na hisia mbaya tangu utotoni.
Jinsi Nilivyoanza Kufurahia
Maisha Mapya

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza ushauri wa Biblia


kuhusu maisha ya familia.
“Siri 12 za Mafanikio Katika
Familia” (Amkeni! Na. 2 2018)
Lengo
N Soma sehemu ya kwanza
ya somo linalofuata.

N Lengo lingine:
( 3:14 Jifunze jinsi Biblia inavyofu-
nua ukweli kuhusu yule ana-
yeutawala ulimwengu huu.
Kwa Nini Ujifunze Biblia?
—Video Nzima

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 1, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
02

Biblia Inatupatia Tumaini


Watu ulimwenguni pote wanakabili matatizo tukate tamaa maishani leo, kama vile umaski-
yanayowafanya wawe na huzuni, wasiwasi, na ni, ukosefu wa haki, magonjwa, na kifo, haya-
hata maumivu. Je, umewahi kupatwa na hali takuwapo tena. Biblia inaahidi kwamba wa-
iliyofanya uhisi hivyo? Labda unateseka kwa nadamu watafurahia kuishi milele katika
sababu ya ugonjwa au kwa sababu umefiwa Paradiso duniani.
na mtu unayempenda. Huenda unajiuliza, ‘Je,
maisha yangu yatabadilika na kuwa mazuri?’ 3. Unawezaje kuwa na hakika kwamba ahadi
Biblia inajibu swali hilo kwa njia yenye kufariji. za Biblia zitatimia?
Watu wengi wangependa kuwa na maisha ma-
1. Biblia inatupatia tumaini gani? zuri, lakini hawana hakika ikiwa matarajio yao
Biblia inaeleza sababu zinazofanya ulimwengu yatatimia. Hata hivyo, ahadi zilizo katika Biblia
ujae matatizo, vilevile inatupatia habari njema zitatimia. Tunaweza kuwa na uhakika kuhu-
kwamba matatizo haya ni ya muda mfupi na su ahadi hizo kwa ‘kuyachunguza Maandiko
yatakwisha hivi karibuni. Ahadi za Biblia zi- kwa uangalifu.’ (Matendo 17:11) Unapojifunza
naweza kukupatia “wakati ujao na tumaini.” Biblia, utapata usadikisho ambao utakusaidia
(Soma Yeremia 29:11, 12.) Ahadi hizo zinatu- kuamini mambo ambayo Biblia inasema kuhu-
saidia kukabiliana na matatizo sasa, kuwa na su wakati ujao.
mtazamo mzuri, na kupata furaha ya kudumu.

2. Biblia inaahidi nini kuhusu wakati ujao?


Biblia inaeleza kwamba wakati ujao “kifo ha-
kitakuwapo tena, wala maombolezo wala
kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”
(Soma Ufunuo 21:4.) Matatizo yanayofanya

9
CH I M BA ZAI DI

Chunguza baadhi ya hali ambazo


Biblia inaahidi kuhusu wakati ujao.
Ona jinsi tumaini ambalo Biblia
inatupatia linavyowasaidia
watu leo.

4. Biblia inatupatia tumaini


la kuishi milele bila matatizo
Ona orodha ifuatayo ya ahadi zilizo katika Biblia. Ni ahadi gani ambazo
unapenda zaidi? Kwa nini?
Soma maandiko yaliyoambatanishwa na ahadi hizi, kisha ufikirie maswali haya:
˙ Je, maandiko haya yanakupatia tumaini? Je, yanaweza kuwapatia tumaini
watu wa familia yako na marafiki?

Wazia ukiishi katika ulimwengu ambao

HAKUNA MTU AMBAYE . . . KILA MTU . . .

˙ atahisi maumivu, atadhoofika ˙ atawaona wapendwa wake


kwa sababu ya kuzeeka, au kufa. wakifufuliwa, na kuishi duniani.
—Isaya 25:8. —Yohana 5:28, 29.
˙ atapatwa na magonjwa au kuishi ˙ atafurahia kuwa na afya nzuri na
na ulemavu.—Isaya 33:24; 35:5, 6. nguvu za ujana.—Ayubu 33:25.
˙ atatendewa bila haki. ˙ atakuwa na chakula tele, makao mazuri, na kazi
—Isaya 32:16, 17. yenye kuridhisha.—Zaburi 72:16; Isaya 65:21, 22.
˙ atateseka kwa sababu ya vita. ˙ atakuwa na amani kwa wingi.
—Zaburi 46:9. —Zaburi 37:11.
˙ atasumbuliwa na mawazo au ku- ˙ ataishi milele katika hali bora.
mbukumbu mbaya.—Isaya 65:17. —Zaburi 37:29.
5. Tumaini la Biblia linaweza
kubadili maisha yako
Watu wengi huvunjika moyo au kukasirika kwa sababu
(
ya matatizo wanayokabili. Wengine hujitahidi sana kuleta
mabadiliko. Ona jinsi ahadi ya Biblia kwamba hali zitabadilika
inavyowasaidia watu leo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie
VIDEO: Nilitaka Kupigania
Haki (4:07)
maswali haya:
˙ Katika video hiyo, ni ukosefu gani wa haki ambao
ulimhangaisha Rafika?
˙ Ingawa ukosefu wa haki alioona haukwisha,
Biblia ilimsaidiaje?

Biblia inatupatia tumaini la wakati ujao ambalo linatusaidia


kuwa na furaha na kutovunjika moyo ingawa tuna matatizo.
Soma Methali 17:22 na Waroma 12:12, kisha mzungumzie
maswali haya:
˙ Je, unafikiri tumaini ambalo Biblia inatupatia linaweza
kubadili maisha yako sasa? Kwa nini?

WATU FULANI HUSEMA: “Ahadi za Biblia kuhusu wakati ujao ni mambo ya kuwaziwa tu.”
˙ Kwa nini unapaswa kuchunguza uthibitisho?

11
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Biblia inatupatia tumaini zuri la
wakati ujao ambalo hutusaidia Jifunze jinsi tumaini
kukabiliana na matatizo. linavyoweza kukusaidia
kukabiliana na matatizo.
“Tumaini—Je, Linaweza
Ungejibuje? Kutusaidia?” (Amkeni!,
Aprili 22, 2004)
˙ Kwa nini watu wanahitaji
tumaini?
˙ Biblia inaahidi nini kuhusu
wakati ujao?
Ona jinsi ambavyo tumaini la
˙ Tumaini la wakati ujao
wakati ujao limewasaidia watu
linaweza kukusaidiaje sasa? wenye magonjwa ya kudumu.
“Je, Biblia Inaweza Kunisaidia
Ikiwa Nina Ugonjwa wa Kudu-
mu?” (Makala iliyo kwenye mta-
ndao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 3:37 Unapotazama video hii


ya muziki, jiwazie wewe na
familia yako mkifurahia maisha
katika Paradiso ya wakati ujao
iliyoahidiwa katika Biblia.
Lengo
Wazia Maisha Paradiso
N Jifunze ahadi za Biblia kwa
kusoma maandiko yaliyo
kwenye somo hili.

N Lengo lingine: Soma jinsi maisha ya


mwanaharakati wa masua-
la ya kijamii yalivyobadilika
alipojifunza kuhusu tumai-
ni la wakati ujao ambalo
linapatikana katika Biblia.
“Sitamani Tena Kuubadili
Ulimwengu” (Mnara wa Mlinzi,
Julai 1, 2013)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 2, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
03

Je, Unaweza Kuiamini Biblia?


Biblia ina ahadi nyingi na pia inatoa ushauri hawakuamini mambo iliyotaja kuhusu habari
mwingi. Labda ungependa kujua mambo ina- hizo. Hata hivyo, sayansi imethibitisha kwa-
yofundisha, lakini huenda una shaka. Je, una- mba habari zilizo katika Biblia ni sahihi. Bib-
weza kuamini ahadi na ushauri wa kitabu kili- lia ‘inategemeka sikuzote, sasa na milele.’
choandikwa zamani sana? Je, kweli unaweza —Zaburi 111:8.
kuamini mambo ambayo Biblia inasema ku-
husu kufurahia maisha sasa na wakati ujao? 3. Kwa nini tunapaswa kuamini
Watu wengi wanaiamini. Wewe pia unaweza mambo ambayo Biblia inasema
kuiamini. kuhusu wakati ujao?
Biblia ina unabii unaotabiri “mambo amba-
1. Je, mambo yaliyoandikwa katika Biblia yo bado hayajafanywa.” (Isaya 46:10) Ilita-
ni ya kweli? biri kwa usahihi matukio ya kihistoria muda
Biblia inasema kwamba ina “maneno sahihi mrefu kabla hayajatokea. Pia, inataja kihusu-
ya kweli.” (Mhubiri 12:10) Inasimulia matukio sa hali zilizopo ulimwenguni leo. Katika somo
halisi yanayohusu watu halisi. (Soma Luka 1:3; hili, tutachunguza baadhi ya unabii ulio katika
3:1, 2.) Wanahistoria wengi na wataalamu wa Biblia. Unabii huo ulitimia kwa usahihi kabisa!
vitu vya kale wamethibitisha usahihi wa tare-
 Unabii unatia ndani ujumbe kutoka kwa Mungu kuhusu waka-
he, watu, mahali, na matukio muhimu yanayo- ti ujao.
tajwa katika Biblia.

2. Kwa nini tunaweza kusema kwamba Biblia


haijapitwa na wakati?
Biblia inataja mambo mbalimbali ambayo ha-
yakujulikana ilipoandikwa. Kwa mfano, ina-
zungumzia mambo ya kisayansi. Watu wengi

13
CH I M BA ZAI DI

Fikiria jinsi Biblia inavyopatana na sayansi, na uchunguze


unabii fulani wenye kuvutia ulio katika Biblia.

4. Sayansi inapatana na Biblia


Nyakati za kale, watu wengi waliamini kwamba
dunia imeshikiliwa na kitu fulani. Onyesha VIDEO.

( VIDEO: Dunia Inaning’inia


Pasipo Kitu (1:14)

Ona jambo ambalo liliandikwa katika kitabu cha Ayubu miaka 3,500
hivi iliyopita. Soma Ayubu 26:7, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kwa nini inashangaza kwamba maneno dunia inaning’inia
“pasipo na kitu” yaliandikwa miaka 3,500 iliyopita?

Mzunguko wa maji duniani ulieleweka vizuri miaka 200 hivi iliyopita. Biblia inafafanua
Hata hivyo, ona jambo ambalo Biblia ilisema miaka 3,500 hivi iliyopita. mzunguko wa maji
wa dunia
Soma Ayubu 36:27, 28, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Ni nini kinachokupendeza kuhusu ufafanuzi huu rahisi
wa mzunguko wa maji?
˙ Je, maandiko uliyosoma yamekusaidia kuiamini zaidi Biblia?

(
5. Biblia ilitabiri matukio muhimu
Soma Isaya 44:27–45:2, kisha mzungumzie swali hili:
VIDEO: Biblia Ilitabiri ˙ Biblia ilitaja kihususa habari gani miaka 200 kabla
Kuharibiwa kwa Jiji ya kuharibiwa kwa jiji la Babiloni?
la Babiloni (0:58)
Onyesha VIDEO.
Historia inathibitisha kwamba Mfalme Koreshi wa Uajemi na jeshi
lake walilishinda jiji la Babiloni mwaka wa 539 K.W.K. Waligeuza
mkondo wa mto uliolinda jiji hilo. Wakaingia katika jiji kupitia ma-
lango yaliyokuwa yameachwa wazi na kuliteka bila kupigana. Leo,
zaidi ya miaka 2,500 imepita na bado jiji la Babiloni ni magofu.
Ona jambo ambalo Biblia ilitabiri.
Soma Isaya 13:19, 20, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Unabii kuhusu Babiloni ulitimizwaje?

 K.W.K. inamaanisha “Kabla ya Wakati wa Kawaida,” na W.K. inamaanisha


“Wakati wa Kawaida.”

Magofu ya Babiloni nchini Iraq

6. Biblia ilitabiri hali tunazoona leo


Biblia inasema kwamba tunaishi katika “siku za
mwisho.” (2 Timotheo 3:1) Ona mambo ambayo
Biblia ilitabiri kuhusu siku za mwisho.
Soma Mathayo 24:6, 7, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Biblia ilitabiri nini kuhusu siku za mwisho?

Soma 2 Timotheo 3:1-5, kisha mzungumzie


maswali haya:
˙ Biblia ilitabiri watu wa siku za mwisho
wangekuwa na tabia gani?
˙ Umejionea mambo gani kati ya hayo
yakitimia leo?

WATU FULANI HUSEMA: “Biblia ni kitabu cha hadithi na hekaya.”


˙ Ni jambo gani linalokupa uhakika kwamba tunaweza kuiamini Biblia?

15
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Matukio ya kihistoria, uthibitisho
wa kisayansi, na unabii unatusaidia Je, Biblia ina habari
kuiamini Biblia. zisizo sahihi kisayansi?
“Je, Sayansi Inapatana
na Biblia?” (Makala iliyo
Ungejibuje? kwenye mtandao)

˙ Je, mambo yaliyoandikwa


katika Biblia ni ya kweli?
˙ Ni mambo gani ya kisayansi
yanayopatana na Biblia?
Ni mambo gani yaliyotabiriwa
˙ Je, unaamini kwamba Biblia
kuhusu “siku za mwisho”?
inatabiri kuhusu wakati ujao?
Kwa nini? “Mambo 6 Yaliyotabiriwa Ka-
tika Biblia Yanayotimia Sasa”
(Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 2011)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 5:22 Jifunze jinsi unabii wa


Biblia kuhusu Milki ya
Ugiriki ulivyotimizwa.
Kuimarishwa na
Lengo “Neno la Kinabii”

N Ili uamini zaidi Biblia, soma ma-


kala au utazame video kwenye
sehemu ya Chunguza Zaidi.

N Lengo lingine: Ona jinsi unabii wa Biblia


ulivyobadili maoni ya
mwanamume huyu.
“Niliamini Hakuna Mungu”
(Mnara wa Mlinzi Na. 5 2017)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 3, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
04

Mungu Ni Nani?
Katika historia yote, wanadamu wameabudu 2. Biblia inatufundisha nini kumhusu Yehova?
miungu ya aina mbalimbali. Hata hivyo, Biblia Biblia inasema kwamba kati ya miungu yote
inamtaja Mungu mmoja ambaye “ni mkuu ku- ambayo watu huabudu, Yehova ndiye Mu-
liko miungu mingine yote.” (2 Mambo ya Nya- ngu pekee wa kweli. Kwa nini? Kuna saba-
kati 2:5) Ni Mungu gani huyo? Na kwa nini bu kadhaa. Yehova ndiye mwenye mamlaka
ni mkuu kuliko miungu mingine yote ambayo yote, na yeye ndiye aliye “Juu Zaidi, juu ya
watu huabudu? Katika somo hili, utajifunza ji- dunia yote.” (Soma Zaburi 83:18.) Yeye ndi-
nsi Mungu huyo anavyojitambulisha kwako. ye “Mweza-Yote,” kwa sababu ana uwezo wa
kufanya chochote anachotaka kufanya. Yeye
1. Mungu anaitwa nani, na ni nini kinachoonye-
ndiye ‘aliyeumba vitu vyote,’ kutia ndani uli-
sha kwamba anataka tulijue jina lake?
mwengu na kila kitu kilicho hai duniani. (Ufu-
Mungu anajitambulisha kwetu kupitia Biblia. nuo 4:8, 11) Yehova peke yake ndiye ameku-
Anasema: “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina la- wepo sikuzote, na ataendelea kuwepo milele.
ngu.” (Soma Isaya 42:5, 8.) Jina “Yehova” li- —Zaburi 90:2.
metafsiriwa kutoka katika Kiebrania na lina-
maanisha “Yeye Husababisha Kuwa.” Yehova
anataka ulijue jina lake, na ulitumie. (Kuto-
ka 3:15) Tunajuaje jambo hilo? Alihakikisha
kwamba jina lake linapatikana zaidi ya mara
7,000 katika Biblia!  Jina Yehova ni la “Mu-
ngu wa kweli juu mbinguni na chini duniani.”
—Kumbukumbu la Torati 4:39.
 Ili kupata habari zaidi kuhusu maana ya jina la Mungu na kwa
nini limeondolewa katika baadhi ya tafsiri za Biblia ona Nyo-
ngeza A4 katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

17
CH I M BA ZAI DI

Chunguza tofauti kati ya majina ya cheo ya Mungu na jina lake la kibinafsi.


Kisha ujifunze jinsi ambavyo amekujulisha jina lake na kwa nini amefanya hivyo.

YE HOVA

(
3. Mungu ana majina mengi ya cheo,
lakini ana jina moja la kibinafsi
VIDEO: Majina Mengi ya Cheo, Ili kuona tofauti kati ya cheo cha mtu na jina lake la kibinafsi,
Lakini Jina Moja la Kibinafsi onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali hili:
(0:41)
˙ Kuna tofauti gani kati ya jina la cheo kama vile “Bwana,”
na jina la kibinafsi?

Biblia inasema kwamba watu huabudu miungu mingi na mabwana


wengi. Soma Zaburi 136:1-3, kisha mzungumzie swali hili:
˙ “Mungu wa miungu” na “Bwana wa mabwana” ni nani?
(
4. Yehova anataka ujue
na kulitumia jina lake
VIDEO: Je, Mungu Ana Jina? Ni nini kinachoonyesha kwamba Yehova anataka ulijue jina lake?
—Kisehemu (3:11) Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Unafikiri Yehova anataka watu walijue jina lake? Kwa nini?

Yehova anataka watu walitumie jina lake. Soma Waroma 10:13,


kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kwa nini tunapaswa kutumia jina Yehova?
˙ Wewe unahisije mtu anapokumbuka jina lako na kulitumia?
˙ Unafikiri Yehova anahisije unapolitumia jina lake?

5. Yehova anataka uwe rafiki yake (

Mwanamke fulani kutoka Kambodia anayeitwa Soten alisema


kwamba kujua jina la Mungu kulimletea “hisia za kipekee.” VIDEO: Jitihada Zangu
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali hili: za Kumtafuta Mungu
wa Kweli (8:19)
˙ Katika video hiyo, Soten alihisije baada ya kujua
jina la Mungu?

Kwa kawaida, ili mtu awe rafiki yako unapaswa kulijua jina lake.
Soma Yakobo 4:8a, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Yehova anataka ufanye nini?
˙ Kujua na kulitumia jina la Mungu kutakusaidiaje
uwe rafiki yake?

WATU FULANI HUSEMA: “Kuna Mungu mmoja tu, na unaweza kumwita jina lolote.”
˙ Je, unaamini kwamba jina la Mungu ni Yehova?
˙ Unaweza kutoa sababu gani ili kuonyesha kwamba Mungu anataka tulitumie jina lake?

19
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova ni jina la Mungu pekee wa
kweli. Anataka tulijue na kulitumia Chunguza sababu tano zenye
jina hilo ili tuwe rafiki zake. kusadikisha zinazothibitisha
kwamba kuna Mungu.
“Je, Kuna Mungu?”
Ungejibuje? (Makala iliyo kwenye mtandao)

˙ Kwa nini Yehova ni tofauti


na miungu mingine ambayo
watu huabudu?
˙ Kwa nini tunapaswa kulitumia
jina la Mungu? Chunguza kwa nini inapata-
na na akili kuamini kwamba
˙ Ni nini kinachoonyesha kwamba
Mungu amekuwepo sikuzote.
Yehova anataka uwe rafiki yake?
“Ni Nani Aliyemuumba
Mungu?” (Mnara wa Mlinzi,
Agosti 1, 2014)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Jifunze kwa nini tunapaswa


kutumia jina la Mungu, hata
kama hatujui jinsi lilivyota-
mkwa nyakati za kale.
Lengo “Yehova Ni Nani?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
N Unapozungumza kumhusu
Mungu, tumia jina lake, Yehova.

N Lengo lingine:
Je, tunaweza kumwita Mungu
kwa jina lolote tunalopenda?
Ona kwa nini tunaweza
kusema kwamba ana jina
moja tu la kibinafsi.
“Mungu Ana Majina
Mangapi?” (Makala iliyo
kwenye mtandao)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 4, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
05

Biblia Ni Ujumbe Kutoka


kwa Mungu
Yehova ametupatia Biblia. Biblia ni zawadi 2. Je, kila mtu duniani anaweza kuipata
nzuri sana ambayo ina vitabu mbalimbali 66. Biblia?
Huenda ukajiuliza: ‘Biblia ilitoka wapi? Ni nani “Kila taifa na kabila na lugha na watu” wana-
aliyeitunga?’ Ili kujibu maswali hayo, tutazu- weza kunufaika na habari njema iliyo katika
ngumzia jinsi ujumbe wa Mungu katika Biblia Biblia. (Soma Ufunuo 14:6.) Mungu amehaki-
ulivyotufikia. kisha kwamba Biblia inapatikana katika lugha
nyingi zaidi kuliko kitabu kingine chochote.
1. Ikiwa Biblia iliandikwa na wanadamu,
Karibu kila mtu anaweza kuipata Biblia. Inapa-
kwa nini tunasema ni Neno la Mungu?
tikana kila mahali na katika lugha nyingi sana.
Biblia iliandikwa na watu 40 kwa kipindi
cha miaka 1,600 hivi, kuanzia mwaka 3. Yehova amehakikishaje kwamba Biblia
wa 1513 K.W.K. hadi 98 W.K. Waandikaji imehifadhiwa ingawa watu wamejaribu
hao walitoka katika malezi mbalimbali. Inga- kuiharibu?
wa hivyo, ujumbe walioandika unapatana. Biblia iliandikwa kwenye vitu vinavyoweza ku-
Linawezekanaje? Hilo linawezekana kwa saba- haribika, kama vile ngozi na mafunjo. Lakini
bu Mungu ndiye Mtungaji wa Biblia. (Soma watu walioipenda Biblia waliinakili kwa mkono
1 Wathesalonike 2:13.) Waandikaji hao hawa- tena na tena kwa makini sana. Ingawa watu
kuandika mawazo yao wenyewe. Badala yake, wenye mamlaka walijaribu kuiharibu, watu fu-
“walisema yaliyotoka kwa Mungu kama wali- lani walihatarisha uhai wao ili kuilinda. Yeho-
vyoongozwa na roho takatifu.” (2 Petro va amehakikisha kwamba hakuna mtu au kitu
1:21) Mungu alitumia roho yake takatifu ku- chochote ambacho kimemzuia kuwasiliana
waongoza au kuwachochea watu hao waandi- nasi kupitia Biblia. Biblia inasema: “Neno la
ke mawazo yake.—2 Timotheo 3:16. Mungu wetu linadumu milele.”—Isaya 40:8.
 Kama itakavyofafanuliwa katika Somo la 7, roho takatifu ni
nguvu ya utendaji ya Mungu.

21
CH I M BA ZAI DI

Jifunze mengi kuhusu jinsi Mungu alivyowaongoza watu kuiandika Biblia, jinsi
alivyoihifadhi, na jinsi alivyohakikisha kwamba watu wote wanaweza kuipata.

4. Biblia inatuambia ni
nani aliyeitunga
Onyesha VIDEO. Kisha soma 2 Timotheo 3:16,
na mzungumzie maswali yanayofuata.

( VIDEO: Ni Nani Aliyeitunga


Biblia?—Kisehemu (2:48)

˙ Ikiwa Biblia iliandikwa na wanadamu,


kwa nini inaitwa Neno la Mungu?
˙ Je, unafikiri inapatana na akili kuamini
Karani anaweza kuandika barua yenye ujumbe kwamba Mungu aliwatumia wanadamu
kutoka kwa bosi wake. Vivyo hivyo, wanadamu kuwasilisha mawazo yake?
waliandika Biblia, lakini ujumbe wake ulitoka
kwa Mungu

5. Biblia iliokoka upinzani mkali (

Kwa kuwa Biblia ilitoka kwa Mungu, basi tunatazamia kwamba


angeilinda ili isiharibiwe. Katika historia yote, watu wenye mamla- VIDEO: Waliithamini Biblia
ka wamejaribu kuiangamiza Biblia. Viongozi wa kidini wamejaribu —Kisehemu (William Tyndale)
kuificha. Lakini licha ya upinzani na vitisho vya kuuawa, watu wengi (6:19)
walihatarisha uhai wao ili kuilinda. Ili ujifunze kuhusu mmoja wao,
onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Baada ya kujua jitihada nyingi zilizofanywa ili kuilinda Biblia,
je, unachochewa kuisoma? Kwa nini?

Soma Zaburi 119:97, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Kwa nini watu wengi walihatarisha uhai wao ili kutafsiri na
kuisambaza Biblia?
6. Kitabu kwa ajili ya watu wote
Biblia ndicho kitabu ambacho kimetafsiriwa na kusambazwa zaidi duniani.
Soma Matendo 10:34, 35, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kwa nini Mungu anataka Neno lake litafsiriwe na kusambazwa kwa wingi?
˙ Wewe binafsi unapendezwa na jambo gani kuhusu Biblia?

Karibu

Asilimia
100
ya watu
ulimwenguni
wanaweza kuipata
Biblia katika lugha
wanayoielewa
Inapatikana
katika lugha
zaidi ya

3,000
ikiwa nzima au
sehemu fulani
ya Biblia

5,000,000,000
Inakadiriwa nakala bilioni tano zimechapishwa,
idadi kubwa kuliko kitabu kingine chochote

WATU FULANI HUSEMA: “Biblia ni kitabu cha zamani kilichoandikwa na wanadamu.”


˙ Wewe una maoni gani?
˙ Ni nini kinachothibitisha kwamba Biblia ni Neno la Mungu?

23
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Biblia ni Neno la Mungu, na
amehakikisha kwamba watu Soma kuhusu historia
wote wanaweza kuipata. ya Biblia—kuanzia hati za
awali hadi tafsiri za kisasa.
“Jinsi Biblia Ilivyotufikia”
Ungejibuje? (Amkeni!, Novemba 2007)

˙ Mungu aliwaongozaje
wanadamu kuandika Biblia?
˙ Ni jambo gani linalokupendeza
kuhusu kuhifadhiwa, kutafsiriwa,
na kusambazwa kwa Biblia? Jifunze kuhusu hatari tatu
ambazo Biblia ilikabili katika
˙ Baada ya kujua jitihada ambazo
jitihada za kuiangamiza.
Mungu amefanya ili kuwasiliana
“Jinsi Biblia Ilivyookoka”
nawe kupitia Biblia, unahisije?
(Mnara wa Mlinzi Na. 4 2016)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 14:26 Ona jinsi watu walivyohatari-


sha uhai wao ili kuitafsiri Biblia.
Waliithamini Biblia

Lengo
N Anza kuisoma Biblia kwa uka-
waida, kwa kutumia chati ya
“Ratiba ya Kusoma Biblia.”

N Lengo lingine: Biblia imenakiliwa na kutafsi-


riwa mara nyingi. Tunawezaje
kuwa na hakika kwamba uju-
mbe wake haujabadilishwa?
“Je, Biblia Imebadilishwa au
Kupotoshwa?” (Makala iliyo
kwenye mtandao)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 5, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
06

Uhai Ulianzaje?
“[Mungu] ndiye chanzo cha uhai.” (Zaburi mba dunia ikiwa mahali pazuri pa kuishi na
36:9) Je, unaamini hivyo? Watu fulani wanafi- makao ya kudumu ya wanadamu. (Soma Isaya
kiri kwamba uhai haukuumbwa, bali ulijitokeza 40:28; 42:5.) Sayansi inathibitisha kwamba
wenyewe. Ikiwa hilo ni kweli, basi tuko hai kwa dunia ni sayari ya kipekee. Dunia ndiyo sayari
sababu ya tukio ambalo halikupangiwa. Lakini pekee inayoweza kuendeleza uhai wa wana-
ikiwa Yehova ndiye aliyeumba uhai, bila sha- damu.
ka maisha yetu yana kusudi. Chunguza jinsi
Biblia inavyoeleza kuhusu chanzo cha uhai na 3. Ni nini kinachofanya wanadamu wawe
kwa nini tunaweza kuamini kwamba inasema tofauti na wanyama?
ukweli. Baada ya kuumba dunia, Yehova aliumba viu-
mbe. Kwanza, aliumba mimea na wanyama
1. Ulimwengu ulitoka wapi? duniani. Kisha, “Mungu akamuumba mtu kwa
Biblia inasema: “Hapo mwanzo Mungu aliu- mfano wake.” (Soma Mwanzo 1:27.) Kwa nini
mba mbingu na dunia.” (Mwanzo 1:1) Wana- wanadamu ni viumbe wa kipekee? Tumeu-
sayansi wengi wanakubali kwamba ulimwengu mbwa kwa mfano wa Mungu, kwa hiyo tuna-
ulikuwa na mwanzo. Mungu aliumbaje uli- weza kuonyesha sifa zake kama vile upendo
mwengu? Alitumia ‘nguvu yake ya utendaji,’ na haki. Vilevile alituumba tukiwa na uwezo
yaani, roho yake takatifu kuumba kila kitu uli- wa kujifunza lugha, kufurahia vitu maridadi,
mwenguni kutia ndani nyota na sayari.—Mwa- na muziki. Tofauti na wanyama, tunaweza ku-
nzo 1:2. mwabudu Muumba wetu.

2. Kwa nini Mungu aliumba dunia?


Yehova “hakuiumba [dunia] tu bila sababu,
lakini aliiumba ili ikaliwe.” (Isaya 45:18) Aliu-
 Somo la 25 litazungumzia Mungu ana kusudi gani kwa wana-
damu.

25
CH I M BA ZAI DI

Chunguza mambo yanayothibitisha kwamba uhai uliumbwa na kwamba


simulizi la Biblia kuhusu uumbaji linapatana na akili. Jifunze mambo
ambayo sifa za wanadamu zinatufundisha kumhusu Mungu.

(
4. Uhai uliumbwa
Wanadamu husifiwa wanapotengeneza vitu kwa kuiga muundo
VIDEO: Kumwamini wa vitu vya asili. Basi ni nani anayepaswa kusifiwa kwa kuumba
Mungu (2:42) vitu vya asili? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Wanadamu wamebuni vitu gani kwa kuiga muundo wa
vitu vya asili?
Je, wajua?
Unaweza kupata makala Kila nyumba ilibuniwa na kujengwa na mtu fulani. Lakini ni
na video kuhusu habari hii nani aliyebuni na kuumba vitu vya asili? Soma Waebrania 3:4,
kwenye mfululizo huu “Je, Ni kisha mzungumzie maswali haya:
Kazi ya Ubuni?” na “Maoni
Kuhusu Chanzo cha Uhai.” ˙ Wewe unavutiwa zaidi na vitu gani vya asili?
˙ Je, inapatana na akili kuamini kwamba ulimwengu
na kila kitu kilichomo kiliumbwa? Kwa nini?

“Bila shaka, kila nyumba hujengwa na mtu fulani,


lakini yule aliyevijenga vitu vyote ni Mungu”
(
5. Simulizi la Biblia kuhusu uumbaji
linapatana na akili
VIDEO: Je, Ulimwengu Uliumbwa? Katika Mwanzo sura ya 1, Biblia inaeleza kuhusu chanzo
—Kisehemu (3:51) cha dunia na uhai uliomo. Je, unaamini simulizi hilo, au je,
ni hadithi ya kutungwa? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie
maswali haya:
˙ Je, Biblia inafundisha kwamba dunia na uhai uliomo
uliumbwa kwa siku sita zenye urefu wa saa 24?
˙ Je, unafikiri simulizi la Biblia kuhusu uumbaji ni sahihi
na linapatana na akili? Kwa nini?

Soma Mwanzo 1:1, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Wanasayansi wanasema kwamba ulimwengu ulikuwa
na mwanzo. Maoni yao yanapatanaje na jambo ambalo
umesoma katika Biblia?

Baadhi ya watu hufikiri kwamba Mungu alitumia mageuzi


kuumba uhai. Soma Mwanzo 1:21, 25, 27, kisha mzungumzie
maswali haya:
˙ Je, Biblia inafundisha kwamba Mungu aliumba uhai
wa hali ya chini akauacha ujigeuze kuwa samaki,
kisha mnyama, na mwishowe kuwa mwanadamu?
Au je, aliumba “aina” mbalimbali za uhai? 

 Katika Biblia, neno “aina” linarejelea kundi kubwa la vitu vilivyo hai.

6. Wanadamu ni viumbe wa kipekee wa Mungu


Sisi ni tofauti na wanyama ambao Yehova aliumba. Soma Mwanzo 1:26,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kwa kuwa tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, uwezo wetu wa
kuonyesha upendo na huruma unatufundisha Mungu ana sifa gani?

WATU FULANI HUSEMA: “Simulizi la Biblia kuhusu uumbaji ni hadithi ya kutungwa.”


˙ Wewe una maoni gani? Kwa nini?

27
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova aliumba ulimwengu
na uhai wa kila aina. Ona jinsi vitu vya
asili vinavyothibitisha
kwamba kuna Muumba.
Ungejibuje? “Vitu vya Asili Vinatufundisha
Nini?” (Amkeni!, Septemba 2006)
˙ Biblia inafundisha nini kuhusu
chanzo cha ulimwengu?
˙ Je, Mungu aliumba uhai wa hali
ya chini kisha akauacha ujigeuze
na kutokeza aina mbalimbali ya
viumbe, au je, aliumba viumbe ( 2:36 Ona jinsi baba anavyomfa-
vyote? fanulia mwanaye simulizi la
Biblia kuhusu uumbaji.
˙ Kwa nini wanadamu ni viumbe
wa kipekee? ‘Yehova Aliumba Vitu Vyote’

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza ikiwa fundisho la


mageuzi linapatana na Biblia.
“Je, Mungu Alitumia Mageuzi
Kuumba Aina Mbalimbali za
Lengo Uhai?” (Makala iliyo kwenye
mtandao)
N Soma makala au utazame video
kwenye mfululizo “Je, Ni Kazi ya
Ubuni?” kwenye jw.org/sw.

N Lengo lingine: Chunguza kama utafiti wa


kisayansi wa vitu vya kale una-
thibitisha kwamba uhai uliu-
mbwa au ulijitokeza wenyewe.
Maswali Matano Muhimu
Kuhusu Chanzo cha Uhai
(broshua)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 6, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
07

Yehova Ana Sifa Gani?


Unapata picha gani unapofikiria kumhusu Ye- na wale waliovunjika moyo; huwaokoa wa-
hova Mungu? Je, unamwogopa na kuhisi kwa- liopondeka roho.” (Zaburi 34:18) Je, una-
mba huwezi kuwa rafiki yake kwa sababu yuko jua kwamba tunaweza kumfurahisha au ku-
mbali sana kama vile nyota zilivyo mbali? Au mhuzunisha Yehova? Mtu anayeamua kufanya
je, unafikiri ni nguvu fulani isiyo na uhai kama mambo mabaya humuumiza na kumhuzuni-
vile mungurumo wa radi? Yehova ana sifa sha. (Zaburi 78:40, 41) Lakini mtu anaye-
gani? Kupitia Neno lake, Biblia, Yehova amee- fanya mambo mazuri anamfurahisha.—Soma
leza baadhi ya sifa zake na kuonyesha kwa- Methali 27:11.
mba anakujali.
3. Yehova ameonyeshaje kwamba
1. Kwa nini hatuwezi kumwona Mungu? anatupenda?
“Mungu ni Roho.” (Yohana 4:24) Yehova hana Sifa kuu zaidi ya Yehova ni upendo. Na kwa
mwili kama wa mwanadamu. Yeye ni Roho na kweli, “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Ye-
anaishi mbinguni, mahali ambapo hatuwezi hova amefunua upendo wake kupitia Biblia na
kuona. vilevile kupitia vitu alivyoumba. (Soma Ma-
tendo 14:17.) Kwa mfano, fikiria jinsi alivyo-
2. Yehova ana sifa gani? tuumba. Ametupatia uwezo wa kuona rangi
Ingawa hatuwezi kumwona Yehova, Yeye yupo maridadi, kusikiliza muziki mzuri, na kufurahia
na tunapojifunza kumhusu tunampenda kwa chakula kitamu. Anataka tufurahie maisha.
sababu ya sifa zake zenye kuvutia. Biblia ina-
sema: “Yehova anapenda haki, naye hatawaa-
cha washikamanifu wake.” (Zaburi 37:28) Pia,
yeye ni “mwenye upendo mwororo sana na
mwenye rehema,” hasa kuelekea watu wa-
naoteseka. (Yakobo 5:11) “Yehova yuko karibu

29
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi ambavyo Yehova


hutimiza mambo mengi mazuri.
Kisha uone jinsi ambavyo amefunua
na kuonyesha sifa zake zenye kuvutia.

4. Roho takatifu ni nguvu


ya Mungu ya utendaji
Kama vile ambavyo sisi hutumia mikono kufanya kazi,
Yehova hutumia roho yake takatifu kutimiza mambo.
Biblia inaeleza kwamba roho takatifu si mtu, bali ni
nguvu ambayo Mungu hutumia kufanya kazi zake.
Soma Luka 11:13 na Matendo 2:17, kisha mzungumzie
maswali haya:
˙ Mungu ‘ataimimina’ roho yake takatifu juu ya wale wa-
naomwomba. Basi, unafikiri roho takatifu ni mtu au ni
nguvu ya Mungu ya utendaji? Kwa nini unajibu hivyo?

Yehova hutumia roho yake takatifu kutimiza mambo


mengi mazuri. Soma Zaburi 33:6 na 2 Petro 1:20, 21,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Yehova ametumia roho yake takatifu katika
njia gani?

5. Yehova ana sifa zenye kuvutia


Musa mtumishi mwaminifu wa Mungu alitamani kumjua Muumba
wake vizuri zaidi. Hivyo Musa alimwambia hivi Yehova: “Nifundishe njia
zako ili nikujue.” (Kutoka 33:13) Basi, Yehova alimwambia Musa baadhi
ya sifa zake. Soma Kutoka 34:4-6, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Ni sifa gani ambazo Yehova alimfunulia Musa?
˙ Ni sifa gani za Yehova ambazo zinakuvutia zaidi?
6. Yehova anawajali watu
Waebrania, waliokuwa watu wa Mungu, walikuwa watu-
mwa nchini Misri. Yehova alihisije walipokuwa wakiteseka?
Cheza REKODI YA KUSIKILIZA na mfuatane na usomaji
huo, au soma Kutoka 3:1-10. Kisha mzungumzie maswali
yanayofuata.

( REKODI YA KUSIKILIZA:
Yehova Aliwajali Walipokuwa
Wakiteseka (2:45)

˙ Simulizi hili linakufundisha nini kuhusu jinsi


Yehova anavyohisi wanadamu wanapoteseka?
—Ona mstari wa 7 na 8.
˙ Je, unafikiri Yehova anataka kuwasaidia wanadamu na je,
ana uwezo wa kufanya hivyo? Kwa nini unafikiri hivyo?

7. Uumbaji unafunua sifa za Yehova


Yehova amefunua sifa zake kupitia vitu alivyoumba.
Onyesha VIDEO. Kisha soma Waroma 1:20, na
mzungumzie swali linalofuata:

( VIDEO: Uumbaji Unafunua


Upendo wa Yehova—Mwili
wa Mwanadamu (1:57)

˙ Unapochunguza uumbaji unaona sifa


gani za Yehova?

WATU FULANI HUSEMA: “Mungu ni nguvu inayopatikana kila mahali, hatuwezi kumjua vizuri.”
˙ Wewe una maoni gani?
˙ Kwa nini unafikiri hivyo?

31
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova ni Roho, hivyo hatuwezi
kumwona. Ana sifa nyingi zenye Jifunze mengi kuhusu
kuvutia kutia ndani upendo. sifa nne kuu za Yehova.
“Mungu Ana Sifa Gani?”
(Mnara wa Mlinzi Na. 1 2019)
Ungejibuje?
˙ Kwa nini hatuwezi kumwona
Yehova?
˙ Roho takatifu ni nini?
˙ Yehova ana sifa gani
Chunguza uthibitisho una-
mbalimbali?
oonyesha kwamba Yehova
hapatikani kila mahali.
“Je, Mungu Yuko Kila Mahali?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Ona kwa nini Biblia inali-


nganisha roho takatifu
na mkono wa Mungu.
“Roho Takatifu Ni Nini?”
Lengo (Makala iliyo kwenye mtandao)

N Soma Zaburi sura ya 23,


kisha ujaribu kutambua
mistari hiyo inafunua nini
kuhusu sifa za Mungu.
Ilikuwa vigumu kwa mwana-
N Lengo lingine: mume fulani kipofu kuamini
kwamba Mungu anamjali.
Ona jambo lililofanya
abadili maoni yake.
“Sasa Ninahisi Kwamba Ni-
naweza Kuwasaidia Wengine”
(Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 2015)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 7, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
08

Unaweza Kuwa
Rafiki ya Yehova
Yehova anataka umjue vizuri. Kwa nini? Ana- Unaweza ‘kumtupia mahangaiko yako yote,
tarajia kwamba kadiri unavyojifunza kuhusu kwa sababu yeye anakujali.’ (1 Petro 5:7)
sifa zake, njia zake na kusudi lake, ndivyo uta- Sikuzote Yehova yuko tayari kuwasaidia, ku-
kavyotamani kuwa rafiki yake. Je, wewe una- wafariji, na kuwasikiliza rafiki zake.—Soma
weza kuwa rafiki ya Mungu? (Soma Zaburi Zaburi 94:18, 19.
25:14.) Unapaswa kufanya nini ili uwe rafiki
yake? Biblia inajibu maswali hayo na inaeleza 3. Yehova anatarajia rafiki zake wafanye nini?
kwa nini urafiki pamoja na Yehova ndio urafiki Yehova anawapenda watu wote, “lakini ana
bora zaidi kuliko urafiki mwingine wowote. urafiki wa karibu na watu wanyoofu.” (Me-
thali 3:32) Yehova anatarajia rafiki zake wafa-
1. Yehova anakualika ufanye nini? nye mambo anayoona kuwa mazuri na waepu-
‘Mkaribie Mungu, naye atakukaribia.’ (Yako- ke mambo mabaya. Baadhi ya watu hufikiri
bo 4:8) Hilo linamaanisha nini? Yehova ana- kwamba hawawezi kufuata kikamili viwango
kualika uwe rafiki yake. Huenda watu fulani vya Yehova kuhusu mema na mabaya. Hata
wakafikiri kwamba ni vigumu kuwa rafiki ya hivyo, Yehova anatuelewa vizuri. Anamkuba-
Mungu kwa sababu hawawezi kumwona. Hata li kila mtu anayempenda kikweli na anayefa-
hivyo, katika Neno lake Biblia, Yehova ameele- nya yote anayoweza ili kumfurahisha.—Zaburi
za mambo yote tunayohitaji kujua kuhusu sifa 147:11; Matendo 10:34, 35.
zake ili tusitawishe urafiki pamoja naye. Tuna-
posoma ujumbe wa Mungu katika Biblia, urafi-
ki wetu pamoja naye huzidi kukua, ingawa ha-
tujawahi kumwona.

2. Kwa nini Yehova ndiye Rafiki bora zaidi


kuliko rafiki mwingine yeyote?
Yehova anakupenda kuliko mtu mwingine ye-
yote. Anataka uwe na furaha na uzungu-
mze naye wakati wowote unapohitaji msaada.

33
CH I M BA ZAI DI

Jifunze mengi kuhusu jinsi unavyoweza kuwa


rafiki ya Yehova, na utambue kwa nini yeye ni
Rafiki bora zaidi kuliko rafiki mwingine yeyote.

5. Mambo ambayo Yehova anatarajia


kutoka kwa rafiki zake
Kwa kawaida sisi hutazamia mambo fulani kutoka kwa rafiki zetu.
˙ Ni mambo gani ambayo ungependa rafiki zako wakufanyie?
4. Abrahamu
alikuwa rafiki Soma 1 Yohana 5:3, kisha mzungumzie swali hili:
ya Yehova ˙ Yehova anatarajia nini kutoka kwa rafiki zake?

Simulizi la Biblia kumhusu Ili kumtii Yehova, tunapaswa kubadili mwenendo na tabia zetu.
Abrahamu (anayeitwa pia Soma Isaya 48:17, 18, kisha mzungumzie swali hili:
Abramu) linatusaidia kuelewa
˙ Kwa nini Yehova anataka rafiki zake wabadili mwenendo
jinsi tunavyoweza kuwa rafiki
na tabia zao?
ya Mungu. Soma kumhusu
Abrahamu katika Mwanzo
12:1-4. Kisha mzungumzie
maswali haya:
˙ Yehova alimwambia
Abrahamu afanye nini?
˙ Yehova alimwahidi nini?
˙ Abrahamu alitendaje
baada ya kupokea
maagizo ya Yehova?

Rafiki mzuri hutukumbusha kufanya mambo yanayoweza kutulinda


na kutunufaisha. Yehova hufanya vivyo hivyo pia kwa rafiki zake
7. Ili tuwe rafiki za
Yehova tunapaswa
kuwasiliana naye
Mawasiliano huimarisha urafiki.
Soma Zaburi 86:6, 11, kisha
mzungumzie maswali haya:
˙ Tunaweza kuzungumza na
Yehova kupitia njia gani?
Rafiki wa karibu watakusaidia unapohitaji ˙ Yehova huzungumza nasi
msaada. Yehova pia atakusaidia kupitia njia gani?

6. Jinsi Yehova anavyowasaidia


rafiki zake
Yehova huwasaidia rafiki zake kukabiliana na matatizo.
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

( VIDEO: Yehova Amenisaidia


Sana (3:21)

˙ Yehova amemsaidiaje mwanamke katika video


hiyo kukabiliana na mawazo na hisia zisizofaa?

Soma Isaya 41:10, 13, kisha mzungumzie maswali haya:


˙ Yehova anaahidi kuwafanyia nini rafiki zake wote?
˙ Je, unafikiri Yehova ni rafiki mzuri? Kwa nini?
Tunazungumza na Yehova kupitia
sala; naye Yehova huzungumza
nasi kupitia Biblia

WATU FULANI HUSEMA: “Haiwezekani kuwa rafiki ya Mungu.”


˙ Unaweza kutumia andiko gani kuonyesha kwamba inawezekana kuwa rafiki ya Yehova?

35
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova anataka kuwa Rafiki yako,
na atakusaidia uwe na uhusiano Urafiki pamoja na Mungu
wa karibu pamoja naye. unaweza kuboreshaje
maisha yako?
“Yehova—Mungu Tunayepa-
Ungejibuje? swa Kumjua” (Mnara wa Mlinzi,
Februari 15, 2003)
˙ Yehova huwasaidiaje rafiki zake?
˙ Kwa nini Yehova anawaagiza
rafiki zake wabadili mwenendo
na tabia zao?
Jifunze jinsi ya kusitawisha
˙ Je, unafikiri ni vigumu kuwa
urafiki pamoja na Mungu.
rafiki ya Yehova? Kwa nini?
“Ninaweza Kuwa Rafiki
ya Mungu Jinsi Gani?”
(Maswali Ambayo Vijana
Huuliza—Majibu Yafanyayo
Kazi, Buku la 2, sura ya 35)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Jifunze kwa nini mwanamke


huyu anahisi kwamba urafiki
wake na Yehova ulibadili
maisha yake.
Lengo “Sikutaka Kufa!”
(Mnara wa Mlinzi Na. 1 2017)
N Mweleze rafiki yako jambo
ambalo umejifunza kumhusu
Yehova.

N Lengo lingine: ( 1:46 Wasikilize vijana wana-


poeleza jinsi wanavyohisi
kumhusu Yehova.
Inamaanisha Nini Kuwa
Rafiki ya Mungu?

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 8, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
09

Mkaribie Mungu Kupitia Sala


Je, wakati mwingine wewe unahisi kwamba 2. Tunapaswa kusali jinsi gani?
unahitaji mwongozo maishani? Je, kuna ma- Biblia inatutia moyo ‘tumwage mioyo yetu
swali muhimu ambayo ungependa kupata ma- mbele za Mungu.’ (Zaburi 62:8) Basi tunapa-
jibu? Je, unahitaji kufarijiwa au kutiwa moyo? swa kusali kwa unyoofu na kutoka moyoni. Tu-
Je, ungependa kuhisi ukiwa karibu zaidi na Ye- naweza kusali kwa sauti au kimyakimya tukiwa
hova? Sala inaweza kukusaidia katika hali hizo tumekaa kwa njia yoyote inayoonyesha kwa-
zote. Lakini tunapaswa kusali kwa njia gani? mba tunamheshimu Yehova. Tunaweza kusali
Je, Mungu husikiliza sala zote? Unaweza kufa- wakati wowote na mahali popote.
nya nini ili uwe na uhakika kwamba atasikiliza
sala zako? Acha tuone. 3. Mungu hujibu sala zetu jinsi gani?
Yeye hujibu kwa njia mbalimbali. Yehova ame-
1. Tunapaswa kusali kwa nani,
tupatia Neno lake, Biblia, ambalo linajibu ma-
na tunaweza kusali kuhusu nini?
swali yetu. Kusoma Neno la Mungu kunaweza
Yesu alifundisha kwamba tunapaswa kusali tu “[kumfanya] asiye na uzoefu awe na heki-
kwa Baba yetu wa mbinguni. Yesu mwenye- ma.” (Zaburi 19:7; soma Yakobo 1:5.) Yeho-
we alisali kwa Yehova. Alisema: “Basi, salini va anaweza kutusaidia kupata amani ya akili
hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni . . . ’ ” (Matha- tunapokabili matatizo. Na anaweza kuwatu-
yo 6:9) Tunaposali kwa Yehova, tunaimarisha mia watumishi wake kutusaidia tunapokuwa
urafiki wetu pamoja naye. na uhitaji.
Tunaweza kusali kuhusu jambo lolote. Bila
shaka, ili Mungu ajibu sala zetu, zinapaswa
kupatana na mapenzi yake. “Tukiomba cho-
chote kulingana na mapenzi [ya Mungu],
yeye hutusikia.” (1 Yohana 5:14) Yesu alitoa
mfano wa mambo tunayoweza kutaja katika
sala zetu. (Soma Mathayo 6:9-13.) Tunawe-
za kusali kuhusu mahangaiko yetu bila kusa-
hau kumshukuru Mungu kwa mambo amba-
yo ametufanyia na pia kumwomba awasaidie
wengine.

37
CH I M BA ZAI DI

Chunguza jinsi unavyoweza kusali kutoka moyoni kwa njia


inayompendeza Mungu, na uone jinsi sala inavyoweza kukusaidia.

4. Mungu ameweka viwango tunavyopaswa (


kufuata kuhusu sala
Ni mambo gani yanayoamua ikiwa Mungu atasikiliza au hatasikiliza VIDEO: Je, Mungu Husikiliza
sala zetu? Onyesha VIDEO. Sala Zote?—Kisehemu (2:42)

Yehova anataka tusali kwake. Soma Zaburi 65:2, kisha mzungumzie


maswali haya:
˙ Je, unafikiri “Msikiaji wa sala” anataka wewe usali kwake?
Kwa nini?

Tunapaswa kujitahidi kuishi kulingana na viwango vya Mungu ili Wakati wa vita, pande zote husali
asikilize sala zetu. Soma Mika 3:4 na 1 Petro 3:12, kisha mzungu- ili kupata ushindi. Je, tunaweza
mzie swali hili: kutazamia Mungu ajibu sala hizo?
˙ Tunaweza kufanya nini ili tuwe na hakika kwamba
Yehova atasikiliza sala zetu?

5. Tunapaswa kusali kutoka moyoni


Watu fulani wamefundishwa kusali kwa kukariri maneno yaleyale.
Lakini je, hivyo ndivyo Mungu anataka tusali kwake? Soma Mathayo 6:7,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Unawezaje kuepuka kusema “mambo yaleyale tena na tena”
katika sala zako?

Kila siku, unaweza kufikiria kuhusu baraka fulani hususa katika maisha
Baba mzuri angependa yako kisha umshukuru Yehova kwa baraka hiyo. Ukifanya hivyo kila siku
mtoto wake azungumze kwa juma moja, utasali kuhusu mambo saba tofauti bila kurudia jambo
naye kutoka moyoni.
lilelile.
Vivyo hivyo, Yehova
anataka tusali kwake
kutoka moyoni
6. Sala ni zawadi kutoka ( VIDEO: Sala Hutusaidia
kwa Mungu Kukabiliana na Matatizo
(1:32)
Sala inaweza kutusaidiaje hasa tunapokabili
matatizo maishani? Onyesha VIDEO.
Je, wajua?
Biblia inatuahidi kwamba sala inaweza kutusaidia
kupata amani ya akili. Soma Wafilipi 4:6, 7, kisha Neno “amina” linamaanisha “na iwe hivyo”
au “bila shaka.” Tangu nyakati za Biblia,
mzungumzie maswali haya:
watu husema “amina” mwishoni mwa sala.
˙ Ingawa wakati fulani matatizo yetu hayaondoki —1 Mambo ya Nyakati 16:36.
tunaposali, sala inaweza kutusaidiaje?
˙ Wewe ungependa kusali kuhusu mambo gani?

7. Tenga wakati wa kusali


Wakati mwingine huenda tukawa na shughuli
nyingi sana hivi kwamba tukasahau kusali. Ni nini
kinachoonyesha kwamba Yesu aliona sala kuwa jambo
muhimu sana? Soma Mathayo 14:23 na Marko 1:35,
kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Yesu alifanya nini ili kupata muda wa kusali?
˙ Unaweza kufanya nini ili upate muda wa kusali?

WATU FULANI HUSEMA: “Sala ni njia ya kukusaidia tu ujihisi vizuri, hakuna anayesikiliza.”
˙ Wewe una maoni gani?

39
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Tunaposali kutoka moyoni tunahisi
tukiwa karibu zaidi na Mungu, tuna- Pata majibu ya maswali
pata amani ya akili, na nguvu tuna- ambayo watu wengi
zohitaji ili kumpendeza Yehova. hujiuliza kuhusu sala.
“Mambo Saba Unayohitaji
Kujua Kuhusu Sala” (Mnara wa
Ungejibuje? Mlinzi, Oktoba 1, 2010)

˙ Tunapaswa kusali kwa nani?


˙ Tunapaswa kusali jinsi gani?
˙ Tunanufaikaje tunaposali?
Jifunze kwa nini ni muhimu
kusali na jinsi unavyoweza
kuboresha sala zako.
“Kwa Nini Ninapaswa Kusali?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza uone Biblia inafundi-


sha tunapaswa kusali kwa nani.
“Je, Ni Sawa Kusali kwa
Watakatifu?” (Makala iliyo
Lengo kwenye mtandao)

N Sali kuhusu jambo linalokuha-


ngaisha, mshukuru Yehova kwa
jambo alilokufanyia, na usali
kuhusu jambo linaloweza
kumnufaisha mtu mwingine. ( 1:22 Katika video hii ya muziki, ona
ikiwa tunaweza kusali mahali
popote au wakati wowote.
N Lengo lingine:
Sali Wakati Wowote

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 9, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
10

Mikutano ya Mashahidi wa Yehova


Inaweza Kukunufaishaje?
Je, umewahi kualikwa uhudhurie mkutano wa hova na sifa zake zenye kupendeza. Una-
Mashahidi wa Yehova? Ikiwa hujawahi kuhu- pojifunza mengi kuhusu jinsi anavyokupenda,
dhuria, huenda ukawa na wasiwasi unapoali- ndivyo utakavyozidi kuwa na uhusiano wa ka-
kwa uhudhurie kwa mara ya kwanza. Huenda ribu naye. Vilevile utajifunza jinsi anavyoweza
ukajiuliza: ‘Ni nini hufanyika katika mikutano kukusaidia uwe na maisha yenye kuridhisha.
hiyo? Kwa nini mikutano hiyo ni muhimu? Kwa —Isaya 48:17, 18.
nini ninapaswa kuhudhuria?’ Katika somo hili
utajifunza jinsi mikutano hiyo inavyoweza ku- 3. Utanufaikaje kwa kushirikiana na wengine
kunufaisha na kukusaidia uwe na uhusiano wa katika mikutano?
karibu zaidi na Mungu. Yehova anatuagiza “tufikiriane ili kucho-
cheana katika upendo na matendo mazuri,
1. Kwa nini ni muhimu sana kukutana pamoja? bila kuacha kukutana pamoja.” (Waebrania
Mwandikaji fulani wa Biblia alitaja sababu mu- 10:24, 25) Katika mikutano yetu, utakuta-
himu zaidi ya kukutana pamoja, alisema: “Ka- na na watu wanaopendana sana na ambao,
tika kutaniko kubwa, nitamsifu Yehova.” (Za- kama wewe, wanataka kujifunza mengi ku-
buri 26:12) Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova mhusu Mungu. Utawasikia wakizungumza ku-
hufurahia sana kukutana pamoja. Ulimwengu- husu mambo yenye kutia moyo kutoka kwenye
ni pote, wao hukutana kila juma ili kumsifu Biblia. (Soma Waroma 1:11, 12.) Vilevile uta-
Mungu, kuimba, na kusali. Kila mwaka, wao wafahamu wengine ambao wamefaulu kuka-
pia hukutana mara chache katika vikundi viku- biliana na matatizo yanayowapata watu wa-
bwa zaidi ili kumwabudu Mungu. liofunga ndoa au ambao hawajafunga ndoa.
Hizo ni baadhi ya sababu chache zinazofanya
2. Utajifunza nini katika mikutano yetu? tutii agizo la Yehova la kukutana pamoja kwa
Katika mikutano, sisi hujifunza Neno la Mu- ukawaida!
ngu, “[tunalifafanua] waziwazi na kueleza
maana yake.” (Soma Nehemia 8:8.) Ukihu-
dhuria mikutano, utajifunza kumhusu Ye-

41
CH I M BA ZAI DI
Wakati wa mkutano
Jifunze mambo yanayotendeka
katika mikutano ya Mashahidi wa
Yehova na kwa nini ni muhimu tuji-
tahidi kuhudhuria mikutano hiyo. B

A
(A) Mikutano yetu inatia ndani hotuba,
maigizo, na video. Mikutano huanza
na kumalizika kwa wimbo na sala

(B) Katika baadhi ya sehemu za mkutano


wasikilizaji hukaribishwa kutoa maelezo

4. Mikutano ya Mashahidi wa Yehova (

Katika karne ya kwanza, Wakristo walikutana kwa ukawaida ili


kumwabudu Yehova. (Waroma 16:3-5) Soma Wakolosai 3:16, VIDEO: Ni Nini Hutendeka
kisha mzungumzie swali hili: Katika Jumba la Ufalme?
(2:12)
˙ Wakristo wa karne ya kwanza walimwabudu Yehova jinsi gani?

Leo, Mashahidi wa Yehova hukutana kwa ukawaida katika maeneo


yao ya ibada. Ili kuona mambo yanayotendeka katika mikutano, Je, wajua?
onyesha VIDEO. Kisha, mtazame picha ya mikutano ya kutaniko Kwenye jw.org, unaweza
iliyo kwenye ukurasa huu na mzungumzie maswali haya: kupata mahali na wakati
ambao mikutano hufanywa
˙ Uliona mambo gani katika Jumba la Ufalme ambayo yametajwa ulimwenguni pote.
kwenye Wakolosai 3:16?
˙ Ni jambo gani lingine lililokupendeza kwenye video au picha
kuhusu mikutano?

Soma 2 Wakorintho 9:7, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Kwa nini hakuna malipo ya kiingilio kwenye mikutano ya
Mashahidi wa Yehova?

Chunguza pamoja na mwalimu wako mambo ambayo yatazungumziwa kwenye mkutano juma hili.
˙ Unafikiri utafurahia au kunufaika zaidi na sehemu gani ya
mkutano?
Kabla na baada ya mkutano

(C) Watu wote wanakaribi-


shwa—watu wenye familia,
C watu ambao hawajafunga
ndoa, waliozeeka, na
watoto

D (D) Hakuna malipo ya kiingilio


wala sadaka zinazokusa-
nywa kwenye mikutano
ya Mashahidi wa Yehova

5. Jitihada inahitajika ili


kuhudhuria mikutano Nazareti
Fikiria hali ilivyokuwa katika familia ya Yesu. Kila mwaka, walitembea
kwa siku kadhaa umbali wa kilomita 100 hivi kwenye eneo lenye
milima kutoka Nazareti hadi Yerusalemu ili kwenda hekaluni.
Soma Luka 2:39-42, kisha mzungumzie maswali haya:
Yerusalemu
˙ Je, unafikiri safari hiyo ya kwenda Yerusalemu ilihitaji jitihada
zozote?
˙ Kwa nini huenda ukahitaji kujitahidi ili uhudhurie mikutano?
˙ Je, unafikiri jitihada hizo ni muhimu? Kwa nini?

Biblia inasema kwamba ni muhimu sana kukutana pamoja ili


kuabudu. Soma Waebrania 10:24, 25, kisha mzungumzie
swali hili:
˙ Kwa nini tunapaswa kuhudhuria mikutano kwa ukawaida?

WATU FULANI HUSEMA: “Si lazima ukusanyike pamoja na watu wengine.


Inatosha kusoma Biblia ukiwa nyumbani.”
˙ Ni andiko au mfano gani ulio katika Biblia unaoonyesha jambo ambalo Yehova anataka tufanye?

43
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Kuhudhuria mikutano kutakusaidia
ujifunze mengi kumhusu Yehova, ( 4:17 Vipi ikiwa una wasiwasi
uimarishe urafiki wako pamoja kuhusu kuhudhuria mkutano?
naye, na umwabudu ukiwa Ona jambo lililomsaidia mwa-
pamoja na watu wengine. namume aliyehisi hivyo
apende mikutano.
Hatutasahau Tulivyo-
Ungejibuje? karibishwa

˙ Kwa nini Yehova anatutia moyo


tukutane pamoja?
˙ Utajifunza mambo gani kwenye ( 4:33 Ona jinsi kijana fulani alivyofu-
mikutano ya Mashahidi wa rahia mikutano na jambo alilo-
Yehova? fanya ili kuendelea kuhudhuria.
Nilifurahia Sana Mikutano!
˙ Unafikiri utanufaika kwa njia gani
nyingine ukihudhuria mikutano?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Jifunze jinsi wengine


wanavyohisi kuhusu
kuhudhuria mikutano.
“Kwa Nini Uhudhurie Mikutano
Lengo Kwenye Jumba la Ufalme?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
N Kuhudhuria mkutano na
kufahamiana na baadhi ya
watu utakaokutana nao huko.

N Lengo lingine: Ona jinsi maisha ya


mwanamume aliyeshirikia-
na na wahalifu yalivyobadilika
alipohudhuria mkutano wa
Mashahidi wa Yehova.
“Nilitembea na Bunduki
Kila Wakati” (Mnara wa Mlinzi,
Julai 1, 2014)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 10, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
11

Jinsi Unavyoweza Kunufaika


Zaidi Unaposoma Biblia
Je, umewahi kuhisi kwamba ni vigumu kuanza kama vile: ‘Habari hii inanifundisha nini ku-
kazi fulani kubwa? Kabla ya kuanza kazi hiyo, mhusu Yehova Mungu? Nitaitumiaje katika
huenda uliigawa katika visehemu vidogo ili iwe maisha yangu? Ninawezaje kutumia mistari hii
rahisi kuikamilisha. Ndivyo ilivyo pia kuhusu kuwasaidia wengine?’
kusoma Biblia. Huenda unajiuliza, ‘Nitaanzia
wapi?’ Katika somo hili, tutachunguza mambo 3. Unawezaje kutenga wakati wa kusoma
rahisi unayoweza kufanya ili ufurahie kusoma Biblia?
na kujifunza Biblia. Je, ni vigumu kwako kupata muda wa kuso-
ma Biblia? Wengi wetu huhisi hivyo. Jitahidi
1. Kwa nini tunapaswa kusoma Biblia kwa kutumia ‘vizuri kabisa wakati wako.’ (Wae-
ukawaida? feso 5:16) Unaweza kufanya hivyo kwa kute-
Mtu anayesoma Biblia au “sheria ya Yeho- nga wakati hususa wa kusoma Biblia kila siku.
va” kwa ukawaida, atakuwa na furaha na ata- Baadhi ya watu hutenga muda wa kusoma
fanikiwa. (Soma Zaburi 1:1-3.) Unaweza kua- Biblia asubuhi mapema. Wengine hupenda ku-
nza kwa kusoma Biblia kwa dakika chache soma mchana, labda wakati wa chakula cha
kila siku. Kadiri unavyozidi kulifahamu Neno la mchana. Na wengine husoma Biblia jioni kab-
Mungu, ndivyo utakavyofurahia zaidi kusoma la ya kulala. Ni wakati gani ambao utakufaa
Biblia. wewe?

2. Ni nini kitakachokusaidia unufaike


unaposoma Biblia?
Ili unufaike zaidi unaposoma Biblia, unahita-
ji kutua na kufikiria mambo unayosoma. Una-
paswa kuisoma na ‘kutafakari.’ (Yoshua 1:8,
maelezo ya chini) Unaposoma, jiulize maswali

45
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi unavyoweza kufurahia kusoma Biblia. Pia, ona jinsi


unavyoweza kujitayarisha vizuri ili unufaike zaidi unapojifunza Biblia.

Kama vile tunavyojifunza


kupenda vyakula vya
aina mbalimbali, vivyo
hivyo tunaweza kujifunza
kufurahia kusoma Biblia

4. Jifunze kufurahia kusoma Biblia Madokezo ya jinsi ya kuanza:


Huenda isiwe rahisi kuanza kusoma Biblia. Hata hivyo,  Chagua tafsiri inayotegemeka na
tunaweza ‘kukuza hamu’ ya kufanya hivyo, kama vile inayoeleweka kwa urahisi. Tumia
mtu anavyojifunza kuzoea ladha ya chakula kipya. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ikiwa
Soma 1 Petro 2:2, kisha mzungumzie swali hili: inapatikana katika lugha yenu.
 Anza kusoma sehemu zinazokuvutia
˙ Je, unafikiri ukisoma Biblia kila siku, utafurahia
zaidi. Ili kupata mapendekezo, ona
na utatamani kuendelea kuisoma?
chati “Ratiba ya Kusoma Biblia.”
 Andika orodha ya sura ulizosoma.
Onyesha VIDEO ili kuona jinsi watu fulani walivyoanza
Tumia “Chati ya Rekodi Yako ya Ku-
kupenda kusoma Biblia. Kisha mzungumzie maswali soma Biblia” iliyo katika chapisho hili.
yanayofuata.
 Tumia programu ya JW Library ˙.
Unaweza kutumia programu hiyo
kusoma na kusikiliza Biblia ukiwa
( VIDEO: Vijana Wanajifunza Kupenda mahali popote, kwa kutumia simu
Neno la Mungu (5:33) au kifaa kingine cha kielektroni.
 Tumia nyongeza zilizo katika
Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Kuna
ramani, chati, na kamusi ambazo
˙ Katika video hiyo, vijana walishinda changamoto zipi? zinaweza kukusaidia ufurahie zaidi
˙ Ni nini kilichowasaidia kuendelea kukazia lengo lao kusoma Biblia.
la kusoma Biblia?
˙ Walifanya nini ili wafurahie zaidi kusoma Biblia?
5. Jitayarishe kabla ya Je, wajua?
kujifunza Biblia Mashahidi wa Yehova wametumia tafsiri
mbalimbali za Biblia. Hata hivyo, tuna-
Soma Zaburi 119:34, kisha mzungumzie swali hili:
pendelea hasa Biblia Takatifu—Tafsiri
˙ Kwa nini ni vizuri kusali kabla ya kusoma Biblia ya Ulimwengu Mpya kwa sababu ni sa-
au unapojitayarisha kujifunza Biblia? hihi, ni rahisi kuielewa, na inatumia jina
la Mungu.—Ona makala iliyo kwenye
Unaweza kunufaikaje zaidi na kila kipindi cha kujifunza? mtandao, “Je, Mashahidi wa Yehova
Wana Biblia Yao Wenyewe?”
Unapotayarisha somo fulani katika kitabu hiki, jaribu
kutumia njia ifuatayo:
(A) Soma mafungu ya kwanza ya somo hilo.
(B) Soma maandiko yaliyotajwa, na uchunguze
jinsi yanavyohusiana na habari hiyo.
(C) Weka alama kwenye maneno au mafungu ya
maneno yanayojibu kila swali; kufanya hivyo
kutakusaidia mnapozungumzia somo hilo
pamoja na mwalimu wako.

A B C

WATU FULANI HUSEMA: “Kujifunza Biblia ni kazi ngumu sana.


Mara nyingi huwa nimechoka na sina wakati wa kujifunza.”
˙ Wewe una maoni gani?

47
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Ili unufaike zaidi na Biblia, panga
ratiba ya kuisoma, sali ili uelewe Chunguza mapendekezo ya-
mambo unayosoma, na ujitayarishe nayoweza kukusaidia unufaike
kabla ya kila kipindi cha kujifunza zaidi unapoisoma Biblia.
Biblia. “Jinsi ya Kunufaika
Zaidi Unapoisoma Biblia”
(Mnara wa Mlinzi Na. 1 2017)
Ungejibuje?
˙ Ni nini kitakachokusaidia unufa-
ike zaidi unaposoma Biblia?
˙ Unaweza kutenga wakati gani wa Jifunze njia tatu za
kusoma na kujifunza Biblia? kusoma Biblia.

˙ Kwa nini ni muhimu kujitayarisha “Biblia Inaweza Kunisaidiaje?


—Sehemu ya 1: Ichunguze
kabla ya kila kipindi cha kujifu-
Biblia Yako” (Makala iliyo
nza Biblia? kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Ona jinsi unavyoweza


kufurahia kusoma Biblia.
“Biblia Inaweza Kunisaidiaje?
—Sehemu ya 2: Fanya Usomaji
Lengo wa Biblia Uwe Wenye Kufura-
hisha” (Makala iliyo kwenye
N Jitayarishe kwa ajili ya kipindi mtandao)
kinachofuata cha kujifunza
kwa kutumia mapendekezo
yaliyo kwenye somo hili.
( 2:06 Pata mapendekezo kutoka
N Lengo lingine: kwa watu waliosoma Biblia
kwa miaka mingi.
Funzo la Kibinafsi Lenye
Matokeo

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 11, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
12

Ni Nini Kitakachokusaidia
Uendelee Kujifunza Biblia?
Kujifunza Biblia ni kama safari. Hata hivyo, 3. Yehova anaweza kukusaidiaje kuendelea
kuna changamoto. Wakati mwingine, huenda kujifunza?
ukawa na shaka kama utaendelea kujifunza Kwa kuwa yeye ni Muumba mweza-yote na Ra-
Biblia. Kwa nini ni muhimu kuendelea kujitahi- fiki yako, Yehova anataka kukusaidia ujifunze
di? Ni nini kitakachokusaidia uendelee licha ya kumhusu. Atakupa “hamu na nguvu za kute-
changamoto? nda.” (Soma Wafilipi 2:13.) Basi, ikiwa nyakati
nyingine unakosa hamu ya kujifunza au kufua-
1. Kwa nini kujifunza Biblia ni jambo muhimu?
ta mambo unayojifunza, anaweza kukusaidia.
“Neno la Mungu liko hai nalo ni lenye nguvu.” Anaweza pia kukupa nguvu za kushinda cha-
(Waebrania 4:12) Biblia ni yenye thamani kwa ngamoto na upinzani. Sali kwa Yehova kwa
sababu inafunua mawazo na hisia za Mungu ukawaida ukimwomba akusaidie uendelee ku-
kukuelekea. Inakusaidia kupata ujuzi, tumaini, jifunza Biblia.—1 Wathesalonike 5:17.
na hekima ya kweli. Jambo muhimu zaidi ni
kwamba Biblia inakusaidia uwe rafiki ya Yeho-
va. Unapojifunza Biblia unaruhusu nguvu zake
zifanye maisha yako yawe bora.

2. Kwa nini ni muhimu kutambua thamani ya


kweli za Biblia?
Kweli zilizo katika Biblia ni kama hazina zenye
thamani. Ndiyo sababu Biblia inatutia moyo
‘tununue kweli na tusiiuze kamwe.’ (Metha-
li 23:23) Tunapotambua thamani ya kweli za
Biblia, tutajitahidi kuendelea kujifunza hata
tukikabili changamoto.—Soma Methali 2:4, 5.

49
CH I M BA ZAI DI

Ona jinsi unavyoweza kuendelea kujifunza Biblia licha ya kuwa na shughuli


nyingi au unapokabili upinzani kutoka kwa wengine. Kisha fikiria jinsi Yehova
anavyoweza kukusaidia uendelee kujifunza.

Ukiweka mchanga kwenye ndoo kisha ujaribu kuongeza mawe,


mawe hayatakuwa na nafasi ya kutosha
˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙˙

Ukiweka mawe kwanza kwenye ndoo utakuwa na nafasi ya kuongeza mchanga.


Vivyo hivyo, ukitanguliza “mambo muhimu zaidi” maishani, utafaulu kuyatimiza
na pia utakuwa na muda wa kufanya mambo mengine

4. Hakikisha kwamba kujifunza Kujifunza Biblia hutimiza uhitaji wetu wa kiroho,


yaani, uhitaji wetu wa kumjua na kumwabudu
Biblia ni jambo muhimu kwako Mungu. Soma Mathayo 5:3, kisha mzungumzie
swali hili:
Nyakati fulani huenda ukahisi una shughuli
nyingi sana hivi kwamba huna wakati wa kuji- ˙ Tutanufaikaje ikiwa tutaona kujifunza Biblia
funza Biblia. Ni nini kinachoweza kukusaidia? kuwa jambo muhimu maishani mwetu?
Soma Wafilipi 1:10, kisha mzungumzie maswali
haya:
˙ Unafikiri ni mambo gani yaliyo “muhimu
zaidi” maishani?
˙ Unaweza kufanya nini ili kujifunza Biblia
kuwe jambo muhimu kwako?
5. Endelea kujifunza licha ya upinzani (

Wakati mwingine, huenda watu wakajaribu kukuvunja


moyo uache kujifunza Biblia. Ona mfano wa Francesco. VIDEO: Alipata Baraka
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata. kwa Kuvumilia (5:22)
˙ Katika video hiyo, familia na marafiki wa Francesco
walitendaje alipowaambia mambo aliyokuwa akijifunza?
˙ Alinufaikaje kwa kuendelea kujifunza Biblia?

Soma 2 Timotheo 2:24, 25, kisha mzungumzie maswali haya:


˙ Marafiki na watu wa familia yako wanahisije kuhusu
mambo unayojifunza?
˙ Kulingana na mistari hii, unapaswa kufanya nini ikiwa
mtu fulani hafurahii kukuona ukijifunza Biblia? Kwa nini?

6. Mtegemee Yehova akusaidie (

Tunapoendelea kumkaribia Yehova, ndivyo tamaa yetu ya ku-


mfurahisha inavyozidi kuongezeka. Hata hivyo, inaweza kuwa VIDEO: Yehova Hutusaidia
vigumu kufanya mabadiliko maishani ili kuishi kulingana na viwa- Kufanya Mabadiliko (3:56)
ngo vyake. Usikate tamaa ikiwa utahisi hivyo. Yehova atakusaidia.
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
˙ Katika video hiyo, Jim alifanya mabadiliko gani
ili amfurahishe Yehova?
˙ Ni nini kilichokuvutia kuhusu mfano wake?

Soma Waebrania 11:6, kisha mzungumzie maswali haya:


˙ Yehova atawafanyia nini wale “wanaomtafuta kwa bidii,”
yaani, wale wanaojitahidi kumjua na kufanya mambo
yanayomfurahisha?
˙ Hilo linakufundisha nini kuhusu jinsi Yehova anavyohisi
anapoona jitihada zako za kujifunza Biblia?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Kwa nini unajifunza Biblia?”


˙ Utajibuje swali hilo?

51
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Ingawa mara nyingi si rahisi
kujifunza Biblia, kufanya hivyo Chunguza mambo manne
kunaweza kukusaidia ufurahie ambayo yamewasaidia
maisha milele. Endelea kumtege- watu wengi kutumia
mea Yehova, naye atakubariki. wakati wao vizuri.
“Jinsi ya Kutumia
Wakati Wako Vizuri”
Ungejibuje? (Amkeni!, Februari 2014)

˙ Kwa nini kweli za Biblia ni zenye


thamani kwako?
˙ Unaweza kuhakikishaje kwamba ( 5:05 Ona jinsi Yehova alivyomsaidia
unatanguliza “mambo muhimu mwanamke fulani ambaye
zaidi”? mume wake hakuelewa
kwa nini anajitahidi
˙ Kwa nini unapaswa kumwomba kumpendeza Mungu.
Yehova akusaidie uendelee kuji- Yehova Anatuimarisha
funza Biblia? Ili Tubebe Mzigo Wetu

Tarehe ambayo sehemu ( 6:30 Ona jinsi mwanamume


hii imekamilishwa fulani alivyonufaika
kwa sababu mke wake
aliendelea kujifunza Biblia.
Nilichunguza Ukweli kwa
Lengo Makini

N Endelea kujifunza Biblia


angalau mara moja kwa wiki.
Ratiba yako ikibadilika, panga
muda tofauti wa kujifunza. Wakati mwingine watu husema
Mashahidi wa Yehova wanavu-
N Lengo lingine: nja familia. Je, huo ni ukweli?
“Je, Mashahidi wa Yehova
Huvunja Familia au Huzi-
imarisha?” (Makala iliyo
kwenye mtandao)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 12, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw 52
MAMBO MAKUU YA
SEHEMU YA 1
Zungumzia maswali yafuatayo pamoja
na mwalimu wako:

1. Ni nini kinachokupendeza kuhusu ahadi 7. Soma Waebrania 10:24, 25.


za wakati ujao zilizo katika Biblia? ˙ Unaweza kunufaikaje kwa kuhudhuria
(Ona Somo la 2.) mikutano ya Mashahidi wa Yehova?
˙ Je, unafikiri jitihada za kuhudhuria
2. Kwa nini unaamini kwamba Biblia ni mikutano ni muhimu?
Neno la Mungu?
(Ona Somo la 10.)
(Ona Somo la 3 na la 5.)
8. Kwa nini ni muhimu kusoma Biblia
3. Kwa nini ni muhimu kutumia jina la Yehova?
kwa ukawaida? Umepanga ratiba
(Ona Somo la 4.)
gani ya kusoma Biblia kila siku?
(Ona Somo la 11.)
4. Biblia inasema kwamba Mungu
ndiye “chanzo cha uhai.” (Zaburi 36:9) 9. Kufikia sasa, umefurahia zaidi jambo
Je, unaamini hivyo? gani kuhusu kujifunza Biblia?
(Ona Somo la 6.)
10. Tangu ulipoanza kujifunza Biblia,
5. Soma Methali 3:32. umekabili changamoto gani? Ni nini
˙ Kwa nini Yehova ndiye anayepaswa kitakachokusaidia uendelee kujifunza?
kuwa Rafiki yetu wa karibu zaidi? (Ona Somo la 12.)
˙ Yehova anatarajia nini kutoka kwa
rafiki zake? Je, unafikiri hilo linafaa? Maswali yako:
(Ona Somo la 7 na 8.)

6. Soma Zaburi 62:8.


˙ Ni mambo gani ambayo umemwambia
Yehova katika sala? Unaweza kusali
kuhusu mambo gani mengine?
˙ Yehova anajibu sala kwa njia gani?
(Ona Somo la 9.)
MASOMO

SEHEMU YA 2 13 Jinsi Dini za Uwongo Zinavyopotosha


Ukweli Kumhusu Mungu
14 Ni Ibada Gani Inayokubalika kwa Mungu?
Wazo Kuu: Ona mambo ambayo 15 Yesu Ni Nani?
Mungu ametufanyia na ibada 16 Yesu Alifanya Nini Alipokuwa Duniani?
inayomfurahisha 17 Yesu Ana Sifa Gani?
18 Jinsi ya Kuwatambua Wakristo wa Kweli
19 Je, Mashahidi wa Yehova Ni
Wakristo wa Kweli?
20 Jinsi Ambavyo Kutaniko
Limepangwa
21 Jinsi Habari Njema Inavyohubiriwa
22 Unawezaje Kuwahubiria Wengine
Habari Njema?
23 Ubatizo—Lengo Muhimu!
24 Malaika Ni Nani na Wanafanya Kazi Gani?
25 Mungu Ana Kusudi Gani kwa Wanadamu?
26 Kwa Nini Wanadamu Wanateseka na
Kupatwa na Mambo Mabaya?
27 Kifo cha Yesu Kinawezaje Kutuokoa?
28 Onyesha Shukrani kwa Mambo Ambayo
Yehova na Yesu Wamekufanyia
29 Ni Nini Hutokea Tunapokufa?
30 Wapendwa Wako Wanaweza Kuwa
Hai Tena!
31 Ufalme wa Mungu Ni Nini?
32 Ufalme wa Mungu Umeanza Kutawala!
33 Ufalme Utatimiza Nini?
13

Jinsi Dini za Uwongo Zinavyopotosha


Ukweli Kumhusu Mungu
Mungu ni upendo. Lakini kwa nini dini zinazo- kusababisha vifo vya watu wengi sana. Baadhi
dai kwamba zinamwakilisha Mungu zimefanya ya viongozi wa dini huishi maisha ya kifahari
mambo mengi sana maovu? Ni kwa sababu dini kwa kuwalazimisha wafuasi wao watoe sadaka.
hizo ni za uwongo; zinapotosha ukweli kumhusu Matendo hayo yanathibitisha kwamba hawa-
Mungu. Zinapotoshaje ukweli kumhusu Mungu? mjui Mungu na kwamba hawapaswi kumwakili-
Mungu anahisije kuhusu hilo? Naye atachukua sha.—Soma 1 Yohana 4:8.
hatua gani?
3. Mungu anahisije kuhusu dini za uwongo?
1. Mafundisho ya dini za uwongo yanapotoshaje Ikiwa wewe unakasirishwa na mambo amba-
ukweli kumhusu Mungu? yo dini za uwongo zinafanya, unafikiri Yeho-
Dini za uwongo “[zimebadili] kweli ya Mungu va anahisije? Anawapenda watu, lakini ana-
kwa ajili ya uwongo.” (Waroma 1:25) Kwa mfa- kasirishwa na viongozi wa dini wanaopotosha
no, dini nyingi hazifundishi wafuasi wake jina ukweli kumhusu na kuwatendea vibaya wafuasi
la Mungu. Hata hivyo, Biblia inasema kwamba wao. Anaahidi kwamba dini za uwongo zitahari-
lazima watu walitumie jina la Mungu. (Waro- biwa na ‘hazitapatikana tena.’ (Ufunuo 18:21)
ma 10:13, 14) Jambo baya linapotokea, baadhi Hivi karibuni, Mungu ataziharibu dini zote za
ya viongozi wa dini husema ni mapenzi ya Mu- uwongo.—Ufunuo 18:8.
ngu. Lakini huo ni uwongo. Mungu hasababi-
shi kamwe mambo maovu. (Soma Yakobo 1:13.)
Inasikitisha kwamba uwongo wa dini umefanya
iwe vigumu kwa watu kumpenda Mungu.

2. Matendo ya dini za uwongo yanapotoshaje


ukweli kumhusu Mungu?
Dini za uwongo huwatendea watu kinyume cha
mapenzi ya Yehova. Biblia inasema kwamba
“dhambi [za dini za uwongo] zimekusanyi-
ka pamoja mpaka mbinguni.” (Ufunuo 18:5)
Kwa karne nyingi, dini za uwongo zimejihusi-
sha na siasa, zimeunga mkono vita na

55
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi Mungu anavyohisi kuhusu dini


za uwongo. Chunguza mambo ambayo dini
hizo zimefanya, na pia kwa nini hilo halipaswi
kukuzuia kujifunza kumhusu Yehova.

4. Si dini zote zinazokubalika


machoni pa Mungu
Watu wengi wanaamini kwamba dini ni kama barabara
mbalimbali zinazotuongoza kwa Mungu. Je, hilo ni kweli?
Soma Mathayo 7:13, 14, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Biblia inasema nini kuhusu barabara inayoongoza
kwenye uzima?

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

( VIDEO: Je, Mungu Anakubali Aina


Zote za Ibada?—Kisehemu (3:22)

˙ Je, kweli Biblia inafundisha kwamba dini nyingi


zinakubalika machoni pa Mungu?

5. Dini za uwongo hazionyeshi ˙ Makanisa mengi yalichukua msimamo gani


wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu?
upendo wa Mungu ˙ Una maoni gani kuhusu msimamo wa
Dini zimepotosha ukweli kumhusu Mungu katika dini hizo?
njia nyingi. Kwa mfano, jambo moja baya sana
ambalo dini zimefanya ni kuunga mkono vita. Soma Yohana 13:34, 35 na 17:16.
Ili kuona mfano mmoja, onyesha VIDEO. Kisha mzungumzie maswali haya:
Kisha mzungumzie maswali yanayofuata. ˙ Unafikiri Yehova anahisije dini
zinapojihusisha katika vita?
( VIDEO: Jinsi Makanisa ˙ Dini za uwongo zimesababisha mambo
Yalivyohusika Katika Vita mengi mabaya. Kutokana na mambo
vya Pili vya Ulimwengu (2:22) uliyojionea, dini zimeshindwa kuiga
upendo wa Mungu katika njia gani?
6. Mungu anataka kuwasaidia watu
watoke katika dini za uwongo
Soma Ufunuo 18:4, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Unahisije kujua kwamba Mungu anataka kuwasai-
dia watu watoke katika dini za uwongo?

 Ili kujua kwa nini kitabu cha Ufunuo kinafafanua dini za uwongo kuwa
mwanamke anayeitwa Babiloni Mkubwa, ona Maelezo ya Ziada 1.

7. Endelea kujifunza kumhusu


Mungu wa kweli
Je, dini za uwongo zinapaswa kuathiri maoni yako ku-
mhusu Mungu? Fikiria mtoto ambaye anakataa kufuata
mwongozo wa hekima kutoka kwa baba yake. Mtoto
huyo anaondoka nyumbani na kuishi maisha mapotovu.
Baba yake haungi mkono matendo ya mtoto huyo.
Kwa nini si sawa kumlaumu baba kwa sababu ya
uasi wa mtoto wake?
˙ Je, ni sawa kumlaumu Yehova na kuacha
kujifunza kumhusu kwa sababu ya matendo
ya dini za uwongo?
Dini za uwongo hazijaonyesha
upendo wa Mungu

WATU FULANI HUSEMA: “Sipendi mambo ya Mungu kwa


sababu dini zimesababisha matatizo mengi.”
˙ Je, wewe unahisi hivyo?
˙ Kwa nini matendo ya dini za uwongo hayapaswi kufanya
uwe na maoni mabaya kumhusu Yehova?
57
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Dini za uwongo zimepotosha ukweli
kumhusu Mungu kupitia mafundisho Chunguza njia mbili
yao ya uwongo na matendo yao ya ambazo dini nyingi
kikatili. Mungu ataziharibu dini za zinamkasirisha Mungu.
uwongo. “Je, Dini Zote Ni Sawa? Je,
Zote Zinaongoza kwa Mungu?
(Makala iliyo kwenye mtandao)
Ungejibuje?
˙ Una maoni gani kuhusu mambo
ambayo dini za uwongo zinafu-
ndisha na matendo yao? Kwa nini Yehova
˙ Yehova anahisije kuhusu dini anataka tumwabudu
za uwongo? tukiwa pamoja na wengine?
˙ Mungu atachukua hatua gani “Je, Ni Lazima Mtu
Awe Katika Dini Fulani?”
dhidi ya dini za uwongo?
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Kasisi fulani alihangaishwa


na dini yake. Lakini hilo
halikumzuia kujifunza
ukweli kumhusu Mungu.
Lengo “Kwa Nini Kasisi Alibadili
Dini?” (Amkeni!, Februari 2015)
N Katika mkutano wa kutaniko
unaofuata muulize mtu mmoja
swali hili, “Kwa nini uliamua
kuwa Shahidi wa Yehova?”
Kwa miaka mingi, dini zime-
N Lengo lingine: fundisha uwongo unaofanya
watu wafikiri kwamba Mungu
hajali na ni mkatili. Jifunze
ukweli kuhusu mambo
matatu yaliyopotoshwa.
“Uwongo Unaofanya
Watu Wasimpende
Mungu” (Mnara wa Mlinzi,
Novemba 1, 2013)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 13, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
14

Ni Ibada Gani Inayokubalika


kwa Mungu?
Kama somo lililotangulia lilivyoonyesha, si dini Ibada yetu inapaswa kuwa “takatifu na yenye
zote zinazokubalika machoni pa Mungu. Hata kukubalika” kwa Yehova. (Waroma 12:1) Hilo li-
hivyo, tunaweza kumwabudu Muumba wetu kwa namaanisha kwamba tunapaswa kuishi kulinga-
njia inayomfurahisha. Ni ‘namna gani ya iba- na na viwango vyake vya maadili. Kwa mfano,
da’ au dini inayokubalika kwake? (Yakobo 1:27, wale wanaompenda Yehova wanapenda na ku-
maelezo ya chini) Chunguza mambo ambayo fuata viwango vyake kuhusu ndoa. Pia, wanae-
Biblia inafundisha. puka mazoea yasiyofaa kama vile kuvuta sigara,
kutumia dawa za kulevya au kunywa pombe ku-
1. Ibada yetu inapaswa kutegemea msingi gani? pita kiasi.
Ibada yetu inapaswa kutegemea Biblia. Yesu ali-
mwambia Mungu hivi: “Neno lako ni kweli.” 3. Kwa nini tunapaswa kumwabudu Yehova
(Yohana 17:17) Baadhi ya dini zinapuuza ukwe- pamoja na waamini wenzetu?
li ulio katika Biblia, Neno la Mungu lililoongozwa Mikutano tunayofanya kila juma hutupatia fursa
na roho. Badala yake, wanafuata mafundisho ya ‘kumsifu Yehova katika kutaniko.’ (Zaburi
na tamaduni za wanadamu. Lakini Yehova hafu- 111:1, 2) Njia moja ambayo tunamsifu Mungu ni
rahishwi na wale ‘wanaopuuza amri ya Mungu.’ kwa kumwimbia nyimbo za sifa. (Soma Zabu-
(Soma Marko 7:9.) Hata hivyo, tunafanya moyo ri 104:33.) Yehova anataka tuhudhurie mikuta-
wake ushangilie tunaposhikamana na Biblia na no kwa sababu anatupenda na anajua kwamba
kufuata ushauri wake. itatusaidia tufurahie maisha milele. Tunapohu-
dhuria mikutano tunatiwa moyo, na tunawatia
2. Tunapaswa kumwabudu Yehova jinsi gani? moyo wengine.
Tunapaswa kumwabudu Yehova peke yake kwa
sababu yeye ndiye Muumba wetu. (Ufunuo  Habari hizo zitazungumziwa zaidi baadaye katika kitabu hiki.

4:11) Hilo linamaanisha kwamba tunapaswa


kumpenda na kumwabudu yeye peke yake,
bila kutumia sanamu, mifano, au picha.—Soma
Isaya 42:8.

59
CH I M BA ZAI DI

Chunguza kwa nini Yehova hataki tutumie sanamu katika ibada.


Jifunze njia mbalimbali tunazoweza kumsifu Mungu.

(
4. Hatupaswi kutumia
sanamu katika ibada yetu
VIDEO: Je, Mungu Anakubali Tunajuaje kwamba Mungu hataki tutumie sanamu katika ibada?
Sanamu Zitumiwe Katika Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.
Ibada? (3:26)
˙ Nyakati za Biblia, ni nini kilichowapata watu wa Mungu
walipomwabudu kwa kutumia sanamu?

Watu fulani hutumia sanamu kumwabudu Mungu ili wajihisi


wakiwa karibu naye. Je, hilo linaweza kufanya Mungu akatae
ibada yao? Soma Kutoka 20:4-6 na Zaburi 106:35, 36,
kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Umeona watu wakitumia sanamu na mifano
gani katika ibada?
˙ Yehova anahisije kuhusu kutumia sanamu?
˙ Unahisije kuhusu kutumia sanamu katika ibada?

5. Tukimwabudu Yehova peke yake (


tutakuwa huru kutoka kwenye
mafundisho ya uwongo VIDEO: Kweli Iliniweka Huru (5:16)
Ona jinsi kumwabudu Yehova kwa njia inayokubalika kunavyo-
weza kutuweka huru kutoka kwenye mafundisho ya uwongo.
Onyesha VIDEO.
Soma Zaburi 91:14, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Yehova anaahidi kutufanyia nini tunapoonyesha kwamba
tunampenda kwa kumwabudu yeye peke yake?
6. Tunamwabudu Mungu 7. Yehova anafurahi
katika mikutano ya kutaniko tunapowaambia wengine
Tunamsifu Yehova na kutiana moyo kwa kuimba
mambo tunayojifunza
na kutoa maelezo katika mikutano ya kutaniko. Kuna njia nyingi tunazoweza kutumia ili kuwaa-
Soma Zaburi 22:22, kisha mzungumzie mbia wengine kweli za Biblia. Soma Zaburi 9:1
maswali haya: na 34:1, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Je, unafurahia kusikiliza maelezo ya ˙ Ni jambo gani ulilojifunza katika Biblia
wengine mikutanoni? ambalo ungependa kuwaambia watu
˙ Je, ungependa kujitayarisha ili utoe wengine?
maelezo?

WATU FULANI HUSEMA: “Haiwezekani kumfurahisha Mungu.”


˙ Wewe una maoni gani?

61
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Tunamfurahisha Muumba wetu
kwa kumwabudu yeye peke yake, Katika simulizi “Situmikii Sana-
kwa kumsifu katika mikutano ya mu Tena,” soma uone kwa nini
kutaniko, na kuwaeleza wengine mwanamke fulani aliacha kutu-
mambo tunayojifunza. mia sanamu katika ibada.
“Biblia Inabadili Maisha”
(Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2011)
Ungejibuje?
˙ Tunawezaje kujifunza jinsi ya
kumwabudu Mungu kwa njia
inayokubalika? Jifunze kuhusu mambo
˙ Kwa nini tunapaswa kumwabudu yanayoweza kukusaidia
Yehova peke yake? utoe maelezo kwenye
mikutano ya kutaniko.
˙ Kwa nini tunapaswa kuabudu
“Msifu Yehova Katika
pamoja na watu wengine wana-
Kutaniko” (Mnara wa Mlinzi,
otaka kumfurahisha Mungu?
Januari 2019)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 3:07 Ona jinsi kijana fulani alivyonu-
faika kwa kuhudhuria mikutano
ya kutaniko ingawa haikuwa
rahisi kwake.
Lengo Yehova Alinitunza

N Toa maelezo kwenye


mkutano wa kutaniko.

N Lengo lingine:
Wengi wanaamini kwamba
msalaba ni ishara ya Ukri-
sto. Je, tunapaswa kuutu-
mia katika ibada yetu?
“Kwa Nini Mashahidi
wa Yehova Hawatumii
Msalaba Katika Ibada?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 14, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
15

Yesu Ni Nani?
Yesu ni mmoja kati ya watu maarufu zaidi kati- la uzazi la bikira aliyeitwa Maria. Na kwa njia
ka historia. Watu wengi wanajua jina lake, laki- hiyo, Yesu alizaliwa akiwa mwanadamu. (Soma
ni hawajui mengi kumhusu. Na wengine wana Luka 1:34, 35.) Yehova alimtuma Yesu duniani ili
maoni mbalimbali kumhusu Yesu. Biblia inafu- awe Masihi, au Kristo, na ili awaokoe wanada-
ndisha nini kumhusu Yesu? mu. Yesu alitimiza unabii wote wa Biblia ku-
mhusu Masihi, na hivyo ikawa rahisi kwa watu
1. Yesu ni nani? kutambua kwamba yeye “ndiye Kristo, Mwana
Yesu ni kiumbe wa roho mwenye nguvu anayei- wa Mungu aliye hai.”—Mathayo 16:16.
shi mbinguni. Yehova Mungu alimuumba kwa-
nza kabla ya vitu vingine vyote. Ndiyo saba- 3. Yesu yuko wapi sasa?
bu anaitwa “mzaliwa wa kwanza wa viumbe Baada ya Yesu kufa akiwa mwanadamu, Yehova
vyote.” (Wakolosai 1:15) Biblia inamwita Yesu alimfufua akiwa kiumbe wa roho na kisha aka-
‘Mwana mzaliwa pekee’ wa Mungu kwa sa- rudi mbinguni. Akiwa huko, “Mungu alimpandi-
babu Yesu peke yake ndiye aliyeumbwa moja sha kwenye cheo cha juu zaidi.” (Wafilipi 2:9)
kwa moja na Yehova. (Yohana 3:16) Yesu ali- Sasa, Yesu ana mamlaka kubwa sana. Cheo
fanya kazi kwa ukaribu na Yehova Baba yake, chake ni cha pili kutoka kwa Yehova.
akimsaidia kuumba vitu vingine vyote. (Soma
 Somo la 26 na 27 litazungumzia kwa nini wanadamu wanahi-
Methali 8:30.) Bado Yesu ana uhusiano wa ka-
taji kuokolewa na jinsi Yesu anavyotuokoa.
ribu na Yehova. Anatumikia kwa ushikamani-
fu akiwa msemaji wa Mungu, yaani, “Neno,”
akiwasilisha ujumbe na maagizo ya Mungu.
—Yohana 1:14.

2. Kwa nini Yesu alikuja duniani?


Miaka elfu mbili hivi iliyopita, Yehova alitumia
roho yake takatifu kuhamisha kimuujiza uhai
wa Yesu kutoka mbinguni hadi kwenye tumbo

63
CH I M BA ZAI DI

Jifunze Yesu ni nani hasa, na kwa nini


ni muhimu sana kujifunza kumhusu.

4. Yesu si Mungu Mweza Yote Soma Mathayo 3:16, 17.


˙ Yesu alipobatizwa, sauti kutoka mbinguni
Ingawa Yesu ni kiumbe wa roho mwenye nguvu ilisema nini?
mbinguni, Biblia inafundisha kwamba anajitiisha
˙ Unafikiri ilikuwa sauti ya nani?
kwa Yehova ambaye ni Mungu wake na Baba yake.
Kwa nini tunasema hivyo? Onyesha VIDEO ili uone
Soma Yohana 14:28.
kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu tofau-
ti kati ya cheo cha Yesu na Mungu mweza yote. ˙ Ni nani aliye na umri mkubwa na mwenye
mamlaka zaidi? Je, ni baba au mwana?
( VIDEO: Je, Yesu Kristo ˙ Yesu alisema Yehova ni Baba yake,
Ni Mungu? (3:22) hilo linatufundisha nini?

Soma Yohana 12:49.


Maandiko yanayofuata yanatusaidia kuelewa uhu- ˙ Je, Yesu anahisi kwamba yeye na Baba yake
siano uliopo kati ya Yehova na Yesu. Soma kila ni mtu yuleyule? Wewe una maoni gani?
andiko kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
Soma Luka 1:30-32.
˙ Malaika alifafanuaje uhusiano uliopo kati ya
Yesu na Yehova Mungu, “Aliye Juu Zaidi”?
5. Ni nini kilichothibitisha 6. Tunanufaika tunapojifunza
kwamba Yesu ndiye Masihi? kumhusu Yesu
Biblia ina unabii mwingi uliowasaidia watu Biblia inakazia umuhimu wa kujifunza kumhusu
kumtambua Masihi, yaani, yule aliyechaguliwa Yesu na jukumu lake. Soma Yohana 14:6
na Mungu ili kuwaokoa wanadamu. Onyesha na 17:3, kisha mzungumzie swali hili:
VIDEO ili uone baadhi ya unabii ambao Yesu
˙ Kwa nini ni muhimu kujifunza
alitimiza alipokuja duniani.
kumhusu Yesu?

( VIDEO: Yesu Atimiza Unabii


(3:03)

Soma unabii huu wa Biblia kisha mzungumzie


maswali yanayofuata:
Soma Mika 5:2 ili uone mahali ambapo
Masihi angezaliwa.
˙ Je, unabii huu ulitimia Yesu alipozaliwa?
—Mathayo 2:1.

Soma Zaburi 34:20 na Zekaria 12:10 uone


mambo yaliyotabiriwa kuhusu kifo cha Masihi.
˙ Je, unabii huo ulitimizwa?
—Yohana 19:33-37.
˙ Je, unafikiri Yesu alipanga ili baadhi ya
unabii huo utimie?
˙ Hilo linakuthibitishia nini kumhusu Yesu?

 Ona Maelezo ya Ziada 2 kuhusu unabii uliotabiri wakati


hususa ambao Yesu angekuja duniani.

Yesu alifungua njia ya kuwa rafiki ya Mungu.


Alifundisha kweli kumhusu Yehova, na kupitia
kwake tunaweza kupata uzima wa milele

WATU FULANI HUSEMA: “Mashahidi wa Yehova hawamwamini Yesu.”


˙ Ungemjibuje mtu anayesema hivyo?

65
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yesu ni kiumbe wa roho mwenye
nguvu. Yeye ni Mwana wa Mungu Jifunze mengi zaidi kuhusu
na ndiye Masihi. jukumu la Yesu akiwa Masihi.
“Je, Unabii wa Kimasihi
Unathibitisha Kwamba
Ungejibuje? Yesu Alikuwa Ndiye Masihi?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
˙ Kwa nini Yesu anaitwa “mzaliwa
wa kwanza wa viumbe vyote”?
˙ Yesu alifanya kazi gani kabla
ya kuja duniani?
˙ Tunajuaje kwamba Yesu ndiye Chunguza uone ikiwa
Biblia inafundisha kwamba
Masihi?
Mungu alikuwa Baba mzazi
wa Yesu jinsi ambavyo
wanadamu huzaliwa.
“Kwa Nini Yesu Anaitwa
Mwana wa Mungu?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza kwa nini Biblia haiu-


ngi mkono fundisho la Utatu.
“Je, Yesu Ni Mungu?”
(Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 2009)
Lengo
N Tazama video ‘Kwa Hakika Mu-
ngu Alimfanya Bwana na Pia
Kristo’—Sehemu ya 1 au usome
Luka sura ya 2 na ya 3 ili ujifu-
nze mengi kuhusu maisha ya Soma jinsi maisha ya mwa-
Yesu alipokuwa duniani. namke fulani yalivyobadilika
alipochunguza kile ambacho
N Lengo lingine: Biblia inasema kumhusu Yesu.
“Mwanamke Myahudi Anaele-
za Sababu Iliyomfanya Achu-
nguze Upya Imani Yake”
(Amkeni!, Mei 2013)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 15, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
16

Yesu Alifanya Nini


Alipokuwa Duniani?
Watu wengi wanapofikiri kumhusu Yesu, wana- Mungu alimpa Yesu nguvu za kutuliza dhoru-
mwona kuwa mtoto mchanga, nabii mwenye ba kubwa, kulisha maelfu ya watu, kuponya wa-
hekima, au mtu anayekaribia kufa. Lakini tu- gonjwa, na hata kufufua waliokufa. (Mathayo
naweza kujifunza mengi kumhusu kwa kuchu- 8:23-27; 14:15-21; Marko 6:56; Luka 7:11-17)
nguza maisha yake alipokuwa duniani. Katika Miujiza ya Yesu ilithibitisha wazi kwamba Mungu
somo hili, tutachunguza baadhi ya mambo mu- alikuwa amemtuma. Pia ilionyesha kwamba Ye-
himu sana ambayo Yesu alifanya na jinsi yana- hova ana nguvu za kutatua matatizo yetu yote.
vyoweza kukusaidia.
3. Tunajifunza nini kutokana na maisha ya Yesu?
1. Ni kazi gani iliyokuwa muhimu zaidi katika Yesu alimtii Yehova nyakati zote. (Soma
maisha ya Yesu? Yohana 8:29.) Licha ya upinzani, Yesu alifa-
Kazi muhimu katika maisha ya Yesu ilikuwa “[ku- nya kwa uaminifu mambo ambayo Baba yake
tangaza] habari njema ya Ufalme wa Mungu.” alitaka afanye katika kipindi chote alichoku-
(Soma Luka 4:43.) Yesu alihubiri habari njema wa duniani. Yesu alithibitisha kwamba inaweze-
kwamba Mungu atasimamisha ufalme, au seri- kana kwa wanadamu kumtumikia Mungu hata
kali ambayo itaondoa matatizo yote ya wana- wanapokabili hali ngumu. Hivyo, Yesu alituachia
damu. Yesu alitangaza kwa bidii ujumbe huo “kielelezo ili [tufuate] hatua zake kwa ukari-
wenye kutia moyo kwa miaka mitatu na nusu. bu.”—1 Petro 2:21.
—Mathayo 9:35.

2. Kwa nini Yesu alifanya miujiza?


Biblia inaeleza “matendo [mengi] yenye ngu-
vu na mambo ya ajabu na ishara ambazo Mu-
ngu alifanya kupitia [Yesu].” (Matendo 2:22)

 Somo la 31-33 litazungumzia kuhusu Ufalme wa Mungu kwa


undani.

67
CH I M BA ZAI DI

Chunguza jinsi Yesu alivyohubiri


habari njema na kufanya miujiza.

4. Yesu alihubiri habari njema 5. Yesu alifundisha


Yesu alitembea mamia ya kilomita kwenye barabara zenye
masomo muhimu
vumbi, akiwahubiria habari njema watu wengi iwezekanavyo. Mbali na kuhubiri habari njema
Soma Luka 8:1, kisha mzungumzie maswali haya: za Ufalme wa Mungu, Yesu alifundi-
˙ Je, Yesu aliwahubiria tu watu waliokusanyika ili sha mambo mengine muhimu. Fiki-
kumsikiliza? ria mifano michache katika Mahubi-
˙ Yesu alifanya jitihada gani ili kuwatafuta watu? ri yake maarufu ya Mlimani. Soma
Mathayo 6:14, 34 na 7:12, kisha
Mungu alitabiri kwamba Masihi angetangaza habari njema. mzungumzie maswali haya:
Soma Isaya 61:1, 2, kisha mzungumzie maswali haya: ˙ Yesu alitoa ushauri gani katika
˙ Yesu alitimizaje unabii huu? mistari hiyo?
˙ Je, unafikiri leo watu wanahitaji kusikia habari njema? ˙ Je, unafikiri ushauri huo una-
weza kuwasaidia watu leo?
Je, wajua?
Mambo mengi tunayojua kumhusu
Yesu yanapatikana katika vitabu vi-
nne vya Biblia vinavyoitwa vitabu
vya Injili, yaani, Mathayo, Marko,
Luka, na Yohana. Kila kitabu cha
Injili kina habari fulani kumhusu
Yesu ambazo hazimo katika vile
vitabu vingine. Habari hizo zinapo-
unganishwa zinatokeza masimulizi
yenye kupendeza kuhusu maisha
ya Yesu.

MATHAYO
alikuwa wa kwanza kuandika kita-
bu cha Injili. Alikazia mafundisho
ya Yesu, hasa mambo ambayo
6. Yesu alifanya miujiza Yesu alifundisha kuhusu Ufalme
wa Mungu.
Yehova alimpa Yesu uwezo wa kufanya miujiza mingi.
MARKO
Ili uone mfano mmoja, soma Marko 5:25-34 au onyesha aliandika kitabu kifupi zaidi
VIDEO. Kisha mzungumzie maswali yanayofuata. cha Injili. Kina habari nyingi
zenye kusisimua.
( VIDEO: Mwanamke Mgonjwa LUKA
Aponywa (5:10) anazungumzia umuhimu wa
sala na jinsi Yesu alivyowatendea
wanawake.
˙ Katika video hiyo, yule mwanamke mgonjwa alikuwa YOHANA
na uhakika gani? alifunua mengi kuhusu utu wa
˙ Ni jambo gani linalokupendeza kuhusu muujiza huo? Yesu kwa kusimulia mazungumzo
mengi kati ya Yesu na marafiki wa
karibu na pia watu wengine.
Soma Yohana 5:36, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Miujiza ya Yesu ‘ilitoa ushahidi’ kuhusu nini au
ilithibitisha nini kumhusu?

WATU FULANI HUSEMA: “Yesu alikuwa mtu mzuri tu, lakini hakuwa Masihi.”
˙ Wewe una maoni gani?

69
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yesu alihubiri kuhusu Ufalme wa
Mungu, alifanya miujiza, na kumtii Ni jambo gani ambalo Yesu
Yehova nyakati zote. alizungumzia zaidi wakati
wa huduma yake duniani?
“Ufalme wa Mungu—Una
Ungejibuje? Umuhimu Gani kwa Yesu?”
(Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 2014)
˙ Ni kazi gani iliyokuwa muhimu
zaidi katika maisha ya Yesu
alipokuwa duniani?
˙ Miujiza ya Yesu inathibitisha
nini? Chunguza mambo yanayo-
thibitisha kwamba kweli
˙ Yesu alifundisha masomo
miujiza ya Yesu ilitukia.
gani muhimu?
“Miujiza ya Yesu Unaweza
Kujifunza Nini?” (Mnara wa
Mlinzi, Julai 15, 2004)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Soma jinsi mfano wa Yesu


wa kujidhabihu ulivyomcho-
chea mwanamume fulani.
“Niliishi Maisha ya Ubinafsi”
Lengo (Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 2014)

N Tazama video ‘Kwa Hakika


Mungu Alimfanya Bwana
Pia Kristo’—Sehemu ya 2
au usome Mathayo sura ya 5
mpaka 7 ili ujifunze mengi The

TIME

29,
Beginning

PLACE

fall Jordan
3:13-17
of

Riv-
Je-

EVENT

er
1:9-11
MATTHEW

Bap-
3:21-
MARK

tism
38
LUKE

of
1:
JOHN

Jesus
Mp Ona matukio muhimu ya
kuhusu huduma ya Yesu. 4:1-13
32-34

tempts

Bethany
Jesus

be-
Judean

4:1-11

yond
Wilderness

Jordan
identified as the Lamb
The
Devil
1:12,
13
Jesus
of
huduma ya Yesu kwa mfua-
tano wa jinsi yalivyotokea.
God 1:15, 29-34 Cana
of Galilee; Capernaum Wedding at ter wine 2:1-12 30,
Cana; Jesus turns wa- into Pass-
over Jerusalem Jesus

N Lengo lingine: “Matukio Muhimu Katika


Maisha ya Yesu Duniani”
(Biblia Takatifu—Tafsiri ya Uli-
mwengu Mpya, Nyongeza A7)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 16, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
17

Yesu Ana Sifa Gani?


Tunapojifunza kuhusu mambo ambayo Yesu vigumu kufanya hivyo. Pia, Yesu alipenda ku-
alisema na kufanya alipokuwa duniani, tuna- zungumza kumhusu Baba yake na kuwasaidia
jifunza sifa ambazo zinatusaidia kumkaribia wengine wawe na urafiki wa karibu na Yehova.
yeye na Yehova Baba yake. Baadhi ya sifa hizo —Yohana 14:23.
zenye kuvutia ni zipi? Na tunawezaje kumwiga
Yesu katika maisha yetu? 3. Yesu ameonyeshaje kwamba
anawapenda watu?
1. Yesu anafanana na Baba yake kwa njia gani? Biblia inasema kwamba Yesu ‘anawapenda
Yesu akiwa mbinguni amemtazama Baba yake sana wanadamu.’ (Methali 8:31) Alionyesha
mwenye upendo na kujifunza kutoka kwake kwamba anawapenda watu kwa kuwatia moyo
kwa mabilioni ya miaka. Na hivyo anafikiri, na kuwasaidia bila ubinafsi. Alifanya miujiza
anahisi, na kutenda kama Baba yake. (Soma iliyoonyesha kwamba ana nguvu na pia ana-
Yohana 5:19.) Yesu anaonyesha sifa za Baba wahurumia watu. (Marko 1:40-42) Aliwate-
yake kikamili hivi kwamba alisema: “Yeyo- ndea watu kwa fadhili bila ubaguzi. Maneno
te ambaye ameniona mimi amemwona Baba yake yaliwafariji na kuwapatia tumaini watu
pia.” (Yohana 14:9) Unapojifunza kuhusu sifa wote wenye moyo mnyoofu waliomsikiliza.
za Yesu, utamjua Yehova vizuri zaidi. Kwa mfa- Yesu alikuwa tayari kuteseka na kufa kwa sa-
no, huruma ya Yesu kuelekea watu inaonye- babu aliwapenda wanadamu wote. Lakini ana-
sha kwamba Yehova anakujali. wapenda hasa wale wanaofuata mafundisho
yake.—Soma Yohana 15:13, 14.
2. Yesu ameonyeshaje kwamba
anampenda Yehova?
Yesu alisema: “Ili ulimwengu ujue kwamba
ninampenda Baba, ninafanya kama vile Baba
alivyoniamuru.” (Yohana 14:31) Alipokuwa
duniani, Yesu alionyesha kwamba anampe-
nda sana Baba yake kwa kumtii hata ilipokuwa

71
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kuhusu sifa za Yesu. Na uchunguze jinsi


unavyoweza kuiga upendo na ukarimu wake.

Yesu alimpenda Baba yake wa mbinguni na


alizungumza naye mara nyingi kupitia sala

4. Yesu anampenda 5. Yesu anawajali watu wenye uhitaji


Baba yake Yesu alitanguliza mahitaji ya watu wengine. Hata alipokuwa
Yesu alituwekea mfano wa amechoka alitumia wakati na nguvu zake kuwasaidia watu.
jinsi ya kuonyesha kwamba Soma Marko 6:30-44, kisha mzungumzie maswali haya:
tunampenda Mungu. Soma Luka ˙ Katika simulizi hili, Yesu alionyeshaje kwamba anawajali
6:12 na Yohana 15:10; 17:26. wengine?—Ona mstari wa 31, 34, 41, na 42.
Baada ya kusoma kila andiko, ˙ Ni nini kilichomchochea Yesu awasaidie watu?
zungumzieni swali hili: —Ona mstari wa 34.
˙ Tunawezaje kumwiga ˙ Kwa kuwa Yesu alionyesha sifa za Yehova,
Yesu na kuonyesha hilo linakufundisha nini kumhusu Yehova?
kwamba tunampenda
˙ Unaweza kumwiga Yesu kwa njia gani ili uonyeshe
Yehova?
kwamba unawajali wengine?
(

6. Yesu ni mkarimu
VIDEO: “Kuna Furaha Zaidi Katika
Yesu alikuwa mkarimu ingawa hakuwa na vitu Kutoa”—Kisehemu (4:00)
vingi vya kimwili, na alitutia moyo tuwe wakarimu.
Soma Matendo 20:35, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kulingana na maneno hayo ya Yesu, tunawezaje
Je, wajua?
kuwa na furaha?
Biblia inatufundisha tusali kwa
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata. Yehova kupitia jina la Yesu. (Soma
Yohana 16:23, 24.) Tunaposali
˙ Tunaweza kutoa katika njia zipi, hata ikiwa hatuna kwa njia hiyo, tunaonyesha kwa-
vitu vingi vya kimwili? mba tunatambua jambo ambalo
Yesu amefanya ili kutusaidia
tuwe rafiki za Yehova.

WATU FULANI HUSEMA: “Mungu hajali tunapoteseka.”


˙ Kwa kuwa Yesu alionyesha sifa za Baba yake, matendo yake
yanathibitishaje kwamba Yehova anatujali?

73
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yesu anampenda Yehova, na pia
anawapenda watu. Kwa kuwa Yesu Chunguza baadhi ya sifa za
anaonyesha sifa za Baba yake, Yesu ambazo tunaweza kuiga.
unapozidi kumjua Yesu ndivyo “Mwige Yesu kwa Kusitawisha
utakavyozidi kumjua Yehova. Sifa Zifuatazo . . .” (Yesu—Njia,
Kweli, na Uzima, ukurasa wa 317)

Ungejibuje?
˙ Kama Yesu, tunawezaje kuonye-
sha kwamba tunampenda
Yehova? Jifunze kwa nini unapaswa
˙ Kama Yesu, tunawezaje kuonye- kusali kupitia jina la Yesu.
sha kwamba tunawapenda watu? “Kwa Nini Tusali Katika Jina
˙ Ni sifa gani ya Yesu inayokuvutia la Yesu?” (Mnara wa Mlinzi,
Februari 1, 2008)
zaidi?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Je, Biblia ina habari zozote


kuhusu sura ya Yesu?
“Yesu Alikuwa na Sura
ya Aina Gani?” (Makala iliyo
Lengo kwenye mtandao)

N Chagua sifa moja ya Yesu, na


ujitahidi kuionyesha juma hili.

N Lengo lingine:
Tunajifunza nini kutokana
na jinsi Yesu alivyowatendea
wanawake?
“Heshima na Staha Chini
ya Utunzaji wa Mungu” (Mnara
wa Mlinzi, Septemba 1, 2012)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 17, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
18

Jinsi ya Kuwatambua
Wakristo wa Kweli
Mabilioni ya watu wanadai kuwa Wakristo. Laki- 3. Wakristo wa kweli wanafanya
ni viwango wanavyofuata maishani na mambo kazi gani kwa bidii?
wanayoamini yanatofautiana. Basi, tunawezaje Yesu aliwapatia wanafunzi wake kazi. ‘Aliwatu-
kuwatambua Wakristo wa kweli? ma wahubiri kuhusu Ufalme wa Mungu.’ (Luka
9:2) Wakristo wa mapema hawakuhubiri tu kati-
1. Inamaanisha nini kuwa Mkristo?
ka sehemu zao za ibada, bali pia walihubiri kati-
Wakristo ni wanafunzi au wafuasi wa Yesu Kri- ka maeneo ya hadharani na kwenye nyumba za
sto. (Soma Matendo 11:26.) Wanaonyeshaje watu. (Soma Matendo 5:42; 17:17.) Vivyo hivyo,
kwamba wao ni wanafunzi wa Yesu? Yesu ali- leo Wakristo wa kweli wanahubiri kweli za Bib-
sema: “Mkikaa katika neno langu, ninyi kwa lia mahali popote ambapo watu wanapatikana.
kweli ni wanafunzi wangu.” (Yohana 8:31) Wanawapenda jirani zao na hivyo wanafurahi
Hilo linamaanisha kwamba Wakristo wa kwe- kutumia wakati na nguvu zao kutangaza uju-
li wanapaswa kutii mafundisho ya Yesu. Kama mbe wa tumaini na faraja unaopatikana katika
mafundisho ya Yesu yalivyotegemea Maandi- Biblia.—Marko 12:31.
ko, mambo ambayo Wakristo wa kweli wanaa-
mini yanapaswa pia kutegemea Biblia.—Soma
Luka 24:27.

2. Wakristo wa kweli wanaonyeshaje upendo?


Yesu aliwaambia hivi wafuasi wake: “Mpenda-
ne kama vile nilivyowapenda.” (Yohana 15:12)
Yesu alionyeshaje kwamba anawapenda wana-
funzi wake? Alitumia muda pamoja nao, aliwatia
moyo na kuwasaidia. Hata alitoa uhai wake kwa
ajili yao. (1 Yohana 3:16) Vivyo hivyo, Wakri-
sto wa kweli hawazungumzi tu kuhusu upendo.
Wanaonyesha kupitia maneno na matendo yao
kwamba wanapendana.

75
CH I M BA ZAI DI

Chunguza jinsi Wakristo wa


kweli walivyo tofauti na watu
ambao hawafuati mfano na
mafundisho ya Yesu.

4. Wanatafuta kweli za Biblia


Baadhi ya watu wanaodai kuwa Wakristo hawaji-
tahidi kutafuta kweli muhimu za Biblia. Onyesha Wakristo wa mapema
VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata. walithamini Neno la Mungu,
waliwahubiria wengine,
na walipendana
( VIDEO: Jinsi Ukristo
Ulivyopotoshwa (5:11)

5. Wanahubiri kweli za Biblia


˙ Baadhi ya makanisa yanayodai kuwa ya
Kabla Yesu hajarudi mbinguni, aliwapatia wa-
Kikristo yamefanyaje iwe vigumu kwa watu
nafunzi wake kazi ambayo inaendelea kufa-
kujifunza mambo ambayo Yesu alifundisha?
nywa mpaka leo. Soma Mathayo 28:19, 20
na Matendo 1:8, kisha mzungumzie swali hili:
Yesu alifundisha kweli za Neno la Mungu.
Soma Yohana 18:37, kisha mzungumzie swali hili: ˙ Kazi ya kuhubiri ingefanywa kufikia
wakati gani, na mpaka wapi?
˙ Kulingana na maneno ya Yesu, tunawezaje ku-
watambua Wakristo “walio upande wa kweli”?
7. Wanapendana
Je, kuna Wakristo ambao wame-
hatarisha uhai wao kwa ajili ya
Wakristo wenzao? Onyesha
VIDEO, kisha mzungumzie
maswali yanayofuata.

VIDEO: Alijitolea Kuuawa


(2:55)

˙ Katika video hiyo, kwa nini


Llyod alihatarisha uhai wake
6. Wanatenda kulingana na ili kumlinda Ndugu Johanson?
mambo wanayohubiri ˙ Je, unafikiri alitenda kama
Mkristo wa kweli?
Ni nini kilichomsadikishia Tom kwamba amewapata
Wakristo wa kweli? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie Soma Yohana 13:34, 35, kisha
maswali yanayofuata. mzungumzie maswali haya:
˙ Wanafunzi wa Yesu, yaani,
( VIDEO: Niliacha Kujihusisha
na Dini (5:20)
Wakristo wa kweli, wanawate-
ndeaje watu wa jamii au taifa
lingine?
˙ Wanafanyaje hivyo wakati
˙ Katika video hiyo, ni nini kilichofanya Tom aache
wa vita?
kujihusisha na dini?
˙ Kwa nini anaamini kwamba amepata kweli?

Matendo yana nguvu kuliko maneno. Soma Mathayo 7:21,


kisha mzungumzie swali hili:
˙ Ni jambo gani lililo muhimu zaidi kwa Yesu—je, ni mambo
tunayodai kuwa tunaamini au ni mambo tunayotenda?

WATU FULANI HUSEMA: “Wakristo wamefanya mambo mengi mabaya.


Je, inawezekana kwamba kuna dini ya kweli miongoni mwao?”
˙ Unaweza kumsomea mtu andiko gani linaloonyesha jinsi ya kuwatambua Wakristo wa kweli?

77
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Wakristo wa kweli wanafuata mafu-
ndisho ya Biblia, wanaonyesha upe- ( 1:13 Jifunze mengi kuhusu kikundi
ndo usio na ubinafsi, na kuhubiri cha watu wanaojitahidi kufuata
kweli za Neno la Mungu. mfano na mafundisho ya
Yesu Kristo.
Mashahidi wa Yehova Ni Nani?
Ungejibuje?
˙ Mambo ambayo Wakristo wa
kweli wanaamini yanategemea
nini?
˙ Ni sifa gani inayowatambulisha Ona jinsi mwanamke aliyekuwa
Wakristo wa kweli? mtawa Mkatoliki alivyopata
“familia ya kweli ya kiroho.”
˙ Wakristo wa kweli wanafanya
kazi gani? “Walitumia Biblia Kujibu
Maswali Yangu Yote!”
(Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 2014)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 3:57 Jifunze jinsi Wakristo wa


kweli wanavyowaonyesha
upendo waabudu wenzao
wanaohitaji msaada.
Lengo Kuwasaidia Ndugu Zetu Msiba
Unapotokea—Kisehemu
N Kama inawezekana, tembelea
ofisi ya tawi ya Mashahidi wa
Yehova iliyo karibu nawe.

N Lengo lingine: Chunguza jinsi Wakristo wa


mapema na Wakristo wa kweli
leo wanavyofanya mambo
ambayo Yesu alisema yange-
watambulisha wafuasi wake.
“Ni Sifa Gani Zinazowata-
mbulisha Wakristo wa Kweli?”
(Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 2012)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 18, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
19

Je, Mashahidi wa Yehova


Ni Wakristo wa Kweli?
Sisi Mashahidi wa Yehova tunaamini kwamba hivi watu wake: “Ninyi ni mashahidi wangu.”
sisi ni Wakristo wa kweli. Kwa nini? Chunguza (Soma Isaya 43:10.) Yesu anaitwa “Shahidi
msingi wa mambo tunayoamini, jina letu la ki- Mwaminifu.” (Ufunuo 1:5) Hivyo, kuanzia mwa-
pekee, na upendo tulio nao miongoni mwetu. ka wa 1931, tuliamua kuitwa Mashahidi wa Yeho-
va. Tunajivunia kuitwa kwa jina hilo.
1. Ni nini msingi wa imani ya Mashahidi
wa Yehova? 3. Mashahidi wa Yehova wanaigaje upendo
Yesu alisema “neno [la Mungu] ni kweli.” wa Yesu?
(Yohana 17:17) Kama Yesu, sikuzote Masha- Yesu aliwapenda sana wanafunzi wake hivi
hidi wa Yehova wametegemea Neno la Mungu kwamba walikuwa kama familia yake. (Soma
kuwa msingi wa imani yao. Fikiria historia ya Marko 3:35.) Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yeho-
Mashahidi wa Yehova. Mwishoni mwa karne va ni familia ya ulimwenguni pote yenye umoja.
ya 19, kikundi cha wanafunzi wa Biblia kilianza Ndiyo sababu tunaitana ndugu na dada. (File-
kuichunguza Biblia kwa makini. Mambo waliyoa- moni 1, 2) Vilevile tunatii amri hii: “Upendeni
mini yalitegemea Neno la Mungu, hata yalipoto- ushirika mzima wa akina ndugu.” (1 Petro 2:17)
fautiana na mafundisho ya makanisa mengine. Mashahidi wa Yehova wanaonyesha upendo
Kisha wakaanza kuzungumza na watu wengine katika njia nyingi, kwa mfano, tunawasaidia
kuhusu kweli hizo za Biblia. waamini wenzetu ulimwenguni pote wanapohi-
taji msaada.
2. Kwa nini tunaitwa Mashahidi wa Yehova?
Yehova anasema kwamba wale wanaomwabu-
du ni Mashahidi wake kwa sababu wanata-
ngaza ukweli kumhusu. (Waebrania 11:4–12:1)
Kwa mfano, nyakati za kale Mungu aliwaambia

 Gazeti letu kuu Mnara wa Mlinzi, limekuwa likitangaza kweli


za Biblia tangu mwaka wa 1879.

79
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kuhusu historia ya Mashahidi wa Yehova, na


uone uthibitisho wa kwamba sisi ni Wakristo wa kweli.

Imani ya Wakristo wa kweli inategemea Biblia nao


huwafundisha wengine mambo wanayojifunza

4. Biblia ndiyo msingi wa imani yetu (

Yehova alitabiri kwamba kweli za Biblia zingefunuliwa.


Soma Danieli 12:4 na maelezo ya chini, kisha mzungumzie VIDEO: Kweli za Biblia
swali hili: Zafunuliwa Upya (7:46)
˙ Watu wa Mungu wangepata nini “kwa wingi”
kwa kuendelea kuchunguza Biblia?

Chunguza jinsi kikundi cha wanafunzi wa Biblia, kutia Je wajua?


ndani Charles Russell, walivyojifunza Neno la Mungu. Nyakati nyingine, tunarekebisha
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata. baadhi ya mambo tunayoamini. Kwa
nini? Kama vile vitu vinavyoonekana
˙ Katika video hiyo, Charles Russell na wanafunzi wenzake
wazi zaidi jua linapochomoza na
wa Biblia walitumia njia gani kujifunza Biblia? kuzidi kung’aa, ndivyo Mungu ana-
vyotufunulia Neno lake hatua kwa
hatua. (Soma Methali 4:18.) Hivyo,
ingawa Biblia haibadiliki, tunareke-
bisha mambo tunayoamini kadiri
tunavyozidi kuielewa Biblia.
5. Tunaishi kulingana
na jina letu
Kwa nini tulichagua kuitwa Mashahidi wa
Yehova? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie
swali linalofuata.

( VIDEO:
Jina Linalotutambulisha (2:56)
Wakristo wa kweli huwaonyesha
upendo watu wanaohitaji msaada

˙ Kwa nini jina Mashahidi wa Yehova linafaa?


6. Tunapendana
Kwa nini Yehova amechagua wanadamu wawe
mashahidi wake? Kwa sababu uwongo mwingi Biblia inasema Wakristo wanapaswa kuungana
umeenezwa kumhusu, hivyo anataka wamta- kama viungo mbalimbali katika mwili wa mwana-
mbulishe kuwa Mungu wa kweli. Fikiria mafu- damu. Soma 1 Wakorintho 12:25, 26, kisha mzu-
ndisho mawili ya uwongo kumhusu. ngumzie maswali haya:
Baadhi ya dini huwafundisha wafuasi wao ˙ Wakristo wa kweli wanapaswa kufanya nini
kwamba Mungu anataka watumie sanamu Wakristo wenzao wanapoteseka?
katika ibada. Je, fundisho hilo ni la kweli? ˙ Umetambua jambo gani kuhusu upendo
Soma Mambo ya Walawi 26:1, kisha mzu- ulio miongoni mwa Mashahidi wa Yehova?
ngumzie maswali haya:
˙ Ukweli ni nini? Yehova ana maoni gani Mashahidi wa Yehova wanapoteseka katika
kuhusu kutumia sanamu? sehemu moja ya dunia, Mashahidi wenzao uli-
mwenguni pote huchukua hatua haraka ili kuwa-
Baadhi ya viongozi wa dini hufundisha kwamba saidia. Ili uone mfano mmoja, onyesha VIDEO.
Yesu ni Mungu. Je, fundisho hilo ni la kweli? Kisha mzungumzie swali linalofuata.
Soma Yohana 20:17, kisha mzungumzie
maswali haya: ( VIDEO: Wakaaji wa Haiti
˙ Ukweli ni nini? Je, Mungu na Yesu ni Wakabiliana na Kimbunga
Matthew (5:30)
mtu yuleyule?
˙ Unahisije unapojua kwamba Yehova
amewatuma Mashahidi wake ili wahubiri ˙ Jitihada za Mashahidi wa Yehova
ukweli kumhusu yeye na Mwana wake? za kutoa msaada zinathibitishaje
kwamba wanapendana?

WATU FULANI HUSEMA: “Mashahidi wa Yehova ni dini mpya.”


˙ Yehova alianza lini kuwaita waabudu wake mashahidi?

81
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Mashahidi wa Yehova ni Wakristo
wa kweli. Sisi ni familia ya waabudu ( 1:01:27 Jifunze mengi kuhusu
walio ulimwenguni pote. Imani yetu historia yetu.
inategemea Biblia na tunatangaza Mashahidi wa Yehova
ukweli kumhusu Yehova. —Imani Yenye Matendo,
Sehemu ya 1: Kutoka Gizani

Ungejibuje?
˙ Kwa nini tulichagua kuitwa
Mashahidi wa Yehova?
˙ Tunaonyeshaje kwamba ( 7:08 Ona mfano mmoja wa jinsi
tunapendana? Mashahidi wa Yehova walivyo-
funua mafundisho ya uwongo.
˙ Je, unafikiri Mashahidi wa
Yehova ni Wakristo wa kweli? Watu wa Mungu Hulitukuza
Jina Lake

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Pata majibu ya maswali


ambayo huenda umejiuliza
kuhusu Mashahidi wa Yehova.
“Maswali Yanayoulizwa Mara
Lengo Nyingi Kuhusu Mashahidi wa
Yehova” (habari zilizo kwenye
N Muulize Shahidi wa Yehova mtandao)
jambo lililomthibitishia
kwamba amepata kweli.

N Lengo lingine: Stephen alikuwa mhalifu


aliyeongozwa na chuki.
Ona jambo aliloona
miongoni mwa Mashahidi
wa Yehova lililomchochea
kufanya mabadiliko.
“Maisha Yangu
Yalizidi Kuwa Mabaya”
(Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2015)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 19, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
20

Jinsi Ambavyo
Kutaniko Limepangwa
Yehova ni Mungu mwenye utaratibu. (1 Wako- la yake, wanatumikia “kwa hiari mbele za Mu-
rintho 14:33) Hivyo, tunatazamia watu wake ngu; si kwa kupenda pato lisilo la haki, bali
wawe na utaratibu. Kutaniko la Kikristo lime- kwa hamu.” (1 Petro 5:1, 2) Wazee husaidiwa na
pangwa jinsi gani? Tunawezaje kuunga mkono watumishi wa huduma ambao baadaye wana-
utaratibu huo? weza kustahili kuwa wazee.
Baraza Linaloongoza huweka rasmi baadhi ya
1. Kichwa cha kutaniko ni nani?
wazee wawe waangalizi wa mzunguko. Waanga-
‘Kristo ndiye kichwa cha kutaniko.’ (Waefeso lizi hao hutembelea makutaniko mbalimbali ili
5:23) Akiwa mbinguni, anaongoza kazi ya watu kutoa mwongozo na kuwatia moyo akina ndu-
wa Yehova ulimwenguni pote. Yesu alimweka gu na dada. Wao huweka rasmi wazee na wa-
rasmi “mtumwa mwaminifu na mwenye busa- tumishi wa huduma, ambao wanapaswa kuti-
ra,” yaani, kikundi kidogo cha wazee wakoma- miza viwango vilivyoonyeshwa katika Maandiko.
vu ambao pia wanaitwa Baraza Linaloongoza. —1 Timotheo 3:1-10, 12; Tito 1:5-9.
(Soma Mathayo 24:45-47.) Kama mitume na
wazee katika karne ya kwanza huko Yerusale- 3. Kila Shahidi wa Yehova ana jukumu gani?
mu, Baraza Linaloongoza hutoa mwongozo kwa Wote katika kutaniko ‘hulisifu jina la Yeho-
makutaniko yote ulimwenguni. (Matendo 15:2) va’ kwa kushiriki katika mikutano na kazi ya
Hata hivyo, wanaume hao si viongozi wa te- kuhubiri kulingana na hali zao.—Soma Zaburi
ngenezo letu. Wanafuata mwongozo wa Yehova 148:12, 13.
na Neno lake na kujitiisha chini ya ukichwa wa
Yesu.

2. Wazee wana jukumu gani?


Wazee ni Wakristo wakomavu wanaofundisha
kwa kutumia Maandiko na kuwachunga watu wa
Yehova kwa kuwasaidia na kuwatia moyo. Ha-
walipwi mshahara kwa kazi wanayofanya. Bada-

83
CH I M BA ZAI DI

Jifunze Yesu ni kiongozi wa aina gani,


jinsi wazee wanavyojitahidi kuiga
mfano wake, na jinsi tunavyoweza
kumtii Yesu na kushirikiana
na wazee wa kutaniko. Wazee hujitahidi kuimarisha hali
yao ya kiroho na ya familia zao

4. Yesu ni kiongozi
mwenye fadhili na
mwenye kuburudisha
Yesu anatupatia mwaliko wenye kupendeza.
Soma Mathayo 11:28-30, kisha mzungu-
mzie swali hili:
˙ Yesu ni kiongozi wa aina gani na anata-
ka tuhisije kuhusu uongozi wake?

Wazee wanaigaje mfano wa Yesu?


Onyesha VIDEO. Wazee wanawajali wote
katika kutaniko
( VIDEO: Wazee Wachukua
Hatua Baada ya Tetemeko 5. Wazee hufundisha
Huko Nepal (4:56)
kwa kuweka mfano
Biblia inafundisha waziwazi jinsi wazee Yesu anataka wazee wawe na maoni gani kuhusu
wanavyopaswa kufanya kazi yao. jukumu lao? Onyesha VIDEO.

Soma Isaya 32:2 na 1 Petro 5:1-3,


( VIDEO: Wazee Ongozeni!
kisha mzungumzie maswali haya:
(7:39)
˙ Unahisije unapojua kwamba wazee
wanajitahidi kuwaburudisha wengine
kwa kumwiga Yesu?
Yesu aliwawekea mfano wale wanaoongoza
˙ Wazee wanamwiga Yesu katika njia kutanikoni. Soma Mathayo 23:8-12, kisha
gani nyingine? mzungumzie swali hili:
˙ Unapochunguza kile ambacho Biblia inasema
kuhusu jinsi wazee wanavyopaswa kutenda,
umeona tofauti gani na viongozi wa
dini nyingine?
6. Jinsi tunavyoweza
kushirikiana na wazee
Biblia inatuonyesha umuhimu wa kushirikiana na wazee.
Soma Waebrania 13:17, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Biblia inatutia moyo tutii na kujinyenyekeza chini ya
wale wanaoongoza, je, ushauri huo unafaa? Kwa nini?

Soma Luka 16:10, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Kwa nini ni muhimu kushirikiana na wazee hata
katika mambo yanayoonekana kuwa madogo?

Wazee wanahubiri kwa ukawaida

Wazee ni walimu. Pia, wanasaidia


kufanya usafi na kazi nyingine

WATU FULANI HUSEMA: “Si lazima ushirikiane na kikundi fulani cha dini.”
˙ Unafikiri kuna manufaa gani ya kumwabudu Mungu kwa kushirikiana na kutaniko?

85
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yesu ndiye kichwa cha kutaniko.
Tunafurahia kushirikiana na wazee ( 4:22 Ona uthibitisho unaoonyesha
wanaotumikia chini ya Yesu kwa saba- jinsi Baraza Linaloongoza na
bu wanatuburudisha na kutufundisha wazee katika kutaniko wana-
kupitia mfano wao mzuri. vyowahangaikia Wakristo leo.
Kuwaimarisha Akina Ndugu
Wakati wa Marufuku
Ungejibuje?
˙ Kichwa cha kutaniko ni nani?
˙ Wazee wanasaidiaje kutaniko?
˙ Kila mwabudu wa Yehova ana ( 4:51 Jifunze kuhusu kazi
ambayo waangalizi wa
jukumu gani?
mzunguko wanafanya.
Maisha ya Mwangalizi
wa Mzunguko Vijijini

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Soma kuhusu jukumu la


wanawake katika kutaniko.
“Je, Mashahidi wa
Yehova Wanawaruhusu
Lengo Wanawake Kufundisha?”
(Mnara wa Mlinzi,
N Kwenye mkutano unaofuata, Septemba 1, 2012)
muulize mzee wa kutaniko
jambo analofurahia kuhusu
kazi anayofanya kutanikoni.
Chunguza jinsi wazee
N Lengo lingine: wanavyojitahidi kuwatia
moyo waamini wenzao.
“Wazee Wakristo Ni ‘Wafa-
nyakazi Wenzi kwa Shangwe
Yetu’ ” (Mnara wa Mlinzi,
Januari 15, 2013)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 20, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
21

Jinsi Habari Njema


Inavyohubiriwa
Hivi karibuni, Yehova atatumia Ufalme wake kuwapata watu nyumbani, tunahubiri pia katika
kuondoa matatizo yetu yote. Hizo ni habari nje- maeneo mengi ya hadharani. Sikuzote tunata-
ma ambazo kila mtu anapaswa kusikia. Yesu ali- futa fursa za kuwaambia wengine kumhusu Ye-
waagiza wafuasi wake wawahubirie watu wote hova na makusudi yake.
ujumbe huo! (Mathayo 28:19, 20) Mashahidi wa
Yehova wametii jinsi gani amri hiyo ya Yesu? 3. Ni nani walio na jukumu la kuhubiri
habari njema?
1. Andiko la Mathayo 24:14 linatimizwaje leo? Wakristo wote wa kweli wanapaswa kuwahubi-
Yesu alitabiri hivi: “Hii habari njema ya Ufalme ria wengine habari njema. Tunachukua jukumu
itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa.” hilo kwa uzito. Tunahubiri kwa bidii kwa saba-
(Mathayo 24:14) Mashahidi wa Yehova wanafu- bu tunajua kwamba uhai wa watu uko hatarini.
rahia kufanya kazi hiyo muhimu. Tunahubiri ha- (Soma 1 Timotheo 4:16.) Hatulipwi mshahara
bari njema ulimwenguni pote katika lugha zaidi tunapofanya kazi hii kwa sababu Biblia inase-
ya elfu moja! Kazi hiyo kubwa inahitaji jitihada ma hivi: “Mlipokea bure, toeni bure.” (Matha-
nyingi na mipango mizuri. Kazi hiyo haiwezi ku- yo 10:7, 8) Si kila mtu ambaye atakubali ujumbe
fanikiwa bila msaada wa Yehova. wetu. Lakini tunaendelea kuhubiri kwa sababu
hiyo ni sehemu ya ibada yetu, na tunamfurahi-
2. Tunafanya jitihada gani ili kuwahubiria watu? sha Yehova.
Tunahubiri mahali popote ambapo tunaweza
kuwapata watu. Kama Wakristo wa karne ya
kwanza, tunahubiri “nyumba kwa nyumba.”
(Matendo 5:42) Kupitia njia hiyo, tunahubi-
ri kikamili na kuwafikia mamilioni ya watu kila
mwaka. Kwa kuwa wakati mwingine si rahisi

87
A
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kuhusu jitihada za Mashahidi


wa Yehova za kuhubiri ulimwenguni pote
na uone jinsi Yehova anavyotusaidia.

B C D

E F

Kuhubiri ulimwenguni pote: (A) Kosta Rika, (B) Marekani, (C) Benin, (D) Thailand, (E) Yap, (F) Sweden

4. Tunajitahidi sana ili kuwafikia watu wote (

Mashahidi wa Yehova hufanya jitihada za pekee ili kuwahubiria


watu habari njema kila mahali. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie VIDEO: Kuhubiri Katika
swali linalofuata. “Sehemu ya Mbali Zaidi
˙ Ni nini kinachokuvutia kuhusu jitihada za Mashahidi wa Yehova ya Dunia.” (7:38)
za kuhubiri?

Soma Mathayo 22:39 na Waroma 10:13-15, kisha mzungumzie


maswali haya:
˙ Kazi yetu ya kuhubiri inaonyeshaje kwamba tunawapenda jirani zetu?
˙ Yehova anahisije kuhusu wale wanaohubiri habari njema?
—Ona mstari wa 15.
5. Sisi ni wafanyakazi 6. Tunatii amri ya
wenzi wa Mungu Mungu ya kuhubiri
Mambo mengi yaliyoonwa yanathibitisha kwa- Katika karne ya kwanza, wapinzani walijaribu
mba Yehova anaongoza kazi yetu. Kwa mfano, kuwazuia wanafunzi wa Yesu ili wasihubiri.
nchini New Zealand, ndugu anayeitwa Paul ali- Wakristo wa mapema walitetea haki yao ya ku-
pokuwa akihubiri nyumba kwa nyumba, alikuta- hubiri kwa “kuithibitisha kisheria habari njema.”
na na mwanamke fulani alasiri moja. Siku hiyo- (Wafilipi 1:7) Mashahidi wa Yehova wanafanya
hiyo asubuhi, mwanamke huyo alikuwa amesali vivyo hivyo leo.
kwa Mungu akitumia jina la Mungu, Yehova,
na akamwomba amtume mtu amtembelee. Onyesha VIDEO.
Paul anasema: “Saa tatu baadaye, nilibisha
mlango wake.” ( VIDEO: Kuitetea Kisheria
Habari Njema (2:28)
Soma 1 Wakorintho 3:9, kisha mzungumzie
swali hili:
˙ Mambo yaliyoonwa, kama hilo lililotokea Soma Matendo 5:27-42, kisha mzungumzie
huko New Zealand, yanathibitishaje kwa- swali hili:
mba Yehova anaongoza kazi ya kuhubiri?
˙ Kwa nini hatutaacha kuhubiri?
Soma Matendo 1:8, kisha mzungumzie —Ona mstari wa 29, 38, na 39.
swali hili:
 Mungu ndiye ametupatia amri ya kuhubiri. Hivyo, Masha-
˙ Kwa nini tunahitaji msaada wa Yehova hidi wa Yehova hawahitaji kibali cha serikali za wanadamu ili
kuhubiri habari njema.
ili tutimize huduma yetu?

Je, wajua?
Katika kila mkutano wetu wa katikati ya
juma, tunapata mazoezi ya jinsi ya kuhubiri.
Ikiwa umewahi kuhudhuria mkutano huo, una
maoni gani kuhusu mazoezi yanayotolewa?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Kwa nini Mashahidi wa Yehova wanahubiri nyumba kwa nyumba?”
˙ Wewe ungejibuje swali hilo?

89
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yesu aliwaagiza wafuasi wake wahu-
biri habari njema katika mataifa yote. ( 5:11 Ona jinsi Mashahidi wa
Yehova anawasaidia watu wake kufa- Yehova wanavyowahubiria
nya kazi hiyo. watu katika majiji makubwa.
Mahubiri ya Pekee ya
Hadharani Jijini Paris
Ungejibuje?
˙ Kazi ya kuhubiri habari njema
inafanywaje ulimwenguni pote?
˙ Kazi yetu ya kuhubiri inaonye-
shaje kwamba tunawapenda ( 5:59 Mashahidi wa Yehova
jirani zetu? wamewasaidiaje wakimbizi?
˙ Je, unafikiri kazi ya kuhubiri Kutosheleza Kiu ya Kiroho
inaweza kutuletea furaha? Miongoni Mwa Wakimbizi
Kwa nini?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 6:29 Sikiliza maelezo ya dada


fulani aliyefurahia kutumia
maisha yake katika utumishi
wa wakati wote.
Ninafurahi Kwamba
Lengo Nilichagua Mradi Huu
N Waulize baadhi ya watu kwenye
Jumba la Ufalme changamoto
walizokabili walipoanza kuhubiri
na baraka ambazo wamepata.
Jifunze kuhusu ushindi wa
kesi mahakamani ambao
N Lengo lingine: umesaidia kuendeleza kazi
ya kuhubiri habari njema.
“Wahubiri wa Ufalme Wanape-
leka Kesi Mahakamani” (Ufalme
wa Mungu Unatawala!, sura ya 13)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 21, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
22

Unawezaje Kuwahubiria
Wengine Habari Njema?
Unapojifunza kweli za Biblia, huenda ukafikiri hivi, ‘Kila mtu
anapaswa kujua habari hizi!’ Ni kweli, kila mtu anapaswa ku-
sikia ujumbe huu! Lakini huenda ukaogopa kuwaambia we-
ngine kuhusu mambo unayojifunza. Tutazungumzia jinsi una-
vyoweza kushinda woga huo na jinsi unavyoweza kufurahia
kuanza kuwaambia wengine habari njema za Biblia. Jinsi unavyoweza kuanza
1. Unawezaje kuwaambia watu unaowafahamu  Unapozungumza na watu
mambo unayojifunza? wa familia yako, anzisha mazu-
ngumzo ya Biblia kwa kusema:
Wanafunzi wa Yesu walisema hivi: “Hatuwezi kuacha kusema “Juma hili nilijifunza jambo
kuhusu mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.” (Mate- lenye kupendeza.”
ndo 4:20) Walipenda sana mambo waliyojifunza hivi kwamba  Zungumzia andiko lenye
walitamani kuwaambia watu wengi iwezekanavyo mambo kutia moyo pamoja na rafiki
hayo. Je, wewe unahisi hivyo pia? Ikiwa ndivyo, tafuta fu- ambaye ni mgonjwa au aliye
rsa za kuwaambia kwa heshima watu wa familia na marafiki na mahangaiko.
mambo unayojifunza.—Soma Wakolosai 4:6.  Mfanyakazi mwenzako akikuuliza
unaendeleaje, mwambie jambo
2. Kwa nini ni muhimu kujiwekea lengo la kuhubiri ulilojifunza katika funzo lako la
pamoja na kutaniko? Biblia au kwenye mkutano wa
Wanafunzi wa Yesu hawakuwahubiria habari njema watu wa- kutaniko.
liowafahamu tu. Yesu aliwatuma “wawili wawili . . . katika  Waonyeshe rafiki zako tovuti
ya jw.org/sw.
kila jiji” ili wahubiri. (Luka 10:1) Utaratibu huo wa kuhubiri
uliwapatia watu wengi zaidi nafasi ya kusikia habari njema.  Waalike wengine katika funzo
lako la Biblia, au uwaonyeshe
Pia, wanafunzi walipata shangwe nyingi kwa kuhubiri pamoja.
jinsi wanavyoweza kuomba
(Luka 10:17) Je, wewe pia unaweza kujiwekea lengo la kuhu- funzo la Biblia kwenye tovuti
biri pamoja na kutaniko? ya jw.org/sw.

91
CH I M BA ZAI DI

Chunguza jinsi unavyoweza kushinda woga na kupata


shangwe inayotokana na kuhubiri habari njema.

3. Yehova atakuwa pamoja nawe


Huenda baadhi ya wanafunzi wa Biblia wanaotaka kuanza
kuhubiri, wakahangaishwa na jinsi watu watakavyowaona,
au jinsi watu watakavyoitikia ujumbe. Je, wajua?
˙ Je, wewe unaogopa kuwaambia wengine mambo Kabla ya kuanza kuhubiri habari
unayojifunza? Kwa nini? njema, Mashahidi wengi wa Yehova
walifikiri hawawezi kamwe kufanya
kazi hiyo. Kwa mfano, Sergey alihisi
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.
kwamba hafai na ilikuwa vigumu
kwake kuzungumza na watu. Lakini
( VIDEO: Nilimwomba Yehova baada ya kujifunza Biblia alisema hivi:
Anipe Ujasiri (4:05) “Ingawa nilikuwa na woga, nilianza
kuwaeleza wengine kuhusu mambo
niliyokuwa nikijifunza. Kwa kusha-
ngaza, nilipozungumza na wengine
˙ Vijana hao Mashahidi walishindaje woga wao? kuhusu Biblia nilipata ujasiri zaidi.
Pia, imani yangu iliimarika hata
Soma Isaya 41:10, kisha mzungumzie swali hili: zaidi.”
˙ Sala inaweza kukusaidiaje ikiwa unaogopa kuhubiri?
5. Kuhubiri habari njema
huleta shangwe
Yehova alimpa Yesu kazi ya kuhubiri
habari njema. Yesu aliionaje kazi hiyo?
Soma Yohana 4:34, kisha mzungumzie
maswali haya:
˙ Tunapokula chakula kizuri tunaende-
leza uhai wetu na tunapata furaha.
Kwa nini Yesu alilinganisha kula cha-
kula na kufanya mapenzi ya Mungu,
kutia ndani kuhubiri habari njema?
˙ Unafikiri utafurahia mambo gani
kwa kuhubiri habari njema?

4. Uwe mwenye heshima Mapendekezo


 Wakati wa mkutano wa katikati ya juma,
Unapowaambia wengine kuhusu habari njema,
sikiliza jinsi unavyoweza kuanzisha mazu-
fikiria jambo utakalosema na jinsi utakavyolisema.
ngumzo.
Soma 2 Timotheo 2:24 na 1 Petro 3:15, kisha mzu-
 Zungumza na mwalimu wako kuhusu
ngumzie maswali haya:
kujiandikisha ili uwe mwanafunzi kwenye
˙ Unaweza kutumiaje ushauri ulio katika mkutano wa katikati ya juma. Migawo
maandiko haya unapozungumza na utakayopewa kwenye mkutano huo ita-
wengine kuhusu Biblia? kusaidia uwe tayari kuwaambia wengine
mambo unayojifunza.
˙ Huenda baadhi ya watu wa familia yako
 Tumia sehemu za “Watu Fulani Husema”
na marafiki wasikubaliane na mambo
au “Huenda Mtu Akauliza” katika masomo
unayowaambia. Unaweza kufanya nini? haya ili kufanya mazoezi ya kujibu maswa-
Utaepuka kufanya nini? li ambayo watu huuliza au unapopingwa.
˙ Kwa nini ni vizuri kutumia maswali kwa
busara badala ya kuwalazimisha waamini
mambo unayosema?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Una habari gani mpya?”


˙ Unawezaje kutumia fursa hiyo kumwambia mambo
ambayo umejifunza kwenye funzo lako la Biblia?

93
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Kuwahubiria wengine habari njema
huleta shangwe na huenda ikawa ( 1:43 Ona njia nne rahisi unazowe-
rahisi kuanza kuhubiri kuliko za kutumia kuhubiri habari
unavyofikiri. njema ukitumia kadi ya
mawasiliano ya jw.org.
Pendekezo la Kutoa Kadi
Ungejibuje? ya Mawasiliano ya jw.org

˙ Kwa nini unapaswa kuwahubiria


wengine habari njema?
˙ Unawezaje kufanya hivyo kwa
heshima? Jifunze kuhusu sifa nne
zinazoweza kukusaidia
˙ Unawezaje kushinda woga
kuhubiri habari njema.
wowote ulio nao kuhusu
kuhubiri? “Je, Uko Tayari Kuwa Mvuvi
wa Watu?” (Mnara wa Mlinzi,
Septemba 2020)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 11:59 Ona mfano wa Biblia unaoweza


kutusaidia kuwa na ujasiri wa
kuhubiri habari njema hata
ikiwa tuna umri mdogo.
Lengo Yehova Atakusaidia Uwe Jasiri

N Mfikirie mtu unayeweza kuzu-


ngumza naye kuhusu habari
njema. Fikiria jambo utakalo-
sema, jinsi utakavyolisema,
na wakati wa kulisema. Ona jinsi unavyoweza
kuzungumzia Biblia pamo-
ja na watu wa familia yako
N Lengo lingine:
ambao bado hawajajifunza
kumhusu Yehova.
“Kuifikia Mioyo ya Watu
wa Ukoo Wasio Waamini”
(Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 2014)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 22, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
23

Ubatizo—Lengo Muhimu!
Yesu alifundisha kwamba ni lazima Wakristo wa- na mfano wa Yesu. (Mathayo 16:24) Kujiweka
batizwe. (Soma Mathayo 28:19, 20.) Lakini uba- wakfu na kubatizwa humwezesha mtu kuwa na
tizo ni nini? Na mtu anapaswa kufanya nini ili uhusiano wa karibu na Yehova na watu wengine
afikie lengo hilo? wanaomwabudu Yehova.

1. Ubatizo ni nini? 3. Mtu anapaswa kuchukua hatua gani kabla ya


Neno “batiza” linatokana na neno la Kigiriki lina- kubatizwa?
lomaanisha “zamisha” ndani ya maji. Yesu ali- Kabla ya kubatizwa, unapaswa kujifunza ku-
pobatizwa, alizamishwa ndani ya Mto Yordani mhusu Yehova na kujenga imani yenye ngu-
na kisha ‘akatoka katika maji.’ (Marko 1:9, 10) vu kwake. (Soma Waebrania 11:6.) Kadiri uju-
Vivyo hivyo, Wakristo wa kweli hubatizwa kwa zi na imani yako inavyozidi kuongezeka, ndivyo
kuzamishwa kabisa ndani ya maji. utakavyompenda Yehova zaidi. Bila shaka, uta-
tamani kuwaambia wengine kumhusu na kui-
2. Ubatizo unamaanisha nini? shi kulingana na viwango vyake. (2 Timotheo
Mtu anapobatizwa, anaonyesha kwamba ameji- 4:2; 1 Yohana 5:3) Mtu anapoanza kuishi “kwa
weka wakfu kwa Yehova Mungu. Mtu anajiweka kumstahili Yehova ili kumpendeza kikamili,”
wakfu jinsi gani? Kabla ya kubatizwa, anatoa inawezekana kwamba ataamua kujiweka wakfu
sala faraghani na kumwambia Yehova kwa- kwa Mungu na kubatizwa.—Wakolosai 1:9, 10.
mba anataka kumtumikia milele. Anaahidi kwa-
mba atamwabudu Yehova peke yake, na jambo  Ikiwa mwanzoni mtu alibatizwa katika dini nyingine, anahitaji
kubatizwa tena. Kwa nini? Kwa sababu dini hiyo haikufundisha
muhimu zaidi maishani mwake litakuwa ku- ukweli ulio katika Biblia.—Ona Matendo 19:1-5 na Somo la 13.
fanya mapenzi ya Mungu. Anaamua ‘kujikana
mwenyewe na kuendelea kufuata’ mafundisho

95
CH I M BA ZAI DI

Ona mambo tunayojifunza kutokana


na ubatizo wa Yesu na jinsi mtu ana-
vyoweza kujitayarisha ili kuchukua
hatua hiyo muhimu.

Tunajiweka wakfu kwa


kumwambia Yehova
kwamba tunataka
kumtumikia milele
Tunapobatizwa tunawaonyesha watazamaji
kwamba tumejiweka wakfu kwa Mungu

4. Mambo tunayojifunza 5. Unaweza kufikia lengo


kutokana na ubatizo wa Yesu la kubatizwa
Soma Mathayo 3:13-17 ili ujifunze mengi Mwanzoni huenda ukawa na wasiwasi kuhu-
kuhusu ubatizo wa Yesu. Kisha mzungumzie su kujiweka wakfu na kubatizwa. Hata hivyo,
maswali haya: unaweza kufanya maendeleo hatua kwa hatua
na mwishowe kupata ujasiri wa kufanya uamuzi
˙ Je, Yesu alikuwa mtoto mchanga
huo muhimu. Ili uone baadhi ya watu waliofanya
alipobatizwa?
hivyo, onyesha VIDEO.
˙ Alibatizwa jinsi gani? Je, alinyunyiziwa
maji?
( VIDEO: Kusitawisha Uhusiano
Pamoja na Yehova (1:11)
Baada ya kubatizwa, Yesu alianza kufanya kazi
ya pekee ambayo Mungu alimpa afanye duniani.
Soma Luka 3:21-23 na Yohana 6:38, kisha
mzungumzie swali hili: Soma Yohana 17:3 na Yakobo 1:5, kisha
mzungumzie swali hili:
˙ Yesu alitanguliza kazi gani maishani
baada ya kubatizwa? ˙ Ni nini kinachoweza kumsaidia mtu
ajitayarishe kwa ajili ya ubatizo?
6. Tunapobatizwa tunajiunga na familia ya Yehova
Tunapobatizwa tunajiunga na familia yenye umoja ya ulimwenguni pote.
Ingawa tumetoka katika maeneo na malezi mbalimbali, sisi sote tunaamini
mambo yaleyale na tunaishi kulingana na viwango vilevile vya maadili.
Soma Zaburi 25:14 na 1 Petro 2:17, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Mtu anapobatizwa anakuwa na uhusiano gani na Yehova na
watu wengine wanaomwabudu?

WATU FULANI HUSEMA: “Mimi siko tayari kubatizwa.”


˙ Ikiwa wewe unahisi hivyo, je, bado unafikiri kwamba ubatizo ni lengo muhimu?

97
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yesu alifundisha kwamba ni lazima
Wakristo wabatizwe. Ili kufikia lengo Jifunze ukweli
hilo, mtu anapaswa kujenga imani kuhusu ubatizo.
yenye nguvu kwa Yehova, kuishi “Ubatizo Ni Nini?”
kulingana na viwango vyake, (Makala iliyo kwenye mtandao)
na kujiweka wakfu kwake.

Ungejibuje?
˙ Ubatizo ni nini, na kwa nini ni
muhimu kubatizwa? Chunguza hatua ambazo
˙ Kuna uhusiano gani kati ya mtu anapaswa kuchukua
kujiweka wakfu na kubatizwa? ili kufikia ubatizo.
˙ Ni hatua gani ambazo mtu “Upendo na Uthamini
Wetu kwa Yehova Hutu-
anapaswa kuchukua kabla ya
chochea Kubatizwa”
kujiweka wakfu na kubatizwa?
(Mnara wa Mlinzi, Machi 2020)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Soma uone kwa nini mwana-


mume fulani hakuongozwa tu
na hisia alipoamua kubatizwa.
“Walitaka Nijithibitishie
Ukweli” (Mnara wa Mlinzi,
Lengo Februari 1, 2013)

N Chunguza orodha zilizo mwi-


shoni mwa Sehemu ya 4, “Je,
Niko Tayari Kuhubiri Pamoja na
Kutaniko?” na “Je, Niko Tayari
Kubatizwa?,” ili uone jinsi una- Chunguza kwa nini ubatizo ni
vyoweza kustahili kubatizwa. lengo muhimu na jinsi unavyo-
weza kujitayarisha ili ubatizwe.
N Lengo lingine: “Nibatizwe?” (Maswali Ambayo
Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo
Kazi, Buku la 2, sura ya 37)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 23, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
24

Malaika Ni Nani na
Wanafanya Kazi Gani?
Yehova anataka tujifunze kuhusu familia yake wamwasi Yehova na baadaye aliwashawishi ma-
iliyo mbinguni. Familia hiyo inatia ndani ma- laika wengine wajiunge naye katika uasi. Malaika
laika ambao wanaitwa “wana . . . wa Mungu.” hao waasi wanaitwa roho waovu. Yehova aliamua
(Ayubu 38:7) Biblia inasema nini kuhusu ma- wafukuzwe kutoka mbinguni waje duniani, nao
laika? Je, wanaweza kuwasaidia au kuwadhuru wataangamizwa.—Soma Ufunuo 12:9, 12.
watu? Je, malaika wote ni sehemu ya familia ya
Mungu? 3. Shetani na roho wake waovu wanatumia
mbinu gani kuwapotosha wanadamu?
1. Malaika ni nani? Shetani na roho waovu huwapotosha watu we-
Yehova aliwaumba malaika kabla ya kuumba du- ngi kupitia zoea baya la kujaribu kuwasiliana na
nia. Malaika wanaishi mbinguni na hatuwezi ku- viumbe wa roho. Kwa mfano, baadhi ya watu
waona kama vile ambavyo hatuwezi kumwo- hutafuta habari kutoka kwa wanajimu, wabashi-
na Yehova. (Waebrania 1:14) Kuna mamilioni ri, na waganga wa kienyeji. Na wengine huta-
ya malaika na kila mmoja wao ana utu wa pe- futa matibabu yanayohusisha roho waovu. Pia,
kee. (Ufunuo 5:11) Malaika ‘wanatekeleza neno watu hudanganywa waamini kwamba wanaweza
la Yehova, wakitii sauti yake.’ (Zaburi 103:20) kuzungumza na watu waliokufa. Lakini Yehova
Nyakati za kale, Yehova aliwatuma malaika wa- anatuonya hivi: “Msiende kwa watu wanaowasi-
peleke ujumbe au kuwasaidia na kuwaokoa watu liana na roho, wala msitafute ushauri kutoka
wake. Leo, malaika wanawaongoza Wakristo kwa kwa wabashiri.” (Mambo ya Walawi 19:31) Ana-
watu wanaotaka kujifunza kumhusu Mungu. tupatia onyo hilo ili kutulinda dhidi ya Shetani na
roho waovu. Wao ni maadui wa Mungu na wana-
2. Shetani na roho wake waovu ni nani? taka kutusababishia madhara.
Baadhi ya malaika hawakuendelea kuwa waa-
minifu kwa Yehova. Malaika wa kwanza aliyea-
si ni yule “anayeitwa Ibilisi na Shetani, ana-
yeipotosha dunia nzima inayokaliwa.” (Ufunuo
12:9) Shetani alitamani kuwatawala viumbe we-
ngine, basi aliwashawishi wanadamu wa kwanza

99
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kuhusu mambo mazuri ambayo malaika


wanafanya, hatari za kuwasiliana na roho waovu,
na jinsi tunavyoweza kujilinda dhidi ya Shetani
na roho waovu.

4. Malaika huwasaidia watu


wajifunze kumhusu Yehova
Malaika wa Mungu hawahubirii watu moja kwa moja. Badala
yake, wanaweza kuwaongoza watu wa Mungu wawahubirie
watu wanaotaka kujifunza kumhusu. Soma Ufunuo 14:6, 7,
kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kwa nini tunahitaji msaada wa malaika tunapohubiri?
˙ Je, unatiwa moyo kujua kwamba malaika wanaweza
kukuongoza uwahubirie watu wanaohitaji kusikia
ujumbe wa Biblia? Kwa nini?

5. Epuka kuwasiliana na roho waovu


Shetani na roho waovu ni maadui wa Yehova. Wao ni adui
zetu pia. Soma Luka 9:38-42, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Roho waovu wanawatendeaje wanadamu?

Hatungependa kujihusisha kwa vyovyote na roho waovu.


Soma Kumbukumbu la Torati 18:10-12, kisha mzungumzie
maswali haya:
˙ Roho waovu wanatumia njia gani kujaribu kutushawishi
na kuwasiliana nasi? Katika eneo unaloishi, watu hutumia
njia gani kuwasiliana na roho waovu?
˙ Yehova anatuagiza tuepuke kabisa mazoea ya kuwasiliana
na roho waovu. Je, unafikiri jambo hilo linafaa? Kwa nini?
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie
maswali yanayofuata.
˙ Je, unafikiri hirizi ambayo binti ya Palesa
alivishwa mkononi ina madhara? Kwa nini?
˙ Unafikiri Palesa alihitaji kufanya nini ili ajilinde
dhidi ya roho waovu?

Sikuzote Wakristo wa kweli wamewapinga roho waovu.


Soma Matendo 19:19 na 1 Wakorintho 10:21, kisha
mzungumzie swali hili:
(
˙ Kwa nini unapaswa kuharibu kitu chochote ulicho
nacho ambacho kinahusiana na roho waovu?
VIDEO: “Mpingeni Ibilisi” (5:02)

6. Shinda vita dhidi ya Shetani


na roho wake waovu
Shetani ndiye mtawala wa roho waovu. Lakini Unaweza kushinda vita dhidi ya Shetani
kiongozi wa malaika waaminifu anaitwa Mikaeli, na roho wake waovu. Soma Yakobo 4:7,
ambalo ni jina lingine la Yesu. Mikaeli ana nguvu kisha mzungumzie swali hili:
kadiri gani? Soma Ufunuo 12:7-9, kisha mzungu-
˙ Unawezaje kujilinda dhidi ya Shetani
mzie maswali haya:
na roho wake waovu?
˙ Ni nani mwenye nguvu zaidi? Je, ni Mikaeli
na malaika zake au ni Shetani na roho wake
waovu?
˙ Je, unafikiri wafuasi wa Yesu wanapaswa
kumwogopa Shetani na roho wake waovu?

WATU FULANI HUSEMA: “Si vibaya kucheza michezo ya video au kutazama


sinema zinazohusiana na roho waovu. Ni njia ya kujifurahisha tu.”
˙ Kwa nini ni hatari kuwa na maoni kama hayo?

101
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Malaika waaminifu hutusaidia.
Shetani na roho wake waovu ni Chunguza uthibitisho unaoo-
maadui wa Yehova, na wanatumia nyesha kwamba Yesu ndiye
mazoea ya kuwasiliana na roho Mikaeli, yule malaika mkuu.
ili kuwapotosha watu. “Yule Malaika Mkuu Mikaeli
Ni Nani?” (Makala iliyo kwenye
mtandao)
Ungejibuje?
˙ Malaika wa Yehova wanawasai-
diaje watu wajifunze kumhusu?
˙ Shetani na roho wake waovu Chunguza uthibitisho
ni nani? unaoonyesha kwamba
Ibilisi si uovu tu ulio ndani
˙ Kwa nini unapaswa kujiepusha
yetu, bali ni kiumbe halisi.
na mazoea ya kuwasiliana
“Je, Ibilisi Ni Kiumbe Halisi?”
na roho waovu?
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Ona jinsi mwanamke


aliyesumbuliwa na roho
waovu alivyowekwa huru.
“Alipata Kusudi Maishani”
Lengo (Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 1993)

N Chunguza ikiwa una vitu vina-


vyohusiana na mazoea ya ku-
wasiliana na roho, kisha usali
ili upate hekima na kuamua ja-
mbo utakalofanya na vitu hivyo. Jifunze jinsi Shetani
anavyotumia mazoea ya
N Lengo lingine: kuwasiliana na roho waovu
ili kuwadanganya watu.
“Ukweli Kuhusu Uchawi na
Ulozi” (Barabara Inayoongoza
Kwenye Uhai wa Milele,
sehemu ya 5)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 24, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
25

Mungu Ana Kusudi Gani


kwa Wanadamu?
Biblia inasema kwamba maisha ya wanadamu ni 2. Tunawezaje kuwa na maisha yenye
‘mafupi na yamejaa taabu.’ (Ayubu 14:1) Je, Mu- kusudi leo?
ngu anataka tuwe na maisha kama hayo? Ikiwa Yehova alituumba tukiwa na ‘uhitaji wa kiroho,’
sivyo, ana kusudi gani kwa wanadamu? Je, ku- yaani, tamaa ya kumjua na kumwabudu. (Soma
sudi hilo litatimizwa? Chunguza majibu yenye Mathayo 5:3-6.) Anataka tuwe na urafiki wa ka-
kufariji yanayopatikana katika Biblia. ribu pamoja naye, ‘tutembee katika njia zake
zote, tumpende,’ na kumtumikia ‘kwa moyo
1. Yehova anataka tuishi maisha ya aina gani?
wetu wote.’ (Kumbukumbu la Torati 10:12; Za-
Yehova anataka tuwe na maisha bora kabisa. buri 25:14) Tunapofanya hivyo, tunakuwa na fu-
Alipowaumba wanadamu wa kwanza Adamu na raha ya kweli hata ingawa tunakabili matatizo.
Hawa, aliwaweka katika paradiso maridadi, bu- Tunapomwabudu Yehova, maisha yetu yanaku-
stani ya Edeni. Kisha “Mungu akawabariki, na wa na kusudi la kweli kwa sababu tunaishi kuli-
Mungu akawaambia: ‘Zaeni, muwe wengi, mui- ngana na viwango vyake.
jaze dunia na kuitiisha.’ ” (Mwanzo 1:28) Yeho-
va alitaka wapate watoto, waifanye dunia nzima
kuwa paradiso na kuwatunza wanyama. Aliku-
sudia kwamba watu wote wawe na afya kamilifu
na waishi milele.
Ingawa mambo ni tofauti leo, kusudi la Mungu
halijabadilika. (Isaya 46:10, 11) Bado anataka
wanadamu watiifu waishi milele katika hali ka-
milifu.—Soma Ufunuo 21:3, 4.

 Katika somo linalofuata, utajifunza kwa nini kusudi la Mungu


halikutimia.

103
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kuhusu upendo mkubwa ambao Yehova alionyesha


alipoumba dunia kwa ajili ya wanadamu na kile ambacho
Neno lake linasema kuhusu kusudi la uhai.

3. Yehova anataka wanadamu (


wafurahie maisha yenye kusudi
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata. VIDEO: Kwa Nini
Mungu Aliiumba Dunia?
˙ Kwa nini Mungu aliiumba dunia yetu maridadi? —Kisehemu (1:41)

Soma Mhubiri 3:11, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Andiko hili linakufundisha nini kumhusu Yehova?
Nyumba iliyoharibika kwa sababu
ya kupuuzwa inaweza kurekebishwa.
Vivyo hivyo, ingawa wanadamu wamekosa
kuitunza dunia, Mungu atairekebisha kwa
ajili ya wale wanaompenda

4. Kusudi la Yehova halijabadilika


Soma Zaburi 37:11, 29 na Isaya 55:11, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Tunajuaje kwamba kusudi la Yehova kwa wanadamu halijabadilika?

5. Kumwabudu Yehova hufanya maisha (


yetu yawe na kusudi la kweli
Tunapata furaha tunapojua kusudi la uhai. VIDEO: Nilijifunza Kuhusu
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata. Kusudi la Uhai (5:03)

˙ Terumi alinufaikaje alipojifunza kusudi la uhai?

Soma Mhubiri 12:13, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Kwa kuwa Yehova ametufanyia mambo mengi sana,
tunawezaje kumwonyesha shukrani?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Maisha yana kusudi gani?”


˙ Wewe ungejibuje swali hilo?

105
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova anataka tufurahie maisha mi-
lele katika hali kamilifu hapa duniani. Chunguza mambo ya-
Tunapomwabudu kwa moyo wetu nayothibitisha kwamba
wote, maisha yetu yanakuwa na bustani ya Edeni ilikuwepo.
kusudi hata sasa. “Je, Bustani ya Edeni Ilikuwa
Halisi au Ni Hadithi Tu?”
(Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2011)
Ungejibuje?
˙ Yehova alikuwa na kusudi gani
alipowaumba Adamu na Hawa?
˙ Tunajuaje kwamba kusudi Chunguza uone kwa nini
la Mungu kwa wanadamu tunaweza kuwa na uhakika
halijabadilika? kwamba dunia itadumu milele.
˙ Unawezaje kupata kusudi “Je, Dunia Itaharibiwa?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
la kweli maishani?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Jifunze Biblia inasema nini


kuhusu jinsi unavyoweza
kupata kusudi maishani.
“Ni Nini Maana ya Uhai?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
Lengo
N Mwambie mtu mwingine
kuhusu kusudi zuri la
Yehova kwa wanadamu.
( 3:55 Ona jinsi mwanamume
N Lengo lingine: aliyefikiri ana kila kitu ali-
vyopata kusudi maishani.
Sasa Nimepata Kusudi
Maishani

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 25, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
26

Kwa Nini Wanadamu Wanateseka


na Kupatwa na Mambo Mabaya?
Jambo baya linapotokea watu hujiuliza, “Kwa na kula.” Baadaye, Adamu “akaanza kula.”
nini jambo hili limetokea?” Tunafurahi sana ku- (Mwanzo 3:6) Wote wawili hawakumtii Mungu.
jua kwamba Biblia inajibu waziwazi swali hilo! Kwa kuwa Adamu na Hawa walikuwa wakami-
lifu, walikuwa na uwezo wa kiasili wa kufanya
1. Shetani alianzishaje uovu ulimwenguni? mambo yaliyo sawa. Lakini kwa kutomtii Mungu
Shetani Ibilisi alimwasi Mungu. Shetani alita- kimakusudi, walitenda dhambi na kukataa uta-
ka kuwatawala viumbe wengine, hivyo aliwasha- wala wake. Uamuzi huo uliwasababishia mateso
wishi wanadamu wa kwanza Adamu na Hawa mengi.—Mwanzo 3:16-19.
wajiunge naye kuasi. Shetani alifanya hivyo ali-
pomdanganya Hawa. (Mwanzo 3:1-5) Alimfanya 3. Uamuzi wa Adamu na Hawa umetuathirije?
afikiri kwamba Yehova alikuwa akimnyima ja- Baada ya Adamu na Hawa kutenda dhambi ha-
mbo fulani zuri. Alidai kwamba wanadamu wa- wakuwa wakamilifu tena, hivyo wakapitisha hali
ngekuwa na furaha zaidi ikiwa hawangemtii Mu- ya kutokamilika kwa wazao wao wote. Biblia ina-
ngu. Shetani alisema uwongo wa kwanza kwa sema hivi kumhusu Adamu: “Kupitia mtu mmo-
kumdanganya Hawa kwamba hangekufa. Hiyo ja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo
ndiyo sababu Biblia inamwita Shetani kuwa kupitia dhambi, basi kifo kikaenea kwa watu
“mwongo na ndiye baba ya uwongo.”—Yoha- wote.”—Waroma 5:12.
na 8:44. Kuna sababu nyingi zinazofanya tuteseke. Wa-
kati fulani tunateseka kwa sababu ya maa-
2. Adamu na Hawa waliamua kufanya nini?
muzi mabaya tunayofanya, au kwa sababu ya
Yehova aliwaonyesha Adamu na Hawa ukari- maamuzi mabaya ya watu wengine. Na wa-
mu mwingi. Aliwaambia wangeweza kula matu- kati mwingine tunateseka kwa sababu tu-
nda ya kila mti katika bustani ya Edeni isipoku- nakuwa mahali pasipofaa wakati usiofaa.
wa mti mmoja. (Mwanzo 2:15-17) Hata hivyo, —Soma Mhubiri 9:11.
waliamua kula matunda ya mti waliokatazwa.
Hawa alianza “kuchuma matunda ya mti huo

107
CH I M BA ZAI DI

Chunguza sababu zinazoonyesha


kwamba Mungu hasababishi uovu
na kuteseka ulimwenguni leo, na Adamu na Hawa walikuwa wakamilifu na
jinsi anavyohisi tunapoteseka. waliishi katika Paradiso. Lakini walimsikiliza
Shetani wakamwasi Yehova

4. Ni nani anayefanya
wanadamu wateseke? (

Watu wengi wanaamini kwamba Mungu ndiye


anayeutawala ulimwengu wote. Je, hilo ni kweli? VIDEO: Ni Nani Anayeutawala
Onyesha VIDEO. Ulimwengu? (1:24)

Soma Yakobo 1:13 na 1 Yohana 5:19,


kisha mzungumzie swali hili:
˙ Je, Mungu ndiye anayesababisha
uovu na kuteseka?

5. Utawala wa Shetani umekuwa (


na matokeo gani?
Onyesha VIDEO. VIDEO: Kwa Nini Mungu
Anaruhusu Kuteseka?
Soma Mwanzo 3:1-6, kisha mzungumzie maswali haya: —Kisehemu (3:07)
˙ Shetani alisema uwongo gani?—Ona mstari wa 4 na 5.
˙ Shetani alisema nini ili kudai kwamba Yehova anawanyima
wanadamu jambo fulani zuri?
˙ Kulingana na madai ya Shetani, je, wanadamu wanamhitaji
Yehova awe Mtawala wao ili wawe na furaha?

Soma Mhubiri 8:9, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Kwa kuwa Yehova si Mtawala wa ulimwengu huu, hali zimekuwaje?
6. Yehova anajali tunapoteseka Je, wajua?
Je, Mungu anajali tunapoteseka? Ona mambo ambayo Shetani aliposema uwongo wa
Mfalme Daudi na mtume Petro waliandika. Soma Zaburi 31:7 kwanza alimchongea Yehova,
na 1 Petro 5:7, kisha mzungumzie swali hili: yaani, alimharibia Yehova sifa
kwa kudai kwamba ni Mtawala
˙ Unahisije unapojua kwamba Yehova anaona na asiye na haki na upendo. Hivi
anajali tunapoteseka? karibuni, Yehova atalitakasa jina
lake atakapoondoa mateso ya-
nayowapata wanadamu. Hilo
linamaanisha, atathibitisha kwa-
mba utawala wake ndio utawala
bora. Kutakaswa kwa jina la Ye-
hova ndilo jambo muhimu zaidi
ulimwenguni.—Mathayo 6:9, 10.

Baada ya Adamu na Hawa kuasi,


ulimwengu ulijaa dhambi,
mateso, na kifo

7. Mungu atakomesha mateso


yote yanayowapata wanadamu
Yehova atakomesha dhambi,
Soma Isaya 65:17 na Ufunuo 21:3, 4, mateso, na kifo. Kwa mara nyingine,
kisha mzungumzie swali hili: wanadamu watakuwa wakamilifu na
˙ Kwa nini inafariji kujua kwamba Yehova ataondoa kuishi katika Paradiso
madhara yote yanayowapata wanadamu?

WATU FULANI HUSEMA: “Kuteseka ni mpango wa Mungu.”


˙ Wewe ungesemaje?

109
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Shetani Ibilisi na wanadamu wawili
wa kwanza ndio waliosababisha uovu Jifunze jinsi Biblia inavyo-
ulio ulimwenguni. Yehova anajali sana fafanua maana ya dhambi.
tunapoteseka na hivi karibuni atao- “Dhambi Ni Nini?” (Makala iliyo
ndoa mateso. kwenye mtandao)

Ungejibuje?
˙ Shetani Ibilisi alimwambia
Hawa uwongo gani?
˙ Uasi wa Adamu na Hawa Soma mengi kuhusu suala
unatuathirije sisi sote? ambalo Shetani Ibilisi alizu-
sha katika bustani ya Edeni.
˙ Tunajuaje kwamba Yehova
anajali tunapoteseka? “Kwa Nini Mungu Anaruhusu
Watu Wateseke?” (Mnara wa
Mlinzi, Januari 1, 2014)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza majibu yenye


kuridhisha ya maswali
fulani magumu.
“Kwa Nini Wayahudi Wengi
Lengo Waliuawa? Kwa Nini Mungu
Hakuzuia?” (Makala iliyo kwenye
N Mweleze mtu mwingine mtandao)
sababu zinazoonyesha kwa-
mba si Mungu anayesababisha
mambo mabaya tunayoona
ulimwenguni. ( 5:09 Ona jambo ambalo mwa-
namume fulani alijifunza
N Lengo lingine: kuhusu mateso aliyoona.
Siko Peke Yangu Tena

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 26, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
27

Kifo cha Yesu Kinawezaje


Kutuokoa?
Sisi hutenda dhambi, tunateseka, na tunakufa mbi tulizofanya na kumwomba Yehova kupi-
kwa sababu wanadamu wa kwanza Adamu na tia Yesu Kristo atusamehe na kujitahidi kabi-
Hawa hawakumtii Mungu. Lakini tuna tumaini. sa kutorudia makosa hayo, tunaweza kufurahia
Yehova ameandaa njia ya kutuweka huru kutoka urafiki wa karibu pamoja na Mungu. (1 Yoha-
kwenye laana ya dhambi na kifo kupitia Mwana na 2:1) Biblia inasema hivi: “Kristo alikufa mara
wake, Yesu Kristo. Biblia inafundisha kwamba moja kwa wakati wote kwa ajili ya dhambi,
Yesu alitoa fidia kupitia kifo chake. Fidia ni ma- mtu mwadilifu kwa ajili ya wasio waadilifu, ili
lipo yanayotolewa ili kumweka mtu huru. Yesu awaongoze ninyi kwa Mungu.”—1 Petro 3:18.
alilipa fidia kwa kutoa uhai wake mkamilifu wa
kibinadamu. (Soma Mathayo 20:28.) Yesu ali- 2. Kifo cha Yesu kitatunufaishaje wakati ujao?
podhabihu kwa hiari haki yake ya kuishi milele Yehova alimtuma Yesu atoe uhai wake mkamili-
duniani, alitufungulia njia ya kupata tena uhai fu wa kibinadamu “ili kila mtu anayemwamini
mkamilifu ambao Adamu na Hawa walipoteza. [Yesu] asiangamizwe bali awe na uzima wa
Pia, Yesu alionyesha kwamba yeye na Yehova milele.” (Yohana 3:16) Kupitia dhabihu ya Yesu,
wanatupenda sana. Somo hili litakusaidia ku- Yehova ataondoa madhara yote yaliyosababi-
thamini zaidi kifo cha Yesu. shwa na Adamu alipokosa kutii. Hilo linamaani-
sha kwamba tukionyesha imani katika dhabihu
1. Kifo cha Yesu kinaweza kutunufaishaje leo? ya Yesu, tutapata nafasi ya kufurahia maisha
Kwa kuwa sisi ni watenda dhambi, tunafanya milele katika dunia paradiso!—Isaya 65:21-23.
mambo mengi yasiyompendeza Yehova. Hata
hivyo, ikiwa tunajuta sana kwa sababu ya dha-

 Dhambi haimaanishi tu kufanya jambo baya. Dhambi pia


inarejelea madhara ambayo tumerithi kutoka kwa Adamu na
Hawa.

111
CH I M BA ZAI DI

Jifunze mengi kuhusu sababu


iliyofanya Yesu atoe uhai wake, na
uchunguze jinsi unavyoweza kunufaika.

Adamu alikuwa mwanamume


mkamilifu aliyekosa kumtii Mungu
na hivyo akawasababishia
wanadamu wote dhambi na kifo

3. Kifo cha Yesu kinatuweka 4. Kifo cha Yesu kinaweza


huru kutoka kwenye dhambi kuwanufaisha watu
na kifo wote
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali
linalofuata. linalofuata.

( VIDEO: Kwa Nini Yesu Alikufa? ( VIDEO: Kwa Nini Yesu Alikufa?
—Sehemu ya 1 (2:01) —Sehemu ya 2 (2:00)

˙ Adamu alipoteza fursa gani alipokosa ˙ Kifo cha mtu mmoja kingewezaje
kumtii Mungu? kuwanufaisha watu wote?

Soma Waroma 5:12, kisha mzungumzie Soma 1 Timotheo 2:5, 6, kisha mzungumzie
swali hili: swali hili:
˙ Dhambi ambayo Adamu alifanya ˙ Adamu alikuwa mwanadamu mkamilifu
imeathirije maisha yako? ambaye aliwasababishia wanadamu wote
dhambi na kifo. Yesu pia alikuwa mwanada-
Soma Yohana 3:16, kisha mzungumzie swali hili: mu mkamilifu. Yesu alitoa jinsi gani “fidia
inayolingana” na uhai ambao Adamu
˙ Kwa nini Yehova alimtuma Mwana wake
alipoteza?
duniani?
Yesu alikuwa mwanamume
mkamilifu aliyemtii Mungu
na kuwafungulia wanadamu
njia ya kuwa wakamilifu na
kupata uzima wa milele

5. Fidia ni zawadi ambayo


Yehova amekupatia
Rafiki za Yehova huona fidia kuwa zawadi waliyo- Unaposoma mistari ifuatayo, wazia jinsi Yehova
pewa kibinafsi. Kwa mfano, soma Wagalatia 2:20, alivyohisi alipomwona Mwana wake akiteseka.
kisha mzungumzie swali hili: Soma Yohana 19:1-7, 16-18, kisha mzungumzie
swali hili:
˙ Mtume Paulo alionyeshaje kwamba aliona
fidia kuwa zawadi aliyopewa kibinafsi? ˙ Unahisije kuhusu jambo ambalo Yehova
na Yesu wamekufanyia?
Adamu alipotenda dhambi, yeye na wazao wake
wote walihukumiwa kifo. Lakini Yehova alimtuma
Mwana wake afe, ili wewe upate nafasi ya kuishi
milele.

HUENDA MTU AKAULIZA: “Inawezekanaje mtu mmoja afe kwa ajili ya watu wote?”
˙ Wewe ungejibuje swali hilo?

113
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Kupitia kifo cha Yesu, Yehova anaweza
kutusamehe dhambi zetu, na tunapa- Jifunze kwa nini uhai mkami-
ta fursa ya kuishi milele. lifu wa Yesu unaitwa fidia.
“Ni kwa Njia Gani Dhabihu
ya Yesu Ilikuwa ‘Fidia kwa Ajili
Ungejibuje? ya Wengi’?” (Makala iliyo kwenye
mtandao)
˙ Kwa nini Yesu alikufa?
˙ Ni kwa njia gani uhai mkamilifu
wa Yesu ulikuwa fidia inayoli-
ngana?
˙ Kifo cha Yesu kinawezaje kuku- Chunguza mambo tunayo-
paswa kufanya ili tuokolewe.
nufaisha?
“Yesu Huokoa—Jinsi Gani?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Je, Yehova anaweza kusa-


mehe hata dhambi nzito?
“Majibu ya Maswali ya Biblia”
(Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 2013)
Lengo
N Unaposali, mshukuru Yehova
kwa ukawaida kwa sababu ya
kutupatia zawadi ya Mwana
wake.
Ona jinsi kujifunza kuhusu dha-
N Lengo lingine: bihu ya Kristo kulivyomsaidia
mwanamume aliyepambana
na kumbukumbu mbaya.
“Kukumbuka Upendo Wangu
wa Kwanza Kumenisaidia
Kuvumilia” (Mnara wa Mlinzi,
Mei 15, 2015)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 27, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
28

Onyesha Shukrani kwa Mambo


Ambayo Yehova na Yesu
Wamekufanyia
Unahisije rafiki yako anapokupatia zawadi nzu- 2. Ni tukio gani la pekee linalotupatia fursa
ri? Bila shaka, unafurahi sana na unataka ku- ya kuonyesha shukrani kwa mambo ambayo
mwonyesha rafiki yako kwamba unaithamini za- Yehova na Yesu wametufanyia?
wadi hiyo. Yehova na Yesu walitupatia zawadi Usiku kabla ya kifo chake, Yesu aliwaambia wa-
bora kuliko zawadi zote. Ni zawadi gani hiyo, na fuasi wake njia nyingine ya kuonyesha shukra-
tunaweza kuonyeshaje kwamba tunaithamini? ni kwa dhabihu yake. Alianzisha tukio la pekee
ambalo Biblia inaliita “Mlo wa Jioni wa Bwana,”
1. Ni kwa njia gani tunaweza kuonyesha
au Ukumbusho wa Kifo cha Kristo. (1 Wako-
shukrani kwa mambo ambayo Mungu
rintho 11:20) Yesu alianzisha tukio hilo ili mi-
na Kristo wametufanyia?
tume wake na Wakristo wote wa kweli waku-
Biblia inatuahidi kwamba “kila mtu anayemwa- mbuke kwamba alitoa uhai wake kwa ajili yetu.
mini [Yesu]” anaweza kuishi milele. (Yoha- Yesu aliamuru hivi kuhusu tukio hilo: “Endeleeni
na 3:16) Hilo linamaanisha nini? Kumwamini kufanya hivi kwa kunikumbuka.” (Luka 22:19)
Yesu kunahusisha mengi. Tunahitaji kuonye- Unapohudhuria Ukumbusho, unaonyesha shu-
sha imani yetu kupitia maamuzi na matendo krani kwa upendo mkubwa ambao Yehova na
yetu. (Yakobo 2:17) Tunapoonyesha imani ku- Yesu wametuonyesha.
pitia matendo na maneno yetu, tunaimarisha
urafiki wetu na Yesu na pia Yehova, Baba yake.
—Soma Yohana 14:21.

115
CH I M BA ZAI DI

Chunguza njia nyingine ambazo tunaweza kuonyesha


shukrani kwa upendo mkubwa ambao Yehova na Yesu
wametuonyesha. Jifunze kwa nini Ukumbusho wa kifo
cha Kristo ni muhimu.

3. Tunaonyesha shukrani
kupitia matendo
Wazia kwamba mtu fulani alikuokoa ili
usizame ndani ya maji. Je, unaweza kusa-
hau jambo ambalo mtu huyo alikufanyia?
Au je, utatafuta njia za kumwonyesha
shukrani kwa jambo alilokufanyia?
Yehova ndiye chanzo cha uhai wetu.
Soma 1 Yohana 4:8-10, kisha mzungu-
Yesu alipenda Neno la Mungu,
mzie maswali haya:
alihubiri habari njema, na
˙ Kwa nini dhabihu ya Yesu ni zawadi kuwasaidia wengine
ya pekee?
˙ Unahisije kuhusu mambo ambayo
Yehova na Yesu wamekufanyia?

Tunaweza kuonyeshaje shukrani kwa


mambo ambayo Yehova na Yesu wame-
tufanyia? Soma 2 Wakorintho 5:15 na
1 Yohana 4:11; 5:3. Baada ya kusoma
kila andiko, zungumzieni swali hili:
˙ Kulingana na andiko hilo, tunawezaje
kuonyesha shukrani?
4. Mwige Yesu
Njia nyingine ya kuonyesha shukrani ni kumwiga Yesu.
Soma 1 Petro 2:21, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Unaweza kufuata hatua za Yesu kwa ukaribu
jinsi gani?
5. Hudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo
Ili uone jambo lililotokea Yesu alipoanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana,
soma Luka 22:14, 19, 20. Kisha mzungumzie maswali haya:
(
˙ Ni nini kilichotokea wakati wa Mlo wa Jioni wa Bwana?
˙ Ni nini kinachowakilishwa na mkate na divai?
VIDEO: Kumbuka Kifo —Ona mstari wa 19 na 20.
cha Yesu (1:42)
Yesu alitaka wanafunzi wake waadhimishe Mlo wa Jioni wa Bwana
mara moja kwa mwaka, katika tarehe inayolingana na siku ya kifo cha-
ke. Hivyo, Mashahidi wa Yehova hukutana kila mwaka ili kukumbuka
kifo cha Kristo wakifuata njia aliyoagiza. Ili ujifunze kuhusu mkutano
huu muhimu, onyesha VIDEO. Kisha mzungumzie swali linalofuata.
˙ Ni nini hufanyika wakati wa Ukumbusho?

Mkate na divai ni mifano. Mkate unawakilisha


mwili mkamilifu wa kibinadamu wa Yesu
ambao aliutoa uwe dhabihu kwa ajili yetu.
Divai inawakilisha damu yake

WATU FULANI HUSEMA: “Ili uokolewe unahitaji tu kumwamini Yesu.”


˙ Unawezaje kutumia Yohana 3:16 na Yakobo 2:17 kuonyesha kwamba mengi zaidi yanahitajika?

117
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Tunaonyesha shukrani kwa mambo
ambayo Yesu ametufanyia kwa ( 9:30 Kifo cha Kristo hutu-
kumwamini, na kuhudhuria chochea kufanya nini?
Ukumbusho wa kifo chake. Aliutumia Mwili Wake
Kumheshimu Yehova

Ungejibuje?
˙ Kumwamini Yesu kunamaanisha
nini?
˙ Ni kwa njia gani unaweza kuo-
nyesha shukrani kwa mambo Jifunze mengi kuhusu imani
ambayo Yehova na Yesu na jinsi ya kuionyesha.
wamekufanyia? “Onyesha Imani Yako
˙ Kwa nini ni muhimu sana Katika Ahadi za Yehova”
(Mnara wa Mlinzi, Oktoba 2016)
kuhudhuria Ukumbusho
wa kifo cha Kristo?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Katika simulizi “Ninajihisi Niki-


wa Safi, Mzima, na Ninafurahia
Kuwa Hai,” ona jinsi maisha ya
mwanamke fulani yalivyobadili-
Lengo ka baada ya kujifunza kuhusu
dhabihu ya Kristo.
N Hudhuria Ukumbusho unaofua- “Biblia Inabadili Maisha”
ta wa kifo cha Kristo. Muulize (Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 2011)
mwalimu wako wa Biblia tarehe
ya Ukumbusho na uandike
kwenye kalenda yako. Ona kwa nini ni watu wachache
wanaokula mkate na kunywa
N Lengo lingine: divai wakati wa Ukumbusho.
“Kwa Nini Mashahidi wa
Yehova Wanaadhimisha Mlo
wa Jioni wa Bwana kwa Njia
Tofauti na Dini Nyingine?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 28, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
29

Ni Nini Hutokea
Tunapokufa?
Je, umewahi kufiwa na mtu unayempenda? Ka- mtu anapokufa nafsi yake huendelea kuishi, la-
tika kipindi hicho kigumu huenda ulijiuliza: ‘Ni kini Biblia haifundishi hivyo. Basi, hakuna mtu
nini hutokea tunapokufa? Je, tutawaona tena anayeteseka baada ya kufa. Pia, kwa sababu
wapendwa wetu wakati ujao?’ Katika somo hili watu waliokufa hawajui jambo lolote, hawawezi
na linalofuata, tutachunguza majibu yenye ku- kutudhuru. Hivyo, hatuhitaji kuwatuliza au ku-
fariji yaliyo katika Biblia. waabudu watu waliokufa, wala kusali kwa aji-
li yao.
1. Ni nini hutokea tunapokufa?
Watu fulani hudai kwamba wana uwezo wa ku-
Yesu alilinganisha kifo na usingizi mzito. Mtu wasiliana na watu waliokufa. Lakini hilo haliwe-
ambaye amelala usingizi mzito hajui kinachoe- zekani. Kama tulivyojifunza, “waliokufa hawajui
ndelea. Kwa nini kifo kinalinganishwa na usingi- jambo lolote kamwe.” Wale wanaofikiri wana-
zi? Baada ya kufa mtu hawezi kuhisi maumivu. wasiliana na wapendwa wao waliokufa, inawe-
Hawezi kuhisi upweke hata kama aliwapenda zekana kwamba wanawasiliana na roho wao-
sana marafiki na watu wa familia yake. Biblia vu ambao hujifanya kuwa watu waliokufa. Kwa
inasema kwamba “waliokufa hawajui jambo lo- hiyo, kujua ukweli kuhusu kifo hutulinda dhidi ya
lote kamwe.”—Soma Mhubiri 9:5. roho waovu. Yehova anatuonya kwamba tusi-
2. Kwa nini ni muhimu kujua ukweli kuhusu kifo? jaribu kuwasiliana na watu waliokufa kwa sa-
babu anajua tukiwasiliana na roho waovu tu-
Watu wengi wanaogopa kifo, hata wanawaogo- tapata madhara.—Soma Kumbukumbu la Torati
pa watu waliokufa! Lakini mambo ambayo Biblia 18:10-12.
inasema kuhusu kifo yanaweza kukufariji. Yesu
alisema: “Kweli itawaweka ninyi huru.” (Yoha-
na 8:32) Baadhi ya dini hufundisha kwamba

119
CH I M BA ZAI DI

Jifunze mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu kifo na uimarishe imani


yako kwa Mungu mwenye upendo, ambaye hawaadhibu watu waliokufa.

3. Jifunze ukweli kuhusu (


hali ya watu waliokufa
Ulimwenguni pote, watu wanaamini mambo mbalimbali kuhusu VIDEO: Wafu Wako Katika Hali
jambo linalotokea tunapokufa. Bila shaka, haiwezekani kwamba Gani?—Kisehemu (1:19)
imani hizo zote ni za kweli.
˙ Katika eneo lenu watu wanaamini nini kuhusu hali ya
watu waliokufa?

Ili kuona jambo ambalo Biblia inafundisha, onyesha VIDEO.


Soma Mhubiri 3:20, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kulingana na andiko hili, ni nini hutokea mtu anapokufa?
˙ Je, kuna sehemu yoyote ya mtu aliyekufa inayoendelea kuishi?

Biblia inatuambia kuhusu kifo cha Lazaro, aliyekuwa rafiki wa karibu


wa Yesu. Soma Yohana 11:11-14, ili uone jambo ambalo Yesu alisema
kuhusu hali ya Lazaro. Kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Yesu alilinganisha kifo na nini?
˙ Hilo linatufundisha nini kuhusu hali ya watu waliokufa?
˙ Una maoni gani kuhusu jinsi Biblia inavyofafanua kifo?
4. Ni muhimu kujua ukweli
kuhusu kifo
Kujua ukweli kuhusu kifo, hutusaidia tusiwaogope
watu waliokufa. Soma Mhubiri 9:10, kisha mzu-
ngumzie swali hili:
˙ Je, watu waliokufa wanaweza kutudhuru?

Ukijifunza ukweli ulio katika Biblia kuhusu watu


waliokufa, hutaamini uwongo wa kwamba tuna-
paswa kuwatuliza au kuwaabudu watu waliokufa.
Soma Isaya 8:19 na Ufunuo 4:11, kisha mzungu-
mzie swali hili:
˙ Unafikiri Yehova anahisije kuhusu mtu ana- Ukweli kuhusu kifo
yeabudu au kutafuta msaada kutoka kwa unatuweka huru
kutoka kwenye desturi
watu waliokufa?
zisizompendeza Yehova

5. Tunapata faraja tunapojifunza


ukweli kuhusu kifo
Watu wengi wamefundishwa kwamba watakapo- Tunapoendelea kujifunza mengi kumhusu Yehova,
kufa wataadhibiwa kwa sababu ya makosa waliyo- ndivyo tunavyozidi kutambua kwamba hawezi ka-
fanya zamani. Lakini inafariji kujua kwamba haku- mwe kuwatesa watu waliokufa. Soma Kumbuku-
na mtu anayeteseka baada ya kufa, hata mtu mbu la Torati 32:4 na 1 Yohana 4:8, kisha mzu-
ambaye alifanya mambo mabaya sana. Soma ngumzie maswali haya:
Waroma 6:7, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Je, Mungu mwenye sifa zinazotajwa
˙ Kama tulivyosoma katika Biblia, mtu anapo- kwenye maandiko hayo anaweza
kufa anawekwa huru au anaondolewa hatia kuwatesa watu waliokufa?
ya dhambi yake. Je, unafikiri kuna mtu aliye- ˙ Je, umefarijika kujua ukweli kuhusu kifo?
kufa ambaye anaendelea kuteseka kwa saba- Kwa nini?
bu ya makosa aliyofanya?

WATU FULANI HUSEMA: “Ninaogopa kwamba nitakapokufa nitateseka.”


˙ Unaweza kuwasomea mistari gani ya Biblia ili kuwafariji?

121
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Mtu anapokufa, uhai wake unakoma.
Watu waliokufa hawateseki wala ha- Ona maana halisi ya neno
wawezi kuwadhuru walio hai. “nafsi” katika Biblia.
“Nafsi Ni Nini?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
Ungejibuje?
˙ Ni nini hutokea tunapokufa?
˙ Kwa nini ni muhimu kujua ukweli
kuhusu kifo?
˙ Kwa nini kujifunza ukweli kuhusu
kifo kunatufariji? ( 3:07 Je, Mungu huwaadhibu watu
waovu katika moto wa mateso?
Je, Watu Watateswa Katika
Moto wa Mateso?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Je, tunapaswa kuwaogopa


watu waliokufa?
Roho za Wafu, Je, Zaweza
Kukusaidia au Kukuumiza?
Lengo Je, Ziko Kweli? (broshua)

N Jitahidi kukumbuka andiko


moja katika somo hili ili
uweze kufafanua hali ya
watu waliokufa.
Ona jinsi mwanamume fulani
N Lengo lingine: alivyofarijika baada ya kujifu-
nza ukweli kuhusu jambo
linalotokea tunapokufa.
“Nilivutiwa na Majibu ya
Biblia Yaliyo Wazi na Yana-
yoeleweka” (Mnara wa Mlinzi,
Februari 1, 2015)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 29, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
30

Wapendwa Wako Wanaweza


Kuwa Hai Tena!
Kifo husababisha majonzi na huzuni nyingi. Lazaro, rafiki ya Yesu alikufa. Ingawa Laza-
Hiyo ndiyo sababu Biblia inasema kifo ni adui. ro alikuwa amekufa na mwili wake ulikuwa ka-
(1 Wakorintho 15:26) Katika Somo la 27, ulijifu- burini kwa siku nne, Yesu alimfufua. Baada ya
nza kwamba Yehova atamwangamiza adui huyo. Yesu kusali kwa Mungu, aliita hivi kwa sauti ku-
Lakini itakuwaje kwa watu ambao tayari wa- bwa: “Lazaro, njoo huku nje!” Kisha “mtu huyo
mekufa? Katika somo hili, utajifunza mengi ku- aliyekuwa amekufa akatoka” akiwa hai! (Yoha-
husu ahadi nyingine ya Yehova yenye kupe- na 11:43, 44) Wazia jinsi marafiki na watu wa fa-
ndeza. Atafufua mabilioni ya watu ili wafurahie milia ya Lazaro walivyofurahi!
kuishi milele. Atafanya wawe hai tena! Je, kwe-
li hilo linawezekana? Je, watafufuliwa ili waishi 3. Kuna tumaini gani kwa wapendwa
mbinguni au duniani? wako waliokufa?
Biblia inaahidi hivi: “Kutakuwa na ufufuo.” (Ma-
1. Yehova atawafanyia nini wapendwa tendo 24:15) Watu ambao Yesu aliwafufua ali-
wetu waliokufa? pokuwa duniani hawakuwa wameenda mbingu-
Yehova anatamani sana kuwafufua watu walio- ni. (Yohana 3:13) Walifurahia kufufuliwa hapa
kufa. Mwanamume mwenye imani Ayubu, aliku- duniani. Vivyo hivyo, hivi karibuni Yesu atafufua
wa na uhakika kwamba ikiwa angekufa Mungu mabilioni ya watu ili wafurahie kuishi milele ka-
hangemsahau. Alimwambia Mungu hivi: “Utai- tika paradiso duniani. Alisema kwamba “wote
ta, nami nitakujibu [kutoka kaburini].”—Soma walio katika makaburi ya ukumbusho” watafu-
Ayubu 14:13-15. fuliwa, kutia ndani wale tunaofikiri wamesahau-
lika lakini wako katika kumbukumbu ya Mungu.
2. Tunajuaje kwamba watu waliokufa —Yohana 5:28, 29.
wanaweza kufufuliwa?
Yesu alipokuwa duniani, Mungu alimpa nguvu
za kuwafufua watu. Yesu alimfufua msichana
mwenye umri wa miaka 12 na mwana wa mja-
ne. (Marko 5:41, 42; Luka 7:12-15) Baadaye,

123
CH I M BA ZAI DI

Chunguza uthibitisho ulio katika Biblia kwamba watu


waliokufa wanaweza kufufuliwa na watafufuliwa wakati ujao.
Jifunze jinsi ufufuo unavyoweza kukufariji na kukupa tumaini.

4. Yesu alithibitisha kwamba ana


uwezo wa kuwafufua waliokufa
Jifunze mengi kuhusu mambo ambayo Yesu alimfanyia
Lazaro rafiki yake. Soma Yohana 11:14, 38-44, kisha
mzungumzie maswali haya:

˙ Tunajuaje kwamba kwa kweli Lazaro alikuwa amekufa?


—Ona mstari wa 39.
˙ Ikiwa Lazaro alikuwa ameenda mbinguni, je, unafikiri
Yesu angemrudisha aishi tena duniani?

Onyesha VIDEO.

( VIDEO: Yesu Amfufua Lazaro (1:16)

5. Watu wengi watafufuliwa!


Soma Zaburi 37:29, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Mabilioni ya watu watakaofufuliwa wataishi wapi?

Yesu atawafufua watu wengi sana, si wale tu waliomwabudu


Yehova. Soma Matendo 24:15, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Ungependa kumwona nani akifufuliwa?
Fikiria jambo hili: Ni rahisi kwa
Yesu kumfufua mtu kama vile
baba anavyomwamsha mtoto
wake ambaye amelala usingizi

6. Ufufuo unaweza kukupatia (


faraja na tumaini
Simulizi la Biblia kuhusu binti ya Yairo limewafariji na kuwatia VIDEO: Tumaini la Ufufuo
moyo watu wengi wanaoomboleza. Soma simulizi hilo la mambo Hutufanya Tuwe Jasiri
yaliyotokea kihalisi kwenye Luka 8:40-42, 49-56. —Jinsi Gani? (3:21)

Kabla ya kumfufua binti ya Yairo, Yesu alimwambia hivi baba yake:


“Usiogope, uwe tu na imani.” (Ona mstari wa 50.) Tumaini la ufufuo
linaweza kukusaidiaje . . .
˙ mpendwa wako anapokufa?
˙ uhai wako unapokuwa hatarini?

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.


˙ Tumaini la ufufuo limewafariji na kuwatia moyo
jinsi gani wazazi wa Phelicity?

WATU FULANI HUSEMA: “Wazo la kuwafufua watu waliokufa ni ndoto tu.”


˙ Wewe una maoni gani?
˙ Unaweza kutumia andiko gani ili kuonyesha kwamba kutakuwa na ufufuo?

125
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Biblia inaahidi kwamba mabilioni
ya watu waliokufa watafufuliwa. Chunguza mambo unayoweza
Yehova anataka waishi tena na kufanya ili kukabiliana na
amempa Yesu nguvu za kuwafufua. huzuni unapofiwa.
“Kukabiliana na Huzuni ya
Kufiwa” (Amkeni! Na. 3, 2018)
Ungejibuje?
˙ Yehova na Yesu wanahisije kuhu-
su kuwafufua watu waliokufa?
˙ Mabilioni ya watu watakaofufuli-
wa wataishi wapi, mbinguni au ( 5:06 Je, kweli kanuni za Biblia
duniani? Kwa nini unajibu hivyo? zinaweza kumsaidia mtu
anayeomboleza?
˙ Kwa nini una uhakika kwamba
wapendwa wako waliokufa wana- Mpendwa Wako Anapokufa
weza kuishi tena?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 2:07 Watoto wanaweza kufanya nini


ili kukabiliana na huzuni mtu
wanayempenda anapokufa?
Fidia
Lengo
N Ikiwa unamfahamu mtu anaye-
omboleza, tafuta muda unao-
faa wa kuzungumza naye kuhu-
su tumaini la ufufuo.
Je, kuna watu watakaofufuliwa
N Lengo lingine: ili waishi mbinguni? Ni nani
ambao hawatafufuliwa?
“Ufufuo Ni Nini?” (Makala iliyo
kwenye mtandao)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 30, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
31

Ufalme wa Mungu Ni Nini?


Ufalme wa Mungu ndio ujumbe muhimu zai- pokuja duniani, mamilioni ya watu wamekuwa
di katika Biblia. Yehova atatumia Ufalme huo wafuasi wake. Lakini watu 144,000 ndio tu wa-
kutimiza kusudi lake la mwanzoni la kuifanya naoenda mbinguni kutawala pamoja na Yesu.
dunia iwe paradiso. Ufalme huo ni nini? Tuna- (Soma Ufunuo 14:1-4.) Wakristo wengine wote
juaje kwamba umeanza kutawala? Ufalme huo walio duniani watakuwa raia wa Ufalme huo.
umetimiza mambo gani? Na utatimiza mambo —Zaburi 37:29.
gani wakati ujao? Maswali hayo yatajibiwa kati-
ka somo hili na masomo mawili yanayofuata. 3. Kwa nini Ufalme wa Mungu ni bora kuliko
serikali za wanadamu?
1. Ufalme wa Mungu ni nini, na Mfalme wake ni Ingawa watawala wa serikali za wanadamu wa-
nani? najitahidi kufanya mambo mazuri, hawana uwe-
Ufalme huo ni serikali iliyoanzishwa na Yeho- zo wa kufanya mambo yote wanayotaka. Baada
va Mungu mwenyewe. Mfalme wa Ufalme huo ya kipindi chao cha kutawala kwisha, huenda
ni Yesu Kristo, na anatawala kutoka mbinguni. watawala wengine wabinafsi wakaanza kutawa-
(Mathayo 4:17; Yohana 18:36) Biblia inasema la na hawawajali raia wao. Lakini kuhusu Yesu
hivi kumhusu Yesu: “Atatawala akiwa Mfalme Mtawala wa Ufalme wa Mungu, hakuna mtawa-
. . . milele.” (Luka 1:32, 33) Akiwa Mfalme wa la mwingine atakayechukua nafasi yake. Mungu
Ufalme wa Mungu, Yesu atatawala watu wote “[ameusimamisha] ufalme ambao hautaanga-
duniani. mizwa kamwe.” (Danieli 2:44) Yesu atatawala
dunia yote, na hatakuwa na ubaguzi. Yesu ni
2. Ni nani wanaotawala pamoja na Yesu? mwenye upendo, fadhili, na haki, naye atawafu-
Yesu anatawala pamoja na wengine. “Watu ku- ndisha watu kuwatendea wengine kwa njia hiyo-
toka katika kila kabila na lugha na watu na hiyo, yaani, kwa upendo, fadhili, na haki.—Soma
taifa . . . watatawala wakiwa wafalme juu ya Isaya 11:9.
dunia.” (Ufunuo 5:9, 10) Ni watu wangapi wata-
kaotawala pamoja na Kristo? Tangu Yesu ali-

127
CH I M BA ZAI DI

Chunguza uone kwa nini Ufalme wa Mungu ni


serikali bora kuliko serikali zote za wanadamu.

4. Serikali yenye nguvu 5. Ni lazima serikali za


itaitawala dunia yote wanadamu ziondolewe
Yesu Kristo ana nguvu nyingi sana za kutawala Kwa nini ni lazima Ufalme wa Mungu uondoe
kuliko mtawala yeyote katika historia. Soma serikali za wanadamu? Onyesha video, kisha
Mathayo 28:18, kisha mzungumzie swali hili: mzungumzie swali linalofuata.
˙ Kwa nini Yesu ana mamlaka kubwa
zaidi kuliko mtawala yeyote wa serikali ( VIDEO: Ufalme wa Mungu
za wanadamu? Ni Nini?—Kisehemu (1:41)

Serikali za wanadamu hubadilika-badilika,


na kila serikali hutawala sehemu fulani ya ˙ Utawala wa serikali za wanadamu
dunia. Namna gani Ufalme wa Mungu? umekuwa na matokeo gani?
Soma Danieli 7:14, kisha mzungumzie
maswali haya: Soma Mhubiri 8:9, kisha mzungumzie
˙ Kwa nini inafurahisha kujua kwamba maswali haya:
Ufalme wa Mungu “hautaangamizwa”? ˙ Je, unafikiri Ufalme wa Mungu
˙ Kwa nini tunafurahi kujua kwamba unapaswa kuondoa serikali za
utaitawala dunia yote? wanadamu? Kwa nini?
7. Sheria za Ufalme wa
Mungu ni bora zaidi
Serikali huweka sheria ambazo zimekusudiwa
kuwanufaisha na kuwalinda raia wake. Ufalme
wa Mungu pia una sheria ambazo zinapaswa
kufuatwa na raia wake. Soma 1 Wakorintho
6:9-11, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Unafikiri ulimwengu utakuwaje kila mtu
atakapofuata sheria za Mungu? 
˙ Je, unafikiri Yehova ana haki ya kuwawekea
sheria raia wa Ufalme wake? Kwa nini?
˙ Ni nini kinachoonyesha kwamba watu
ambao hawafuati sheria hizo wanaweza
kubadilika?—Ona mstari wa 11.
Yehova amewachagua wanaume na wanawake kutoka  Baadhi ya sheria hizo zitazungumziwa katika Sehemu ya 3.
katika malezi mbalimbali watawale pamoja na Yesu

6. Watawala wa Ufalme wa
Mungu wanaelewa hali yetu
Kwa kuwa Mfalme wetu, Yesu, aliwahi kuwa Serikali huweka sheria ili kuwalinda na kuwanufaisha
mwanadamu, anaweza ‘kuusikitikia udhaifu raia wake. Ufalme wa Mungu una sheria bora
wetu.’ (Waebrania 4:15) Wanaume na wanawake zinazowalinda na kuwanufaisha raia wake
waaminifu 144,000 ambao watatawala pamoja
na Yesu wamechaguliwa na Yehova “kutoka
katika kila kabila na lugha na watu na taifa.”
—Ufunuo 5:9.
˙ Je, unafarijika kujua kwamba Yesu na
watawala wenzake wanaelewa hali za
wanadamu? Kwa nini?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Ufalme wa Mungu ni nini?”


˙ Unawezaje kujibu swali hilo?

129
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Ufalme wa Mungu ni serikali halisi
iliyo mbinguni ambayo itaitawala Chunguza uone Yesu
dunia yote. alisema utawala wa Mungu
utatawala kutokea wapi.
“Je, Ufalme wa Mungu Umo
Ungejibuje? Moyoni Mwako?” (Makala iliyo
kwenye mtandao)
˙ Watawala wa Ufalme wa
Mungu ni nani?
˙ Kwa nini Ufalme wa Mungu
ni bora kuliko serikali zote
za wanadamu? ( 1:43 Kwa nini Mashahidi wa Yehova
wanachagua kuwa washikama-
˙ Yehova anatarajia raia
nifu kwa Ufalme wa Mungu ba-
wa Ufalme wake wafanye
dala ya serikali za wanadamu?
mambo gani?
Kuunga Mkono Ufalme
wa Mungu

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza jinsi Biblia inavyo-


fafanua wale 144,000 ambao
wamechaguliwa na Yehova
kutawala pamoja na Yesu.
Lengo “Ni Nani Wanaoenda
Mbinguni?” (Makala iliyo
N Soma kuhusu utawala wa Yesu kwenye mtandao)
katika Isaya 11:1-10, kisha uchu-
nguze jinsi unavyotofautiana
na utawala wa wanadamu.
Ni nini kilichomsadikishia
N Lengo lingine: mwanamke aliyekuwa gere-
zani kwamba Mungu peke
yake ndiye anayeweza kuleta
ulimwengu wenye haki?
“Jinsi Nilivyopata Suluhisho
la Ukosefu wa Haki”
(Amkeni!, Novemba 2011)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 31, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
32

Ufalme wa Mungu
Umeanza Kutawala!
Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mbinguni nza kutawala mbinguni akiwa Mfalme wa
mwaka wa 1914. Pia, siku za mwisho za uta- Ufalme wa Mungu. Baadhi ya mambo aliyota-
wala wa wanadamu zilianza mwaka huo. Tuna- ja ni vita, upungufu wa chakula, na mateteme-
juaje? Tutachunguza mambo ambayo Biblia ili- ko ya ardhi. (Soma Mathayo 24:7.) Pia, Biblia
tabiri, hali zinazoendelea ulimwenguni leo, na ilitabiri kwamba tabia za watu katika “siku za
jinsi ambavyo watu wamekuwa wakitenda tangu mwisho” zingefanya hali ziwe “ngumu kushu-
mwaka wa 1914. ghulika nazo.” (2 Timotheo 3:1-5) Hali na tabia
hizo zimeonekana waziwazi hasa tangu mwaka
1. Biblia ilitabiri nini? wa 1914.
Kitabu cha Biblia cha Danieli kinaonyesha kwa-
mba Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala 3. Kwa nini hali zimekuwa mbaya sana tangu
mwishoni mwa kipindi kinachoitwa “nyakati Ufalme wa Mungu ulipoanza kutawala?
saba.” (Danieli 4:16, 17) Karne nyingi baadaye, Muda mfupi baada ya kuwa Mfalme wa Ufalme
Yesu alisema kipindi hicho kinaitwa “nyakati zi- wa Mungu, Yesu alipigana vita mbinguni dhidi
lizowekwa za mataifa,” na alifundisha kwamba ya Shetani na roho waovu. Shetani alishindwa
bado kilikuwa kinaendelea. (Luka 21:24) Kama katika vita hivyo. Biblia inasema: “[alitupwa]
tutakavyoona, zile nyakati saba ziliisha mwaka chini duniani, na malaika zake wakatupwa
wa 1914. chini pamoja naye.” (Ufunuo 12:9, 12) Sheta-
ni ana hasira kali kwa sababu anajua kwamba
2. Tangu mwaka wa 1914, hali zimekuwaje ataangamizwa. Kwa hiyo, anasababisha mau-
na watu wamekuwa wakitendaje? mivu na kuteseka ulimwenguni pote. Ndiyo sa-
Wanafunzi wa Yesu walimwuliza hivi: “Ni nini babu hali ni mbaya sana ulimwenguni! Ufalme
itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya wa Mungu utaondoa matatizo hayo yote.
umalizio wa mfumo wa mambo?” (Mathayo
24:3) Yesu aliwajibu kwa kutabiri mambo me-
ngi ambayo yangetokea wakati ambapo angea-

131
CH I M BA ZAI DI

Chunguza kwa nini tunaamini kwamba Ufalme wa Mungu


ulianza kutawala mwaka wa 1914 na jinsi hilo linavyotuhusu.

4. Mfuatano wa matukio (E) Utawala wake ulikatizwa jinsi gani?


—Soma Danieli 4:29-33.
katika Biblia unaongoza
(F) Ni nini kilichompata Nebukadneza
kwenye mwaka wa 1914 baada ya “nyakati saba” kwisha?
—Soma Danieli 4:34-36.
Onyesha VIDEO.
Katika utimizo wa pili wa unabii huu . . .
( VIDEO: Ufalme wa Mungu Ulianza
Kutawala Mwaka wa 1914 (5:03) (G) Mti huo uliwakilisha nani?
—Soma 1 Mambo ya Nyakati 29:23.
(H) Utawala wao ulikatizwaje? Tunajuaje
Mungu alifanya Mfalme Nebukadneza wa kwamba bado utawala wao ulikuwa
jiji la kale la Babiloni aote ndoto ya kinabii. umekatizwa Yesu alipokuwa duniani?
Ndoto hiyo na ufafanuzi wa Danieli unahusu —Soma Luka 21:24.
utawala wa Nebukadneza na Ufalme wa Mungu. (I) Utawala huo ulirudishwa lini na wapi?
—Soma Danieli 4:17.
Soma Danieli 4:20-26, kisha utumie chati
kujibu maswali yanayofuata:
(A) Nebukadneza aliona nini katika ndoto
yake?—Ona mstari wa 20 na 21. Zile nyakati saba zina urefu gani?
(B) Ni nini kingeupata mti?—Ona mstari wa 23. Baadhi ya mistari ya Biblia hueleweka kwa ku-
(C) Ni nini kingetokea baada ya zile “nyakati chunguza mistari mingine ya Biblia. Kwa mfano,
saba” kwisha?—Ona mstari wa 26. kitabu cha Biblia cha Ufunuo kinasema kwa-
mba nyakati tatu na nusu ni sawa na siku 1,260.
(Ufunuo 12:6, 14) Nyakati saba ni mara mbili ya
Katika utimizo wa kwanza wa unabii huu . . .
nyakati tatu na nusu, yaani, siku 2,520. Nyakati
(D) Mti ulimwakilisha nani? nyingine, Biblia hutumia siku moja kuwakilisha
—Ona mstari wa 22. mwaka mmoja. (Ezekieli 4:6) Ndivyo ilivyo kuhu-
su zile nyakati saba zinazotajwa katika kitabu
 Ona makala mbili za mwisho kwenye sehemu ya Chunguza cha Danieli, zinawakilisha miaka 2,520.
Zaidi katika somo hili.

132
Jinsi Ile Ndoto ya Mti Inavyohusiana
na Ufalme wa Mungu

UNABII (Danieli 4:20-36)

(A) Mti mkubwa sana (B) “Ukateni na kuuangusha mti”


na acheni “nyakati saba zipite”

(C) “Utarudishiwa
tena ufalme wako”

Utawala Utawala
Utawala wakatizwa warudishwa
UTIMIZO WA KWANZA

(D) Nebukadneza, (E) Baada ya mwaka wa 606 K.W.K., (F) Nebukadneza arudiwa
Mfalme wa Babiloni Nebukadneza arukwa na akili na na fahamu na anaanza
anashindwa kutawala kwa miaka saba kutawala tena

UTIMIZO WA PILI

607 K.W.K. Miaka 2,520 1914 W.K.


(G) Wafalme Waisraeli (H) Yerusalemu laharibiwa na kukatiza (I) Yesu aanza kutawala
ambao waliwakilisha utawala wa wafalme Waisraeli kwa miaka mbinguni akiwa Mfalme
utawala wa Mungu 2,520 wa Ufalme wa Mungu
(
5. Ulimwengu umebadilika
tangu mwaka wa 1914
VIDEO: Ulimwengu Onyesha VIDEO.
Umebadilika Tangu
Mwaka wa 1914 (1:10) Yesu alitabiri kuhusu hali ambazo zingekuwa ulimwenguni
wakati ambapo angeanza kutawala. Soma Luka 21:9-11,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Umesikia au kujionea nini kati ya mambo hayo yaliyotabiriwa?

Mtume Paulo alifafanua jinsi ambavyo watu wangetenda wakati wa


siku za mwisho za utawala wa wanadamu. Soma 2 Timotheo 3:1-5,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Umejionea watu wakiwa na tabia gani kati ya tabia hizo?
Unapojifunza jambo linaloweza
kuwasaidia au kuwaokoa wengine,
unapaswa kufanya nini?

6. Utawala wa Ufalme wa Mungu


unapaswa kutuchochea kutenda
Soma Mathayo 24:3, 14, kisha mzungumzie
maswali haya:
˙ Ni kazi gani muhimu inayoonyesha kwamba
Ufalme wa Mungu unatawala?
˙ Unawezaje kushiriki kufanya kazi hiyo?

Sasa Ufalme wa Mungu unatawala, na hivi karibuni


utaitawala dunia yote. Soma Waebrania 10:24, 25,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kila mmoja wetu anapaswa kufanya nini
‘kadiri tunavyoona siku ile ikikaribia’?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Kwa nini Mashahidi wa Yehova


wanasema mwaka wa 1914 ni muhimu sana?”
˙ Wewe ungesemaje?

135
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Unabii wa Biblia, mfuatano wa matu-
kio, na hali zilizo ulimwenguni zinathi- Chunguza mambo
bitisha kwamba sasa Ufalme wa Mu- ambayo wanahistoria
ngu unatawala. Tunaonyesha kwamba na watu wengine husema
tunaamini hilo kwa kuhubiri kuhusu kuhusu mabadiliko ulimwe-
Ufalme na kuhudhuria mikutano ya nguni tangu mwaka wa 1914.
kutaniko. “Maadili Yalipoporomoka
Ghafula” (Amkeni!, Aprili 2007)
Ungejibuje?
˙ Ni nini kilichotokea baada ya
nyakati saba zilizotabiriwa katika Soma uone jinsi unabii ulio ka-
kitabu cha Biblia cha Danieli? tika Mathayo 24:14 ulivyobadili
maisha ya mwanamume fulani.
˙ Ni nini kinachokuthibitishia kwa-
mba Ufalme wa Mungu ulianza “Nilipenda Mchezo wa
kutawala mwaka wa 1914? Besiboli Kuliko Kitu Kingine
Chochote!” (Mnara wa Mlinzi,
˙ Unaweza kuonyeshaje kwamba Na. 3 2017)
unaamini Ufalme wa Mungu
unatawala?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Tunajuaje kwamba unabii


ulio katika Danieli sura ya 4
unahusu Ufalme wa Mungu?
“Ufalme wa Mungu Ulianza
Lengo Kutawala Lini? (Sehemu ya 1)”
(Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 2014)
N Jitahidi kustahili kuwa
mhubiri wa habari njema.

N Lengo lingine:
Ni nini kinachoonyesha kwa-
mba nyakati saba zinazotajwa
katika Danieli sura ya 4 ziliisha
mwaka wa 1914?
“Ufalme wa Mungu
Ulianza Kutawala Lini?
(Sehemu ya 2)” (Mnara wa
Mlinzi, Novemba 1, 2014)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 32, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
33

Ufalme wa Mungu
Utatimiza Nini?
Tayari Ufalme wa Mungu umeanza kutawala. 3. Ufalme wa Mungu utatimiza nini baada
Hivi karibuni utafanya mabadiliko makubwa du- ya waovu kuangamizwa?
niani. Tutachunguza baadhi ya mambo mazuri Baada ya waovu kuangamizwa, Yesu atatawala
ambayo tunatazamia kufurahia chini ya utawala akiwa Mfalme kwa miaka elfu moja. Wakati huo,
wa Ufalme wa Mungu. Yesu na watawala wenzake 144,000 watawasai-
dia wanadamu walio duniani kuwa wakamilifu
1. Ufalme wa Mungu utaletaje amani
na wasio na dhambi. Mwishoni mwa kipindi hi-
na haki duniani?
cho, dunia itakuwa paradiso maridadi, na watu
Yesu, Mfalme wa Ufalme wa Mungu, atawaa- wote watakuwa na furaha kwa sababu ya kutii
ngamiza watu waovu na serikali zote katika vita sheria za Yehova. Kisha Yesu atamrudishia uta-
vya Har–Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Waka- wala Yehova Baba yake. Wakati huo, ‘jina la Ye-
ti huo, ahadi hii ya Biblia itatimizwa kikamili: hova litakuwa limetakaswa’ kikamili. (Matha-
“Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawa- yo 6:9, 10) Yehova atakuwa amethibitika kuwa
takuwepo tena.” (Zaburi 37:10) Kupitia Ufalme Mtawala mzuri anayewajali raia wake. Kisha Ye-
huo, Yesu atahakikisha kwamba kuna amani na hova atamwangamiza Shetani, roho waovu, na
haki duniani pote.—Soma Isaya 11:4. watu wengine watakaoasi utawala wa Mungu.
2. Maisha yatakuwaje mapenzi ya Mungu (Ufunuo 20:7-10) Hali kamilifu zitakazoletwa na
yatakapotimizwa duniani? Ufalme wa Mungu zitadumu milele.
Chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu, “waa-
dilifu wataimiliki dunia, nao wataishi humo
milele.” (Zaburi 37:29) Wazia kuishi katika uli-
mwengu ambao kila mtu ni mwadilifu, watu
wote wanampenda Yehova na wanapendana!
Watu hawatakuwa wagonjwa tena, na kila mtu
ataishi milele.

137
CH I M BA ZAI DI

Chunguza kwa nini tunaweza kuamini kwa-


mba Mungu atatumia Ufalme kutimiza ahadi
zote zilizo katika Biblia kuhusu wakati ujao.

4. Ufalme wa Mungu utakomesha


serikali za wanadamu
“Mwanadamu amemtawala mwanadamu mwenzake
kwa kumuumiza.” (Mhubiri 8:9) Kupitia Ufalme wake,
Yehova ataondoa ukosefu huo wa haki.
Soma Danieli 2:44 na 2 Wathesalonike 1:6-8,
kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Yehova na Mwana wake, Yesu, watachukua hatua gani dhidi
ya serikali za wanadamu na wale wanaoziunga mkono?
˙ Mambo ambayo umejifunza kumhusu Yehova na Yesu
yanakuhakikishiaje kwamba watatenda kwa haki
na bila upendeleo?

(
5. Yesu ndiye Mfalme bora
Akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, Yesu atafanya
VIDEO: Yesu Alionyesha
mambo mengi ili kuwasaidia raia wake. Onyesha VIDEO
Mambo Ambayo Ufalme ili uone kwamba Yesu amethibitisha anatamani kuwasaidia
Utatimiza (1:13) watu na Mungu amempa nguvu za kufanya hivyo.
Yesu alipokuwa duniani, alionyesha mambo ambayo Ufalme
wa Mungu utatimiza. Kati ya baraka zilizoonyeshwa, ni baraka
gani unayotazamia kwa hamu? Soma Maandiko yaliyoonyeshwa
ili kujifunza mengi kuhusu baraka hizo.
YESU ALIPOKUWA YESU AKIWA
DUNIANI . . . MBINGUNI . . .

˙ alikuwa na nguvu za kudhibiti ˙ ataondoa uchafuzi wa mazingira


hali ya hewa.—Marko 4:36-41. duniani.—Isaya 35:1, 2.
˙ alilisha maelfu ya watu kimuujiza. ˙ ataondoa tatizo la njaa
—Mathayo 14:17-21. ulimwenguni.—Zaburi 72:16.
˙ aliponya watu wenye magonjwa ˙ atahakikisha watu wote wana
mbalimbali.—Luka 18:35-43. afya kamilifu.—Isaya 33:24.
˙ aliwafufua watu waliokufa. ˙ ataondoa madhara yanayosababishwa
—Luka 8:49-55. na kifo.—Ufunuo 21:3, 4.

6. Ufalme wa Mungu utaleta


wakati ujao ulio bora
Ufalme wa Mungu utatimiza kikamili kusudi ambalo
Yehova alikuwa nalo mwanzoni kuelekea wanadamu.
Wanadamu wataishi milele katika paradiso duniani.
Onyesha VIDEO ili uone jinsi Yehova anavyomtumia
Mwana wake, Yesu, kutimiza kusudi lake.

( VIDEO: Kionjo cha Wakati Ujao


Wenye Kupendeza (4:35)

Soma Zaburi 145:16, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Unahisije kujua kwamba Yehova “[atatosheleza]
tamaa ya kila kitu kilicho hai”?

WATU FULANI HUSEMA: “Ikiwa wanadamu wote watashirikiana, tunaweza kutatua


matatizo ulimwenguni.”
˙ Ufalme wa Mungu utatatua matatizo gani ambayo serikali za wanadamu zimeshindwa kutatua?

139
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Ufalme wa Mungu utatimiza malengo
yake yote. Utaifanya dunia yote kuwa Jifunze maana ya
paradiso iliyojaa watu wema watakao- Har–Magedoni.
mwabudu Yehova milele. “Vita vya Har–Magedoni
Ni Nini?” (Makala iliyo
kwenye mtandao)
Ungejibuje?
˙ Ufalme wa Mungu utalitakasaje
jina la Yehova?
˙ Kwa nini tunaweza kuamini kwa-
mba Ufalme wa Mungu utatimiza Chunguza kile kitakachotukia
ahadi zilizo katika Biblia? wakati utawala wa miaka
elfu moja wa Yesu na
˙ Ni jambo gani unalotazamia kwa
baada ya hapo.
hamu kati ya mambo ambayo
“Ni Nini Kitakachotokea
Ufalme wa Mungu utatimiza?
Katika Siku ya Hukumu?”
(Mnara wa Mlinzi,
Septemba 1, 2012)

Tarehe ambayo sehemu ( 1:50 Ona jinsi familia zinavyoweza


hii imekamilishwa kutafakari pamoja kuhusu
baraka za wakati ujao za
Ufalme wa Mungu.
Jiwazie Ukiwa Katika
Lengo Paradiso

N Tumia trakti Ufalme wa


Mungu Ni Nini? kuanzisha
mazungumzo.
Katika makala “Nilikuwa na Ma-
N Lengo lingine: swali Mengi Yaliyonisumbua,”
ona jinsi mwasi wa kisiasa
alivyopata majibu ya maswali
yaliyokuwa yakimhangaisha.
“Biblia Inabadili Maisha”
(Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2012)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 33, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw 140
MAMBO MAKUU YA
SEHEMU YA 2
Zungumzia maswali yafuatayo pamoja
na mwalimu wako:

1. Mungu atachukua hatua gani 9. Unaweza kujilindaje dhidi ya


dhidi ya dini za uwongo? Shetani na roho waovu?
(Ona Somo la 13.) (Ona Somo la 24.)

2. Soma Kutoka 20:4-6. 10. Kusudi la Mungu kwa wanadamu ni nini?


(Ona Somo la 25.)
˙ Yehova anahisije watu wanapodai kwamba
wanamwabudu kwa kutumia sanamu? 11. Kwa nini wanadamu huteseka na kufa?
(Ona Somo la 14.) (Ona Somo la 26.)

3. Yesu ni nani? 12. Soma Yohana 3:16.


(Ona Somo la 15.) ˙ Yehova amefanya nini ili kutuokoa
kutoka katika dhambi na kifo?
4. Unapenda sifa gani za Yesu?
(Ona Somo la 27.)
(Ona Somo la 17.)
13. Soma Mhubiri 9:5.
5. Soma Yohana 13:34, 35 na Matendo 5:42.
˙ Ni nini hutokea mtu anapokufa?
˙ Ni nani wanaotenda kupatana na Ukristo
wa kweli leo? Ni nini kinachokuthibitishia ˙ Yesu atafanya nini kuhusu mabilioni
kwamba wao ni Wakristo wa kweli? ya watu waliokufa?
(Ona Somo la 18 na 19.) (Ona Somo la 29 na 30.)

6. Kichwa cha kutaniko ni nani, 14. Kwa nini Ufalme wa Mungu ni bora
naye anaongozaje kutaniko? kuliko serikali nyingine zote?
(Ona Somo la 31 na 33.)
(Ona Somo la 20.)
15. Je, unaamini kwamba Ufalme
7. Soma Mathayo 24:14.
wa Mungu unatawala? Kwa nini?
˙ Unabii huu unatimizwaje leo? Ufalme huo ulianza kutawala lini?
˙ Umezungumza na nani kuhusu (Ona Somo la 32.)
habari njema?
Maswali yako:
(Ona Somo la 21 na 22.)

8. Je, unafikiri kwamba ubatizo ni


lengo muhimu? Kwa nini?
(Ona Somo la 23.)
SEHEMU YA 3
Wazo Kuu: Jifunze mambo
ambayo Mungu anataka
waabudu wake wafanye

MASOMO
34 Tunaweza Kuonyeshaje Kwamba
Tunampenda Yehova?
35 Jinsi ya Kufanya Maamuzi Mazuri
36 Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote
37 Maoni ya Biblia Kuhusu Pesa na Kazi
38 Thamini Zawadi ya Uhai
39 Maoni ya Mungu Kuhusu Damu
40 Tunawezaje Kuwa Safi Machoni pa Mungu?
41 Biblia Inasema Nini Kuhusu Ngono?
42 Biblia Inasema Nini Kuhusu Useja na Ndoa?
43 Wakristo Wanapaswa Kuwa na Maoni
Gani Kuhusu Kileo?
44 Je, Sherehe Zote Zinamfurahisha Mungu?
45 Inamaanisha Nini Kutounga Mkono
Upande Wowote?
46 Kwa Nini Unapaswa Kujiweka Wakfu
na Kubatizwa?
47 Je, Uko Tayari Kubatizwa?
34

Tunaweza Kuonyeshaje
Kwamba Tunampenda Yehova?
Tangu ulipoanza kujifunza Biblia, je, upendo 2. Kwa nini inaweza kuwa vigumu kwetu
wako kwa Mungu umeongezeka? Je, ungependa kumpenda Yehova?
kuendelea kuimarisha urafiki wako na Mungu? “Mwadilifu ana matatizo mengi.” (Zaburi
Ikiwa ndivyo, kumbuka kwamba Yehova ana- 34:19) Sote tunapambana na hali yetu ya kuto-
poona upendo wako kwake ukizidi kuongezeka, kamilika. Huenda pia tukakabili matatizo ya kiu-
ndivyo atakavyoendelea kukupenda na kukujali chumi, ukosefu wa haki, na matatizo mengine.
zaidi. Unawezaje kumwonyesha kwamba una- Tunapokabili matatizo, huenda isiwe rahisi kwe-
mpenda? tu kumtii Yehova. Kwa sababu matatizo yana-
weza kufanya iwe vigumu kumtii Yehova. Laki-
1. Tunawezaje kumwonyesha Yehova
ni ikiwa utakuwa mwaminifu na kumtii Yehova,
kwamba tunampenda?
utaonyesha kwamba unampenda kuliko kitu ki-
Tunaonyesha kwamba tunampenda Yehova kwa ngine chochote. Na utathibitisha kwamba wewe
kumtii. (Soma 1 Yohana 5:3.) Yehova hamla- ni mshikamanifu kwake. Naye atakuwa mshi-
zimishi mtu yeyote amtii. Badala yake, ame- kamanifu kwako. Hatakuacha kamwe.—Soma
mpa kila mmoja wetu nafasi ya kuamua ikiwa Zaburi 4:3.
tutamtii au la. Kwa nini? Yehova anataka tuwe
“watiifu kutoka moyoni.” (Waroma 6:17) Hilo li-
namaanisha kwamba anataka tumtii si kwa ku-
lazimishwa, bali kwa sababu tunampenda. Se-
hemu ya 3 na ya 4 ya kitabu hiki imekusudiwa
kukusaidia kuonyesha kwamba unampenda Ye-
hova kwa kufanya mambo yanayomfurahisha
na kuepuka mambo anayochukia.

143
CH I M BA ZAI DI

Chunguza kwa nini Yehova anafurahi


unapomtii, na ujifunze jinsi unavyoweza
kuendelea kuwa mwaminifu kwake.

3. Suala linalokuhusu
Katika kitabu cha Biblia cha Ayubu, Shetani alitokeza
madai si dhidi ya Ayubu tu, bali pia dhidi ya kila mtu
anayetaka kumtumikia Yehova. Soma Ayubu 1:1, 6-2:10,
kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kulingana na madai ya Shetani, kwa nini Ayubu
alimtii Yehova?—Ona Ayubu 1:9-11.
˙ Shetani anadai nini kuhusu wanadamu wote,
kutia ndani wewe?—Ona Ayubu 2:4.

Soma Ayubu 27:5b, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Ayubu alithibitishaje kwamba alimpenda
Ayubu alithibitisha kwamba ana-
sana Yehova? mpenda Yehova kwa kuendelea
kuwa mshikamanifu kwake

4. Fanya moyo wa
Yehova ushangilie
Soma Methali 27:11, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Yehova anahisije unapotenda kwa hekima na kumtii?
Kwa nini?
5. Unaweza kuwa mshikamanifu kwa Yehova (

Upendo wetu kwa Yehova hutuchochea kuwaambia wengine kumhusu.


Ushikamanifu wetu kwake hutuchochea kufanya hivyo hata inapoku- VIDEO: Tetea Imani Yako Licha
wa vigumu. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata. ya Upinzani (5:09)
˙ Je, wakati mwingine ni vigumu kwako kuwaambia wengine
kumhusu Yehova?
˙ Katika video hiyo, ni nini kilichomsaidia Grayson ashinde woga
wake?

Ni rahisi kuwa washikamanifu kwa Yehova ikiwa tunapenda mambo anayopenda na


kuchukia mambo anayochukia. Soma Zaburi 97:10, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kutokana na mambo uliyojifunza, ni baadhi ya mambo gani ambayo Yehova anapenda?
Na anachukia mambo gani?
˙ Unawezaje kujifunza kupenda mambo mazuri na kuchukia mambo mabaya?

6. Tunanufaika
tunapomtii Yehova
Sikuzote kumtii Yehova ndilo jambo bora.
Soma Isaya 48:17, 18, kisha mzungumzie
maswali haya:
Tunathibitisha kwamba
tunampenda Yehova ˙ Je, tunaweza kuwa na hakika kwamba
tunapoendelea kuwa sikuzote Yehova anajua jambo linalotufaa
washikamanifu kwake kabisa? Kwa nini?
˙ Kufikia sasa, umenufaikaje kwa
kujifunza Biblia na kumhusu Mungu
wa kweli, Yehova?

WATU FULANI HUSEMA: “Mungu hajali ninachofanya.”


˙ Unaweza kutumia andiko gani kuthibitisha kwamba matendo yetu yanaweza
kumfurahisha au kumhuzunisha Yehova?

145
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Unaweza kuonyesha kwamba una-
mpenda Yehova kwa kumtii na kue- ( 16:49 Ona jinsi unavyoweza
ndelea kuwa mshikamanifu kwake kuwa mshikamanifu kwa
hata unapokabili changamoto. Yehova na kutaniko?
“Kwa Mtu Mshikamanifu
Unatenda kwa Ushikamanifu”
Ungejibuje?
˙ Mfano wa Ayubu umekufundisha
nini?
˙ Utathibitishaje kwamba unampe-
nda Yehova? Jifunze kuhusu madai ya
Shetani dhidi ya wanadamu.
˙ Ni nini ambacho kitakusaidia
uendelee kuwa mshikamanifu “Ayubu Adumisha Utimilifu”
kwa Yehova? (Biblia—Ina Ujumbe Gani?
sehemu ya 6)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 8:18 Ona jinsi vijana na watoto wa-
navyoweza kuonyesha kwamba
wanampenda Yehova.
Mfurahishe Yehova
Lengo
N Weka akilini maneno ya andiko
la Methali 27:11, na uyafikirie
inapokuwa vigumu kwako
kumtii Yehova.
( 4:00 Vijana wanawezaje kuendelea
N Lengo lingine: kuwa washikamanifu kwa Mu-
ngu hata wanaposhinikizwa
na vijana wenzao?
Simama Imara Unaposhiniki-
zwa na Marafiki!

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 34, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
35

Jinsi ya Kufanya
Maamuzi Mazuri
Kila mtu hufanya maamuzi. Maamuzi tunayo- lewa maoni ya Mungu kuhusu jambo fulani tu-
fanya yanaweza kuwa na matokeo mazuri au naposoma simulizi la Biblia. Tunapoelewa jinsi
mabaya na yanaweza kuathiri urafiki wetu na Yehova anavyohisi, tunaweza kufanya maamuzi
Yehova. Kwa mfano, huenda tukahitaji kuamua yanayomfurahisha.
mahali tutakapoishi, kazi tutakayofanya, au iki-
wa tutafunga ndoa. Tunapofanya maamuzi ma- 2. Unapaswa kufikiria mambo gani kabla ya
zuri, tunakuwa na maisha yenye furaha na tuna- kufanya uamuzi?
mfurahisha Yehova. Biblia inasema: “Mwerevu hutafakari kila ha-
tua.” (Methali 14:15) Hilo linamaanisha kwamba
1. Biblia inaweza kukusaidiaje kufanya maamuzi kabla ya kufanya uamuzi tunapaswa kufikiria
mazuri? kwa makini mambo yote yanayohusika. Unapo-
Kabla ya kufanya uamuzi, sali kwa Yehova chunguza kila jambo, jiulize hivi: ‘Ni kanuni gani
umwombe akusaidie kisha uchunguze maoni za Biblia zinazohusika? Ni uamuzi gani ambao
yake katika Biblia kuhusu jambo hilo. (Soma utaniletea amani ya akili? Uamuzi wangu utaku-
Methali 2:3-6.) Wakati fulani, Yehova hutuambia wa na matokeo gani kwa watu wengine? Jambo
jambo hususa la kufanya. Ikiwa kuna amri husu- muhimu zaidi, je, uamuzi huu utamfurahisha Ye-
sa, jambo la busara ni kutii mwongozo huo. hova?’—Kumbukumbu la Torati 32:29.
Namna gani ikiwa hakuna amri hususa katika Yehova ana haki ya kutuamulia mambo mema
Biblia kuhusu jambo unalopaswa kufanya? Bado na mabaya. Tunapoelewa vizuri sheria na kanuni
Yehova atakuongoza “katika njia unayopaswa zake na kuazimia kuzifuata, tunazoeza dhamiri
kutembea.” (Isaya 48:17) Jinsi gani? Unawe- yetu. Dhamiri ni uwezo ulio ndani yetu wa kuta-
za kupata kanuni ambazo zitakuongoza. Ka- mbua mambo yanayofaa na yasiyofaa. (Waro-
nuni za Biblia ni kweli za msingi zinazofunua ma 2:14, 15) Tukizoeza dhamiri yetu, itatusaidia
mawazo na hisia za Mungu. Kwa kawaida tunae- kufanya maamuzi mazuri.

147
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi dhamiri na kanuni za Biblia


zinavyoweza kutusaidia kufanya maamuzi.

3. Fuata mwongozo 4. Zoeza dhamiri yako


wa Biblia kufanya maamuzi mazuri
Kanuni za Biblia zinaweza kutusaidiaje kufanya Kunapokuwa na amri hususa ya Maandiko
maamuzi? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie kuhusu jambo, ni rahisi kufanya uamuzi una-
maswali yanayofuata. ofaa. Lakini vipi ikiwa hakuna amri hususa?
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali
( VIDEO: Acha Kanuni za Biblia linalofuata.
Zikuongoze (5:54)
( VIDEO: “Dumisha Dhamiri
Njema” (5:13)
˙ Yehova ametupatia zawadi gani ya pekee?
˙ Kwa nini Yehova alitupatia uhuru wa
kujiamulia? ˙ Dada katika video hiyo alichukua hatua
gani ili kuzoeza dhamiri yake na kufanya
˙ Ametupatia nini ili kutusaidia kufanya
uamuzi uliomfurahisha Yehova?
maamuzi bora?
Kwa nini hatupaswi kuwaomba watu wengine
Ili uone mfano wa kanuni ya Biblia, soma
watufanyie maamuzi? Soma Waebrania 5:14,
Waefeso 5:15, 16. Kisha mzungumzie jinsi
kisha mzungumzie maswali haya:
unavyoweza ‘kutumia vizuri kabisa wakati
wako’ ili . . . ˙ Ingawa huenda ikawa rahisi kuwaomba
wengine watufanyie maamuzi, tunapaswa
˙ kusoma Biblia kwa ukawaida.
kuwa na uwezo wa kutofautisha nini?
˙ kuwa mume, mke, mzazi, mwana,
˙ Ni mambo gani yanayoweza kutusaidia
au binti bora.
kuzoeza dhamiri yetu na kufanya maamuzi
˙ kuhudhuria mikutano ya kutaniko. mazuri?

Dhamiri ni kama ramani inayotuongoza


kufanya maamuzi maishani
5. Heshimu dhamiri za watu wengine Hatua zinazotusaidia kufanya
Maamuzi yetu hutofautiana na maamuzi ya watu wengine. maamuzi mazuri
Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunaheshimu dhamiri za
watu wengine? Fikiria hali mbili zinazofuata:
Hali ya 1: Dada anayependa kujipamba anahamia kutaniko
ambalo dada wengi wanakwazika wanapoona watu wakijipamba.
Soma Waroma 15:1 na 1 Wakorintho 10:23, 24,
1. Mwombe Yehova akusaidie
kisha mzungumzie maswali haya: kuamua jambo la kufanya.
˙ Kulingana na maandiko haya, dada huyo anaweza —Yakobo 1:5.
kuamua kufanya nini? Utafanya nini unaposhughulika
na mtu ambaye dhamiri yake inamkataza kufanya jambo
ambalo dhamiri yako inakubali?

Hali ya 2: Ndugu ambaye anajua kwamba Biblia haikatazi


kunywa kileo kwa kiasi, lakini anaamua kutokunywa kileo.
Anakaribishwa kwenye tafrija ambapo anaona akina ndugu 2. Fanya utafiti katika Biblia
wakinywa kileo. na machapisho yanayotegemea
Biblia ili upate kanuni zinazohusi-
Soma Mhubiri 7:16 na Waroma 14:1, 10, ka. Unaweza pia kuzungumza
kisha mzungumzie maswali haya: na Wakristo wenye uzoefu.

˙ Kulingana na maandiko haya, ndugu huyo anaweza


kuamua kufanya nini? Utafanya nini ukimwona
mtu anafanya jambo ambalo dhamiri yako
inakuzuia kufanya?

3. Fikiria matokeo ya uamuzi


utakaofanya, yaani, jinsi utaka-
vyoathiri dhamiri yako na dhamiri
za watu wengine.

WATU FULANI HUSEMA: “Una haki ya kufanya chochote unachopenda,


bila kujali maoni ya watu wengine.”
˙ Kwa nini tunapaswa kufikiria maoni ya Mungu, na maoni ya watu wengine?

149
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Tunafanya maamuzi mazuri tunapo-
chunguza maoni ya Yehova kuhusu Unawezaje kufanya maamuzi
jambo fulani na kufikiria ikiwa maa- yatakayoimarisha urafiki
muzi yetu yatawasaidia watu wengine wako na Mungu?
au kuwasababishia madhara. “Fanya Maamuzi Ambayo
Yanamletea Mungu Heshima”
(Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 2011)
Ungejibuje?
˙ Unawezaje kufanya maamuzi
yanayomfurahisha Yehova?
˙ Unawezaje kuizoeza dhamiri ( 9:50 Jifunze jinsi Yehova
yako? anavyotupatia ushauri.
˙ Unaweza kuonyesha jinsi gani Yehova Anawaongoza
kwamba unaheshimu dhamiri Watu Wake
za watu wengine?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 5:46 Ona mambo yaliyomsaidia


mwanamume fulani kufanya
uamuzi mgumu.
Yehova Anahakikisha
Lengo Tunapata Mambo Mazuri

N Fikiria uamuzi ambao utafanya


hivi karibuni. Kisha utumie ha-
tua tatu zilizotajwa katika kisa-
nduku: “Hatua Zinazotusaidia
Kufanya Maamuzi Mazuri.” Jifunze kufanya mambo ya-
nayomfurahisha Yehova hata
kama hakuna sheria hususa.
N Lengo lingine:
“Je, Sikuzote Unahitaji Amri
ya Biblia?” (Mnara wa Mlinzi,
Desemba 1, 2003)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 35, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
36

Uwe Mnyoofu
Katika Mambo Yote
Sote tunapenda kuwa na marafiki wanyoofu. Ye- zetu Wakristo, au maofisa wa serikali, hatusemi
hova anataka rafiki zake wawe wanyoofu pia. uwongo wala kutoa habari zinazopotosha. Watu
Lakini si rahisi kuwa wanyoofu kwa sababu tu- wanyoofu hawawaibii au kuwapotosha watu we-
naishi katika ulimwengu uliojaa watu wasio wa- ngine. (Soma Methali 24:28 na Waefeso 4:28.)
nyoofu. Kuna manufaa gani ya kuwa wanyoofu Na wanalipa kodi zote wanazodaiwa. (Waro-
katika mambo yote? ma 13:5-7) Kwa njia hizo na nyinginezo, “[tuna-
jiendesha] kwa unyoofu katika mambo yote.”
1. Ni sababu gani muhimu zaidi ya kuwa —Waebrania 13:18.
wanyoofu?
Tunapowatendea wengine kwa unyoofu, tu- 3. Kuna manufaa gani za kuwa wanyoofu?
namwonyesha Yehova kwamba tunampenda Tunapojulikana kuwa watu wanyoofu ni rahi-
na tunamheshimu. Kumbuka kwamba Yehova si kwa watu wengine kutuamini. Pia, tunacha-
anajua mambo yote tunayofikiria na kutenda. ngia hali ya usalama na upendo katika kutaniko.
(Waebrania 4:13) Anaona tunapotenda kwa Tunafurahia dhamiri safi. Tunapokuwa wanyoo-
unyoofu na jambo hilo linamfurahisha. Neno fu, “[tunalipamba] fundisho la Mwokozi wetu,
lake linasema: “Yehova humchukia mtu mwe- Mungu,” na tunawavuta watu wengine wajiunge
nye hila, lakini ana urafiki wa karibu na watu nasi kumwabudu Yehova.—Tito 2:10.
wanyoofu.”—Methali 3:32.

2. Tunawezaje kutenda kwa unyoofu katika


maisha yetu ya kila siku?
Yehova anataka “kila mtu amwambie mwenza-
ke ukweli.” (Zekaria 8:16, 17) Hilo linamaani-
sha nini? Iwe tunazungumza na watu wa fami-
lia yetu, wafanyakazi wenzetu, ndugu na dada

151
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kwa nini unyoofu ni jambo muhimu kwa Yehova, na jinsi


unavyoweza kuwa mnyoofu katika hali mbalimbali maishani.

4. Unyoofu humfurahisha
Yehova
Soma Zaburi 44:21 na Malaki 3:16,
kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kwa nini si jambo la hekima kufikiri
kwamba tunaweza kuficha ukweli?
˙ Unafikiri Yehova anahisije tunapoamua
kusema ukweli, hata inapokuwa vigumu
kufanya hivyo?

Watoto wanaposema ukweli wanawafurahisha wazazi wao.


Tunaposema ukweli tunamfurahisha Yehova

(
5. Tenda kwa unyoofu nyakati zote
Watu wengi hufikiri kwamba haiwezekani kuwa mnyoofu
VIDEO: Ni Mambo Gani
nyakati zote. Hata hivyo, chunguza kwa nini tunapaswa
Yanayoleta Shangwe? kuwa wanyoofu kila wakati. Onyesha VIDEO.
—Dhamiri Safi (2:32) Soma Waebrania 13:18, kisha mzungumzie jinsi
tunavyoweza kuwa wanyoofu . . .
˙ katika familia.
˙ kazini au shuleni.
˙ katika hali nyingine.
6. Tunanufaika tunapokuwa
wanyoofu
Nyakati nyingine tunaweza kupatwa na matatizo
kwa sababu ya kuwa wanyoofu. Lakini ukweli ni kwa-
mba tutanufaika tunapokuwa wanyoofu sikuzote.
Soma Zaburi 34:12-16, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Unyoofu unaweza kukusaidiaje kuwa na
maisha bora?

Wafanyakazi wanyoofu
huaminiwa na waajiri wao

Waume na wake wanyoofu


huimarisha ndoa zao

Raia wanyoofu huheshimiwa


na maofisa wa serikali

WATU FULANI HUSEMA: “Uwongo mdogo ni jambo la kawaida.”


˙ Kwa nini unaamini kwamba Yehova anachukia uwongo wa kila aina?

153
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova anataka rafiki zake wawe
wanyoofu katika mambo yote ( 1:44 Wazazi wanaweza kuwasaidiaje
wanayosema na kutenda. watoto wao wawe wanyoofu?
Sema Kweli

Ungejibuje?
˙ Tunaweza kuwa wanyoofu
katika njia gani?
˙ Kwa nini si jambo la hekima
kufikiri kwamba tunaweza
kuficha ukweli? ( 9:09 Tunapata manufaa gani
tunapotimiza ahadi zetu?
˙ Kwa nini ungependa kuwa
mnyoofu nyakati zote? Timiza Ahadi, Upate Baraka

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza kwa nini tuna-


paswa kulipa kodi hata
kama zinatumiwa vibaya.
“Je, Ni Lazima Ulipe Kodi?”
Lengo (Mnara wa Mlinzi, Septemba 1,
2011)
N Jiulize hivi, ‘Je, Yehova ananio-
na kuwa mtu mnyoofu?’ Unahi-
taji kuwa mnyoofu zaidi katika
mambo gani?
Nini kilichomchochea mwana-
N Lengo lingine: mume fulani asiye mnyoofu
abadili maisha yake?
“Nilijifunza Kwamba
Yehova Ni Mwenye Rehema
na Mwenye Kusamehe”
(Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 2015)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 36, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
37

Maoni ya Biblia
Kuhusu Pesa na Kazi
Je, umewahi kulemewa na mahangaiko kuhu- na vitu tulivyo navyo, tunaepuka mahangaiko
su kazi au pesa? Huenda ikawa vigumu kushu- ya kutafuta vitu vingi zaidi. Tunaepuka madeni
ghulikia mahitaji yetu na wakati huohuo kumto- yasiyo ya lazima. (Methali 22:7) Na tunaepuka
lea Yehova ibada anayostahili. Biblia inatupatia hatari ya kucheza kamari au kunaswa na njia za
ushauri unaoweza kutusaidia. kupata utajiri wa haraka.

1. Biblia inasema nini kuhusu kazi? 3. Tunawezaje kutumia pesa zetu kwa ukarimu?
Mungu anataka tufurahie kazi yetu. Biblia ina- Yehova ni Mungu mkarimu na tunamwiga tu-
sema hivi: “Hakuna jambo bora analoweza napokuwa “wakarimu, tayari kushiriki vitu na
kufanya mtu kuliko . . . kufurahia kazi yake wengine.” (1 Timotheo 6:18) Tunaweza kutumia
ngumu.” (Mhubiri 2:24) Yehova ni mfanyakazi pesa zetu kwa ukarimu kwa kutoa michango ka-
mwenye bidii. Tunapomwiga kwa kufanya kazi tika kutaniko na kuwasaidia watu wengine wa-
kwa bidii, tunamfurahisha na tunaridhika. naohitaji msaada, hasa waabudu wenzetu. Ye-
Kufanya kazi ni muhimu. Lakini hatupaswi ka- hova anapendezwa hasa na nia yetu ya kutoa,
mwe kuruhusu kazi iwe muhimu kuliko ibada bali si kiasi tunachotoa. Tunapotoa kwa ukarimu
yetu kwa Yehova. (Yohana 6:27) Yehova anatua- kutoka moyoni, tunakuwa na furaha na tuna-
hidi kwamba tukimtanguliza, atatuandalia ma- mfurahisha Yehova.—Soma Matendo 20:35.
hitaji yetu ya kimwili.

2. Biblia inasema nini kuhusu pesa?


Biblia inasema ‘pesa ni ulinzi,’ lakini pia inatuo-
nya kwamba pesa peke yake haziwezi kutule-
tea furaha. (Mhubiri 7:12) Basi tunatiwa moyo
tusipende pesa bali ‘turidhike na vitu tulivyo
navyo.’ (Soma Waebrania 13:5.) Tunaporidhika

155
CH I M BA ZAI DI

Jifunze manufaa ya kuwa na mtazamo uliosawazika


kuhusu kazi na jinsi ya kuridhika.

4. Mheshimu Yehova kupitia (


mazoea yako ya kufanya kazi
Urafiki wetu na Yehova unapaswa kutuchochea kuwa VIDEO: Fanya Kazi kwa
na mtazamo unaofaa kuhusu kazi. Onyesha VIDEO, Nafsi Yote Kwa Ajili ya
kisha mzungumzie maswali yanayofuata. Yehova (4:39)

˙ Katika video hiyo, ulifurahia nini kuhusu mtazamo


wa Jason na mwenendo wake kazini?
˙ Jason alifanya nini ili kuwa na usawaziko kuhusu kazi?

Soma Wakolosai 3:23, 24, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Kwa nini ni muhimu kuwa na mtazamo unaofaa kuhusu kazi?

Kufanya kazi ni muhimu. Lakini hatupaswi kamwe kuruhusu kazi iwe muhimu kuliko ibada yetu kwa Yehova
5. Tunanufaika tunaporidhika 6. Yehova
Watu wengi hujitahidi kutafuta pesa nyingi iwezekanavyo.
atatuandalia
Lakini Biblia inatoa ushauri tofauti. Soma 1 Timotheo 6:6-8, mahitaji yetu
kisha mzungumzie swali hili:
Inapokuwa vigumu kupata kazi au
˙ Biblia inatutia moyo tufanye nini? pesa, tunapata nafasi ya kuonye-
sha kama kweli tunamtegemea Ye-
Tunaweza kuwa na furaha hata tukiwa na vitu vichache sana. hova. Onyesha VIDEO ili kuona
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata. jinsi tunavyoweza kukabiliana na
matatizo ya kifedha, kisha mzu-
( VIDEO: “Ridhika na Vitu vya Sasa” ngumzie maswali yanayofuata.
(3:20)
(

˙ Ingawa familia hizo hazina pesa nyingi, kwa nini


wana furaha? VIDEO: Yehova Atatutimizia
Mahitaji Yetu (6:31)
Namna gani ikiwa tuna vitu vingi na bado tunatamani
kupata vingi zaidi? Yesu alitoa mfano unaoonyesha hatari
ya kufanya hivyo. Soma Luka 12:15-21, kisha mzungumzie ˙ Katika video hiyo, ndugu
swali hili: huyo alikabili changamoto
˙ Umejifunza nini kutokana na mfano wa Yesu? gani?
—Ona mstari wa 15. ˙ Alifanya nini ili kukabiliana
na changamoto hizo?
Soma na ulinganishe Methali 10:22 na 1 Timotheo 6:10.
Kisha mzungumzie maswali haya: Soma Mathayo 6:25-34,
˙ Unafikiri ni jambo gani lililo muhimu zaidi? Kuwa rafiki kisha mzungumzie swali hili:
ya Yehova, au kuwa na pesa nyingi sana? Kwa nini? ˙ Yehova amewaahidi nini
˙ Ni matatizo gani yanayosababishwa na kutafuta wale wanaomtanguliza?
pesa nyingi zaidi?

WATU FULANI HUSEMA: “Lazima nifanye kazi kwa bidii ili kuiandalia
familia yangu. Siwezi kuhudhuria mikutano ya kutaniko kila juma.”
˙ Ni andiko gani linalokuthibitishia kwamba kutanguliza ibada yako
kwa Yehova ndio uamuzi bora?
157
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Tunahitaji kazi na pesa lakini
mambo hayo hayapaswi kamwe Chunguza uone kama
kutuzuia kumtumikia Yehova. Biblia inafundisha kwamba
ni vibaya kuwa na pesa.
“Je, Pesa Ndio Chanzo cha
Ungejibuje? Uovu Wote?” (Makala iliyo
kwenye mtandao)
˙ Ni nini kinachoweza kukusaidia
uwe na usawaziko kuhusu kazi?
˙ Kuridhika kunaweza kukunufai-
shaje?
˙ Unaweza kuonyeshaje kwamba Jifunze jinsi tunavyoweza
kutumia pesa zetu kwa njia
unaamini ahadi ya Yehova ya ku-
inayomfurahisha Mungu.
waandalia mahitaji watu wake?
“Biblia Inasema Nini Kuhusu
Kutoa?” (Makala iliyo kwenye
mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Je, kucheza kamari


kuna madhara yoyote?
“Maoni ya Biblia
—Kucheza Kamari”
Lengo (Amkeni!, Machi 2015)

N Chunguza uone ikiwa kazi yako


imefanya ukose kuhudhuria
mikutano kwa ukawaida katika
miezi michache iliyopita. Ikiwa
ndivyo, chukua hatua ili ureke- Ona jambo lililomchochea mtu
bishe hali hiyo. aliyekuwa mwizi na mcheza-
kamari abadili maisha yake.
N Lengo lingine: “Nilipenda Sana Mashindano
ya Farasi” (Mnara wa Mlinzi,
Novemba 1, 2011)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 37, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
38

Thamini Zawadi ya Uhai


Tunaweza kufurahia kufanya mambo mengi kwa hova. (Soma Mathayo 10:29-31.) Yehova hu-
sababu tuko hai. Hata tunapokabili matatizo, huzunika sana mtu anaposababisha kimakusu-
bado kuna mambo tunayoweza kufurahia mai- di kifo cha mtu mwingine, au hata kifo chake
shani. Tunawezaje kumwonyesha Yehova kwa- mwenyewe. (Kutoka 20:13) Yehova huhuzunika
mba tunathamini zawadi ya uhai? Na ni saba- pia tunapohatarisha uhai wetu isivyo lazima au
bu gani muhimu zaidi inayotuchochea kufanya tunapokosa kuchukua tahadhari ili kulinda uhai
hivyo? wa wengine. Tunapolinda uhai wetu na kuheshi-
mu uhai wa watu wengine, tunaonyesha kwa-
1. Kwa nini tunapaswa kuuthamini uhai? mba tunathamini zawadi bora ya uhai.
Tunapaswa kuuthamini uhai kwa sababu ni za-
wadi kutoka kwa Baba yetu mwenye upendo, Ye-  Yehova anawajali sana watu waliovunjika moyo.
(Zaburi 34:18) Anaelewa hisia zenye kuhuzunisha ambazo hu-
hova. Yeye “ndiye chanzo cha uhai,” yaani, aliu- fanya watu fulani watamani kujiua, na anataka kuwasaidia. Ili
mba kila kitu kilicho hai. (Zaburi 36:9) “Yeye kuona jinsi anavyowasaidia watu washinde hisia hizo, soma
makala “Ninataka Kufa—Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ikiwa Ni-
mwenyewe huwapa watu wote uhai na pumzi nawazia Kujiua?” iliyo kwenye sehemu ya Chunguza Zaidi kati-
na vitu vyote.” (Matendo 17:25, 28) Yehova ka somo hili.
anatupatia vitu tunavyohitaji ili kuendelea kuwa
hai. Zaidi ya hilo, amehakikisha kwamba tuna-
weza kufurahia maisha.—Soma Matendo 14:17.

2. Tunawezaje kumwonyesha Yehova kwamba


tunathamini zawadi ya uhai?
Tangu ulipokuwa tumboni kabla hujazaliwa, Ye-
hova alikutunza. Katika Biblia, Daudi mtumishi
wa Yehova alisali hivi: “Macho yako hata ya-
liniona nikiwa kiinitete.” (Zaburi 139:16) Uhai
wako ni wenye thamani kubwa machoni pa Ye-

159
CH I M BA ZAI DI

Jifunze baadhi ya njia unazoweza kuonyesha


kwamba unathamini zawadi ya uhai.

3. Tunza afya yako


Wakristo waliojiweka wakfu hutumia maisha
yao yote kumtumikia Yehova. Ni kana kwamba
wameitoa miili yao iwe dhabihu kwa Mungu.
Soma Waroma 12:1, 2, kisha mzungumzie
maswali haya:
˙ Ni nini kinachopaswa kukuchochea
utunze afya yako?
˙ Unaweza kufanya hivyo kwa njia gani?

4. Chukua tahadhari ili kuwalinda


wengine wasijeruhiwe au kufa
Biblia inatutia moyo tuepuke kufanya mambo
ambayo ni hatari. Onyesha VIDEO ili ujifunze
baadhi ya njia za kudumisha usalama.

( VIDEO: Zingatia Usalama (8:34)

Soma Methali 22:3, kisha mzungumzie jinsi unavyoweza


kulinda usalama wako na wa watu wengine . . .
˙ unapokuwa nyumbani.
˙ unapokuwa kazini.
˙ wakati wa michezo.
˙ unapoendesha au kusafiri
katika chombo cha usafiri.
5. Heshimu uhai wa mtoto
ambaye hajazaliwa
Daudi alifafanua jinsi Yehova anavyopendezwa na ukuzi wa
mtoto katika tumbo la mama yake. Soma Zaburi 139:13-17,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kulingana na maoni ya Yehova, je, uhai wa mtu huanza
mimba inapotungwa au mtoto anapozaliwa?

Sheria ambazo Yehova aliwapa Waisraeli wa kale ziliwalinda


akina mama na watoto wao ambao hawajazaliwa. Soma
Kutoka 21:22, 23, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Yehova alimwonaje mtu aliyesababisha bila kukusudia
kifo cha mtoto ambaye hajazaliwa?
˙ Yehova atahisije ikiwa mtu atafanya hivyo kimakusudi? 
˙ Unaonaje maoni ya Mungu kuhusu jambo hilo?

Onyesha VIDEO.
Hata mwanamke anayethamini uhai huenda
akahisi kwamba hali zinamlazimu kutoa mimba.
Soma Isaya 41:10, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Ikiwa mwanamke anakabili mkazo wa kutoa mimba
anapaswa kutafuta msaada kwa nani? Kwa nini?

 Wale ambao wamewahi kutoa mimba hawapaswi kulemewa na hisia za hatia,


Yehova anaweza kuwasamehe. Ili kupata habari zaidi, soma makala “Biblia Inase-
ma Nini Kuhusu Kutoa Mimba?” iliyo kwenye sehemu ya Chunguza Zaidi katika
somo hili.

VIDEO: Thamini Uhai Kama


Yehova Anavyouthamini (5:00)

WATU FULANI HUSEMA: “Mwanamke ana haki ya kutoa mimba kwa sababu ni mwili wake.”
˙ Ni nini kinachokusadikishia kwamba Yehova anathamini uhai wa mama na mtoto ambaye
bado hajazaliwa?

161
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Biblia inatufundisha kwamba tunapa-
swa kupenda, kuheshimu, na kulinda ( 2:41 Tunawezaje kumshukuru
zawadi ya uhai ambayo Yehova ame- Yehova kwa zawadi ya uhai?
tupatia. Hilo linatia ndani uhai wetu Wimbo 141—Muujiza wa Uhai
na uhai wa watu wengine.

Ungejibuje?
˙ Kwa nini uhai wa mwanadamu
ni wenye thamani machoni
pa Yehova? Ona jibu la swali hili, Je, Mungu
˙ Yehova anahisije mtu anapo- anaweza kumsamehe mwana-
sababisha kimakusudi kifo mke ambaye amewahi kutoa
cha mwanadamu? mimba?
“Biblia Inasema Nini Kuhusu
˙ Ni nini ambacho unathamini
Kutoa Mimba?” (Makala iliyo
kuhusu zawadi ya uhai?
kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Jifunze jinsi maoni ya Mungu


kuhusu uhai yanavyopaswa
kutuongoza tunapochagua
burudani.
Lengo “ ‘Michezo Hatari’
—Je, Ujihatarishe?”
N Chunguza njia moja ambayo (Amkeni!, Oktoba 8, 2000)
unaweza kulinda afya yako.

N Lengo lingine:
Namna gani ikiwa mtu
anafikiria kujiua? Ona jinsi
Biblia inavyoweza kumsaidia.
“Ninataka Kufa—Je, Biblia
Inaweza Kunisaidia Ikiwa
Ninawazia Kujiua?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 38, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
39

Maoni ya Mungu Kuhusu Damu


Damu ni muhimu sana. Bila damu hatuwezi kue- ka, hungekubali. Vivyo hivyo, amri ya Mungu
ndelea kuwa hai. Akiwa Muumba wetu, Mungu kwamba tujiepushe na damu inamaanisha ha-
ana haki ya kuweka sheria kuhusu damu. Ame- tupaswi kula au kunywa damu, wala kula nya-
toa maagizo gani kuhusu damu? Je, tunaweza ma ya mnyama ambaye hajatolewa damu. Wala
kula damu au kutiwa mishipani? Na unawezaje hatupaswi kula chakula ambacho kimechanga-
kufanya maamuzi mazuri kuhusu damu? nywa na damu.
Namna gani kutumia damu katika matibabu?
1. Yehova ana maoni gani kuhusu damu?
Baadhi ya matibabu yanavunja sheria za Mungu
Nyakati za kale, Yehova aliwaambia hivi waa- moja kwa moja. Matibabu hayo yanatia nda-
budu wake: “Uhai wa kila kiumbe umo katika ni kutiwa damu mishipani. Iwe ni damu nzima
damu yake.” (Mambo ya Walawi 17:14) Kulinga- au sehemu kuu za damu, yaani, chembe nyeku-
na na maoni ya Yehova, damu inawakilisha uhai. ndu, chembe nyeupe, vigandisha-damu, na pla-
Kwa kuwa uhai ni zawadi takatifu kutoka kwa zima. Kuhusu matibabu fulani, huenda isioneka-
Mungu, basi pia damu ni takatifu. ne wazi kama yanavunja sheria ya Mungu au la.
2. Mungu anakataza matumizi gani ya damu? Baadhi ya matibabu hayo yanahusisha kutumia
visehemu vilivyotolewa kwenye mojawapo ya
Kabla ya Ukristo, Yehova aliwaamuru waabu- sehemu kuu za damu. Na matibabu mengine ya-
du wake wasile damu. (Soma Mwanzo 9:4 na nahusisha matumizi ya damu ya mgonjwa mwe-
Mambo ya Walawi 17:10.) Baadaye, kupitia ba- nyewe. Tunapofikiria matibabu hayo, kila mmoja
raza linaloongoza aliwaagiza Wakristo ‘wae- wetu anapaswa kufanya uamuzi wake mwenye-
ndelee kujiepusha na damu.’—Soma Matendo we.—Wagalatia 6:5.
15:28, 29.
Kujiepusha na damu kunamaanisha nini? Iki-  Ona Somo la 35, “Jinsi ya Kufanya Maamuzi Mazuri.”
wa daktari angekuambia ujiepushe na pombe,
ungeacha kunywa pombe. Hata hivyo, je, unge-
kula chakula kilichochanganywa na pombe, au
ungekubali kutiwa pombe mishipani? Bila sha-

163
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi ya kufanya maamuzi kuhusu


matibabu yanayohusisha damu.

3. Fanya maamuzi
yanayomfurahisha
Yehova kuhusu
matibabu
Unawezaje kufanya maamuzi ya matibabu ya-
nayopatana na maoni ya Mungu kuhusu damu?
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie umuhimu
wa kufuata hatua zinazoonyeshwa hapa.

( VIDEO: Jinsi ya Kufanya


Maamuzi ya Matibabu
4. Mashahidi wa Yehova
Yanayohusisha Damu (5:47) hutafuta matibabu bora
Inawezekana kutii sheria ya Mungu kuhusu
˙ Sali ili upate hekima.—Yakobo 1:5 damu na wakati huohuo kupata matibabu
˙ Fanya utafiti kuhusu kanuni za Biblia bora yasiyohusisha damu. Onyesha VIDEO.
na jinsi ya kuzitumia.—Methali 13:16.
˙ Chunguza matibabu mbalimbali ( VIDEO: Mahojiano na Profesa
yanayopatikana katika eneo lenu. Masimo P. Franchi M.D.
(1:36)
˙ Amua matibabu ambayo huwezi
kamwe kuyakubali.
˙ Hakikisha kwamba utabaki na dhamiri Soma Tito 3:2, kisha mzungumzie swali hili:
safi baada ya kufanya uamuzi. ˙ Kwa nini tunapaswa kuzungumza na
—Matendo 24:16. madaktari kwa heshima na upole?
˙ Tambua kwamba hakuna mtu anayepaswa
kukufanyia uamuzi kuhusu mambo yanayo-
husisha dhamiri, iwe ni mwenzi wako wa
ndoa, mzee wa kutaniko, au mwalimu
wako wa Biblia.—Waroma 14:12.
˙ Andika uamuzi wako.

 Ona jambo kuu la 5, “Matibabu Yanayohusisha Visehemu


vya Damu” na Maelezo ya Ziada 3, “Matibabu Yanayohusisha
Damu.”
Matibabu yasiyokubalika Mkristo atajifanyia uamuzi

Plazima ya damu . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Visehemu


vya plazima
Chembe nyeupe . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Visehemu
vya chembe nyeupe
Vigandisha-damu . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Visehemu
vya vigandisha-damu
Chembe nyekundu . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Visehemu
vya chembe nyekundu

5. Matibabu yanayohusisha
visehemu vya damu Inapohusu visehemu vya damu, kila Mkristo ana-
paswa kujifanyia uamuzi wake mwenyewe unaote-
Damu ina sehemu kuu nne—chembe nyekundu, gemea dhamiri yake iliyozoezwa na Biblia. Huenda
chembe nyeupe, vigandisha-damu, na plazima. baadhi ya Wakristo wakakataa matibabu au mbinu
Sehemu hizo zina sehemu nyingine ndogo zaidi za matibabu zinazohusisha visehemu vya damu.
zinazoitwa visehemu vya damu. Baadhi ya vise- Na wengine wanaweza kuhisi kwamba dhamiri
hemu hivyo huongezwa katika dawa zinazotumiwa zao zinawaruhusu kukubali visehemu vya damu.
kutibu magonjwa au kuzuia kuvuja kwa damu.
Unapofanya maamuzi yako, fikiria swali hili:
 Baadhi ya madaktari huona sehemu nne kuu za damu kuwa ˙ Ninawezaje kumweleza daktari sababu
visehemu vya damu. Kwa hiyo, unapaswa kuhakikisha daktari
anaelewa uamuzi wako kwamba hutakubali kutiwa mishipani yangu ya kukubali au kukataa matumizi
damu nzima, chembe nyekundu, chembe nyeupe, vigandisha- ya visehemu fulani vya damu?
damu, au plazima.

HUENDA MTU AKAULIZA: “Kuna ubaya gani kuongezwa damu mwilini?”


˙ Wewe una maoni gani?

165
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova anataka tuione damu
kuwa takatifu. Unapaswa kufikiria mambo
gani unapofanya maamuzi
ya matibabu yanayohusisha
Ungejibuje? damu yako mwenyewe?
“Maswali Kutoka kwa
˙ Kwa nini Yehova anaiona Wasomaji” (Mnara wa Mlinzi,
damu kuwa takatifu? Oktoba 15, 2000)
˙ Tunajuaje kwamba amri
ya Mungu ya kujiepusha na
damu inahusisha kuepuka
kutiwa damu mishipani? Unapaswa kuzingatia mambo
gani unapoamua ikiwa utaku-
˙ Unawezaje kufanya maamuzi
bali visehemu vya damu?
mazuri kuhusu matibabu yana-
yohusisha damu? “Maswali Kutoka kwa
Wasomaji” (Mnara wa Mlinzi,
Juni 15, 2004)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Ni nini kilichomfanya daktari


fulani aamini kwamba maoni ya
Yehova kuhusu damu yanafaa?
“Nilikubali Maoni ya Mungu
Lengo Kuhusu Damu” (Amkeni!,
Desemba 8, 2003)
N Tumia makala zilizo kwenye
sehemu ya Chunguza Zaidi
unapofanya maamuzi kuhusu
(1) kutiwa damu mishipani,
(2) dawa zilizochanganywa na ( 10:23 Jifunze jinsi wazee walio kwe-
visehemu vya damu, na (3) ma- nye Halmashauri za Uhusiano
na Hospitali wanavyowasaidia
tumizi ya damu yako mwenyewe
ndugu na dada zao.
wakati wa matibabu. Kisha
uandike maamuzi yako. Yehova Huwategemeza
Wagonjwa
N Lengo lingine:

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 39, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
40

Tunawezaje Kuwa Safi


Machoni pa Mungu?
Wazia mama anayemtayarisha mtoto wake paswa kumfurahisha Yehova, basi tunajitahidi
mdogo ili aende shuleni. Anahakikisha kwamba kabisa kuepuka mawazo yasiyofaa. (Zaburi
mtoto ameoga na nguo zake ni safi. Kufanya hi- 104:34) Pia, tunajitahidi kuepuka maneno ma-
vyo kunamsaidia mtoto wake awe na afya nzu- chafu.—Soma Wakolosai 3:8.
ri na watu wengine wanaona kwamba wazazi Ni nini kingine kinachoweza kutuchafua kimwi-
wake wanamtunza vizuri. Vivyo hivyo, Baba yetu li au kiadili? Kuna vitu vinavyoweza kuchafua
mwenye upendo Yehova, anataka tuwe safi ki- mwili wetu. Kwa hiyo, tunaepuka kuvuta siga-
mwili na kiadili. Tunapokuwa safi, tunanufaika ra, kutumia tumbaku, kutafuna miraa au miru-
na tunamletea utukufu. ngi, na kutumia dawa za kulevya. Tunapoepuka
vitu hivyo, tunakuwa na afya bora na tunao-
1. Tunawezaje kuwa safi kimwili?
nyesha kwamba tunaheshimu zawadi ya uhai.
Yehova anatuambia hivi: “Lazima muwe wa- Pia, tunajitahidi kuwa na maadili safi kwa kue-
takatifu.” (1 Petro 1:16) Kuwa watakatifu ku- puka mazoea machafu kama vile kupiga pu-
nahusisha kuwa safi kimwili na kiadili. Tunawe- nyeto na kutazama ponografia. (Zaburi 119:37;
za kuwa safi kimwili kwa kuoga kwa ukawaida na Waefeso 5:5) Inaweza kuwa vigumu kushinda
kudumisha nguo, nyumba, na magari yetu yaki- mazoea hayo, lakini Yehova anaweza kutusaidia
wa safi. Pia, tunaweza kusaidia kufanya usafi kuyashinda.—Soma Isaya 41:13.
katika Jumba letu la Ufalme. Tunapodumisha
usafi wa kimwili tunamletea Yehova utukufu.
—2 Wakorintho 6:3, 4.

2. Ili tuwe safi, tunapaswa kuepuka


mazoea gani?
Biblia inatuhimiza “tujisafishe kila unajisi wa
mwili na roho.” (2 Wakorintho 7:1) Hivyo, tu-
najitahidi kuepuka jambo lolote linaloweza ku-
chafua mwili au akili zetu. Mawazo yetu yana-

167
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi tunavyoweza kumheshimu


Yehova kwa kuwa safi kimwili, na jinsi
tunavyoweza kushinda mazoea machafu.

3. Usafi wa kimwili
unamtukuza Yehova
Tunaweza kuelewa maoni ya Yehova
kuhusu usafi kwa kuchunguza amri
alizowapa Waisraeli wa kale. Soma Yehova anaweza kutusaidia
Kutoka 19:10 na 30:17-19, kisha kushinda zoea lolote baya
mzungumzie maswali haya:
˙ Kulingana na mistari hii, Yehova
ana maoni gani kuhusu usafi wa 4. Shinda mazoea mabaya
kimwili?
˙ Ni mazoea gani yatakayokusaidia Ikiwa wewe ni mraibu wa kuvuta sigara au kutumia
kudumisha usafi wa kimwili? dawa za kulevya, huenda unaelewa jinsi ilivyo vigumu
kushinda mazoea hayo. Ni nini ambacho kitakusaidia?
Tunahitaji muda na jitihada ili kudu- Fikiria madhara unayopata kutokana na mazoea hayo.
misha usafi wa kimwili. Hata hivyo, Soma Mathayo 22:37-39, kisha mzungumzie jinsi kuvuta
tunaweza kudumisha usafi mahali sigara au kutumia dawa za kulevya kunavyoathiri . . .
popote tunapoishi iwe sisi ni maskini ˙ urafiki wa mtu na Yehova.
au matajiri. Onyesha VIDEO, kisha
˙ familia ya mtu huyo na watu wanaomzunguka.
mzungumzie swali linalofuata.
Chukua hatua ambazo zitakusaidia kushinda mazoea
( mabaya. Onyesha VIDEO.

( VIDEO: Kuonyesha Sifa ya Kujizuia


VIDEO: Mungu Anawapenda Watu
(2:47)
Walio Safi (4:10)

˙ Watu tunaowahubiria wanawezaje Soma Wafilipi 4:13, kisha mzungumzie swali hili:
kumheshimu Yehova ikiwa tuna- ˙ Kuwa na mazoea mazuri ya kusali, kujifunza Biblia,
tumia vifaa safi na nadhifu? na kuhudhuria mikutano kunawezaje kumsaidia mtu
apate nguvu za kushinda mazoea mabaya?

 Gazeti lenye kichwa “Jinsi ya Kuacha Kuvuta Sigara,” lililo kwenye se-
hemu ya Chunguza Zaidi katika somo hili, linaeleza hatua ambazo mtu
anapaswa kuchukua ili kushinda uraibu.
5. Jitahidi kushinda mawazo
na mazoea machafu
(
Soma Wakolosai 3:5, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Tunajuaje kwamba kutazama ponografia, kutuma ujumbe
au picha za ngono, na kupiga punyeto ni mazoea machafu VIDEO: Chukua Hatua ili
machoni pa Yehova? Uendelee Kuwa Safi (1:51)
˙ Je, inawezekana kufuata sheria za Yehova kuhusu usafi wa
maadili? Kwa nini?

Jifunze jinsi ya kushinda mawazo machafu. Usife moyo, endelea


Onyesha VIDEO. kupambana!
Huenda ukajiambia hivi, ‘Nimeshi-
Yesu alitoa mfano unaoonyesha kwamba tunapaswa
ndwa, hakuna haja ya kuendelea
kuchukua hatua thabiti ili tuendelee kudumisha maadili safi. kupambana.’ Lakini fikiria jambo
Soma Mathayo 5:29, 30, kisha mzungumzie swali hili: hili: Mkimbiaji anapoanguka
˙ Ingawa Yesu hakumaanisha tunapaswa kujisababishia ma- haimaanishi kwamba hawezi
kuendelea na mbio hizo, pia
jeraha ya kimwili, alionyesha kwamba tunapaswa kuchukua
haimaanishi kwamba anapaswa
hatua fulani. Mtu anapaswa kuchukua hatua gani thabiti ili
kurudi nyuma na kuanza tena.
kuepuka mawazo machafu?  Vivyo hivyo, hata unapolemewa
na kurudia zoea hilo, haimaanishi
Ikiwa unapambana ili kushinda mawazo machafu, kwamba huwezi kulishinda. Wala
Yehova anathamini jitihada zako. Soma Zaburi 103:13, 14, haimaanishi kwamba jitihada uli-
kisha mzungumzie swali hili: zofanya ni za bure. Ni jambo la
kawaida kujikwaa. Lakini usife
˙ Ikiwa unapambana na zoea chafu, andiko hili linawezaje moyo! Kwa msaada wa Yehova,
kukusaidia uendelee kupambana? unaweza kushinda zoea baya.
 Ili kupata msaada wa kushinda zoea la kupiga punyeto, ona “Ninaweza
Kushinda Jinsi Gani Mazoea ya Kupiga Punyeto?” katika kitabu Maswali
Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1, sura ya 25.

WATU FULANI HUSEMA: “Mimi ni mraibu. Siwezi kuacha.”


˙ Unaweza kutumia andiko gani kumsaidia mtu huyo aone kwamba
Yehova anaweza kumsaidia aache zoea baya?

169
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Tunamfurahisha Yehova tunapodumi-
sha mwili, mawazo, na mwenendo ( 3:01 Ni mambo gani rahisi una-
wetu ukiwa safi. yoweza kufanya ili kudumisha
usafi wa kimwili hata kama
huna vitu vingi vya kimwili?
Ungejibuje? Usafi na Afya—Kunawa
Mikono
˙ Kwa nini ni muhimu sana
kudumisha usafi?
˙ Unawezaje kudumisha usafi
wa kimwili?
˙ Unawezaje kudumisha mawazo Ona hatua unazoweza kuchu-
kua ili uache kuvuta sigara.
na mwenendo wako ukiwa safi?
“Jinsi ya Kuacha Kuvuta
Sigara” (Amkeni!, Mei 2010)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza madhara ya


kutazama ponografia.
“Ponografia
—Je, Ina Madhara?”
Lengo (Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 2013)

N Mwombe Yehova akusaidie uta-


mbue sehemu fulani ya maisha
yako unayohitaji kuboresha ili
uwe safi.
Ona jinsi mwanamume
N Lengo lingine: fulani alivyoshinda zoea
la kutazama ponografia.
“Nilishindwa Mara
Nyingi Kabla ya Kushinda”
(Mnara wa Mlinzi Na. 4 2016)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 40, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
41

Biblia Inasema Nini


Kuhusu Ngono?
Watu wengi hawapendi kuzungumza kuhusu 2. Uasherati ni nini?
ngono. Hata hivyo, Biblia inazungumza kuhusu Biblia inatuambia kwamba “waasherati . . .
ngono kwa njia iliyo wazi na ya heshima. Tuna- hawataurithi Ufalme wa Mungu.” (1 Wakori-
nufaika na mambo ambayo Biblia inasema, na ntho 6:9, 10) Waandikaji wa Biblia walioandika
tunatarajia iwe hivyo kwa sababu Yehova ndiye kwa lugha ya Kigiriki, walitumia neno por·neia
Muumba wetu. Basi anajua mambo yanayotufaa kumaanisha uasherati. Neno hilo linatia ndani
kabisa. Anatuambia mambo tunayopaswa kufa- (1) kufanya ngono na mtu ambaye si mume
nya ili kumfurahisha, na mambo yatakayotusai- au mke wako, (2) ngono kati ya watu wa jinsia
dia kufurahia maisha milele. moja, na (3) kufanya ngono na mnyama. ‘Tuna-
pojiepusha na uasherati,’ tunanufaika na pia tu-
1. Yehova ana maoni gani kuhusu ngono?
namfurahisha Yehova.—1 Wathesalonike 4:3.
Ngono ni zawadi kutoka kwa Yehova. Anataka
mwanamume na mwanamke waliofunga ndoa  Vitendo hivyo vya ngono visivyo halali vinatia ndani mambo
mbalimbali kama vile kufanya ngono kwa mdomo, ngono ya
wafurahie zawadi hiyo. Zawadi hiyo inasaidia mkundu, kupapasa viungo vya uzazi vya mtu mwingine ili kua-
mume na mke kupata watoto, na pia kuonye- msha hamu ya ngono, na ngono kati ya mwanamume na mwa-
shana upendo mwororo kwa njia ya asili na ye- namke ambao hawajafunga ndoa.
nye kufurahisha. Ndiyo sababu Neno la Mu-
ngu linasema hivi: “Na ushangilie pamoja na
mke wa ujana wako.” (Methali 5:18, 19) Yehova
anatarajia Mkristo aliyefunga ndoa awe mshika-
manifu kwa mwenzi wake wa ndoa. Hivyo, we-
nzi wa ndoa hawapaswi kamwe kufanya uzinzi.
—Soma Waebrania 13:4.

171
CH I M BA ZAI DI

Chunguza jinsi unavyoweza kuepuka


uasherati na jinsi utakavyonufaika
kwa kudumisha maadili safi.

3. Ukimbieni uasherati 4. Unaweza kupinga


vishawishi
Mwanamume mwaminifu Yosefu alikataa
kufanya uasherati aliposhawishiwa kufanya Ni nini kinachoweza kufanya iwe vigumu
ngono na mke wa mtu mwingine. Soma Mwanzo kupinga kishawishi cha kufanya uasherati?
39:1-12, kisha mzungumzie maswali haya: Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali
˙ Ni sababu gani iliyofanya Yosefu akimbie? linalofuata.
—Ona mstari wa 9.
˙ Je, unafikiri Yosefu alifanya uamuzi ( VIDEO: Shinda Vishawishi
kwa Kusoma Biblia (3:02)
unaofaa? Kwa nini?

Leo, vijana wanawezaje kumwiga Yosefu na


kukimbia uasherati? Onyesha VIDEO. ˙ Ndugu katika video hiyo alifanya nini
alipotambua kwamba mawazo na matendo
VIDEO: Ukimbie Uasherati
yake yangefanya akose kuwa mwaminifu
(
(5:14) kwa mke wake?

Wakati mwingine, hata Wakristo waaminifu


hupambana ili kudumisha mawazo safi.
Yehova anataka sisi sote tujiepushe na Unawezaje kuacha kufikiria mawazo machafu?
uasherati. Soma 1 Wakorintho 6:18, Soma Wafilipi 4:8, kisha mzungumzie maswali
kisha mzungumzie maswali haya: haya:
˙ Ni hali gani ambazo zinaweza kufanya ˙ Tunapaswa kufikiria mambo gani?
mtu ashawishike kufanya uasherati?
˙ Kusoma Biblia na kuwa na shughuli nyingi
˙ Unawezaje kuukimbia uasherati? katika utumishi wa Yehova, kunawezaje ku-
tusaidia kupinga vishawishi vya kutenda
dhambi?
5. Viwango vya Yehova Baadhi ya watu wanafikiri kwamba mambo amba-
yo Biblia inafundisha kuhusu ngono kati ya watu
hutunufaisha wa jinsia moja, si jambo la upendo kuwaelekea
watu hao. Lakini Yehova ni Mungu mwenye
Yehova anajua mambo yanayotufaa kabisa.
upendo na anataka watu wote wafurahie maisha
Anatufundisha jinsi ya kudumisha maadili safi na
milele. Ili tustahili kuishi milele, lazima tufuate
manufaa ya kufanya hivyo. Soma Methali 7:7-27
viwango vyake vya maadili. Soma 1 Wakorintho
au onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali
6:9-11, kisha mzungumzie swali hili:
yanayofuata.
˙ Je, Mungu anachukizwa tu na ngono
VIDEO: Kijana Asiye na Busara kati ya watu wa jinsia moja au kuna
(
(9:31) mambo mengine yanayomchukiza?

Ili tumfurahishe Mungu, sisi sote tunahitaji


kufanya mabadiliko. Je, tunanufaika tunapofanya
˙ Kijana huyo aliingiaje katika kishawishi? mabadiliko hayo? Soma Zaburi 19:8, 11, kisha
—Ona Methali 7:8, 9. mzungumzie maswali haya:
˙ Kulingana na Methali 7:23, 26, uasherati
˙ Je, unafikiri viwango vya Yehova kuhusu
unaweza kuwa na matokeo mabaya sana.
maadili vinafaa? Kwa nini?
Tukidumisha maadili safi tutaepuka
matatizo gani?
˙ Kuwa na maadili safi kunawezaje
kutusaidia kufurahia maisha milele?

Yehova amewasaidia watu wengi


watii viwango vyake vya maadili.
Anaweza kukusaidia pia

WATU FULANI HUSEMA: “Ni sawa kwa watu wawili kufanya ngono ikiwa wanapendana.”
˙ Wewe una maoni gani?

173
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Ngono ni zawadi ambayo Yehova
amempa mume na mke ili waifurahie. Jifunze kwa nini Mungu
anataka mwanamume na
mwanamke wafunge ndoa
Ungejibuje? kabla ya kuishi pamoja.
“Biblia Inasema Nini
˙ Uasherati unatia ndani Kuhusu Kuishi Pamoja
mambo gani? Bila Kufunga Ndoa?”
˙ Ni nini ambacho kitatusaidia (Makala iliyo kwenye mtandao)
kuepuka uasherati?
˙ Tunanufaikaje tunapofuata viwa-
ngo vya maadili vya Yehova? Jifunze kwa nini viwango
vya Biblia kuhusu ngono
kati ya watu wa jinsia
moja havichochei chuki.
“Je, Ni Kosa Kufanya Ngono
Kati ya Watu wa Jinsia Moja?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Jifunze jinsi sheria za Mungu


zinavyotulinda inapohusu
matendo yote ya ngono.
“Je, Ngono ya
Lengo Mdomo Ni Ngono?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
N Weka akilini maneno ya andiko
moja au mawili katika somo hili
ambayo yatakusaidia kupinga
vishawishi vya kujihusisha na
upotovu wa maadili. Katika simulizi “Walinionyesha
Heshima,” ona jambo lililo-
mchochea mtu aliyekuwa na
N Lengo lingine:
zoea la kufanya ngono na watu
wa jinsia yake abadili maisha
yake ili amfurahishe Mungu.
“Biblia Inabadili Maisha”
(Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 2011)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 41, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
42

Biblia Inasema Nini


Kuhusu Useja na Ndoa?
Katika tamaduni fulani, inaaminiwa kwamba sheria wanaahidi kwamba watapendana, wata-
mtu hawezi kuwa na furaha ikiwa hajafunga heshimiana, na kutunzana. Kwa hiyo, wanajihisi
ndoa. Hata hivyo, si watu wote waliofunga ndoa wakiwa salama zaidi tofauti na mwanamume
walio na furaha na si waseja wote wasio na fura- na mwanamke wanaoishi pamoja bila kufunga
ha. Biblia inasema kwamba useja na ndoa ni za- ndoa. Na ndoa inaandaa mazingira salama ya
wadi kutoka kwa Yehova. kulea watoto.

1. Kuna manufaa gani ya kuwa mseja? 3. Yehova ana maoni gani kuhusu ndoa?
Biblia inasema hivi: “Yeyote anayefunga ndoa Yehova alipoanzisha ndoa ya kwanza alisema
anafanya vema, lakini yeyote asiyefunga ndoa hivi: “Mwanamume atamwacha baba yake na
atafanya vema zaidi.” (Soma 1 Wakorintho mama yake naye atashikamana na mke wake.”
7:32, 33, 38.) Ni katika njia gani mseja anaweza (Mwanzo 2:24) Yehova anataka mume na mke
‘kufanya vema zaidi’? Wakristo waseja hawa- wapendane na waishi pamoja maisha yao yote.
na jukumu la kumtunza mwenzi wa ndoa. Kwa Anaruhusu talaka ikiwa mwenzi mmoja wa ndoa
hiyo, wana uhuru mwingi. Kwa mfano, baadhi anafanya uzinzi. Katika hali kama hiyo, Yehova
yao wanaweza kupanua huduma yao kwa kuha- anamruhusu mwenzi asiye na hatia aamue ikiwa
mia katika nchi nyingine ili kuhubiri habari nje- atatafuta talaka. (Mathayo 19:9) Yehova ana-
ma. Jambo muhimu zaidi, wanaweza kutumia kataza Wakristo kuwa na ndoa za wake wengi.
muda mwingi zaidi kumkaribia Yehova. —1 Timotheo 3:2.

2. Kuna manufaa gani ya kufunga ndoa kisheria?  Ona Maelezo ya Ziada 4 kuhusu kutengana ikiwa hakuna ha-
tia ya uzinzi.
Kama ilivyo na useja, ndoa ina manufaa ya kipe-
kee. Biblia inasema kwamba “wawili ni afadhali
kuliko mmoja.” (Mhubiri 4:9) Hilo ni kweli hasa
kwa Wakristo wanaofuata kanuni za Biblia ka-
tika ndoa yao. Wakristo wanaofunga ndoa ki-

175
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi unavyoweza kuwa


na furaha na kumfurahisha Yehova,
iwe wewe ni mseja au umefunga ndoa.

4. Tumia vizuri
Wanyama wawili walio tofauti sana wakifungwa
zawadi ya useja nira pamoja, wataumia. Vivyo hivyo, Mkristo
anayefunga ndoa na mwenzi ambaye si
Yesu aliona useja kuwa zawadi. (Matha- mwamini atapatwa na matatizo mengi
yo 19:11, 12) Soma Mathayo 4:23, kisha
mzungumzie swali hili:
˙ Yesu alitumiaje zawadi ya useja kumtumikia
Baba yake na kuwasaidia wengine? 5. Chagua mwenzi wa
Kama Yesu, Wakristo wanaweza kufurahia
ndoa kwa hekima
zawadi ya useja. Onyesha VIDEO, kisha Kuchagua mwenzi wa ndoa ni mojawapo
mzungumzie swali linalofuata. ya uamuzi muhimu zaidi ambao utafanya.
Soma Mathayo 19:4-6, 9, kisha mzungumzie
( VIDEO: Waseja Waaminifu swali hili:
(3:15)
˙ Kwa nini Mkristo anapaswa kufikiria
kwa makini kabla ya kufanya uamuzi
wa kufunga ndoa?
˙ Wakristo wanawezaje kutumia zawadi
ya useja kwa njia yenye kuthawabisha? Biblia inaweza kukusaidia kutambua sifa za
mwenzi wa ndoa anayekufaa. Jambo muhimu
zaidi, chagua mwenzi wa ndoa ambaye ana-
Je, wajua? mpenda Yehova. Soma 1 Wakorintho 7:39
Biblia haitaji umri wa kufunga ndoa. na 2 Wakorintho 6:14. Kisha mzungumzie
Hata hivyo, inawatia moyo vijana wasubiri maswali haya:
hadi ‘wapite upeo wa ujana,’ kipindi ambacho
hisia zenye nguvu za ngono zinaweza kufanya ˙ Kwa nini Mkristo anapaswa kufunga
iwe vigumu kwa kijana kufanya uamuzi kwa ndoa tu na Mkristo mwenzake?
hekima.—1 Wakorintho 7:36. ˙ Unafikiri Yehova atahisije tukiamua
kufunga ndoa na mtu ambaye hampendi
Yehova?

 Katika tamaduni fulani, wazazi huamua mtu atakayefunga


ndoa na mwana au binti yao. Katika visa kama hivyo, wazazi
wenye upendo huchunguza kwanza ikiwa mtu huyo anampe-
nda Yehova, bali si uwezo wake wa kifedha, au jinsi watu wa-
navyomwona katika jamii.
6. Sitawisha maoni ya
Yehova kuhusu ndoa
Katika Israeli la kale, baadhi ya wanaume waliwapa 7. Fuata viwango vya
talaka wake zao kwa sababu ya ubinafsi. Soma
Malaki 2:13, 14, 16, kisha mzungumzie swali hili: Yehova kuhusu ndoa
˙ Kwa nini Yehova anachukia watu wanapotalikia- Huenda mtu akahitaji kufanya jitihada nyi-
na kwa sababu zisizo na msingi wa Maandiko? ngi ili kufuata viwango vya Yehova kuhusu
ndoa. Lakini Yehova anawabariki wale
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata. wanaofanya hivyo. Onyesha VIDEO.

( VIDEO: Ndoa—Kifungo ( VIDEO: Unaweza Kufuata


cha Kudumu (4:31) Viwango vya Yehova Kuhusu
Ndoa (4:14)

˙ Ikiwa umefunga ndoa na mtu ambaye Soma Waebrania 13:4, kisha mzungumzie
si mwamini, unaweza kufanya nini ili maswali haya:
kuwa na ndoa yenye furaha?
˙ Je, unafikiri viwango vya Yehova
kuhusu ndoa vinafaa? Kwa nini?

Yehova anatarajia Wakristo waandikishe


kisheria ndoa na talaka zao kwa sababu
katika nchi nyingi, hiyo ni sheria iliyowekwa
na serikali. Soma Tito 3:1, kisha mzungu-
mzie swali hili:

˙ Ikiwa umefunga ndoa, je, umehakiki-


sha kwamba ndoa yenu imeandikishwa
kisheria serikalini?

 Ikiwa unaishi na mtu ambaye hujafunga naye ndoa,


unaweza kuamua kumwacha au kufunga naye ndoa,
huo ni uamuzi wako.

Uzinzi na talaka husababisha maumivu mengi


kwa mwenzi asiye na hatia na pia kwa watoto

HUENDA MTU AKAULIZA: “Kwa nini ufunge ndoa? Mwanamume na mwanamke


wanaweza kuishi pamoja bila kufunga ndoa.”
˙ Wewe una maoni gani?

177
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Useja na ndoa ni zawadi kutoka kwa
Yehova. Waseja na watu waliofunga Kuoa au kuolewa “katika Bwa-
ndoa wanaweza kuwa na furaha na na tu” kunamaanisha nini?
kuridhika maishani ikiwa wataishi “Maswali Kutoka kwa
kulingana na viwango vya Yehova. Wasomaji” (Mnara wa Mlinzi,
Julai 1, 2004)

Ungejibuje?
˙ Mtu anawezaje kutumia vizuri
useja wake?
˙ Kwa nini Biblia inasema kwamba ( 17:05 Ona video tatu fupi
Mkristo anapaswa kufunga ndoa zinazoweza kukusaidia
tu na Mkristo mwenzake? kufanya maamuzi mazuri
kuhusu uchumba na ndoa.
˙ Ni nini msingi pekee wa
Kujitayarisha kwa Ajili
Kimaandiko kuhusu talaka?
ya Ndoa

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 1:56 Jifunze kwa nini ndugu


mmoja anahisi kwamba
jambo ambalo Yehova
amempa ni lenye thamani
kuliko vitu vyote alivyoacha.
Lengo
Nilitarajia Mchumba Wangu
N Ikiwa ndoa yenu haijaandiki- Angejifunza Ukweli
shwa kisheria serikalini, chu-
nguza jambo unalopaswa kufa-
nya ili kuiandikisha kisheria.
Ni baadhi ya mambo gani
N Lengo lingine: ambayo mtu anapaswa kufiki-
ria kabla ya kuamua kutengana
au kutafuta talaka?
“Heshimu ‘Kile Ambacho
Mungu Ameunganisha’ ”
(Mnara wa Mlinzi, Desemba 2018)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 42, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
43

Wakristo Wanapaswa Kuwa


na Maoni Gani Kuhusu Kileo?
Ulimwenguni pote, watu wana maoni mbalimba- ni, hatupaswi kunywa sana hivi kwamba tushi-
li kuhusu kileo. Baadhi ya watu hufurahia ku- ndwe kufikiri vizuri, kudhibiti maneno na mate-
nywa kileo wakiwa na marafiki. Wengine hua- ndo yetu, au kujisababishia madhara ya kiafya.
mua kwamba hawatakunywa kileo kamwe. Na Ikiwa hatuwezi kudhibiti kiasi cha kileo tunacho-
wengine hunywa kwa wingi mpaka wanalewa. kunywa, tunapaswa kuamua kuacha kabisa ku-
Biblia inasema nini kuhusu kileo? nywa kileo.

1. Je, ni kosa kunywa kileo? 3. Tunawezaje kuheshimu uamuzi wa


Biblia haikatazi kunywa kileo. Badala yake, kati watu wengine kuhusu kileo?
ya zawadi nyingi ambazo Mungu ametupa- Kila mtu anapaswa kujifanyia uamuzi inapohusu
tia, Biblia inataja “divai inayofanya moyo wa kunywa kileo. Hatupaswi kumhukumu mtu ana-
mwanadamu ushangilie.” (Zaburi 104:14, 15) yeamua kunywa kileo kwa kiasi, wala hatupa-
Baadhi ya wanaume na wanawake waamini- swi kumlazimisha mtu ambaye hataki kunywa
fu wanaotajwa katika Biblia walikunywa kileo. kileo. (Waroma 14:10) Tunaamua kwamba hatu-
—1 Timotheo 5:23. takunywa kileo ikiwa baada ya kunywa tutawa-
sababishia wengine matatizo. (Soma Waroma
2. Biblia inatoa ushauri gani kwa wale 14:21.) Tunatafuta “si faida [yetu wenyewe],
wanaoamua kunywa kileo? bali faida ya yule mtu mwingine.”—Soma 1 Wa-
Yehova anakataza ulevi na kunywa kileo kupita korintho 10:23, 24.
kiasi. (Wagalatia 5:21) Neno lake linasema hivi:
“Usiwe miongoni mwa watu wanaokunywa di-
vai nyingi mno.” (Methali 23:20) Hivyo, ikiwa
tutaamua kunywa kileo, hata tukiwa faragha-

179
CH I M BA ZAI DI

Chunguza kanuni za Biblia ambazo zitakusaidia kuamua ikiwa


utakunywa kileo na kiasi ambacho utakunywa. Vilevile, chunguza
jambo la kufanya ikiwa unapambana na tatizo la kunywa kupita kiasi.

4. Amua kama utakunywa kileo ˙ Ikiwa unashindwa kudhibiti kiasi


unachokunywa.
Yesu alikuwa na maoni gani kuhusu kunywa kileo? ˙ Ikiwa sheria ya nchi haikuruhusu
Ili upate jibu, chunguza muujiza wa kwanza aliofa- kunywa kileo.
nya. Soma Yohana 2:1-11, kisha mzungumzie ma- ˙ Ukiwa pamoja na mtu ambaye ameamua
swali haya: hatakunywa kileo kwa sababu zamani alishi-
˙ Kutokana na muujiza huo, Yesu ana maoni ndwa kudhibiti kiasi cha kileo alichokunywa.
gani kuhusu kileo na wale wanaokunywa ki-
leo? Je, utaandaa kileo kwenye harusi au tafrija?
Ili kuona jambo litakalokusaidia kuamua,
˙ Kwa kuwa Yesu hakukataza kunywa kileo,
onyesha VIDEO.
Mkristo anapaswa kumwonaje mtu anayea-
mua kunywa kileo?
( VIDEO: Je, Niandae Kileo?
Hata hivyo, ingawa Mkristo yuko huru kunywa ki- (2:41)
leo, hilo halimaanishi kwamba sikuzote ni jambo la
busara kufanya hivyo. Soma Methali 22:3, kisha
uchunguze jinsi mambo yafuatayo yanavyoweza Soma Waroma 13:13 na 1 Wakorintho 10:31, 32.
kukusaidia kuamua kama utakunywa kileo: Baada ya kusoma kila andiko, zungumzieni
˙ Ikiwa utaendesha gari au kutumia mashine. swali hili:
˙ Ikiwa wewe ni mjamzito. ˙ Kutumia kanuni hii kunaweza kukusaidiaje
˙ Ikiwa daktari amekushauri usinywe kileo. kufanya uamuzi unaomfurahisha Yehova?

Kila Mkristo anapaswa kujifanyia


uamuzi ikiwa atakunywa kileo au la.
Hata ikiwa anaona ni sawa kunywa kileo,
huenda wakati mwingine akaamua kutokunywa
5. Amua kiasi ambacho Tunawezaje kuepuka kunywa kileo kupita kiasi?
Tunahitaji kuwa na sifa ya kiasi, na kutambua mi-
utakunywa paka yetu. Soma Methali 11:2, kisha mzungumzie
swali hili:
Ikiwa unaamua kunywa kileo, kumbuka jambo hili:
Ingawa Yehova hakatazi kunywa kileo, anakataza ˙ Kwa nini ni vizuri kujiwekea kiasi hususa
kunywa kileo kupita kiasi. Kwa nini? Soma Hosea cha kileo ambacho utakunywa?
4:11, 18, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Ni nini kinachoweza kutokea ikiwa mtu
atakunywa kileo kupita kiasi?

6. Jinsi ya kushinda zoea (


la kunywa kupita kiasi
Ona jambo lililomsaidia mwanamume fulani ashinde VIDEO: ‘Nilichoshwa na
zoea la kunywa kileo kupita kiasi. Onyesha VIDEO, Maisha Yangu’ (6:32)
kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
˙ Katika video hiyo, Dmitry alitendaje baada ya kunywa kileo?
˙ Je, ilikuwa rahisi kwake kuacha mara moja zoea hilo?
˙ Mwishowe, nini kilichomsaidia kushinda uraibu wa kunywa kileo?

Soma 1 Wakorintho 6:10, 11, kisha mzungumzie maswali haya:


˙ Kwa nini ulevi ni kosa zito?
˙ Ni nini kinachoonyesha kwamba mtu aliye na zoea
la kunywa kupita kiasi anaweza kubadilika?

Soma Mathayo 5:30, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Kukata mkono kunamaanisha kwamba mtu anapaswa kuacha
tabia fulani ili amfurahishe Yehova. Unaweza kufanya nini ikiwa
unapambana kushinda zoea la kunywa kileo kupita kiasi? 

Soma 1 Wakorintho 15:33, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Rafiki zako wanawezaje kufanya unywe kileo kupita kiasi?

 Wale ambao ni waraibu wa kunywa kileo, wanahitaji kutafuta msaada wa wataalamu


ili waache zoea hilo. Madaktari wengi wanapendekeza kwamba mtu aliyekuwa na tatizo
la kunywa kileo kupita kiasi anapaswa kuacha kabisa kunywa kileo.

HUENDA MTU AKAULIZA: “Je, ni vibaya kunywa pombe?”


˙ Wewe ungejibuje swali hilo?

181
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova amewapa wanadamu kileo
ili wafurahie. Lakini anakataza ulevi ( 2:31 Vijana wanawezaje
na kunywa kupita kiasi. kufanya maamuzi mazuri
kuhusu kunywa kileo?
Fikiria Madhara Kabla
Ungejibuje? ya Kunywa

˙ Biblia inasema nini kuhusu ku-


nywa kileo?
˙ Kuna hatari gani ya kunywa kileo
kupita kiasi?
˙ Tunawezaje kuheshimu uamuzi Chunguza hatua unazopaswa
kuchukua ili ushinde zoea la
wa watu wengine kuhusu kunywa
kunywa kileo kupita kiasi.
kileo?
“Mtazamo Unaofaa Kuhusu
Pombe” (Mnara wa Mlinzi,
Januari 1, 2010)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Je, Mkristo anaweza


kushiriki kugonga glasi
na kutakiana heri?
“Maswali Kutoka kwa
Lengo Wasomaji” (Mnara wa Mlinzi,
Februari 15, 2007)
N Ikiwa unaamua kunywa kileo,
fikiria hali zinazohusika, kisha
ujiwekee kiasi hususa ambacho
utakunywa.
Katika simulizi “Nilikuwa
N Lengo lingine: Mtungi wa Pombe Usiojaa,”
ona jinsi mwanamume fulani
alivyoshinda zoea la kunywa
kileo kupita kiasi.
“Biblia Inabadili Maisha”
(Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 2012)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 43, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
44

Je, Sherehe Zote


Zinamfurahisha Mungu?
Yehova anataka tufurahie maisha na tuwe na nembo za taifa au uhuru wa nchi. (1 Yohana
pindi za kusherehekea. Lakini, je, sherehe na 5:21) Na sherehe nyingine hutukuza harakati za
sikukuu zote zinamfurahisha? Tunawezaje kuo- kisiasa au za kijamii. Yehova atahisije ikiwa tuta-
nyesha kwamba tunampenda Yehova inapohusu mtukuza mtu au shirika fulani, hasa ikiwa mtu
sherehe na sikukuu? au shirika hilo linaendeleza mawazo yaliyo ki-
nyume na kusudi lake?
1. Kwa nini sikukuu nyingi hazimfurahishi
Yehova? 3. Ni tabia gani zinazoweza kufanya
Huenda ukashangaa kujua kwamba sikukuu nyi- sherehe zisikubalike?
ngi hazitegemei mafundisho ya kimaandiko au Biblia inakataza “kunywa kupita kiasi, karamu
zina asili ya kipagani. Sikukuu hizo zinahu- zenye vurugu, [na] mashindano ya kunywa.”
siana na dini za uwongo. Huenda zinahusiana (1 Petro 4:3) Katika sherehe fulani, watu hute-
na zoea la kuwasiliana na roho waovu, au zi- nda jinsi wanavyotaka na kujihusisha na upoto-
naunga mkono fundisho la kwamba nafsi hai- vu wa maadili. Ili tuendelee kuwa rafiki za Yeho-
wezi kufa. Baadhi ya sherehe hizo zinahusiana va, tunahitaji kujitenga kabisa na ukosefu huo
na ushirikina au itikadi ya bahati. (Isaya 65:11) wa maadili.
Yehova anawaamuru hivi waabudu wake: ‘Jite-
ngeni na mwache kugusa kitu kichafu.’—2 Wa-
korintho 6:17.

2. Yehova anahisije kuhusu sherehe


zinazowatukuza wanadamu?
Yehova anatuonya ili tusinaswe na mtego
wa ‘kuwatumaini wanadamu.’ (Soma Yere-
mia 17:5.) Baadhi ya sikukuu huwatukuza wata-
wala au wanajeshi. Sherehe nyingine hutukuza

 Chunguza Maelezo ya Ziada 5 ili uone jinsi unavyoweza kute-


nda watu wanaposherehekea sikukuu.

183
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi unavyoweza


kumfurahisha Yehova kwa
kufanya maamuzi ya hekima
kuhusu sikukuu na sherehe.

4. Epuka sherehe zinazomvunjia


Yehova heshima
Soma Waefeso 5:10, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Tunapaswa kuhakikisha nini tunapoamua ikiwa
tutasherehekea sikukuu fulani?
˙ Ni sikukuu gani ambazo ni maarufu katika eneo unaloishi? Jinsi tunavyoweza kujua ikiwa
sherehe fulani haimfurahishi
˙ Je, unafikiri sikukuu hizo zinamfurahisha Yehova?
Mungu
Kwa mfano, umewahi kujiuliza Mungu ana maoni gani  Je, inategemea mafundisho
kuhusu sherehe za siku ya kuzaliwa? Biblia haitaji hata yasiyopatana na Maandiko?
mwabudu mmoja wa Yehova ambaye alisherehekea siku Ili kujua, chunguza chanzo chake.
ya kuzaliwa, lakini inataja sherehe mbili za siku ya kuzaliwa  Je, inawatukuza wanadamu,
ambazo zilisherehekewa na watu ambao hawakumwabudu mashirika, au nembo za taifa?
Yehova. Soma Mwanzo 40:20-22 na Mathayo 14:6-10. Tunamtukuza Yehova peke yake,
Kisha mzungumzie maswali haya: na tunaamini kwamba yeye ndiye
anayeweza kusuluhisha matatizo
˙ Sherehe hizo mbili za siku ya kuzaliwa zina ulimwenguni.
mambo gani yanayofanana?  Je, desturi na mazoea yake
˙ Kulingana na masimulizi hayo ya Biblia, unafikiri Yehova yanapingana na viwango vya
ana maoni gani kuhusu sherehe za siku ya kuzaliwa? Biblia? Tunapaswa kuendelea
kuwa safi kiadili.
Lakini bado huenda ukajiuliza, ‘Je, kweli Yehova anajali ikiwa ni-
tasherehekea siku ya kuzaliwa au sherehe nyingine isiyopatana
na Maandiko?’ Soma Kutoka 32:1-8. Kisha, onyesha VIDEO
(
na mzungumzie maswali yanayofuata.
˙ Kwa nini tunapaswa kuhakikisha kwamba tunafanya
mambo yanayokubalika kwa Yehova? VIDEO: Sikukuu na Sherehe
˙ Tunawezaje kufanya hivyo? Zisizompendeza Mungu (5:07)
5. Wasaidie wengine waheshimu imani yako (

Huenda ikawa vigumu kukataa wengine wanapokushinikiza


ushiriki katika sherehe ambazo hazimfurahishi Yehova. VIDEO: Tumia Busara
Waeleze maamuzi yako kwa subira na kwa busara. Ili kuona Unapoeleza Kuhusu
mfano wa jinsi unavyoweza kufanya hivyo, onyesha VIDEO. Imani Yako (2:02)
Soma Mathayo 7:12, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kulingana na mstari huu, je, unapaswa kuwaambia
watu wa familia yako wasio waamini kwamba hawapaswi
kusherehekea sikukuu fulani?
˙ Unaweza kufanya nini ili kuwahakikishia watu wa familia
yako kwamba ingawa hutasherehekea pamoja nao,
bado unawapenda na kuwajali?

6. Yehova anataka tuwe na furaha


Yehova anataka tuwe na pindi zenye kufurahisha pamoja
na marafiki na watu wa familia zetu. Soma Mhubiri 8:15,
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Mstari huu unaonyeshaje kwamba Yehova anataka
tuwe na furaha?

Yehova anataka watu wake wawe na wakati mzuri wa kufurahia


maisha pamoja. Onyesha VIDEO ili uone jinsi jambo hilo linavyo-
onekana wazi wakati wa makusanyiko yetu ya kimataifa.
Soma Wagalatia 6:10, kisha mzungumzie maswali haya:
(
˙ Je, tunahitaji kusherehekea sikukuu zilizo maarufu ili
kuonyesha kwamba ‘tunawatendea wengine mema?’
˙ Ni jambo gani ambalo lingekuletea furaha zaidi, VIDEO: Kuonyesha Ukarimu
je, ni kulazimika kutoa zawadi kwa sababu ni wakati Wakati wa Makusanyiko ya
wa sikukuu, au kutoa zawadi wakati wowote? Kimataifa (5:40)
˙ Mara kwa mara, Mashahidi wa Yehova hupanga
pindi za pekee kwa ajili ya watoto wao na hata
kuwapa zawadi wakati wowote. Ikiwa una watoto,
ni mambo gani ya pekee unayoweza kuwafanyia?

WATU FULANI HUSEMA: “Vyanzo vya sikukuu si muhimu. Jambo muhimu


ni kuwa na muda wa kufurahia pamoja na familia na marafiki.”
˙ Wewe una maoni gani?

185
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova anataka tuwe na pindi za fu-
raha pamoja na familia na marafiki. Chunguza baadhi
Lakini pia anataka tuepuke sikukuu ya sikukuu ambazo
ambazo hazimfurahishi. Wakristo hawasherehekei.
“Kwa Nini Mashahidi wa
Yehova Hawasherehekei
Ungejibuje? Sikukuu Fulani?” (Makala
iliyo kwenye mtandao)
˙ Tunapaswa kujiuliza maswali
gani ili kujua ikiwa sherehe fulani
haimfurahishi Yehova?
˙ Tunawezaje kuwasaidia marafiki Chunguza sababu nne zi-
na watu wa familia zetu waelewe nazofanya tuamini kwamba
maamuzi yetu kuhusu sikukuu? sherehe za siku ya kuzaliwa
hazimfurahishi Mungu.
˙ Tunajuaje kwamba Yehova anata-
“Kwa Nini Mashahidi wa
ka tuwe na pindi za kufurahia
Yehova Hawasherehekei
maisha?
Siku za Kuzaliwa?” (Makala
iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 2:04 Ona jinsi kijana fulani alivyote-
nda kwa busara alipodhihakiwa
shuleni kwa sababu hasherehe-
kei Krismasi.
Lengo Tenda kwa Busara
Unapodhihakiwa
N Tumia mambo ambayo
umejifunza katika somo hili ku-
chunguza sikukuu ambazo watu
wanapenda katika eneo lenu.
Mamilioni ya Wakristo wamea-
N Lengo lingine: mua kwamba hawatasherehe-
kea Krismasi. Wanahisije kuhu-
su uamuzi wao?
“Wamepata Jambo Bora
Kuliko Krismasi” (Mnara wa
Mlinzi, Desemba 1, 2012)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 44, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
45

Inamaanisha Nini Kutounga


Mkono Upande Wowote?
Yesu aliwafundisha wafuasi wake kwamba 2. Tunawezaje kuonyesha kwamba hatuungi
hawapaswi kuwa “sehemu ya ulimwengu.” mkono upande wowote?
(Yohana 15:19) Hilo linahusisha kutounga mko- Kama Yesu, sisi pia hatujihusishi na siasa. Watu
no upande wowote katika vita au siasa za uli- walipoona muujiza mmoja wa Yesu, walitaka ku-
mwengu. Ukweli ni kwamba si rahisi sikuzo- mfanya awe Mfalme wao duniani, lakini alika-
te kutounga mkono upande wowote. Huenda taa. (Yohana 6:15) Kwa nini alikataa? Kwa sa-
watu wakatudhihaki kwa sababu ya msimamo babu baadaye alisema hivi: “Ufalme wangu si
wetu. Tunawezaje kuepuka kuunga mkono upa- sehemu ya ulimwengu huu.” (Yohana 18:36)
nde wowote na kuendelea kuwa washikamanifu Tukiwa wanafunzi wa Yesu, tunaonyesha kwa
kwa Yehova Mungu? njia mbalimbali kwamba hatuungi mkono upa-
nde wowote. Kwa mfano, hatushiriki katika vita.
1. Wakristo wa kweli wana maoni gani kuhusu
(Soma Mika 4:3.) Tunaheshimu nembo za taifa
serikali za wanadamu?
kama vile bendera, lakini hatuziabudu. (1 Yo-
Wakristo wanaheshimu serikali. Tunatii mane- hana 5:21) Na hatuungi mkono wala kupinga
no haya ya Yesu: “Mlipeni Kaisari vitu vya Kai- mgombeaji au chama chochote cha kisiasa.
sari.” Hilo linamaanisha tunatii sheria za nchi, Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba sisi ni
kama vile kulipa kodi. (Marko 12:17) Biblia ina- washikamanifu kabisa kwa serikali ya Mungu,
fundisha kwamba serikali za wanadamu zina- yaani, Ufalme wake.
tawala kwa sababu Yehova ameruhusu ziwepo.
(Waroma 13:1) Basi, tunaelewa kwamba seri-
kali za wanadamu zina mamlaka ya kadiri au
yenye mipaka. Tunaamini kwamba Mungu ata-
tumia Ufalme wake wa mbinguni kuondoa ma-
tatizo ya wanadamu.

187
CH I M BA ZAI DI

Chunguza hali ambazo zinaweza kufanya iwe vigumu


kutounga mkono upande wowote na jinsi unavyoweza
kufanya maamuzi yanayomfurahisha Yehova.

3. Wakristo wa kweli hawaungi (


mkono upande wowote
Yesu na wafuasi wake walituwekea mfano. Soma Waroma 13:1, 5-7 VIDEO: Wakristo wa Kweli
na 1 Petro 2:13, 14. Kisha, onyesha VIDEO na mzungumzie maswali Hawaungi Mkono Upande
yanayofuata. Wowote—Sehemu ya 1 (4:28)

˙ Kwa nini tunapaswa kuheshimu serikali za wanadamu?


˙ Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunajitiisha chini ya (
serikali hizo?

Wakati wa vita, huenda mataifa fulani yakadai kwamba hayaungi VIDEO: Wakristo wa Kweli
mkono upande wowote, lakini yanasaidia pande zote zinazozozana. Hawaungi Mkono Upande
Kutounga mkono upande wowote kunamaanisha nini hasa? Soma Wowote—Sehemu ya 2 (3:09)
Yohana 17:16. Kisha, onyesha VIDEO na mzungumzie swali linalo-
fuata.
(
˙ Inamaanisha nini kutounga mkono upande wowote?

Tunapaswa kufanya nini ikiwa serikali za wanadamu zinatuamuru VIDEO: Wakristo wa Kweli
tufanye jambo linalopingana na sheria ya Mungu? Soma Matendo Hawaungi Mkono Upande
5:28, 29. Kisha, onyesha VIDEO na mzungumzie maswali yanayo- Wowote—Sehemu ya 3 (1:18)
fuata.
˙ Sheria za wanadamu zinapopingana na sheria za Mungu,
tunapaswa kutii sheria za nani?
˙ Unafikiri ni katika hali gani Wakristo hawapaswi kutii
serikali za wanadamu?
4. Onyesha kwamba huungi mkono upande (
wowote kupitia mawazo na matendo yako
Soma 1 Yohana 5:21. Kisha, onyesha VIDEO na mzungumzie VIDEO: Wakristo wa
maswali yanayofuata. Kweli Wanahitaji Ujasiri
—Ili Wasiunge Mkono
˙ Katika video hiyo, kwa nini Ayenge alikataa kujiunga Upande Wowote (2:50)
na chama cha kisiasa au kushiriki katika sherehe za
kitaifa, kama vile kupiga saluti mbele ya bendera?
˙ Je, unafikiri alifanya uamuzi wa hekima? (

Msimamo wetu wa kutounga mkono upande


wowote unaweza kujaribiwa katika hali gani nyingine? VIDEO: Masomo Kutoka
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata. kwa Mnara wa Mlinzi
—Usiunge Mkono Upande
˙ Tunawezaje kuonyesha kwamba hatuungi mkono upande Wowote Katika Ulimwengu
wowote kunapokuwa na mashindano ya michezo kati ya Huu Uliogawanyika (5:16)
mataifa mbalimbali?
˙ Tunawezaje kuendelea kutounga mkono upande wowote, iwe
maamuzi ya wanasiasa yatatunufaisha au kutuletea madhara?
˙ Msimamo wetu wa kutounga mkono upande wowote unawezaje
kuathiriwa na mambo tunayosikia katika vyombo vya habari au
watu tunaoshirikiana nao?

Ni katika hali
gani ambazo Mkristo
anapaswa kudumisha
msimamo wa kutounga
mkono upande wowote
kupitia mawazo na
matendo yake?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Kwa nini hupigi saluti mbele ya bendera au kuimba wimbo wa taifa?”
˙ Wewe ungejibuje?

189
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Wakristo hujitahidi sana kutounga
mkono upande wowote wa kisiasa ( 3:14 Huenda tukahitaji kudhabi-
kwa mawazo, maneno, na hu mambo gani ili tusiunge
matendo yao. mkono upande wowote?
Yehova Hajatuacha Kamwe

Ungejibuje?
˙ Tunapaswa kuwa na maoni gani
kuhusu serikali za wanadamu?
˙ Kwa nini hatuungi mkono
upande wowote wa kisiasa? ( 4:25 Familia zinaweza kufanya nini
ili kujitayarisha mapema kwa
˙ Ni hali gani zinazoweza kufanya
ajili ya hali zinazoweza kujaribu
iwe vigumu kutounga mkono
msimamo wao wa kutounga
upande wowote? mkono upande wowote?
Dumisha Msimamo wa Kutou-
nga Mkono Upande Wowote
Katika Sherehe za Umma

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 5:19 Kwa nini kutetea nchi sio he-
shima kubwa zaidi ambayo
mtu anaweza kupata?
“Mambo Yote Yanawezekana
Lengo na Mungu”

N Fikiria hali ambayo inaweza


kujaribu msimamo wako wa ku-
tounga mkono upande wowote,
kisha uamue mapema jambo
utakalofanya. Chunguza jinsi ya kutokuwa
sehemu ya ulimwengu unapo-
fanya maamuzi kuhusu kazi.
N Lengo lingine:
“Kila Mmoja Ataubeba
Mzigo Wake Mwenyewe”
(Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 2006)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 45, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
46

Kwa Nini Unapaswa Kujiweka


Wakfu na Kubatizwa?
Tunajiweka wakfu kwa Yehova tunapomwahidi 2. Yehova anawapa baraka gani Mashahidi
katika sala kwamba tutamwabudu yeye peke wake waliobatizwa?
yake na kutanguliza mapenzi yake maishani. Unapobatizwa, unajiunga na familia ya Yeho-
(Zaburi 40:8) Hatua inayofuata ni kubatizwa. va yenye furaha. Kisha utajionea upendo wake
Unapobatizwa, unaowaonyesha wengine kwa- kwa njia nyingi sana na utazidi kumkaribia hata
mba umejiweka wakfu. Uamuzi wa kujiweka zaidi. (Soma Malaki 3:16-18.) Yehova atakuwa
wakfu kwa Yehova ndio uamuzi muhimu zaidi kama Baba kwako, isitoshe utakuwa na familia
maishani. Ni nini ambacho kitakuchochea ufa- ya kiroho ya akina ndugu na dada ulimwengu-
nye uamuzi huo muhimu sana na utakaobadi- ni pote wanaompenda Yehova na wanaokupe-
li maisha yako? nda pia. (Soma Marko 10:29, 30.) Bila shaka,
lazima uchukue hatua fulani kabla ya kubati-
1. Ni nini ambacho humchochea mtu
zwa. Unapaswa kujifunza kumhusu Yehova, ku-
ajiweke wakfu?
mpenda, na kuwa na imani katika Mwana wake.
Tunachochewa na upendo kujiweka wakfu kwa Mwishowe, lazima ujiweke wakfu kwa Yehova.
Yehova. (1 Yohana 4:10, 19) Biblia inatuhimi- Ukichukua hatua hizo kisha ubatizwe, utaku-
za hivi: “[Mpende] Yehova Mungu wako kwa wa umeanza kutembea katika barabara inayoo-
moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na ngoza kwenye uzima wa milele. Neno la Mungu
kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” linasema hivi: “Ubatizo . . . unawaokoa ninyi
(Marko 12:30) Tunaonyesha kwamba tuna- sasa pia.”—1 Petro 3:21.
mpenda Mungu si kwa maneno tu, bali
pia kwa matendo yetu. Kama vile mwanamu-
me na mwanamke wanaopendana sana wana-
vyoamua kufunga ndoa, vivyo hivyo kumpenda
Yehova hutuchochea kujiweka wakfu kwake na
kubatizwa.

191
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kwa nini ni muhimu


kwako kujiweka wakfu kwa
Yehova na kubatizwa.

3. Sisi sote
tunapaswa
kuchagua yule
tutakayemtumikia
Katika taifa la kale la Israeli, 4. Tafakari upendo ambao
baadhi ya watu walifikiri kwa-
mba wangemwabudu Yehova
Yehova amekuonyesha
na pia mungu wa uwongo Baali. Yehova ametupatia zawadi nyingi zenye thamani.
Lakini Yehova alimtuma nabii Tunaweza kumpatia nini? Onyesha VIDEO.
wake Eliya arekebishe maoni
hayo yasiyo sahihi. Soma 1 Wa-
falme 18:21, kisha mzungumzie ( VIDEO: Kumtolea Mungu
Zawadi (3:04)
swali hili:
˙ Waisraeli walipaswa
kufanya uamuzi gani?
Yehova amekuonyesha kwa njia gani kwamba anakupenda?
Soma Zaburi 104:14, 15 na 1 Yohana 4:9, 10, kisha
Kama Waisraeli, sisi pia tuna-
mzungumzie maswali haya:
paswa kuchagua yule tutaka-
yemtumikia. Soma Luka 16:13, ˙ Ni zawadi gani kutoka kwa Yehova ambazo hasa
kisha mzungumzie maswali zinakuchochea kumshukuru?
haya: ˙ Zawadi hizo zinafanya uhisije kumhusu Yehova?
˙ Kwa nini hatupaswi
kumwabudu Yehova na Tunapopokea zawadi ambayo tunaipenda, tunachochewa
wakati huohuo kuabudu kumwonyesha shukrani yule aliyetupatia zawadi hiyo. Soma
mtu au kitu kingine? Kumbukumbu la Torati 16:17, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Tunamwonyeshaje Yehova ˙ Unapofikiria mambo yote ambayo Yehova amekufanyia,
kwamba tumechagua unachochewa kufanya nini?
kumwabudu yeye?
5. Kujiweka wakfu huleta baraka nyingi (

Watu wengi wanaamini kwamba umaarufu, kazi nzuri,


au pesa zitawafanya wawe na furaha. Je, hilo ni kweli? VIDEO: Mchezo wa
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata. Mpira Ulikuwa Jambo
˙ Ingawa mwanamichezo katika video hiyo alipenda Kuu Maishani (5:45)
kucheza mpira, kwa nini aliacha kucheza mpira?
˙ Aliamua kujiweka wakfu kwa Yehova bali si kucheza
mpira. Je, unafikiri alifanya uamuzi sahihi? Kwa nini?

Kabla mtume Paulo hajawa Mkristo, alikuwa na kazi nzuri sana.


Alikuwa amesomea sheria ya Wayahudi na mwalimu wake alikuwa
mashuhuri. Lakini aliacha hayo yote ili awe Mkristo. Je, Paulo alijuta?
Soma Wafilipi 3:8, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kwa nini Paulo alisema kwamba mambo aliyofanya
kabla ya kuwa Mkristo yalikuwa “takataka nyingi”?
˙ Uamuzi wake ulimletea baraka gani?
˙ Unafikiri ni nini ambacho kitafanya uwe na maisha bora, je, ni
kumtumikia Yehova au ni kufuatia malengo mengine maishani?

Baada ya kuwa Mkristo,


Paulo alipata faida nyingi
kuliko mambo aliyoacha

WATU FULANI HUSEMA: “Si lazima umtumikie Mungu, furahia maisha.”


˙ Kwa nini unafikiri ni muhimu kujiweka wakfu kwa Yehova?

193
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Kumpenda Yehova hutuchochea
kujiweka wakfu kwake na kubatizwa. ( 6:52 Ona sababu iliyofanya
mwanamuziki na mwana-
michezo waamue kujiweka
Ungejibuje? wakfu kwa Yehova.
Vijana Huuliza—Nitayatumiaje
˙ Kwa nini tunapaswa kumpenda Maisha Yangu?—Kukumbuka
Yehova kwa moyo wetu wote na Yaliyopita
kumwabudu yeye peke yake?
˙ Yehova huwapa baraka gani
Mashahidi wake waliobatizwa?
˙ Je, ungependa kujiweka wakfu Chunguza sababu zaidi
za kujiweka wakfu.
kwa Yehova?
“Kwa Nini Ujiweke Wakfu
kwa Yehova?” (Mnara wa Mlinzi,
Januari 15, 2010)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 4:30 Katika video hii ya muziki,


ona shangwe ambayo wale
wanaojiweka wakfu kwa
Yehova wanapata.
Lengo Ninajitoa Kwako

N Unapotayarisha somo linalo-


fuata, chunguza mambo amba-
yo huenda yanakuzuia kujiweka
wakfu kwa Yehova.
Katika simulizi “Kwa Miaka
N Lengo lingine: Mingi Nilijiuliza, ‘Kwa Nini
Tuko Hai?’ ”ona jambo
lililomchochea mwanamke
fulani achunguze mambo
aliyotanguliza maishani.
“Biblia Inabadili
Maisha” (Mnara wa Mlinzi,
Novemba 1, 2012)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 46, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
47

Je, Uko Tayari Kubatizwa?


Tayari umejifunza mambo mengi kumhusu Ye- akusamehe. Vilevile, unaepuka kabisa mwene-
hova katika funzo lako la Biblia. Labda ume- ndo mbaya na kuazimia kuishi maisha yanayo-
fanya mabadiliko fulani ili kufuata mambo uli- mfurahisha Mungu. Isitoshe, unaanza kushiri-
yojifunza. Hata hivyo, huenda kuna sababu kiana na kutaniko kwa kuhudhuria mikutano na
inayokuzuia kujiweka wakfu kwa Yehova na ku- kuhubiri ukiwa mhubiri ambaye hajabatizwa.
batizwa. Katika somo hili, tutazungumzia baa-
dhi ya mambo yanayoweza kumzuia mtu kubati- 3. Kwa nini hupaswi kuruhusu woga ukuzuie?
zwa na jinsi unavyoweza kushinda changamoto Huenda wengine wakahisi kwamba hawawezi
hizo. kuishi kulingana na ahadi waliyomtolea Yeho-
va. Ni kweli kwamba wakati mwingine utakosea,
1. Unahitaji kuwa na ujuzi mwingi kadiri kama ilivyokuwa kwa wanaume na wanawake
gani kabla ya kubatizwa? waaminifu wanaotajwa katika Biblia. Lakini Ye-
Ili ubatizwe, unahitaji kuwa na “ujuzi sahihi wa hova hatarajii watumishi wake wawe wakamili-
kweli.” (1 Timotheo 2:4) Hilo halimaanishi kwa- fu. (Soma Zaburi 103:13, 14.) Anafurahi kuo-
mba kabla ya kubatizwa unapaswa kujua majibu na ukijitahidi kufanya mambo mazuri kulingana
ya maswali yote ya Biblia ambayo huenda watu na uwezo wako, naye atakusaidia! Yehova ana-
wakakuuliza. Hata Wakristo ambao walibatizwa tuhakikishia kwamba hakuna kitu ‘kinachowe-
miaka mingi iliyopita bado wanaendelea kujifu- za kututenga na upendo wake.’—Soma Waro-
nza. (Wakolosai 1:9, 10) Lakini unahitaji kuelewa ma 8:38, 39.
mafundisho ya msingi ya Biblia. Wazee wa kuta-
niko watakusaidia kujua ikiwa una ujuzi wa ku-
tosha.

2. Unapaswa kuchukua hatua gani


kabla ya kubatizwa?
Kabla ya kubatizwa, unapaswa ‘kutubu na ku-
geuka.’ (Soma Matendo 3:19.) Hilo linamaani-
sha kwamba unajuta sana kwa sababu ya dha-
mbi ulizofanya zamani na unamwomba Yehova

195
CH I M BA ZAI DI

Ona jinsi kumjua Yehova vizuri zaidi


na kukubali msaada wake kunavyoweza
kukusaidia kushinda mambo ambayo
yanaweza kukuzuia kubatizwa.

4. Mjue Yehova
vizuri zaidi
Unahitaji kumjua Yehova vizuri kadiri gani
kabla ya kubatizwa? Unahitaji kuwa na
ujuzi unaokuchochea kumpenda na kuta- 5. Shinda mambo yanayoweza
mani kumfurahisha. Onyesha VIDEO ili kukuzuia kubatizwa
uone jinsi ambavyo wanafunzi wa Biblia
ulimwenguni pote wamefanya hivyo. Tunapoamua kujiweka wakfu na kubatizwa,
Kisha mzungumzie swali linalofuata. sisi sote hukabili changamoto. Ili kuona mfano,
onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali
VIDEO: Barabara yanayofuata.
(
Inayoongoza Kwenye
Ubatizo (3:56) ( VIDEO: Kumpenda Yehova Hutusaidia
Kushinda Vizuizi (5:22)

˙ Katika video hiyo, ni nini kilichowa-


saidia wanafunzi hao wa Biblia waji-
tayarishe kwa ajili ya ubatizo? ˙ Katika video hiyo, Narangerel alihitaji kushinda
vizuizi gani ili aanze kumtumikia Yehova?
Soma Waroma 12:2, kisha mzungumzie ˙ Kumpenda Yehova kulimsaidiaje kushinda
maswali haya: vizuizi hivyo?
˙ Je, una shaka yoyote kuhusu mafu-
ndisho ya Biblia au ikiwa Mashahidi Soma Methali 29:25 na 2 Timotheo 1:7,
wa Yehova wanafundisha ukweli? kisha mzungumzie swali hili:
˙ Ikiwa una shaka, unaweza kufanya ˙ Tutapata wapi ujasiri wa kushinda vizuizi?
nini?
7. Onyesha shukrani kwa
upendo ambao Yehova
amekuonyesha
Kadiri unavyozidi kufikiria jinsi Yehova
anavyokupenda, ndivyo utakavyozidi
kuwa mwenye shukrani na kutamani
kuendelea kumtumikia milele. Soma Za-
buri 40:5, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Ni baraka gani kutoka kwa Yehova
ambazo hasa zinakuchochea
kumshukuru?

Nabii Yeremia alimpenda Yehova


na neno lake, na alithamini sana
kuwa na pendeleo la kutangaza jina
la Yehova. Alisema hivi: “Neno lako
likawa furaha na shangwe ya moyo
6. Uwe na hakika kwamba wangu, kwa maana nimeitwa kwa jina
Yehova atakusaidia lako, Ee Yehova Mungu.” (Yeremia 15:16)
Jibu maswali haya:
Yehova atakusaidia kufanya mambo yanayomfurahisha. ˙ Kwa nini ni pendeleo la pekee
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali kuwa Shahidi wa Yehova?
yanayofuata.
˙ Je, ungependa kubatizwa na
kuwa Shahidi wa Yehova?
( VIDEO: Yehova Mungu Atakusaidia
(2:50) ˙ Je, kuna jambo lolote linalokuzuia
kubatizwa?
˙ Unafikiri unahitaji kufanya nini
ili ufikie lengo la kubatizwa?
˙ Katika video hiyo, ni nini kilichofanya mwanafunzi
huyo wa Biblia asite kubatizwa?
˙ Alijifunza jambo gani ambalo lilimsaidia
kumtegemea Yehova zaidi?

Soma Isaya 41:10, 13, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Unawezaje kuwa na hakika kwamba utatimiza
ahadi unayotoa unapojiweka wakfu?

WATU FULANI HUSEMA: “Ninaogopa kwamba nikibatizwa nitashindwa


kutimiza mambo ambayo niliahidi.”
˙ Je, unahisi hivyo?

197
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova atakusaidia ushinde jambo
lolote linalokuzuia kubatizwa. Chunguza mambo ambayo
yanapaswa kuwa msingi wa
uamuzi wako wa kubatizwa.
Ungejibuje? “Je, Uko Tayari Kubatizwa?”
(Mnara wa Mlinzi, Machi 2020)
˙ Unahitaji ujuzi mwingi kadiri
gani kuhusu Biblia kabla ya
kubatizwa?
˙ Huenda ukahitaji kufanya maba-
diliko gani kabla ya kubatizwa?
˙ Kwa nini hupaswi kuruhusu woga Jifunze jinsi ya kushinda cha-
ngamoto hususa zinazoweza
ukuzuie kubatizwa?
kukuzuia kubatizwa.
“Ni Nini Kinachonizuia
Kubatizwa?” (Mnara wa Mlinzi,
Machi 2019)

Tarehe ambayo sehemu hii ( 1:10 Ona jinsi mwanamume


imekamilishwa fulani alivyoshinda vizuizi
vikubwa ili abatizwe.
‘Kwa Nini Unasita Kubatizwa?’

Lengo
N Chunguza “Je, Niko Tayari Ku-
hubiri Pamoja na Kutaniko?” na
“Je, Niko Tayari Kubatizwa?”
mwishoni mwa Sehemu ya 4. ( 7:21 Mwanzoni, mwanamume ana-
yeitwa Ataa alisita kubatizwa.
N Lengo lingine: Ona jambo lililomchochea
achukue hatua hii muhimu.
Je, Kweli Ninastahili
Baraka Hizi Zote?

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 47, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw 198
MAMBO MAKUU YA
SEHEMU YA 3
Zungumzia maswali yafuatayo
pamoja na mwalimu wako:

1. Soma Methali 27:11. 8. Soma 1 Wakorintho 6:9, 10.


˙ Kwa nini unapaswa kuwa ˙ Biblia ina maoni gani kuhusu ngono?
mshikamanifu kwa Yehova? Je, unakubaliana na maoni hayo?
(Ona Somo la 34.) ˙ Biblia inatoa mwongozo gani
kuhusu kunywa kileo?
2. Unawezaje kufanya maamuzi mazuri (Ona Somo la 41 na 43.)
ikiwa Biblia haitaji amri hususa?
(Ona Somo la 35.) 9. Soma Mathayo 19:4-6, 9.
˙ Mungu ameweka viwango gani
3. Unawezaje kuwa mnyoofu kuhusu ndoa?
katika mambo yote?
˙ Kwa nini ndoa na talaka zinapaswa
(Ona Somo la 36.)
kuandikishwa kisheria?
(Ona Somo la 42.)
4. Soma Mathayo 6:33.
˙ Unawezaje kuendelea “kuutafuta 10. Ni baadhi ya sherehe na sikukuu gani
kwanza Ufalme” inapohusu kazi na pesa? ambazo hazimfurahishi Yehova, na kwa nini?
(Ona Somo la 37.) (Ona Somo la 44.)

11. Soma Yohana 17:16 na Matendo 5:29.


5. Ni kwa njia gani unaweza kuonyesha
kwamba unathamini uhai kama ˙ Unawezaje kuepuka kuunga mkono
Yehova anavyouthamini? upande wowote?
(Ona Somo la 38.) ˙ Ikiwa sheria za wanadamu zinapingana na
sheria za Mungu, unapaswa kufanya nini?
6. Soma Matendo 15:29. (Ona Somo la 45.)
˙ Unawezaje kutii amri ya Yehova 12. Soma Marko 12:30.
kuhusu damu?
˙ Unawezaje kuonyesha kwamba
˙ Je, unafikiri maagizo yake yanafaa? unampenda Yehova?
(Ona Somo la 39.) (Ona Somo la 46 na 47.)
7. Soma 2 Wakorintho 7:1. Maswali yako:
˙ Inamaanisha nini kuwa safi
kimwili na kiadili?
(Ona Somo la 40.)
SEHEMU YA 4
Wazo Kuu: Jifunze jinsi
unavyoweza kubaki katika
upendo wa Mungu

MASOMO
48 Chagua Marafiki Wako kwa Hekima
49 Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa
na Furaha—Sehemu ya 1
50 Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa
na Furaha—Sehemu ya 2
51 Unawezaje Kumfurahisha Yehova
Kupitia Mazungumzo Yako?
52 Kwa Nini Mavazi na Mwonekano
Wetu Ni Muhimu?
53 Chagua Burudani Inayomfurahisha Yehova
54 Jukumu la “Mtumwa Mwaminifu
na Mwenye Busara”
55 Unga Mkono Kutaniko Lenu
56 Dumisha Umoja Katika Kutaniko
57 Ukitenda Dhambi Nzito Unapaswa
Kufanya Nini?
58 Endelea Kuwa Mshikamanifu kwa Yehova
59 Unaweza Kuvumilia Mateso
60 Endelea Kuimarisha Urafiki Wako na Yehova
48

Chagua Marafiki Wako kwa Hekima


Tunafurahi kushirikiana na marafiki wazuri ka- tuchague marafiki kwa hekima! Ikiwa marafiki
tika pindi za furaha. Pia, marafiki wazuri hu- wetu wanampenda Mungu, tutanufaika tunapo-
tuimarisha tunapokabili matatizo. Lakini Biblia shirikiana nao, nao watanufaika pia. Kwa kufa-
inatuonya kwamba si kila mtu anafaa kuwa rafi- nya hivyo, ‘tutaendelea kutiana moyo na kuje-
ki yetu wa karibu. Basi unawezaje kuchagua ma- ngana.’—1 Wathesalonike 5:11.
rafiki wazuri? Fikiria maswali yafuatayo.
2. Yehova anahisije kuhusu marafiki
1. Marafiki unaochagua wanaathirije tabia yako? unaochagua?
Sisi huiga tabia za watu tunaoshirikiana nao. Yehova huchagua marafiki wake kwa makini.
Tunaweza kuiga tabia nzuri au mbaya, iwe tuna- “Ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.”
shirikiana nao moja kwa moja au kwenye mita- (Methali 3:32) Yehova atahisije ikiwa tutacha-
ndao ya kijamii. Biblia inasema hivi: “Anayete- gua marafiki ambao hawampendi? Atahuzunika
mbea na wenye hekima atakuwa na hekima, sana! (Soma Yakobo 4:4.) Lakini ili tumfurahi-
lakini anayeshirikiana na wapumbavu [wale she Yehova na tuwe rafiki zake, tunapa-
ambao hawampendi Yehova] ataumia.” (Me- swa kuepuka kushirikiana na watu wenye ma-
thali 13:20) Marafiki wanaompenda na kumwa- zoea mabaya. Tunapaswa kumkaribia Yehova
budu Yehova wanaweza kukusaidia kuwa na na kushirikiana na wale wanaompenda.—Zaburi
uhusiano wa karibu pamoja naye, na kukusai- 15:1-4.
dia kufanya maamuzi mazuri. Lakini tukishiri-
kiana kwa ukaribu na watu ambao hawampe-
ndi Yehova, uhusiano wetu pamoja na Yehova
utadhoofika. Ndiyo sababu Biblia inatutia moyo

201
CH I M BA ZAI DI

Chunguza kwa nini ni muhimu kuchagua marafiki wanaofaa


na uone jinsi ya kujenga urafiki utakaokunufaisha.

3. Epuka kushirikiana 4. Tunaweza kuchagua marafiki


na watu wabaya wenye umri na hali mbalimbali
Watu wasiompenda Mungu na viwango Biblia inazungumza kuhusu Daudi na Yonathani,
vyake si marafiki wazuri. Onyesha VIDEO, wanaume walioishi katika taifa la kale la Israeli.
kisha mzungumzie swali linalofuata. Umri wao na hali zao zilitofautiana sana, lakini
walikuwa marafiki wa karibu. Soma 1 Samweli 18:1,
( VIDEO: Jifunze Kukataa kisha mzungumzie swali hili:
Mashirika Mabaya (6:17)
˙ Kwa nini hatupaswi kuchagua tu marafiki
wenye umri au hali kama zetu?

˙ Tunawezaje kuanza kushirikiana Soma Waroma 1:11, 12, kisha mzungumzie


na watu wabaya bila kujua? swali hili:
˙ Marafiki wanaompenda Yehova wanaweza
Soma 1 Wakorintho 15:33, kisha
kutiana moyo jinsi gani?
mzungumzie maswali haya:
˙ Ni watu gani ambao hupaswi Katika video inayofuata, ona jinsi ndugu mmoja
kushirikiana nao? Kwa nini? kijana alivyopata marafiki mahali asipotarajia.
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali
Soma Zaburi 119:63, kisha mzungumzie yanayofuata.
swali hili:
˙ Unapaswa kuchagua marafiki wa ( VIDEO: Pata Marafiki Mahali
aina gani? Usipotarajia (5:06)

˙ Katika video hiyo, kwa nini wazazi wa Akil


walikuwa na wasiwasi kuhusu marafiki
alioshirikiana nao shuleni?
˙ Kwa nini mwanzoni alivutiwa na marafiki hao?
˙ Ni nini ambacho kilimsaidia kushinda hisia
za upweke?

Tunda moja lililooza linaweza kuharibu


matunda mengine yote. Rafiki mmoja
mbaya anawezaje kukuathiri?
Ili uwe na marafiki wazuri,
unapaswa kuwa rafiki mzuri

5. Jinsi ya kusitawisha urafiki mzuri (

Jifunze jinsi unavyoweza kupata marafiki wazuri,


na jinsi unavyoweza kuwa rafiki mzuri. Onyesha VIDEO. VIDEO: Rafiki wa Kweli
Soma Methali 18:24 na 27:17, kisha mzungumzie maswali haya: Ni Nani? (4:14)

˙ Marafiki wa kweli wanawezaje kusaidiana?


˙ Je, una marafiki wazuri kama hao? Ikiwa huna,
unawezaje kusitawisha urafiki kama huo?

Soma Wafilipi 2:4, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Ili uwe na marafiki wazuri, unapaswa kuwa rafiki mzuri.
Unawezaje kuwa rafiki mzuri?

WATU FULANI HUSEMA: “Bora kuwa na rafiki yeyote kuliko kukosa rafiki.”
˙ Wewe una maoni gani?

203
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Tunapochagua marafiki kwa
hekima, tunamfurahisha Yehova Ona jinsi marafiki wazuri
na kujinufaisha pia. wanavyoweza kutusaidia
wakati wa matatizo.
“Imarisha Urafiki
Ungejibuje? Wako Pamoja na Wengine
Kabla ya Mwisho Kufika”
˙ Kwa nini Yehova angependa (Mnara wa Mlinzi, Novemba 2019)
tuchague marafiki wazuri?
˙ Tunapaswa kuepuka marafiki
wa aina gani?
˙ Unawezaje kusitawisha urafiki Chunguza mambo
unayoweza kufanya ili
imara na watu wanaofaa?
kupata marafiki wazuri.
“Ninaweza Kupata Marafiki
Wazuri Jinsi Gani?” (Maswali
Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Ya-
fanyayo Kazi, Buku la 1, sura ya 8)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 4:12 Unapaswa kujua nini


kuhusu kuwa na marafiki
kwenye mitandao ya kijamii?
Tumia Mitandao ya Kijamii
Lengo kwa Hekima

N Wafahamu watu wengi


zaidi kutanikoni.

N Lengo lingine:
Katika simulizi “Nilitamani
Sana Kuwa na Baba,” ona sa-
babu zilizofanya mwanamume
fulani atafute marafiki wapya.
“Biblia Inabadili Maisha”
(Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 2012)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 48, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
49

Jinsi Familia Yako Inavyoweza


Kuwa na Furaha—Sehemu ya 1
Mwanamume na mwanamke waliofunga ndoa 2. Biblia inawapa wake ushauri gani?
hivi karibuni, hutumaini kwamba furaha waliyo- Neno la Mungu linasema “mke anapaswa ku-
kuwa nayo siku ya harusi itadumu milele. Na hilo mheshimu sana mume wake.” (Waefeso 5:33)
linawezekana. Wakristo ambao wamekuwa kati- Anawezaje kufanya hivyo? Anaweza kufikiria
ka ndoa kwa muda mrefu, na ambao wamejita- sifa nzuri za mume wake na jitihada anazofa-
hidi kabisa kufuata ushauri wa Biblia wanajua nya ili kumtunza yeye na watoto wao. Anaonye-
kwamba hilo linawezekana. sha heshima kwa kuunga mkono maamuzi ya
mume wake na kuzungumza naye kwa fadhi-
1. Biblia inatoa ushauri gani kwa waume?
li. Pia, anasema mambo mazuri kumhusu mume
Yehova amempa mume jukumu la kuwa kichwa wake anapozungumza na watu wengine, hata
cha familia. (Soma Waefeso 5:23.) Yehova ana- kama mume wake si mwabudu wa Yehova.
tarajia mume afanye maamuzi yatakayoinu-
faisha familia. Biblia inawashauri hivi waume: 3. Mume na mke wanawezaje kuimarisha
“Endeleeni kuwapenda wake zenu.” (Waefe- ndoa yao?
so 5:25) Hilo linamaanisha nini? Mume mwenye Biblia inasema hivi kuhusu watu waliofunga
upendo humtendea mke wake kwa fadhili wana- ndoa: “Hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
pokuwa nyumbani na pia hadharani. Anahakiki- (Mathayo 19:5) Hilo linamaanisha kwamba wa-
sha kwamba mke wake yuko salama na anafa- napaswa kujitahidi sana kuepuka jambo lolote
nya yote anayoweza ili kumtimizia mahitaji yake linaloweza kudhoofisha upendo kati yao. Wana-
ya kimwili na ya kihisia. (1 Timotheo 5:8) Jambo fanya hivyo kwa kutumia muda mwingi pamoja,
muhimu zaidi, anamsaidia mke wake kusitawi- na pia kuzungumza waziwazi na kwa upendo ku-
sha urafiki wa karibu na Yehova. (Mathayo 4:4) husu mawazo na hisia zao. Hawaruhusu mtu
Kwa mfano, anaweza kusali na kusoma Bib- au kitu kingine chochote kuwa muhimu kuliko
lia pamoja na mke wake. Mume anapomtendea mwenzi wao wa ndoa, isipokuwa Yehova. Wana-
mke wake kwa upendo na kumjali, anadumisha kuwa waangalifu sana ili wasisitawishe uhusia-
urafiki mzuri na Yehova.—Soma 1 Petro 3:7. no usiofaa na mtu mwingine yeyote.

205
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kanuni za Biblia ambazo zinaweza


kuimarisha ndoa yenu.

4. Mume—mpende na
kumjali mke wako
5. Mke—mpende
Biblia inasema kwamba “waume wanapaswa na kumheshimu
kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.”
(Waefeso 5:28, 29) Hilo linamaanisha nini?
mume wako
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali Biblia inamtia moyo mke amheshimu mume
linalofuata. wake, iwe mume ni mtumishi wa Yehova au la.
Soma 1 Petro 3:1, 2, kisha mzungumzie
( VIDEO: Mume, Mpende Mke maswali haya:
Wako Kama Unavyojipenda
Mwenyewe (9:53) ˙ Ikiwa mume wako si mwamini, bila shaka
unatamani sana awe mwabudu wa Yehova.
Unafikiri ni njia gani nzuri ya kumsaidia,
˙ Ni kwa njia gani mume anaweza kuonyesha je, ni kumhubiria kila wakati au ni kuwa mke
kwamba anampenda na kumjali mke wake? mwenye fadhili, heshima, na tabia nzuri?
Kwa nini?
Soma Wakolosai 3:12, kisha mzungumzie
swali hili: Mume na mke wanaweza kufanya maamuzi ma-
˙ Mume anawezaje kuonyesha sifa hizi zuri pamoja. Hata hivyo, wakati mwingine hue-
katika ndoa yake? nda mke asikubaliane na maoni ya mume wake.
Katika hali hiyo, mke anaweza kueleza maoni
yake kwa utulivu na heshima, lakini anapaswa
6. Mnaweza kushinda
matatizo katika ndoa
Hakuna ndoa iliyo kamilifu. Kwa hiyo, mume
na mke wanapaswa kushirikiana ili kushinda
matatizo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie
maswali yanayofuata.

( VIDEO: Jinsi ya Kuimarisha


Kifungo cha Ndoa (5:44)

˙ Katika video hiyo, ni mambo gani yanayoo-


nyesha kwamba uhusiano kati ya mume na
mke ulianza kudhoofika?
˙ Walifanya nini ili kuimarisha ndoa yao?

Soma 1 Wakorintho 10:24 na Wakolosai 3:13.


Baada ya kusoma kila andiko, zungumzieni
swali hili:
˙ Kufuata ushauri huo kunawezaje
kuimarisha ndoa?

Biblia inasema kwamba tunapaswa kuheshi-


miana. Kumheshimu mtu kunatia ndani kumte-
ndea kwa njia ya fadhili na staha. Soma Waroma
12:10, kisha mzungumzie maswali haya:
kutambua kwamba Yehova amempa mume juku-
mu la kufanya maamuzi yatakayoinufaisha fa- ˙ Je, mume au mke anapaswa kutarajia kwa-
milia. Mke anapaswa kufanya yote anayoweza ili mba mwenzi wake ndiye anayepaswa kuwa
kuunga mkono uamuzi wa mume wake. Akifanya wa kwanza kuonyesha heshima? Kwa nini?
hivyo, atachangia mazingira yenye furaha nyu-
mbani. Soma 1 Petro 3:3-5, kisha mzungumzie
swali hili:
˙ Yehova anahisije mke anapomheshimu
mume wake?

WATU FULANI HUSEMA: “Mimi na mwenzi wangu hatuna uhusiano wa karibu kama zamani.”
˙ Unawezaje kuwaeleza kwamba Biblia inaweza kuwasaidia?

207
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Mume na mke wanaweza kuwa
na furaha ikiwa wanapendana, Jifunze mapendekezo yana-
wanaheshimiana, na kutumia yoweza kuwasaidia muwe
kanuni za Biblia. na familia yenye furaha.
Unaweza Kuwa na Familia
Yenye Furaha (broshua)
Ungejibuje?
˙ Mume anawezaje kuchangia
furaha katika ndoa?
˙ Mke anawezaje kuchangia
furaha katika ndoa? ( 4:26 Tazama video ya muziki ina-
yoonyesha baraka za kufuata
˙ Ikiwa umefunga ndoa, ni kanuni
ushauri wa Mungu katika ndoa.
gani ya Biblia inayoweza kuimari-
sha ndoa yenu? Nimezama Katika Mapenzi

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza maana ya kujitiisha


chini ya ukichwa wa mume.
“Wanawake—Kwa Nini
Mjitiishe Chini ya Ukichwa?”
Lengo (Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 2010)

N Ikiwa umefunga ndoa, zungu-


mzia pamoja na mwenzi wako
mojawapo ya makala kuhusu
ndoa iliyo kwenye jw.org/sw.
( 7:12 Ona jinsi ushauri wa Biblia
N Lengo lingine: unavyoweza kuwasaidia
wale waliofunga ndoa.
Biblia Iliokoa Ndoa Yetu

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 49, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
50

Jinsi Familia Yako Inavyoweza


Kuwa na Furaha—Sehemu ya 2
Watoto ni zawadi kutoka kwa Yehova. Anataka 3. Mnawezaje kumkaribia Mungu zaidi
wazazi waitunze zawadi hiyo. Yehova ameandaa mkiwa familia?
ushauri wenye hekima unaoweza kuwasaidia wa- Ikiwa wewe ni mzazi, bila shaka unataka wato-
zazi kuwalea watoto. Pia, ameandaa ushauri to wako wampende Yehova kama wewe unavyo-
unaoweza kuwasaidia watoto kuchangia furaha mpenda. Unawezaje kufanikiwa kufanya hivyo?
katika familia. Kwa kufuata ushauri huu wa Biblia: “Nawe la-
zima uyakazie [maneno ya Yehova] kwa wa-
1. Yehova amewapatia wazazi ushauri gani?
nao na kuongea kuyahusu unapoketi nyumbani
Yehova anataka wazazi wawapende watoto wao mwako na unapotembea barabarani.” (Kumbu-
na watumie muda mwingi iwezekanavyo pamoja kumbu la Torati 6:7) ‘Kukazia’ kunamaanisha ku-
nao. Pia, Yehova anataka wazazi wawalinde wa- fundisha jambo kwa kulirudia. Huenda unajua
toto wao wasipate madhara na watumie kanu- kwamba ili watoto wakumbuke jambo unalowa-
ni za Biblia kama msingi wa kuwazoeza watoto fundisha unahitaji kulirudia tena na tena. Andi-
wao. (Methali 1:8) Anawaambia hivi akina baba: ko hili linamaanisha kwamba unapaswa kuwa na
“Endeleeni kuwalea [watoto wenu] katika . . . muda wa kuzungumza na watoto wako kwa uka-
maagizo ya Yehova.” (Soma Waefeso 6:4.) Ye- waida kumhusu Yehova. Ni vizuri kutenga wakati
hova anafurahi wazazi wanapofuata mwongozo kila juma ili kumwabudu Yehova mkiwa familia.
wake wanapowalea watoto wao, na pia wana- Ikiwa huna watoto, bado unaweza kunufaika iki-
poepuka kumpa mtu mwingine jukumu hilo. wa utatenga wakati kila juma ili kujifunza Neno la
2. Yehova anawapa watoto ushauri gani? Mungu.
Yehova anawaagiza hivi watoto: “Watiini waza-
zi wenu.” (Soma Wakolosai 3:20.) Watoto wa-
napowaheshimu na kuwatii wazazi wao, wana-
mfurahisha Yehova na wazazi wao pia. (Methali
23:22-25) Yesu aliweka mfano mzuri alipokuwa
mtoto. Ingawa alikuwa mkamilifu, aliwatii na ku-
waheshimu wazazi wake.—Luka 2:51, 52.

209
CH I M BA ZAI DI

Chunguza mapendekezo yanayoweza kuchangia


furaha na usalama katika familia.

4. Wafundishe watoto
wako kwa upendo
Kumfundisha mtoto kunaweza kutokeza changamoto.
Biblia inawezaje kukusaidia? Soma Yakobo 1:19, 20,
kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Wazazi wanaweza kuonyeshaje upendo
wanapozungumza na watoto wao?
˙ Kwa nini mzazi hapaswi kamwe kuwatia
watoto wake nidhamu akiwa amekasirika? 

 Katika Biblia, “nidhamu” inatia ndani kufundisha, kuongoza,


na kurekebisha. Lakini haihusishi kamwe kumtendea mtoto
vibaya au kwa ukatili.—Methali 4:1.

(
5. Walinde watoto wako
Ili uwalinde watoto wako wasitendewe vibaya kingono,
VIDEO: Walinde Watoto Wako
ni muhimu sana uzungumze waziwazi na kila mtoto kuhusu
Kutokana na Uovu (2:58) ngono. Huenda isiwe rahisi kufanya hivyo. Onyesha VIDEO,
kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
˙ Kwa nini ni vigumu kwa baadhi ya wazazi kuzungumza
na watoto wao kuhusu ngono?
Je, wajua?
˙ Wazazi fulani wametumia njia gani kuwaeleza watoto
Mashahidi wa Yehova wameandaa wao kuhusu ngono?
habari nyingi zinazoweza kuwasai-
dia wazazi kuwaeleza watoto wao Kama ilivyotabiriwa, uovu unazidi kuongezeka katika
kuhusu ngono, na jinsi ya kuwalinda ulimwengu wa Shetani. Soma 2 Timotheo 3:1, 13,
wasitendewe vibaya kingono? Kwa kisha mzungumzie swali hili:
mfano, tazama:
˙ Baadhi ya watu waovu waliotajwa kwenye mstari wa 13
 Walinde Watoto Wako (video)
wanawatendea watoto vibaya kingono. Basi, kwa nini ni
 Jifunze Kutoka kwa Mwalimu muhimu kwa wazazi kuzungumza waziwazi na watoto wao
Mkuu, sura ya 10 na 32
kuhusu ngono na kuwaeleza jinsi wanavyoweza kujilinda
 “Wafundishe Watoto Wako Kuhu- dhidi ya watu wanaoweza kuwatendea vibaya?
su Ngono” (Amkeni! Na. 5 2016)
6. Waheshimu wazazi wako ˙ Kwa nini ni muhimu kijana azungumze
kwa heshima na wazazi wake?
Watoto na vijana wanaweza kuwaonyesha wazazi ˙ Kijana anawezaje kuzungumza na wazazi
wao heshima kupitia jinsi wanavyozungumza nao. wake kwa heshima?
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yana-
yofuata. Soma Methali 1:8, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kijana anapaswa kutendaje anapopata
( VIDEO: Ninawezaje Kuzungumza mwongozo kutoka kwa wazazi wake?
na Wazazi Wangu? (2:19)

7. Jinsi ya kumwabudu ( VIDEO: Ibada ya Familia


Yehova mkiwa familia —Changamoto na Baraka
(8:04)
Familia za Mashahidi wa Yehova hutenga muda hususa
kila juma ili kumwabudu Yehova pamoja. Ibada hiyo ya
familia inahusisha mambo gani? Mambo mnayoweza kufanya
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata. katika ibada ya familia:
˙ Familia inawezaje kupanga ratiba ya kufanya Ibada  Kutayarisha mikutano ya kutaniko.
ya Familia kwa ukawaida?  Kusoma na kuzungumzia simulizi la
˙ Wazazi wanawezaje kufanya ibada ya familia iwe ye- Biblia ambalo familia yenu itafurahia.
nye kunufaisha na kufurahisha?—Ona picha mwa-  Ikiwa mna watoto, pakua au uchapishe
nzoni mwa somo hili. mojawapo ya makala ya watoto iliyo
kwenye jw.org/sw.
˙ Ni nini kinachoweza kufanya iwe vigumu kwa familia
yenu kujifunza pamoja?  Ikiwa mna vijana, zungumzieni
mojawapo ya makala kuhusu
Katika taifa la kale la Israeli, Yehova alitaka familia vijana kwenye jw.org/sw.
zizungumze kwa ukawaida kuhusu Maandiko. Soma  Igizeni simulizi la Biblia pamoja
Kumbukumbu la Torati 6:6, 7, kisha mzungumzie na watoto wenu.
swali hili:  Tazameni na mzungumzie mojawapo
ya video kwenye jw.org/sw.
˙ Unawezaje kutumia kanuni hii?

WATU FULANI HUSEMA: “Watoto hawawezi kuielewa Biblia.”


˙ Wewe una maoni gani?

211
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova anataka wazazi wawapende,
wawafundishe, na kuwalinda watoto Mtoto anapaswa kujifunza ma-
wao, pia, anataka watoto wawaheshi- somo gani yatakayomsaidia
mu na kuwatii wazazi wao, na anataka atakapokuwa mtu mzima?
familia zimwabudu pamoja. “Masomo Sita Muhimu
ya Kuwafundisha Watoto”
(Amkeni! Na. 2 2019)
Ungejibuje?
˙ Wazazi wanawezaje kuwafundi-
sha na kuwalinda watoto wao?
˙ Watoto wanawezaje kuwaheshi- Jifunze ushauri ambao
mu wazazi wao? Biblia inawapa wale wanao-
watunza wazazi waliozeeka.
˙ Kuna manufaa gani ya kutenga
wakati kila juma ili kumwabudu “Biblia Inasema Nini Kuhusu
Kutunza Wazazi Waliozeeka?”
Yehova mkiwa familia?
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 5:58 Ona mwanamume ambaye


hakujua jinsi ya kuwalea
watoto alivyofanikiwa
kuwa baba mzuri.
Lengo Yehova Alitufundisha
Kuwalea Watoto Wetu
N Waombe wengine kutanikoni
wakueleze mambo mnayoweza
kufanya katika ibada yenu ya
familia.
Jifunze jinsi akina baba wana-
N Lengo lingine: vyoweza kuimarisha uhusiano
wao na watoto wao wa kiume.
“Akina Baba Wanawezaje
Kuwa na Uhusiano wa
Karibu na Wana Wao?”
(Mnara wa Mlinzi, Novemba 1,
2011)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 50, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
51

Unawezaje Kumfurahisha Yehova


Kupitia Mazungumzo Yako?
Yehova alipotuumba alitupatia zawadi nzuri nye kuudhi, yanayokusudiwa kuumiza hisia za
sana, yaani, uwezo wa kuzungumza. Je, anaja- mtu mwingine. Pia, tunapaswa kuepuka kupiga
li jinsi tunavyotumia zawadi hiyo? Bila shaka, porojo na kuwachongea wengine.—Soma Me-
anajali! (Soma Yakobo 1:26.) Basi, tunawezaje thali 16:28.
kutumia uwezo wetu wa kuzungumza kwa njia
inayomfurahisha Yehova? 3. Ni nini ambacho kitatusaidia kuzungumza
kwa njia itakayowajenga wengine?
1. Tunawezaje kutumia vizuri zawadi ya Mara nyingi mambo tunayosema yanafunua
kuzungumza? kile kilicho moyoni mwetu au jambo ambalo
Biblia inatuambia hivi: “Endeleeni kutiana tunafikiria. (Luka 6:45) Basi, tunapaswa ku-
moyo na kujengana.” (1 Wathesalonike 5:11) jizoeza kufikiria mambo yenye kujenga, yaa-
Je, kuna watu ambao unafikiri wanahitaji kutiwa ni, mambo yaliyo ya uadilifu, yaliyo safi kiadili,
moyo? Unaweza kufanya nini ili kuwatia moyo? yanayopendeka, na yanayostahili sifa. (Wafili-
Wahakikishie kwamba unawajali. Labda una- pi 4:8) Ili tukazie fikira mambo hayo, tunapa-
weza kuwaambia mambo mazuri unayopenda swa kuchagua burudani na marafiki wetu kwa
kuwahusu. Je, kuna andiko ambalo linaweza ku- hekima. (Methali 13:20) Pia, tunahitaji kufikiria
mtia moyo mtu fulani unayemjua? Kuna maa- kwa makini mambo tutakayosema kabla ya ku-
ndiko mengi ambayo unaweza kutumia. Kumbu- zungumza. Fikiria jinsi maneno yako yatakavyo-
ka kwamba unaweza pia kuwatia moyo sana waathiri wengine. Biblia inasema hivi: “Mane-
kupitia jinsi unavyozungumza nao. Basi, siku- no yanayosemwa bila kufikiri huchoma kama
zote jitahidi kuzungumza kwa fadhili na upole. upanga, lakini ulimi wa mwenye hekima hupo-
—Methali 15:1. nya.”—Methali 12:18.

2. Tunapaswa kuepuka mazungumzo


ya aina gani?
Biblia inasema: “Neno lililooza lisitoke kinywa-
ni mwenu.” (Soma Waefeso 4:29.) Hilo lina-
maanisha kwamba hatupaswi kutumia lugha
chafu, au kusema maneno yasiyo ya fadhili, ye-

213
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kuzungumza kwa njia itakayomfurahisha


Yehova na itakayowatia moyo wengine.

Ni mambo gani yanayoweza


kuathiri jinsi tunavyozungumza?

4. Uwe mwangalifu kuhusu Soma 1 Wakorintho 15:33, kisha mzungumzie


swali hili:
mambo unayosema
˙ Njia yako ya kuzungumza inaweza kuathiri-
Wakati fulani, sisi husema mambo bila kufikiri waje na burudani na marafiki unaochagua?
na kujuta baadaye. (Yakobo 3:2) Soma Wagalatia
5:22, 23, kisha mzungumzie maswali haya: Soma Mhubiri 3:1, 7, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kati ya sifa hizo, unaweza kumwomba Yehova ˙ Ni wakati gani ambao huenda ikawa jambo
akupe sifa gani ambazo zitakusaidia kudhibi- la hekima kukaa kimya au kusubiri wakati
ti mambo unayosema? Sifa hizo zinawezaje unaofaa ili kuzungumza?
kukusaidia?
5. Sema mambo mazuri 6. Uwe na fadhili unapozungumza
kuwahusu wengine na watu wa familia yako
Tunawezaje kuepuka kusema mambo Yehova anataka tuzungumze na watu wa familia
yanayowaumiza wengine au kusema yetu kwa njia ya fadhili na upendo. Onyesha VIDEO,
mambo yasiyo ya fadhili? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.
kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
( VIDEO: Upendo na Heshima
( VIDEO: Sema ‘Neno Jema kwa Hufanya Familia Ziwe na
Ajili ya Kuwajenga’ Wengine Umoja (3:08)
(4:07)

˙ Ni nini ambacho kitakusaidia uzungumze


˙ Katika video hiyo, kwa nini ndugu kwa fadhili na watu wa familia yako?
huyo alitaka kubadili jinsi alivyozu-
ngumza kuhusu wengine? Soma Waefeso 4:31, 32, kisha mzungumzie
˙ Alifanya nini ili abadili njia yake ya swali hili:
kuzungumza? ˙ Tunaweza kuzungumza jinsi gani na watu
wa familia yetu ili kuwajenga?
Soma Mhubiri 7:16, kisha mzungumzie
swali hili: Yehova alionyesha jinsi alivyohisi kumhusu
˙ Tunapaswa kukumbuka nini tunapo- Yesu, Mwana wake. Soma Mathayo 17:5,
shawishiwa kusema mambo yasiyofaa kisha mzungumzie swali hili:
kuhusu mtu mwingine? ˙ Unawezaje kumwiga Yehova unapozungumza
na watu wa familia yako?
Soma Mhubiri 7:21, 22, kisha mzungumzie
swali hili:
˙ Mistari hii inawezaje kukusaidia
usikasirike mtu anaposema mambo
yasiyofaa kukuhusu?

Tafuta fursa za kuwapongeza wengine

WATU FULANI HUSEMA: “Mimi husema ninachofikiria. Sijali wengine watahisije.”


˙ Je, unakubaliana na maoni hayo? Kwa nini?

215
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Maneno yana nguvu. Tunapaswa
kufikiria kwa makini mambo tunayo- ( 8:04 Ni nini ambacho kitatusaidia
sema, wakati wa kuyasema, na jinsi kuzungumza kwa njia inayo-
tunavyoyasema. wajenga wengine?
Sitawisha Ulimi wa
Wenye Hekima
Ungejibuje?
˙ Unaweza kutumia njia gani kuzu-
ngumza mambo yanayowajenga
wengine?
˙ Tunapaswa kuepuka mazungu- Jifunze mambo yatakayoku-
mzo ya aina gani? saidia kuepuka lugha chafu.
˙ Ni nini ambacho kitatusaidia “Je, Kweli Kutumia
ili sikuzote tuzungumze kwa Lugha Chafu Ni Vibaya?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
njia ya fadhili na inayojenga?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 2:36 Jifunze jinsi unavyoweza


kuepuka kunaswa na mtego
wa kupiga porojo.
Ninawezaje Kuepuka
Lengo Kupiga Porojo?

N Juma hili, jitahidi kumpongeza


mtu katika familia yenu au
kutanikoni.

N Lengo lingine: Ona jinsi Yehova alivyomsaidia


mwanamume fulani aache
kutumia lugha chafu.
“Nilianza Kufikiria kwa Uzito
Mwelekeo wa Maisha Yangu”
(Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 2013)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 51, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
52

Kwa Nini Mavazi na Mwonekano


Wetu Ni Muhimu?
Sisi sote tunapenda kuchagua mavazi tutakayo- kwamba ‘tunamtumikia Mungu,’ ili iwe rahisi
vaa na jinsi tutakavyojipamba. Kuna kanuni za kwa wengine kuona kwamba tunamwabudu Mu-
Biblia zinazoweza kutusaidia kuchagua mavazi ngu wa kweli.—1 Wakorintho 10:31.
na mapambo tunayopenda, na pia yatakayo-
mfurahisha Yehova. Tutazungumzia baadhi ya 2. Kwa nini tunapaswa kuwafikiria waabudu
kanuni hizo katika somo hili. wenzetu tunapochagua mavazi?
Ingawa tuna uhuru wa kuchagua mavazi tuta-
1. Tunapaswa kuongozwa na kanuni gani kayovaa, tunapaswa kufikiria jinsi mwoneka-
tunapochagua mavazi na mapambo? no wetu utakavyowaathiri wengine. Tunajitahi-
Tunapaswa kuchagua “mavazi yanayofaa, kwa di sana kuepuka kumkwaza mtu yeyote. Badala
kiasi na utimamu wa akili,” na kudumisha yake, ‘tunampendeza jirani yetu kwa mema ili
mwonekano safi ambao unaonyesha kwamba kumjenga.’—Soma Waroma 15:1, 2.
‘tunamtumikia Mungu.’ (1 Timotheo 2:9, 10) Fi-
kiria kanuni hizi nne: (1) Tunapaswa kuvaa “ma- 3. Mwonekano wetu unawezaje kuwavutia
vazi yanayofaa.” Kama vile ambavyo umejionea watu kwenye ibada ya kweli?
katika mikutano ya kutaniko, watu wa Yeho- Ingawa tunajitahidi kuvalia kwa njia inayofaa pi-
va wana mapendezi mbalimbali, lakini mavazi ndi zote, tunajitahidi hasa kuvalia vizuri tunapo-
na mitindo yetu ya nywele huonyesha kwamba hudhuria mikutano ya kutaniko na tunaposhiriki
tunamheshimu Mungu tunayemwabudu. (2) Ku- katika huduma. Hatungependa kuwakengeusha
valia “kwa kiasi” humaanisha kwamba mwone- watu wasikazie fikira ujumbe muhimu tunaowa-
kano wetu haupaswi kuchochea hisia za ngono, pelekea. Badala yake, mwonekano wetu unawe-
wala hatupaswi kujielekezea fikira sana. (3) Tu- za kuwavutia watu kujifunza kweli na ‘kulipa-
naonyesha kwamba tuna “utimamu wa akili” mba fundisho la Mwokozi wetu.’—Tito 2:10.
kwa kuepuka kufuata kila mtindo wa mavazi
au mapambo yanayopendwa na wengi. (4) Si-
kuzote mwonekano wetu unapaswa kuonyesha

217
CH I M BA ZAI DI

Chunguza jinsi tunavyoweza kuhakikisha kwamba mavazi na


mwonekano wetu unawasaidia wengine watambue sisi ni Wakristo.

Mwonekano wetu
unaweza kuonyesha
kwamba tunawaheshimu
watu wenye mamlaka.
Ingawa Yehova huona
jinsi tulivyo moyoni,
mwonekano wetu pia
unapaswa kumheshimu

4. Mwonekano wetu mzuri ˙ Je, unafikiri mwonekano wetu ni muhimu


tunapohudhuria mikutano na tunaposhiriki
unamheshimu Yehova katika huduma? Kwa nini?
Ni sababu gani muhimu zaidi inayofanya tufikirie
kwa makini mwonekano wetu? Soma Zaburi 47:2,
kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Kwa kuwa tunamwakilisha Yehova,
tunapaswa kuvalia kwa njia gani?
5. Jinsi ya kufanya Ingawa Wakristo hawako chini ya Sheria ya Musa,
Sheria hiyo inatusaidia kujua maoni ya Yehova.
maamuzi mazuri kuhusu Soma Kumbukumbu la Torati 22:5, kisha mzu-
mavazi na mapambo ngumzie swali hili:

Onyesha VIDEO. ˙ Kwa nini tunapaswa kuepuka kuvaa na


kujipamba kwa njia inayofanya mwanamume
aonekane kama mwanamke au mwanamke
( VIDEO: “Fanyeni Mambo Yote kuonekana kama mwanamume?
kwa Utukufu wa Mungu”
(10:18)
Soma 1 Wakorintho 10:32, 33 na
1 Yohana 2:15, 16, kisha mzungumzie
Iwe mavazi yetu ni ya bei ghali au bei rahisi, maswali haya:
yanapaswa kuwa safi na yanayofaa hali hususa.
˙ Kwa nini tunapaswa kuepuka mwonekano
Soma 1 Wakorintho 10:24 na 1 Timotheo 2:9, 10.
unaoweza kuwaudhi wengine katika eneo
Kisha mzungumzie kwa nini tunapaswa kuepuka
tunaloishi au kutanikoni?
kuvaa . . .
˙ Ni mitindo gani ya mavazi na mapambo
˙ mavazi yasiyo safi na yasiyo nadhifu. inayopendwa katika eneo unaloishi?
˙ mavazi yanayobana sana, yanayoonyesha ˙ Je, unafikiri baadhi ya mitindo hiyo huenda
sehemu za mwili, au yanayochochea hisia isimfae Mkristo? Kwa nini?
za ngono.

Tunaweza kuvaa na kujipamba kwa njia


mbalimbali na bado tukamfurahisha Yehova

WATU FULANI HUSEMA: “Nina haki ya kuvaa kwa njia yoyote ninayotaka.”
˙ Je, unakubaliana na maoni hayo? Kwa nini?

219
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Tunapofanya maamuzi mazuri
kuhusu mwonekano wetu, tuna- Chunguza jinsi mavazi yako
onyesha kwamba tunamheshimu yanavyoweza kuathiri maoni
Yehova na watu wengine. ya wengine kukuhusu.
“Mwonekano Wangu
Unanitambulishaje?”
Ungejibuje? (Makala iliyo kwenye mtandao)

˙ Kwa nini jinsi tunavyovalia na ku-


jipamba ni muhimu kwa Yehova?
˙ Ni kanuni gani zinazopaswa ku-
tuongoza tunapofanya maamuzi Jifunze kwa nini ni jambo la he-
kuhusu mwonekano wetu? kima kufikiria kwa makini kabla
ya kuamua kujichanja chale,
˙ Mwonekano wetu unawezaje
yaani, kuchora tattoo mwilini.
kuathiri maoni ya wengine
“Biblia Inasema Nini
kuhusu ibada ya kweli?
Kuhusu Kujichanja Chale?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Chunguza kanuni nyingine


zinazopaswa kuongoza
maamuzi yetu.
“Je, Mtindo Wako wa
Lengo Mavazi Unamtukuza Mungu?”
(Mnara wa Mlinzi, Septemba 2016)
N Chunguza uone ikiwa unapaswa
kufanya marekebisho kuhusu
mavazi au mapambo yako.

N Lengo lingine: Mwanamke fulani aliyetaka


kumfurahisha Mungu alijifunza
jinsi gani kuheshimu maoni ya
wengine kuhusu mavazi?
“Mavazi na Mapambo Yalini-
zuia Kufanya Maendeleo”
(Amkeni!, Desemba 22, 2003)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 52, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
53

Chagua Burudani
Inayomfurahisha Yehova
Yehova ni “Mungu mwenye furaha.” (1 Timo- Ikiwa tutachagua marafiki wanaompenda Ye-
theo 1:11) Anataka tuwe na furaha na tufurahie hova, wanaweza kutujenga na kutusaidia ku-
maisha. Anafurahi tunapotenga muda ili kuji- chagua burudani inayofaa. Kama tulivyojifu-
furahisha. Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya nza katika Somo la 48, mtu “anayetembea na
kutumia wakati wetu wa kupumzika katika njia wenye hekima atakuwa na hekima.” Kinyume
inayofurahisha na yenye kuridhisha, na wakati chake, tunaposhirikiana kwa ukawaida na watu
uleule inayomfurahisha Yehova. wasiopenda viwango vya Mungu ‘tutaumia.’
—Methali 13:20.
1. Tunapaswa kukumbuka nini tunapochagua
burudani? 2. Kwa nini hatupaswi kutumia muda mwingi
Unapenda kufanya nini unapopumzika? Baa- katika burudani?
dhi ya watu wanapenda kupumzika nyumba- Hata ikiwa burudani tunazochagua zinafaa, tu-
ni wakisoma kitabu, kusikiliza muziki, kuta- napaswa kuwa makini tusitumie muda mwingi
zama sinema, au kutumia Intaneti. Wengine sana. Kwa sababu huenda tukakosa muda wa
hufurahia kutumia wakati pamoja na marafi- kutosha kufanya mambo yaliyo muhimu zaidi.
ki wakipanda milima, kuogelea, au kucheza mi- Biblia inatuhimiza ‘tutumie vizuri kabisa waka-
chezo mbalimbali. Lolote lile tunalochagua ti wetu.’—Soma Waefeso 5:15, 16.
kufanya, tunapaswa kuhakikisha kwamba tuna-
chagua burudani ‘inayokubalika kwa Bwana.’
(Waefeso 5:10) Ni muhimu kuchagua burudani
inayofaa kwa sababu burudani nyingi zinazope-
ndwa leo zinahusisha mambo ambayo Yehova
anachukia kama vile ukatili, ukosefu wa maadi-
li katika ngono, au kuwasiliana na roho waovu.
(Soma Zaburi 11:5.) Ni nini ambacho kitatusai-
dia kuchagua burudani kwa hekima?

221
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi ya kufanya maamuzi mazuri kuhusu burudani.

3. Epuka burudani zisizofaa (

Kwa nini tunapaswa kuwa makini tunapochagua burudani?


Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata. VIDEO: Nichague Burudani ya
˙ Michezo ya kale ya Waroma inafanana jinsi gani Aina Gani? (4:39)
na baadhi ya burudani za leo?
˙ Katika video hiyo, Danny alijifunza nini kuhusu burudani?
Jinsi ya kuchagua
Soma Waroma 12:9, kisha mzungumzie swali hili:
burudani kwa hekima
˙ Mstari huu unawezaje kukusaidia kuchagua
Jiulize hivi:
burudani inayofaa?
 Nini? Je, burudani hii inahusi-
Ni baadhi ya mambo gani ambayo Yehova anachukia? sha jambo lolote ambalo Yeho-
Soma Methali 6:16, 17 na Wagalatia 5:19-21. Baada ya va anachukia?
kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili:  Lini? Je, burudani hii itachukua
muda wa mambo yaliyo muhi-
˙ Ni mambo gani yaliyotajwa katika mistari hii
mu zaidi?
ambayo ni ya kawaida katika burudani za leo?
 Nani? Je, burudani hii itafanya
nishirikiane kwa ukaribu au kwa
ukawaida na watu ambao hawa-
mpendi Yehova?

Ili tuwe salama, tunapaswa kukaa mbali kabisa na hatari.


Hivyo, tunapaswa kuepuka burudani yoyote tunayohisi
kwamba haifai
4. Tumia muda wako kwa hekima (

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.


˙ Ingawa ndugu katika video hiyo hakuwa akitazama VIDEO: Unatumiaje Muda Wako?
jambo lisilofaa, tatizo lilikuwa wapi? (2:45)

Soma Wafilipi 1:10, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Mstari huu unaweza kutusaidiaje kuamua
muda tutakaotumia katika burudani?

5. Chagua burudani zinazofaa


Ingawa baadhi ya burudani hazimfurahishi Yehova,
kuna mambo mengi sana yanayofaa tunayoweza
kufanya ili kujifurahisha. Soma Mhubiri 8:15 na
Wafilipi 4:8, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Unapenda kufurahia burudani gani?

Unaweza kufurahia burudani zinazofaa

WATU FULANI HUSEMA: “Hakuna ubaya wa kufurahia burudani zenye ukatili,


ukosefu wa maadili, au kuwasiliana na roho waovu ikiwa sifanyi mambo hayo.”
˙ Wewe ungesemaje?

223
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova anataka tuchague na
kufurahia burudani zinazofaa. Ni nani aliye na jukumu la
kutuchagulia burudani?
“Je, Mashahidi wa Yehova
Ungejibuje? Huwakataza Wafuasi Wao
Sinema, Vitabu, au Nyimbo
˙ Wakristo wanapaswa kuepuka Fulani?” (Makala iliyo kwenye
burudani za aina gani? mtandao)
˙ Kwa nini tunapaswa kuwa
waangalifu kuhusu muda
tunaotumia katika burudani?
˙ Kwa nini unapaswa kuchagua Jifunze jinsi unavyoweza
kufanya maamuzi mazuri
burudani zinazomfurahisha
kuhusu burudani.
Yehova?
“Je, Tafrija Unayochagua
Inakujenga?” (Mnara wa Mlinzi,
Oktoba 15, 2011)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Katika simulizi “Nilishinda


Chuki Niliyokuwa Nayo,”
ona sababu iliyofanya
mwanamume fulani aba-
dili burudani aliyopenda.
Lengo
“Biblia Inabadili Maisha”
N Tumia sanduku “Jinsi ya Ku- (Mnara wa Mlinzi,
Februari 1, 2010)
chagua Burudani kwa Hekima,”
kuchunguza burudani unazo-
penda.
( 2:02 Ona jinsi mama fulani
N Lengo lingine: anavyofanya uamuzi wa
hekima kuhusu burudani
zinazohusisha hadithi za
ulimwengu wa roho waovu.
Epuka Burudani Zenye Mazoea
ya Kuwasiliana na Roho

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 53, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
54

Jukumu la “Mtumwa Mwaminifu


na Mwenye Busara”
Yesu ndiye Kichwa cha kutaniko la Kikristo. 2. Mtumwa mwaminifu anaandaa chakula
(Waefeso 5:23) Leo, Yesu akiwa mbinguni anao- gani cha kiroho?
ngoza wafuasi wake duniani kupitia “mtumwa Yesu alisema kwamba mtumwa mwaminifu
mwaminifu na mwenye busara.” (Soma Mathayo ‘angewapa Wakristo wenzake chakula chao
24:45.) Kwa kuwa aliwekwa rasmi na Yesu, “mtu- kwa wakati unaofaa.’ (Mathayo 24:45b) Kama
mwa” huyo ana mamlaka kwa kadiri fulani, laki- vile chakula cha kimwili kinavyotusaidia kue-
ni bado anaendelea kuwa mtumwa wa Kristo na ndelea kuwa na nguvu na afya, chakula cha ki-
kuwatumikia ndugu za Kristo. Mtumwa huyo ni roho, yaani, mwongozo kutoka katika Neno la
nani? Naye anatutunza jinsi gani? Mungu, hutupatia nguvu tunazohitaji ili kuende-
lea kuwa washikamanifu kwa Yehova na kuti-
1. “Mtumwa mwaminifu na mwenye busara”
miza kazi ambayo Yesu ametupatia. (1 Timo-
ni nani?
theo 4:6) Tunapata chakula hicho cha kiroho
Sikuzote, Yehova ametumia mwanamume fulani kupitia mikutano, makusanyiko ya mzunguko na
au kikundi kidogo cha wanaume kuwaongoza ya eneo, na pia kupitia machapisho na video zi-
watu wake. (Malaki 2:7; Waebrania 1:1) Baada nazotegemea Biblia ambazo hutusaidia kuelewa
ya kifo cha Yesu, mitume na wazee huko Yerusa- mapenzi ya Mungu na kuimarisha urafiki wetu
lemu ndio walioongoza. (Matendo15:2) Kwa ku- naye.
fuata kielelezo hicho, leo kikundi kidogo cha wa-
zee, yaani, Baraza Linaloongoza la Mashahidi
wa Yehova, huandaa chakula cha kiroho na kue-
lekeza kazi ya kuhubiri. Kikundi hicho ni “mtu-
mwa mwaminifu na mwenye busara ambaye
[Yesu] alimweka rasmi.” (Mathayo 24:45a) Wa-
shiriki wote wa Baraza Linaloongoza ni Wakristo
watiwa-mafuta. Baada ya uhai wao kufikia mwi-
sho hapa duniani, wana tumaini la kutawala pa-
moja na Kristo katika Ufalme wake mbinguni.

225
CH I M BA ZAI DI

Jifunze kwa nini tunahitaji “mtumwa


mwaminifu na mwenye busara,” yaani,
Baraza Linaloongoza.

Baraza Linaloongoza huandaa chakula cha


kiroho, mwongozo, na msaada hususa kwa
Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote

3. Watu wa Yehova wanapaswa 4. Mtumwa mwaminifu


kupangwa kwa utaratibu hupanga kazi yetu
Chini ya mwongozo wa Yesu, Baraza Linaloongo-
ya kuhubiri
za hupanga kazi ya Mashahidi wa Yehova. Kuli- Kazi ya kuhubiri ndiyo kazi muhimu zaidi ambayo
kuwa na mpango kama huo katika kutaniko la Wakristo wa karne ya kwanza walifanya. Soma
Kikristo la karne ya kwanza. Onyesha VIDEO. Matendo 8:14, 25, kisha mzungumzie maswali
haya:
( VIDEO: Tunahitaji Tengenezo
(9:23)
˙ Kati ya Wakristo wa karne ya kwanza,
ni nani walioelekeza kazi ya kuhubiri?
˙ Petro na Yohana waliitikiaje mwongozo
kutoka kwa mitume wenzao?
Soma 1 Wakorintho 14:33, 40, kisha
mzungumzie swali hili: Kazi ya kuhubiri ndiyo kazi muhimu zaidi
˙ Mistari hii inaonyeshaje kwamba inayopangwa na Baraza Linaloongoza.
Yehova anataka Mashahidi wake Onyesha VIDEO.
wawe na utaratibu?
( VIDEO: Tunakazia Fikira Kazi
ya Kuhubiri (1:37)
5. Mtumwa mwaminifu
huandaa mwongozo
Baraza Linaloongoza huandaa mwongozo kwa
Wakristo ulimwenguni pote. Wanaamuaje mwongozo
unaofaa kutolewa? Chunguza jinsi baraza linaloongoza
la Wakristo wa karne ya kwanza lilivyofanya hivyo.
Soma Matendo 15:1, 2, kisha mzungumzie maswali
haya:
˙ Ni suala gani lililosababisha kutoelewana
kati ya Wakristo wa karne ya kwanza?
˙ Paulo, Barnaba, na wengine walitafuta
wapi mwongozo ili kutatua suala hilo?

Soma Matendo 15:12-18, 23-29, kisha


mzungumzie swali hili:
˙ Kabla ya kufanya uamuzi fulani, baraza linaloo-
ngoza lilichunguza nini ili kupata mwongozo wa
Mungu kuhusiana na jambo hilo?—Ona mstari
wa 12, 15, na 28.

Soma Matendo 15:30, 31 na 16:4, 5, kisha


mzungumzie maswali haya:
˙ Wakristo wa karne ya kwanza waliitikiaje
Yesu alikazia umuhimu wa kazi ya mwongozo uliotolewa na baraza linaloongoza?
kuhubiri. Soma Marko 13:10, kisha ˙ Yehova aliwabariki jinsi gani walipotii
mzungumzie maswali haya: mwongozo huo?
˙ Kwa nini Baraza Linaloongoza
linaona kazi ya kuhubiri kuwa Soma 2 Timotheo 3:16 na Yakobo 1:5, kisha
kazi muhimu sana? mzungumzie swali hili:
˙ Kwa nini tunahitaji “mtumwa ˙ Baraza Linaloongoza hutafuta wapi mwongozo
mwaminifu na mwenye busara” ili kufanya maamuzi leo?
ili kupanga kazi hii inayofanywa
ulimwenguni pote?

WATU FULANI HUSEMA: “Ukisikiliza Baraza Linaloongoza, unawafuata wanadamu.”


˙ Ni nini kinachokuthibitishia kwamba Yesu anaelekeza Baraza Linaloongoza?

227
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Baraza Linaloongoza ndiye “mtumwa
mwaminifu na mwenye busara” aliye- Jifunze jinsi Baraza Lina-
wekwa rasmi na Kristo. Wanatoa loongoza lilivyopangwa
mwongozo na kuandaa chakula cha ili kufanya kazi yake.
kiroho kwa Wakristo duniani pote. “Baraza Linaloongoza la Ma-
shahidi wa Yehova Ni Nini?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
Ungejibuje?
˙ Ni nani aliyemweka rasmi
“mtumwa mwaminifu na
mwenye busara”? ( 17:18 Jifunze jinsi Baraza Lina-
˙ Baraza Linaloongoza hututunza loongoza linavyohakikisha
jinsi gani? kwamba tunapokea chakula
cha kiroho kinachofaa.
˙ Je, unaamini kwamba Baraza
Kutokeza Machapisho Sahihi
Linaloongoza ndiye “mtumwa
mwaminifu na mwenye busara”?

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 7:04 Washiriki wa Baraza Linaloo-


ngoza wanahisije kuhusu kazi
ambayo Yesu amewapa?
Pendeleo la Pekee
Lengo
N Kama andiko la 2 Wathesa-
lonike 3:1 linavyotutia moyo,
sali kwa ukawaida kwa Yehova
ukimwomba abariki kazi ya
Baraza Linaloongoza. ( 9:39 Mikutano na makusanyiko
yetu yanathibitishaje kwamba
Yehova anaelekeza Baraza
N Lengo lingine:
Linaloongoza?
Yehova Anawafundisha
Watu Wake

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 54, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
55

Unga Mkono Kutaniko Lenu


Ulimwenguni pote, mamilioni ya watu wana- nga mkono kwa bidii kazi ya kuhubiri kwa ku-
mwabudu Yehova kwa shangwe katika maelfu tumikia wakiwa mapainia. Baadhi ya Mashahi-
ya makutaniko. Wanafurahi kupokea maagizo di wanaweza kusaidia katika ujenzi wa majengo
na mwongozo, na wanaunga mkono kutaniko ya ibada au kuhamia katika kutaniko linalohitaji
kwa bidii katika njia nyingi. Je, unahisi hivyo ku- msaada kwa njia nyingine.
husu kutaniko lenu?
2. Tunawezaje kutumia pesa na mali zetu
1. Unawezaje kutumia muda na nguvu zako kuunga mkono kutaniko?
kuunga mkono kutaniko? Tunaweza ‘kumheshimu Yehova kwa vitu vyetu
Sisi sote tunaweza kuunga mkono kutaniko. vyenye thamani.’ (Methali 3:9) Tunafurahi kuwa
Kwa mfano, je, katika kutaniko lenu kuna watu na pendeleo la kutoa michango ya pesa na mali
wenye umri mkubwa au wenye matatizo ya nyingine ili kuunga mkono kutaniko letu na kazi
afya? Je, unaweza kuwasaidia kufika kwenye ya kuhubiri ulimwenguni pote. (Soma 2 Wakori-
mikutano? Au je, unaweza kuwasaidia kwa njia ntho 9:7.) Michango yetu hutumiwa pia kutoa
nyingine, kama vile kufanya ununuzi au kazi za msaada wakati wa misiba. Wengi huamua “ku-
nyumbani? (Soma Yakobo 1:27.) Pia, tunaweza weka kando kitu fulani” kwa ukawaida ili kutoa
kujitolea kusafisha na kudumisha Jumba letu mchango. (Soma 1 Wakorintho 16:2.) Tunawe-
la Ufalme. Hakuna mtu anayetulazimisha kufa- za kuweka michango yetu katika masanduku ya
nya mambo hayo. Kumpenda Mungu na ndugu michango yaliyo kwenye sehemu zetu za iba-
zetu hutuchochea ‘kujitoa wenyewe kwa hiari.’ da au mtandaoni kupitia donate.jw.org. Yehova
—Zaburi 110:3. anatupatia nafasi ya kuonyesha kwamba tuna-
Mashahidi waliobatizwa wanaweza kuunga mpenda kupitia jinsi tunavyoamua kutumia mali
mkono kutaniko kwa njia nyingine. Akina ndugu zetu.
wenye sifa za kustahili wanaweza kutumikia wa-
kiwa watumishi wa huduma, na baadaye wakiwa
wazee. Akina ndugu na dada wanaweza kuu-

229
CH I M BA ZAI DI

Chunguza baadhi ya njia unazoweza


kuunga mkono kutaniko.

3. Tunaweza kutumia
mali zetu
Yehova na Yesu wanawapenda watu wanaotoa kwa uchangamfu.
(
Kwa mfano, Yesu alimsifu mjane maskini ambaye alitoa mchango
mdogo sana. Soma Luka 21:1-4, kisha mzungumzie maswali haya:
˙ Je, tunahitaji kutoa mchango wa pesa nyingi VIDEO: ‘Jaza Mkono Zawadi
ili kumfurahisha Yehova? kwa Ajili ya Yehova’ (4:47)
˙ Yehova na Yesu wanahisije tunapotoa
michango kwa hiari?

Ili ujifunze jinsi michango yetu inavyotumiwa,


Onyesha VIDEO. Kisha mzungumzie swali linalofuata.
˙ Michango hutumiwaje kutegemeza makutaniko ulimwenguni pote?
4. Tunaweza kujitolea kusaidia (

Katika nyakati za Biblia, waabudu wa Yehova walifanya kazi kwa bidii


ili kudumisha sehemu zao za ibada. Lakini hilo lilihusisha mengi zaidi VIDEO: Kutunza Maeneo
ya kutoa mchango wa pesa. Soma 2 Mambo ya Nyakati 34:9-11, Yetu ya Ibada (3:31)
kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kila Mwisraeli alisaidiaje kutunza nyumba ya Yehova,
au mahali pa ibada?

Ili uone jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyoiga mfano huo,


onyesha VIDEO. Kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
˙ Kwa nini ni muhimu kudumisha Jumba letu la Ufalme
likiwa safi na katika hali nzuri?
˙ Unaweza kusaidia katika njia gani?

5. Akina ndugu Biblia inataja sifa ambazo akina ndugu wanahitaji


ili wastahili kutumikia wakiwa watumishi wa hudu-
wanaweza kujitahidi ma au wazee. Soma 1 Timotheo 3:1-13, kisha
kufikia mapendeleo zaidi mzungumzie maswali haya:

Maandiko yanawatia moyo wanaume Wakristo ˙ Akina ndugu wanaotamani kutumikia


wajitahidi kufanya mengi zaidi ili kuunga mkono wakiwa watumishi wa huduma na wazee
kutaniko. Ili uone mfano, onyesha VIDEO. wanapaswa kuwa na sifa gani?
Kisha ujibu swali linalofuata. ˙ Familia zao zinapaswa kuwa na sifa gani?
—Ona mstari wa 4 na 11.
( VIDEO: Akina Ndugu–Jitahidini ˙ Akina ndugu wanapojitahidi kutimiza sifa
Kufikia Kazi Njema (5:19) hizo, kila mmoja katika kutaniko hunufaikaje?

˙ Katika video hiyo, Ryan alifanya jitihada gani


ili kuunga mkono kutaniko kikamili zaidi?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Mashahidi wa Yehova wanapata wapi pesa za kuendeleza kazi yao?”
˙ Wewe ungejibuje?

231
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova anathamini sana jitihada zetu
za kuunga mkono kutaniko kupitia Chunguza kwa nini leo
muda, nguvu, na mali zetu. Mungu hajawawekea
waabudu wake sheria
ya kutoa sehemu ya kumi.
Ungejibuje? “Biblia Inasema Nini Kuhusu
Kutoa Fungu la Kumi?”
˙ Tunawezaje kutumia muda (Makala iliyo kwenye mtandao)
na nguvu zetu kuunga mkono
kutaniko?
˙ Tunawezaje kutumia mali zetu
kuunga mkono kutaniko? Jifunze maana ya ‘kujitahidi ku-
fikia mapendeleo’ kutanikoni.
˙ Ungependa kuunga mkono
kutaniko kupitia njia gani? “Je, ‘Unajitahidi Kufikia’
Mapendeleo?” (Mnara wa
Mlinzi, Septemba 15, 2014)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 4:25 Ona baadhi ya Mashahidi


wenye ujasiri wanaojidhabihu
sana ili kuwapelekea waabudu
wenzao machapisho.
Lengo Usambazaji wa Machapisho
ya Biblia Nchini Kongo
N Jitolee kusafisha na kudumisha
mahali ambapo kutaniko lenu
hufanyia mikutano.

N Lengo lingine: Ona jinsi kazi yetu


inavyotegemezwa kifedha
kwa njia tofauti sana na
mashirika mengine ya kidini.
“Kazi ya Mashahidi wa
Yehova Inagharimiwaje?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 55, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
56

Dumisha Umoja Katika Kutaniko


Tunapokuwa pamoja na waabudu wenzetu, tu- 3. Utafanya nini hali ya kutoelewana ikitokea
nahisi kama Mfalme Daudi aliyesema hivi: “Jinsi kati yako na Mkristo mwenzako?
ilivyo vema na jinsi inavyopendeza ndugu kukaa Ingawa tuna umoja, sisi si wakamilifu. Waka-
pamoja kwa umoja!” (Zaburi 133:1) Umoja wetu ti fulani, tunaweza kuwavunja moyo waabudu
haujitokezi wenyewe. Kila mmoja wetu anacha- wenzetu au kuwaumiza hisia. Kwa hiyo, Neno
ngia kudumisha umoja huo. la Mungu linatuhimiza hivi: “Endeleeni . . .
kusameheana,” kisha linaongeza hivi: “Kama
1. Watu wa Mungu wana jambo gani la pekee?
vile Yehova alivyowasamehe kwa hiari, nanyi
Unapohudhuria mkutano wa kutaniko katika lazima mfanye vivyo hivyo.” (Soma Wakolosai
nchi nyingine, huenda usielewe lugha inayozu- 3:13.) Sisi humkosea Yehova mara nyingi sana,
ngumzwa, lakini utastarehe na kuhisi kwamba hata hivyo bado anatusamehe. Basi anataka
umekaribishwa. Kwa nini? Kwa sababu duniani tuwasamehe ndugu zetu. Ukigundua kwamba
pote tunajifunza Biblia kwa kutumia machapi- umemkosea mtu fulani, chukua hatua ya kwa-
sho yaleyale. Na tunafanya yote tunayoweza ili nza ili kusuluhisha tatizo hilo.—Soma Mathayo
kuonyeshana upendo. Hata iwe tunaishi wapi, 5:23, 24.
sisi sote ‘tunaliitia jina la Yehova na kumwabu-
du kwa umoja.’—Sefania 3:9, maelezo ya chini.  Maelezo ya Ziada 7 yanazungumzia jinsi ya kusuluhisha
matatizo ya kibiashara na kisheria.
2. Unaweza kufanya nini ili kuchangia umoja?
“Pendaneni sana kutoka moyoni.” (1 Petro
1:22) Unawezaje kufuata ushauri huo? Badala
ya kukazia fikira udhaifu wa wengine, kazia fiki-
ra sifa zao nzuri. Jitahidi kuwafahamu ndugu na
dada wenye malezi mbalimbali badala ya kushi-
rikiana tu na wale walio na mapendezi kama
yako. Pia, tunapaswa kujitahidi kabisa kuondoa
hisia zozote za ubaguzi ambazo huenda tunazo.
—Soma 1 Petro 2:17.

 Maelezo ya Ziada 6 yanazungumzia jinsi upendo unavyo-


wachochea Wakristo waepuke kueneza magonjwa yanayoa-
mbukiza.

233
CH I M BA ZAI DI

Chunguza njia unazoweza kuchangia


umoja na amani katika kutaniko.

4. Epuka ubaguzi 5. Samehe kwa hiari


Tunapaswa kuwapenda ndugu zetu wote.
na ufanye amani
Lakini huenda ikawa vigumu kushirikiana na Yehova hutusamehe kwa hiari ingawa
mtu ambaye tunamwona kuwa tofauti. Ni nini yeye hahitaji kamwe sisi tumsamehe.
kitakachotusaidia? Soma Matendo 10:34, 35, Soma Zaburi 86:5, kisha mzungumzie
kisha mzungumzie maswali haya: maswali haya:
˙ Yehova anakubali watu wa kila aina wawe ˙ Yehova husamehe kwa njia kubwa
Mashahidi wake. Unawezaje kuwa na maoni jinsi gani?
kama ya Yehova kuhusu watu walio na
malezi tofauti na yako? ˙ Kwa nini unathamini msamaha wake?

˙ Ni ubaguzi wa aina gani ulio katika eneo ˙ Ni hali gani zinazoweza kusababisha
lenu ambao ungependa kuepuka? kutoelewana kati yetu na watu wengine?

Soma 2 Wakorintho 6:11-13, kisha mzungumzie Tunawezaje kumwiga Yehova na kuendelea ku-
swali hili: shirikiana na ndugu na dada zetu kwa umoja?
Soma Methali 19:11, kisha mzungumzie
˙ Unawezaje kuimarisha upendo kati yako swali hili:
na ndugu na dada walio na malezi tofauti
na yako? ˙ Mtu anapofanya jambo linalokuudhi au
kukukasirisha, unaweza kufanya nini ili
kusuluhisha hali hiyo?
6. Kazia fikira sifa nzuri
za ndugu na dada zako
Tunapozidi kuwafahamu ndugu na dada zetu,
tunatambua sifa zao nzuri na pia udhaifu wao.
Tunawezaje kukazia fikira sifa zao nzuri?
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali
linalofuata.

( VIDEO: Boresha Utu Wako


wa Kikristo! (5:10)

˙ Ni nini kinachoweza kukusaidia kuona


sifa nzuri za ndugu na dada zako?

Yehova hukazia fikira sifa zetu nzuri.


Soma 2 Mambo ya Nyakati 16:9a,
kisha mzungumzie swali hili:
Utachukua hatua gani ili kufanya amani?
˙ Unahisije kujua kwamba Yehova
anakazia fikira sifa zako nzuri?

Wakati fulani sisi huwakosea wengine. Unapa-


swa kufanya nini hilo linapotokea? Onyesha
VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

( VIDEO: Kufanya Amani Huleta


Baraka (6:01)

˙ Katika video hiyo, dada huyo alichukua ha-


tua gani ili kufanya amani?

Hata almasi maridadi ina kasoro lakini


bado ni yenye thamani. Vivyo hivyo,
ndugu na dada zetu wote si wakamilifu,
lakini ni wenye thamani mbele za Yehova

WATU FULANI HUSEMA: “Ili nimsamehe mtu, lazima kwanza aniombe msamaha.”
˙ Kwa nini tunapaswa kuwa tayari kuwasamehe wengine?

235
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Unaweza kudumisha umoja kutaniko-
ni kwa kuwasamehe na kuwapenda ( 7:01 Jifunze jinsi mfano ambao
ndugu na dada zako wote. Yesu alitoa unavyoweza
kutusaidia kuepuka
kuwahukumu wengine.
Ungejibuje? Toa Boriti

˙ Unawezaje kuepuka ubaguzi?


˙ Utafanya nini hali ya kutoelewa-
na ikitokea kati yako na Mkristo
mwenzako?
˙ Kwa nini unapaswa kuiga mfano Je, tunahitaji kuomba msa-
maha hata ikiwa tunahisi
wa Yehova wa kuwasamehe
kwamba hatujakosea?
wengine?
“Kuomba Msamaha—Ni Njia
Bora ya Kufanya Amani”
(Mnara wa Mlinzi, Novemba 1,
2002)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 6:42 Jifunze jinsi wanaume wawili


waliolelewa kwenye nchi yenye
ubaguzi wa rangi, walivyojifu-
nza kushirikiana kwa umoja.
Lengo Johny na Gideon: Walikuwa
Maadui, Sasa Ni Ndugu
N Ikiwa ni vigumu kwako kushiri-
kiana na Mkristo fulani, jitahidi
kumjua vizuri na utambue sifa
zake nzuri.
Jifunze jinsi ya kutatua hali
N Lengo lingine: ya kutoelewana kati yako na
Mkristo mwenzako kabla hai-
javuruga amani kutanikoni.
“Suluhisha kwa Upendo Hali
ya Kutoelewana” (Mnara wa Mli-
nzi, Mei 2016)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 56, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
57

Ukitenda Dhambi Nzito


Unapaswa Kufanya Nini?
Ingawa unampenda sana Yehova na unajitahidi 2. Yehova anawatumiaje wazee kutusaidia
kuepuka kufanya jambo lolote ambalo litamuu- tunapofanya dhambi?
miza, pindi nyingine utafanya makosa. Hata hi- Tunapotenda dhambi nzito, Yehova anatuambia
vyo, kuna dhambi ambazo ni nzito kuliko dha- ‘tuwaite wazee wa kutaniko.’ (Soma Yakobo
mbi nyingine. (1 Wakorintho 6:9, 10) Ukitenda 5:14, 15.) Wanaume hao waliowekwa rasmi wa-
dhambi nzito, kumbuka kwamba bado Yehova nampenda Yehova na kondoo wake. Wamezoe-
anakupenda; yuko tayari kukusamehe na kuku- zwa jinsi ya kutusaidia kurekebisha uhusiano
saidia. wetu na Yehova.—Wagalatia 6:1.
1. Tunapaswa kufanya nini ili kupata Wazee wanatusaidiaje tunapotenda dhambi nzi-
msamaha wa Yehova? to? Wazee wawili au watatu wataturekebisha
kwa kutumia Maandiko. Pia, watatupatia ma-
Wale wanaompenda Yehova, huhuzunika sana
dokezo na ushauri unaofaa ili kutusaidia kue-
wanapotambua kwamba wamefanya dhambi
puka kutenda dhambi tena. Huenda wakatuwe-
nzito. Lakini wanapata faraja kupitia ahadi hii
kea vizuizi katika utendaji fulani wa Kikristo kwa
ambayo Yehova amewapa watu wake: “Ingawa
muda, mpaka hali yetu ya kiroho itakapoimari-
dhambi zenu ni kama rangi nyekundu, zitafa-
ka. Mtu aliyetenda dhambi nzito anapokosa ku-
nywa kuwa nyeupe kama theluji.” (Isaya 1:18)
tubu, wazee watamtenga na ushirika ili asiwaa-
Ikiwa tutatubu kikweli, Yehova atatusamehe ka-
thiri wengine kutanikoni.
bisa. Tunatubu jinsi gani? Tunahuzunika sana
kwa sababu ya dhambi tuliyofanya, tunaacha
kufanya makosa, na kumsihi Yehova atusame-
he. Kisha, tunajitahidi kubadili mawazo yasiyo-
faa au tabia zilizotuongoza kwenye dhambi, na
kujitahidi kuishi kulingana na viwango safi vya
Yehova.—Soma Isaya 55:6, 7.

237
CH I M BA ZAI DI

Jifunze mengi ili uelewe na kuthamini jinsi Yehova


anavyotusaidia ikiwa tutatenda dhambi nzito.

3. Kuungama dhambi zetu


hutusaidia kurekebisha
uhusiano wetu na Yehova
Tunapotenda dhambi yoyote ile tunamuumiza
Yehova, hivyo tunapaswa kuungama kwake.
Soma Zaburi 32:1-5, kisha mzungumzie
swali hili: Ungama dhambi zako, uwe mnyoofu
kwa wazee wa kutaniko, na ukubali
˙ Kwa nini ni vizuri tuungame dhambi zetu
msaada wenye upendo kutoka
kwa Yehova badala ya kujaribu kuzificha?
kwa Yehova
Baada ya kuungama dhambi zetu kwa Yehova,
tutapata kitulizo kwa kutafuta msaada kwa wazee. Tunapaswa kuzungumza na wazee waziwazi na
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali kwa unyoofu kwa sababu wanataka kutusaidia.
linalofuata. Soma Yakobo 5:16, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kwa nini ni rahisi kwa wazee kutusaidia
( VIDEO: “Yehova Huwatia
tunapokuwa wanyoofu?
Nidhamu Wale Anaowapenda”
(3:01)

˙ Katika video hiyo, wazee walimsaidiaje


Canon amrudie Yehova?
4. Manufaa ya mpango
wa kutenga na ushirika
Mtu ambaye ametenda dhambi nzito akikataa
kufuata viwango vya Yehova, hataruhusiwa kue-
ndelea kushirikiana na kutaniko. Atatengwa na
ushirika, na hatutashirikiana naye wala kuzu-
ngumza naye. Soma 1 Wakorintho 5:6, 11 na
2 Yohana 9-11, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Kama vile chachu inavyochachisha
5. Yehova hutusamehe
donge lote la mkate, kushirikiana na tunapotubu
mtenda dhambi asiyetubu kunawezaje
kuathiri kutaniko? Yesu alitumia mfano unaotusaidia kuele-
wa jinsi Yehova anavyohisi mtu anapotubu.
Baadaye, wengi ambao walitengwa na ushirika Soma Luka 15:1-7, kisha mzungumzie swali hili:
hurudi kutanikoni. Ingawa nidhamu waliyopokea ˙ Simulizi hili linakufundisha nini
ilikuwa na maumivu, iliwasaidia kutambua uzito kumhusu Yehova?
wa makosa yao. (Zaburi 141:5) Onyesha VIDEO,
kisha mzungumzie swali linalofuata. Soma Ezekieli 33:11, kisha mzungumzie
swali hili:
( VIDEO: Uwe Mshikamanifu
˙ Tunawezaje kuonyesha kwamba
kwa Hukumu za Yehova (9:28)
tumetubu kikweli?

˙ Katika video hiyo, Sonja alinufaikaje na


mpango wa kutenga na ushirika?
Kama mchungaji,
Mpango wa kutenga na ushirika . . . Yehova anawajali
sana kondoo wake
˙ unaheshimu jina la Yehova jinsi gani?
˙ unaonyeshaje kwamba Yehova ni mwenye
usawaziko na upendo?

WATU FULANI HUSEMA: “Ninaogopa kuwaambia wazee nimefanya


dhambi kwa sababu nitatengwa na ushirika.”
˙ Unaweza kumwambia nini mtu anayehisi hivyo?

239
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Tunapotenda dhambi nzito, Yehova
atatusamehe ikiwa tutatubu kikweli ( 5:02 Ona jinsi mwanamume
na kuazimia kuacha dhambi. fulani alivyojionea rehema ya
Yehova kama inavyofafanuliwa
kwenye Isaya 1:18.
Ungejibuje? Kamwe Usitilie Shaka
Rehema ya Yehova
˙ Kwa nini ni vizuri tuungame
dhambi zetu kwa Yehova?
˙ Tunapaswa kufanya nini ili
tusamehewe dhambi zetu?
˙ Kwa nini tunapaswa kutafuta Mpango wa kutenga na
ushirika unawanufaishaje
msaada wa wazee tunapotenda
wote wanaohusika?
dhambi nzito?
“Kutenga na Ushirika Ni
Mpango Wenye Upendo”
(Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 2015)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Jifunze jinsi unavyoweza


kumfafanulia mtu ambaye
si Shahidi mpango wa
kutenga na ushirika.
Lengo “Je, Mashahidi wa Yehova Hu-
waepuka Watu Ambao Zamani
N Wafahamu wazee wa Walishirikiana na Dini Yao?”
(Makala iliyo kwenye mtandao)
kutaniko lenu.

N Lengo lingine:
Katika simulizi “Nilihitaji
Kumrudia Yehova,” jifunze
kwa nini mwanamume aliyeku-
wa ameacha kweli anahisi kwa-
mba Yehova alimvuta arudi.
“Biblia Inabadili Maisha”
(Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 2012)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 57, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
58

Endelea Kuwa Mshikamanifu


kwa Yehova
Wakristo wa kweli wameazimia kwamba hawa- Utafanya nini ikiwa mtu unayemfahamu amea-
taruhusu kamwe kitu au mtu yeyote aharibu mua kwamba hataki tena kuwa Shahidi wa
uhusiano wao na Yehova. Tuna hakika wewe pia Yehova? Tunaweza kuvunjika moyo mtu tu-
unahisi hivyo. Yehova anathamini ushikamani- nayempenda anapofanya hivyo. Huenda tu-
fu wako. (Soma 1 Mambo ya Nyakati 28:9.) Ni kalazimika kuchagua kuwa washikamanifu kwa
hali gani zinazoweza kufanya iwe vigumu kwako mtu huyo au kwa Yehova. Tunapaswa kuazi-
kuendelea kuwa mshikamanifu kwa Yehova, na mia kuendelea kuwa washikamanifu kwa Mungu
ni nini kinachoweza kukusaidia? badala ya mtu au kitu kingine chochote. (Ma-
thayo 10:37) Basi tunatii amri ya Yehova kwa-
1. Wengine wanawezaje kufanya iwe mba tunapaswa kuacha kushirikiana na mtu
vigumu kwetu kuendelea kuwa kama huyo.—Soma 1 Wakorintho 5:11.
washikamanifu kwa Yehova?
Watu fulani watajaribu kutushawishi tuache ku- 2. Ni maamuzi gani yanayoweza kuonyesha
mtumikia Yehova. Je, kuna watu wanaowe- kwamba sisi ni washikamanifu kwa Yehova?
za kufanya jambo baya hivyo? Baadhi ya watu Upendo wetu kwa Yehova utatuchochea kue-
ambao wameacha kumtumikia Yehova, wanae- puka kushirikiana kwa njia yoyote na dini za
neza uwongo kuhusu tengenezo la Mungu ili ku- uwongo. Hatupaswi kufanya kazi au kushi-
haribu imani yetu. Watu hao wanaitwa waasi- rikiana na shirika lolote la kidini wala kuji-
imani. Pia, baadhi ya viongozi wa dini hueneza husisha na shughuli zozote zinazohusiana na
uwongo kutuhusu ili kuwafanya watu wasio dini za uwongo. Yehova anatuonya hivi: “To-
waangalifu waache kumtumikia Yehova. Ni ha- keni [katika Babiloni Mkubwa], watu wangu.”
tari kubishana na watu wanaotupinga, kusoma —Ufunuo 18:2, 4.
vitabu na mijadala yao kwenye mitandao, ku-
tembelea tovuti zao, au kutazama video zao.
Yesu alisema hivi kuhusu wale wanaojaribu ku-
wavunja moyo wengine waache kuwa washika-
manifu kwa Yehova: “Waacheni. Wao ni viongo-
zi vipofu. Basi, kipofu akimwongoza kipofu,
wote wawili watatumbukia ndani ya shimo.”
—Mathayo 15:14.

241
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi unavyoweza kuepuka kumruhusu mtu yeyote avunje ushikamanifu


wako kwa Yehova. Pia, chunguza jinsi unavyoweza kuonyesha kwamba wewe
ni mshikamanifu kwa kujitenga na Babiloni Mkubwa.

4. Uwe mshikamanifu kwa


Mungu, Mkristo mwenzako
anapotenda dhambi
3. Jihadhari na Unapotambua kwamba mtu fulani kutanikoni amefanya
dhambi nzito, unapaswa kuchukua hatua gani? Fikiria kanuni
walimu wa uwongo iliyo katika Sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli wa kale.
Tunapaswa kutendaje tunapo- Soma Mambo ya Walawi 5:1.
sikia habari zisizofaa kuhusu Kulingana na mstari huo, tunapotambua kwamba mtu fulani
tengenezo la Yehova? Soma amefanya dhambi nzito, tunapaswa kuwaambia wazee habari
Methali 14:15, kisha mzungu- tunazojua. Hata hivyo, kabla ya kuchukua hatua hiyo, ni jambo
mzie swali hili: la fadhili kumhimiza mtu huyo aende kwa wazee na kuungama
˙ Kwa nini hatupaswi kuwa dhambi yake. Asipofanya hivyo, ushikamanifu wetu kwa Yehova
wepesi kuamini kila jambo utatuchochea kuwaambia wazee habari tunazojua. Kuchukua
tunalosikia? hatua hizo kunaonyeshaje upendo mshikamanifu kwa . . .
˙ Yehova Mungu?
Soma 2 Yohana 10, kisha
˙ mtu aliyetenda dhambi?
mzungumzie maswali haya:
˙ watu wengine kutanikoni?
˙ Tunapaswa kuwatendeaje
waasi-imani?
˙ Mbali na kuepuka kushi-
rikiana na waasi-imani
moja kwa moja, ni mambo
gani mengine tunayopaswa
kuepuka ili tusishawishiwe
na mafundisho yao?
˙ Unafikiri Yehova atahisije
ikiwa tutasikiliza mambo
yasiyofaa yanayosemwa
kumhusu au kuhusu
tengenezo lake?

Ikiwa Mkristo mwenzako


yuko hatarini, msaidie!
Utafanya nini ukiombwa
utoe mchango wa kusaidia
mashirika ya kidini?

5. Jitenge na Babiloni Mkubwa (

Onyesha VIDEO.
Soma Luka 4:8 na Ufunuo 18:4, 5, kisha ujibu maswali haya: VIDEO: Tokeni Katika Babiloni
Mkubwa! (5:06)
˙ Je, bado jina langu limeandikwa kwenye orodha ya wafuasi
wa dini ya uwongo?
˙ Je, ninashirikiana na shirika linalohusiana na dini nyingine?
˙ Je, kazi yangu inaunga mkono dini ya uwongo kwa njia yoyote?
˙ Je, kuna hatua nyingine ambayo ninahitaji kuchukua ili
kujitenga na dini ya uwongo?
˙ Ikiwa nimejibu ndiyo kwa mojawapo ya maswali hayo,
ninapaswa kufanya mabadiliko gani?

Katika visa hivyo vyote, fanya uamuzi utakaokuacha ukiwa na dhamiri


safi na utakaoonyesha kwamba wewe ni mshikamanifu kwa Yehova.

WATU FULANI HUSEMA: “Ninahitaji kujua mambo ambayo waasi-imani


wanasema kuhusu Mashahidi wa Yehova ili nitetee ukweli.”
˙ Je, hilo ni jambo la hekima? Kwa nini?

243
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Ili tuendelee kuwa washikamanifu kwa
Yehova, tunapaswa kuepuka kushiri- Jifunze jinsi unavyopaswa
kiana na watu ambao si washikamani- kutenda unaposikia habari
fu kwake. Pia, tunapaswa kujitenga za uwongo kuhusu Mashahidi
kabisa na dini za uwongo. wa Yehova.
“Je, Una Habari Kamili?”
(Mnara wa Mlinzi, Agosti 2018)
Ungejibuje?
˙ Kwa nini hatupaswi kutazama,
kusoma, au kusikiliza habari
za waasi-imani? Unawezaje kutambua mashiri-
˙ Tunapaswa kuwatendeaje wale ka au shughuli zinazounga
ambao hawataki tena kuwa mkono Babiloni Mkubwa?
Mashahidi wa Yehova? “Uwe na Mengi ya Kufanya
Katika Kipindi cha Mwisho
˙ Tunawezaje kutii agizo la kutoka
cha ‘Siku za Mwisho’ ”
kwenye dini za uwongo?
(Mnara wa Mlinzi, Oktoba 2019,
fungu la 16-18)

Tarehe ambayo somo limekamilishwa ( 9:26 Baadhi ya wapinzani


wamefanya nini ili kujaribu
kudhoofisha imani yetu?
Jihadhari na Udanganyifu
Lengo
N Ikiwa unashirikiana kwa njia yo-
yote na dini za uwongo, chukua
hatua ili ujitenge na dini hizo.

N Lengo lingine: Katika simulizi “Nimekuwa


Nikimtafuta Mungu Tangu
Utotoni,” soma kuhusu kuhani
wa dini ya Shinto aliyeacha ku-
shirikiana na dini ya uwongo.
“Biblia Inabadili Maisha”
(Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2011)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 58, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
59

Unaweza Kuvumilia Mateso


Wakristo wote wanatarajia kwamba watakabili Tunaweza pia kuimarisha ujasiri wetu kwa ku-
upinzani au hata mateso. Je, hilo linapaswa ku- hubiri kwa ukawaida. Tunapohubiri tunajifu-
tuogopesha? nza kumtegemea Yehova na kuepuka mtego wa
kuwaogopa wanadamu. (Methali 29:25) Ukisita-
1. Kwa nini tunatarajia kuteswa? wisha ujasiri wa kuhubiri sasa, utakuwa tayari
Biblia inasema hivi waziwazi: “Wote wanaota- kuendelea kuhubiri hata ikiwa serikali itajaribu
mani kuishi kwa ujitoaji-kimungu katika ushi- kutuzuia kuhubiri.—1 Wathesalonike 2:2.
rika na Kristo Yesu watateswa pia.” (2 Timo-
theo 3:12) Yesu aliteswa kwa sababu hakuwa 3. Tunanufaikaje tunapovumilia mateso?
sehemu ya ulimwengu wa Shetani. Sisi pia si se- Bila shaka, hatufurahi tunapoteswa, lakini tu-
hemu ya ulimwengu, kwa hiyo hatushangai tu- napovumilia mateso, imani yetu inaimarika.
napoteswa na serikali za wanadamu au mashiri- Tunamkaribia Yehova kwa sababu tunajionea
ka ya kidini.—Yohana 15:18, 19. jinsi anavyotusaidia tunapohisi kwamba hatu-
na nguvu za kuendelea kuvumilia. (Soma Yako-
2. Tunawezaje kujitayarisha kwa bo 1:2-4.) Yehova anaumia anapoona tukite-
ajili ya mateso? seka, lakini anafurahi kuona tukivumilia. Biblia
Sasa ndio wakati wa kujifunza kumtegemea Ye- inasema hivi: “Ikiwa mnavumilia mateso kwa
hova kabisa. Tenga muda kila siku ili kusali kwa- sababu ya kufanya mema, jambo hilo linaku-
ke na kusoma Neno lake. Hudhuria mikutano ya balika kwa Mungu.” (1 Petro 2:20) Tukiende-
kutaniko kwa ukawaida. Kufanya mambo hayo lea kuvumilia kwa uaminifu, Yehova atatupa-
kutakupatia nguvu unazohitaji ili ukabili mate- tia thawabu ya kuishi milele katika ulimwengu
so kwa ujasiri, hata kama yanatoka kwa watu ambao tutamwabudu bila upinzani wowote.
wa familia yako. Mtume Paulo, ambaye aliteswa —Mathayo 24:13.
mara nyingi, aliandika hivi: “Yehova ni msaidizi
wangu; sitaogopa.”—Waebrania 13:6.

245
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi tunavyoweza kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova hata


tunapokabili mateso, na baraka ambazo tutapata kwa kufanya hivyo.

4. Unaweza kuvumilia 5. Endelea kumwabudu


upinzani kutoka kwa Yehova licha ya kuteswa
watu wa familia
Yesu alijua kwamba baadhi ya watu katika familia Tunahitaji ujasiri ili kumtumikia Yehova
zetu watajaribu kutuzuia kumwabudu Yehova. Soma watu wengine wanapojaribu kutuzuia
Mathayo 10:34-36, kisha mzungumzie swali hili: kumtumikia. Onyesha VIDEO, kisha
mzungumzie swali linalofuata.
˙ Mtu anapoamua kumtumikia Yehova, watu
wa familia yake wanaweza kumtendeaje?
( VIDEO: Kuonyesha Ujasiri
Ili uone mfano wa jambo hilo, onyesha VIDEO, Licha ya Mnyanyaso (6:27)
kisha mzungumzie swali linalofuata.

( VIDEO: Yehova Alituchukua ˙ Mfano uliowekwa na akina ndugu


(5:13) na dada katika video hiyo unakui-
marishaje?

Soma Matendo 5:27-29 na Waebrania


˙ Utafanya nini ikiwa mtu wa familia au rafiki
10:24, 25. Baada ya kusoma kila andiko,
atajaribu kukuzuia kumtumikia Yehova?
zungumzieni swali hili:
Soma Zaburi 27:10 na Marko 10:29, 30. Baada ˙ Kwa nini ni muhimu sana kuendelea
ya kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili: kumwabudu Yehova hata ikiwa serikali
inatuzuia kuhubiri au kuhudhuria
˙ Ahadi hii inawezaje kukusaidia unapokabili upi-
mikutano?
nzani kutoka kwa watu wa familia au marafiki?
6. Yehova atakusaidia uvumilie (

Mashahidi wa Yehova wenye umri na malezi mbalimbali


wameendelea kumtumikia Yehova kwa ushikamanifu hata VIDEO: Yehova Mungu
wanapoteswa. Ili uone jambo lililowasaidia, onyesha VIDEO. Ataniimarisha (3:41)
Kisha mzungumzie swali linalofuata.
˙ Katika video hiyo, ni nini kilichowasaidia Mashahidi
hao kuvumilia?

Soma Waroma 8:35, 37-39 na Wafilipi 4:13. Baada ya


kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili:
˙ Andiko hili linakuhakikishiaje kwamba unaweza
kuvumilia jaribu lolote?

Soma Mathayo 5:10-12, kisha mzungumzie swali hili:


˙ Kwa nini unaweza kuwa na furaha hata unapoteswa?

Mamilioni ya watumishi
wa Yehova wameendelea
kumtumikia kwa uaminifu
licha ya upinzani. Wewe
pia unaweza!

WATU FULANI HUSEMA: “Mimi siwezi kuvumilia mateso.”


˙ Ni maandiko gani yanayoweza kuwasaidia watu hao kupata ujasiri?

247
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Yehova anathamini jitihada zetu
za kumtumikia licha ya mateso. ( 2:34 Ona ndugu kijana akieleza
Kwa msaada wake, tunaweza jinsi Yehova alivyomsaidia
kufanikiwa kuvumilia! kuvumilia alipofungwa gere-
zani kwa sababu ya kutounga
mkono upande wowote.
Ungejibuje? Kuvumilia Licha ya Mnyanyaso

˙ Kwa nini Wakristo wanapaswa


kutarajia kwamba watateswa?
˙ Unaweza kufanya nini sasa
ili uwe tayari utakapokabili ( 7:15 Ona jambo lililowasaidia
mateso? wenzi fulani wa ndoa
waendelee kumtumikia
˙ Ni nini kinachoweza kukusaidia
Yehova kwa uaminifu
uwe na uhakika kwamba unawe- kwa miaka mingi
za kuendelea kumtumikia Yehova licha ya upinzani.
hata unapokabili jaribu lolote?
Kumtumikia Yehova
Wakati wa Mabadiliko

Tarehe ambayo somo limekamilishwa Jifunze jinsi unavyoweza


kukabili mateso kwa ujasiri.
“Jitayarishe Sasa
kwa Ajili ya Mateso”
Lengo (Mnara wa Mlinzi, Julai 2019)

N Muulize hivi Mkristo mwenzako,


“Je, kuna mtu yeyote ambaye
amewahi kujaribu kukuzuia
kumtumikia Yehova? Ulishu-
ghulikiaje hali hiyo?” Tunapaswa kuonaje upinzani
kutoka kwa watu wa familia,
na tunawezaje kufanikiwa
N Lengo lingine:
kukabiliana na hali hiyo?
“Kweli Huleta, ‘Si Amani,
Bali Upanga’ ” (Mnara wa Mlinzi,
Oktoba 2017)

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 59, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw
60

Endelea Kuimarisha
Urafiki Wako na Yehova
Katika masomo haya ya kujifunza Biblia, umeji- ndelea kujifunza Neno la Mungu na kuhudhuria
funza mambo mengi kumhusu Yehova. Mambo mikutano ya kutaniko, utajifunza mambo ma-
ambayo umejifunza yamekusaidia kumpenda pya kumhusu Yehova na sifa zake. Tafuta njia
sana na huenda yamekuchochea kujiweka wak- za kuiga utu wake kikamili zaidi katika mai-
fu kwake na kubatizwa. Ikiwa bado hujachukua sha yako. Endelea kufanya mabadiliko yoyote
hatua hiyo, labda unafikiria kufanya hivyo hivi yanayohitajika ili kumfurahisha Yehova.
karibuni. Lakini baada ya kubatizwa, bado una-
hitaji kuendelea kumkaribia Yehova. Unaweza 3. Yehova atakusaidiaje uendelee kumkaribia?
kuendelea kumkaribia Yehova milele. Jinsi gani? Biblia inasema hivi: ‘Mungu atamaliza mazoezi
yako, atakufanya uwe imara, atakutia nguvu,
1. Kwa nini unapaswa kuendelea kuimarisha atakupa msingi imara.’ (1 Petro 5:10) Sisi sote
urafiki wako na Yehova? hushawishiwa kufanya mambo mabaya. Lakini
Tunapaswa kujitahidi kuendelea kuimarisha Yehova hutupatia msaada tunaohitaji ili tupinge
urafiki wetu na Yehova. Kwa nini? “Ili tusipepe- vishawishi hivyo. (Zaburi 139:23, 24) Anaahidi
rushwe kamwe” mbali naye. (Waebrania 2:1) Ni kwamba atakupa hamu na nguvu za kuendelea
nini kinachoweza kutusaidia tuendelee kumtu- kumtumikia kwa uaminifu.—Soma Wafilipi 2:13.
mikia Yehova kwa uaminifu? Ni kwa kuwa na bi-
dii katika kazi ya kuhubiri na kutafuta njia nyi-
ngine za kumtumikia Mungu wetu kikamili zaidi.
(Soma Wafilipi 3:16.) Kumtumikia Yehova ndiyo
maisha bora zaidi!—Zaburi 84:10.

2. Unapaswa kuendelea kufanya nini kingine?


Ingawa umekamilisha masomo haya ya kuji-
funza Biblia, bado utaendelea kuishi maisha
ya Kikristo. Biblia inasema kwamba tunapaswa
“kuvaa utu mpya.” (Waefeso 4:23, 24) Unapoe-

249
CH I M BA ZAI DI

Jifunze jinsi unavyoweza kuendelea kumkaribia


Yehova na jinsi atakavyokubariki.

4. Endelea kuwasiliana na 5. Jiwekee malengo ya kiroho


Rafiki yako wa karibu zaidi Kujiwekea malengo katika utumishi wa Yehova kuta-
Kusali na kujifunza Biblia kumekusaidia uwe kusaidia uendelee kumkaribia zaidi. Onyesha VIDEO,
rafiki ya Yehova. Mambo hayo yanawezaje kisha mzungumzie swali linalofuata.
kukusaidia umkaribie hata zaidi?
( VIDEO: Maisha Bora Zaidi
Soma Zaburi 62:8, kisha mzungumzie (3:31)
swali hili:
˙ Ili kuimarisha urafiki wako na Yehova,
unawezaje kuboresha sala zako? ˙ Katika video hiyo, Cameron alinufaikaje
kwa kujiwekea malengo ya kiroho?
Soma Zaburi 1:2, na maelezo ya chini,
kisha mzungumzie swali hili: Si kila mtu anayeweza kuhamia katika nchi nyingine
˙ Ili kuimarisha urafiki wako na Yehova, ili kuhubiri. Hata hivyo, sisi sote tunaweza kujiwekea
unawezaje kuboresha usomaji wako malengo tunayoweza kutimiza. Soma Methali 21:5,
wa Biblia? kisha ufikirie malengo unayoweza kujiwekea . . .
˙ katika kutaniko.
Unaweza kufanya nini ili unufaike zaidi na
˙ katika utumishi wa shambani.
funzo lako la kibinafsi? Ili kupata mapende-
kezo, onyesha VIDEO, kisha mzungumzie
Kanuni iliyo katika andiko hilo inawezaje
maswali yanayofuata.
kukusaidia kutimiza malengo yako?

( VIDEO: Boresha Funzo Lako la


Kibinafsi (5:22) Malengo unayoweza kujiwekea

 Kuboresha sala zako.


˙ Unaweza kutumia madokezo gani  Kusoma Biblia nzima.
yaliyo katika video hiyo?  Kumfahamu kila mtu katika kutaniko lenu.
˙ Ungependa kujifunza kuhusu  Kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia.
habari gani?  Kutumikia ukiwa painia msaidizi au
painia wa kawaida.
 Ikiwa wewe ni ndugu, unaweza kujitahidi
kuwa mtumishi wa huduma.
6. Furahia maisha milele!
Soma Zaburi 22:26, kisha mzungumzie swali hili:
˙ Unaweza kufanya nini ili ufurahie maisha
sasa na milele?
MUHTASARI CH U N G U ZA ZAI DI
Endelea kuimarisha urafiki wako
na Yehova na ujiwekee malengo ( 9:20 Yehova anathamini nini zaidi,
ya kiroho. Nawe utafurahia je, ni tendo moja kubwa la
maisha sasa na milele! ujitoaji au ni kumtumikia kwa
uaminifu maisha yetu yote?
Uwe Mwaminifu Kama
Ungejibuje? Abrahamu

˙ Kwa nini unaweza kuwa


na uhakika kwamba Yehova
atakusaidia uendelee kumtu-
mikia kwa uaminifu? ( 5:25 Hata mtumishi mwaminifu
˙ Unawezaje kuimarisha urafiki wa Yehova anaweza kupoteza
wako na Yehova? shangwe. Ona jinsi ya kupata
shangwe tena.
˙ Malengo ya kiroho yanawezaje
Pata Shangwe Tena Kupitia
kukusaidia umkaribie Yehova
Kujifunza na Kutafakari
zaidi?

Tarehe ambayo masomo haya Unawezaje kujiwekea malengo


ya Biblia yamekamilishwa ya kiroho na kuyatimiza?
“Tumia Miradi ya Kiroho ili
Kumtukuza Muumba Wako”
(Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 2004)
Lengo la Muda Mrefu
N Soma vitabu Mkaribie Yehova
na “Njoo Uwe Mfuasi Wangu.”
Machapisho haya yatakusaidia
uendelee kumkaribia zaidi Baba Kwa nini ni muhimu kuwa
yako wa mbinguni na Mwana Mkristo mkomavu, na una-
wake. wezaje kufanya hivyo?
“Songa Mbele Kuelekea Uko-
mavu—‘Ile Siku Kuu ya Yehova
Iko Karibu’ ” (Mnara wa Mlinzi,
Mei 15, 2009)
MKARIBIE
YEHOVA ‘NJOO UWE
MFUASI WANGU’

Tumia alama hii kufungua marejeo yote


ya SOMO LA 60, au utazame chapisho
Furahia Maisha Milele! kwenye jw.org/sw 252
MAMBO MAKUU YA
SEHEMU YA 4
Zungumzia maswali yafuatayo pamoja
na mwalimu wako:

1. Soma Methali 13:20. 8. Soma Zaburi 133:1.


˙ Kwa nini ni muhimu kuchagua marafiki ˙ Unaweza kuchangia umoja katika
wako kwa hekima? kutaniko kupitia njia gani?
(Ona Somo la 48.) (Ona Somo la 56.)

2. Ni ushauri gani wa Biblia unaoweza 9. Tunawezaje kupokea msaada wa Yehova


kukusaidia ikiwa wewe ni . . .
ikiwa tutatenda dhambi nzito?
˙ mume au mke? (Ona Somo la 57.)
˙ mzazi au mtoto?
(Ona Somo la 49 na 50.) 10. Soma 1 Mambo ya Nyakati 28:9 na
maelezo ya chini.
3. Ni mazungumzo ya aina gani yanayomfura- ˙ Unawezaje kuonyesha kwamba ‘umejitoa
hisha Yehova? Ni mazungumzo ya aina gani kikamili’ kwa Yehova wengine wanapopinga
ambayo hayamfurahishi Yehova? ibada ya kweli au wanapoacha kweli?
(Ona Somo la 51.)
˙ Je, unahitaji kufanya mabadiliko yoyote ili
4. Ni kanuni gani za Biblia ambazo uendelee kuwa mshikamanifu kwa Yehova
zitakusaidia kufanya maamuzi mazuri na kujitenga na dini ya uwongo?
kuhusu mwonekano wako? (Ona Somo la 58.)
(Ona Somo la 52.)
11. Unawezaje kujitayarisha kwa ajili ya mateso?
5. Unawezaje kuchagua burudani (Ona Somo la 59.)
inayomfurahisha Yehova?
(Ona Somo la 53.)
12. Unapanga kufanya nini ili uendelee
6. Soma Mathayo 24:45-47. kuimarisha urafiki wako na Yehova?
(Ona Somo la 60.)
˙ “Mtumwa mwaminifu na mwenye
busara” ni nani? Maswali yako:
(Ona Somo la 54.)

7. Unawezaje kuunga mkono kutaniko kwa


kutumia muda, nguvu, na mali zako?
(Ona Somo la 55.)
Je, Niko Tayari Kuhubiri
Pamoja na Kutaniko?
Unaweza kuwa mhubiri ambaye
hajabatizwa ikiwa . . .
˙ Unajifunza Biblia kwa ukawaida, unasali,
na kuhudhuria mikutano ya kutaniko.
˙ Unapenda na kuamini mambo unayojifunza na
unataka kuwaambia wengine kuyahusu.
˙ Unampenda Yehova na unachagua marafiki wa
karibu kati ya wale wanaompenda.
˙ Umejitenga na shirika lolote la kisiasa au
la dini za uwongo.
˙ Unaishi kulingana na viwango vya Yehova na
unataka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova.

Ikiwa unahisi kwamba uko tayari kuhubiri na kutaniko, mwalimu wako wa Biblia anaweza
kufanya mpango ili ukutane na wazee na kuzungumzia jinsi unavyoweza kustahili.

Je, Niko Tayari Kubatizwa?


Unaweza kubatizwa ikiwa . . .
˙ Wewe ni mhubiri ambaye hajabatizwa.
˙ Unashiriki kwa ukawaida katika kazi ya
kuhubiri kulingana na uwezo wako.
˙ Unaunga mkono na kufuata mwongozo wa
“mtumwa mwaminifu na mwenye busara.”
—Mathayo 24:45-47.
˙ Umejiweka wakfu kwa Yehova kupitia sala
na unataka kumtumikia milele.

Ikiwa unahisi kwamba uko tayari kubatizwa, mwalimu wako wa Biblia anaweza
kufanya mpango ili ukutane na wazee na kuzungumzia jinsi unavyoweza kustahili.

254
Maelezo ya Ziada

1. Jinsi ya Kumtambua Babiloni Mkubwa 3. Matibabu Yanayohusisha Damu


Tunajuaje kwamba “Babiloni Mkubwa” anawakilisha dini zote za Matibabu fulani yanahusisha kutumia damu ya mgonjwa. Wa-
uwongo? (Ufunuo 17:5) Fikiria mambo yafuatayo: kristo hawakubali baadhi ya matibabu hayo. Kwa mfano, kutoa
mchango wa damu au mtu kuhifadhi damu yake, labda kwa ma-
˙ Anapatikana ulimwenguni pote. Babiloni Mkubwa
juma kadhaa kabla ya kufanyiwa upasuaji.—Kumbukumbu la To-
anafafanuliwa kuwa mwanamke aliyeketi juu ya “uma-
rati 15:23.
ti na mataifa.” Ana “ufalme juu ya wafalme wa dunia.”
—Ufunuo 17:15, 18. Hata hivyo, huenda matibabu mengine yakakubalika. Matibabu
˙ Yeye si mfumo wa kisiasa au wa kibiashara. “Wafalme hayo yanatia ndani kutoa damu ili ifanyiwe vipimo, kuchuja na
wa dunia” na “wafanyabiashara” hawaangamizwi pamo- kusafisha damu (hemodialysis), uzimuaji wa damu (hemodilu-
ja naye.—Ufunuo 18:9, 15. tion), kutumia mashine ya uokoaji wa chembe za damu (cell-
salvage) na mashine ya kusaidia moyo au mapafu kufanya kazi
˙ Anapotosha ukweli kumhusu Mungu. Anaitwa ka- (heart-lung bypass machine). Kila Mkristo anapaswa kuamua
haba kwa sababu anafanya mapatano na serikali za mwenyewe jinsi damu yake itakavyotumiwa wakati wa matibabu,
ulimwengu ili ajinufaishe kifedha na kwa njia nyingi- jinsi itakavyofanyiwa vipimo, au ikiwa itatolewa na kurudishwa
ne. (Ufunuo 17:1, 2) Anawapotosha watu wa mataifa mwilini bila kuhifadhiwa. Huenda kila daktari akatumia mbinu
yote. Na amesababisha vifo vya watu wengi.—Ufunuo hizo kwa njia tofauti. Hivyo, Mkristo anapaswa kujua vizuri jinsi
18:23, 24. ambavyo damu yake itatumiwa kabla ya kukubali kufanyiwa upa-
suaji, vipimo, au matibabu yoyote. Fikiria maswali yafuatayo:
2. Masihi Angetokea Lini? ˙ Namna gani ikiwa damu yangu itaelekezwa nje ya mwili
Biblia ilitabiri kwamba majuma 69 yangepita kabla ya Masihi wangu na kukatiza mzunguko wa damu kwa muda
kutokea.—Soma Danieli 9:25. fulani? Je, dhamiri yangu itaniruhusu kuona damu
hiyo kuwa bado sehemu ya mwili wangu na kwamba
Majuma 69 yalianza lini? Yalianza mwaka wa 455 K.W.K. haipaswi ‘kumwagwa ardhini’?—Kumbukumbu la Torati
Wakati huo, Gavana Nehemia aliwasili Yerusalemu 12:23, 24.
ili “kurudisha na kujenga upya” jiji hilo.—Danieli 9:25;
˙ Namna gani ikiwa wakati wa matibabu kiasi fulani cha
Nehemia 2:1, 5-8.
damu yangu kitatolewa ili kuboreshwa kisha kirudishwe
Yale majuma 69 yalikuwa na urefu gani? Katika baadhi mwilini mwangu? Je, hilo litasumbua dhamiri yangu ili-
ya unabii wa Biblia, siku moja huwakilisha mwaka mmo- yozoezwa na Biblia, au nitakubali matibabu hayo?
ja. (Hesabu 14:34; Ezekieli 4:6) Basi, juma moja lina-
wakilisha miaka saba. Katika unabii huu, majuma 69 ni
miaka 483 (yaani, 69 mara 7).
4. Mume na Mke Kutengana
Yale majuma 69 yaliisha lini? Tukihesabu miaka 483 Neno la Mungu linahimiza mume na mke wasitengane na linase-
kuanzia mwaka wa 455 K.W.K. tunafika kwenye mwaka ma waziwazi kwamba kutengana hakumpi yeyote kati yao haki
wa 29 W.K. Huo ndio mwaka hususa ambao Yesu aliba- ya kuoa au kuolewa tena. (1 Wakorintho 7:10, 11) Hata hivyo,
tizwa na kuwa Masihi!—Luka 3:1, 2, 21, 22. baadhi ya Wakristo wameamua kutengana kwa sababu ya hali
fulani.
 Kuanzia mwaka wa 455 K.W.K. hadi mwaka wa 1 K.W.K. ni miaka 454.
Kuanzia mwaka wa 1 K.W.K. hadi mwaka wa 1 W.K. ni mwaka mmoja ˙ Kukataa kimakusudi kutegemeza familia: Mume ana-
(hakukuwa na mwaka wa sufuri). Na kuanzia mwaka wa 1 W.K. hadi pokataa kuandalia familia yake kimwili, hivi kwamba
mwaka wa 29 W.K. ni miaka 28. Jumla ni miaka 483. familia yake inakosa mahitaji ya lazima maishani.—1 Ti-
motheo 5:8.

455 K.W.K. 406 K.W.K. 29 W.K.


“Neno la kurudisha Yerusalemu Masihi atokea
. . . Yerusalemu” lajengwa upya (abatizwa)

“Majuma 7” (Miaka 49) “Majuma 62” (Miaka 434)

Miaka 483
Maelezo ya Ziada

˙ Kutendewa vibaya kimwili: Mwenzi wa ndoa anapo- Mtu aliye na ugonjwa wa kuambukiza anawezaje kutii amri hiyo?
tendewa vibaya kimwili au kujeruhiwa kufikia hatua Mtu huyo hapaswi kujaribu kuwakumbatia au kuwabusu watu
ya kwamba uhai wake unakuwa hatarini.—Wagalatia wengine. Hapaswi kukasirika ikiwa wengine watakataa kumkari-
5:19-21. bisha nyumbani kwao kwa sababu wanataka kulinda familia zao.
Na kabla ya kubatizwa, anapaswa kumjulisha mratibu wa bara-
˙ Kuhatarisha kabisa uhusiano wa mtu pamoja na Ye-
za la wazee kuhusu ugonjwa wake ili abatizwe kwa njia ambayo
hova: Mwenzi wa ndoa anapompinga kabisa mume au
itawalinda wengine watakaobatizwa. Kabla ya kuanza uchumba,
mke wake hivi kwamba anashindwa kumtumikia Yehova.
mtu ambaye huenda ana ugonjwa wa kuambukiza anapaswa ku-
—Matendo 5:29.
kubali kwa hiari kufanyiwa vipimo vya damu. Ukifanya hivyo,
utaonyesha kwamba unawajali wengine kwa ‘kuangalia, si faida
5. Sikukuu na Sherehe zako mwenyewe, bali pia faida za wengine.’—Wafilipi 2:4.
Wakristo hawashiriki katika sikukuu ambazo hazimfurahishi Ye- 7. Masuala ya Kibiashara na Kisheria
hova. Lakini kila Mkristo anapaswa kuongozwa na dhamiri yake
iliyozoezwa na Biblia kuamua jinsi atakavyotenda watu wengine Tunaweza kuepuka matatizo mengi kwa kuandika makubalia-
wanaposherehekea sikukuu hizo. Fikiria mifano michache. no yote ya kifedha, hata ikiwa yanahusisha Mkristo mwenzetu.
(Yeremia 32:9-12) Hata hivyo, huenda matatizo madogo yakato-
˙ Mtu anapokutakia sikukuu njema. Unaweza kumjibu,
kea kati ya Wakristo kuhusu pesa au mambo mengine. Wanapa-
“Asante.” Ikiwa mtu huyo anataka kujifunza mengi, una-
swa kutatua matatizo hayo haraka na kwa amani, kati yao we-
weza kumweleza kwa nini husherehekei sikukuu hiyo.
nyewe.
˙ Mwenzi wako wa ndoa, ambaye si Shahidi wa Ye-
hova, anakukaribisha kwenye mlo pamoja na watu Hata hivyo, tunapaswa kushughulikiaje matatizo makubwa kama
wa ukoo wakati wa sikukuu. Ikiwa dhamiri yako inaku- vile ulaghai au uchongezi? (Soma Mathayo 18:15-17.) Yesu alitu-
ruhusu kwenda, unaweza kumweleza mapema mwenzi fundisha hatua tatu ambazo tunapaswa kufuata:
wako kwamba ikiwa mlo huo utahusisha desturi za kipa- (1) Jaribuni kutatua jambo hilo kati yenu wenyewe.
gani, basi hutashiriki katika desturi hizo. —Ona mstari wa 15.
˙ Mwajiri wako anakupa zawadi ya pesa wakati wa si- (2) Hilo lisipowezekana, nenda na Mkristo mmoja au wawili
kukuu. Je, unapaswa kukataa pesa hizo? Unaweza ku- walio wakomavu kiroho.—Ona mstari wa 16.
kubali. Je, mwajiri wako anaona pesa hizo kuwa zawadi
(3) Ikiwa bado mnashindwa kutatua jambo hilo, basi unawe-
ya sikukuu, au ni njia ya kukuonyesha shukrani kwa sa-
za kuwajulisha wazee wa kutaniko.—Ona mstari wa 17.
babu ya kazi nzuri uliyofanya?
Katika visa vingi, hatupaswi kuwapeleka ndugu zetu mahakama-
˙ Mtu fulani anakupatia zawadi wakati wa sikukuu. ni kwa sababu hilo linaweza kuchafua jina la Yehova na kutaniko.
Huenda mtu huyo akasema: “Ninajua husherehekei si- (1 Wakorintho 6:1-8) Hata hivyo, kuna visa ambavyo vinapaswa
kukuu hii, lakini ningependa kukupatia zawadi hii.” Lab- kusuluhishwa kisheria: kwa mfano, kesi za talaka, kupewa ruhu-
da mtu huyo anaonyesha tu fadhili. Hata hivyo, je, kuna sa mahakamani ya kuwatunza na kuwalea watoto, kuamua mali-
sababu inayoonyesha kwamba anajaribu imani yako au po ya talaka, kupata malipo ya bima, kesi ya kufilisika, au kui-
anataka ushiriki katika sikukuu hiyo? Baada ya kufikiria dhinisha wasia. Mkristo anayeenda mahakamani ili kusuluhisha
mambo hayo, wewe mwenyewe utaamua ikiwa utapokea masuala kama hayo kwa njia ya amani havunji ushauri wa Biblia.
au kukataa zawadi hiyo. Tunapofanya maamuzi yoyote,
tungependa kubaki na dhamiri safi na kuendelea kuwa Ikiwa kisa hicho kinahusisha uhalifu mkubwa kama vile ubakaji,
waaminifu kwa Yehova.—Matendo 23:1. kumtendea mtoto vibaya, kupigwa, wizi wa kiasi kikubwa cha
mali, au mauaji, Mkristo anapotoa taarifa kwa wenye mamlaka
havunji ushauri wa Biblia.
6. Magonjwa ya Kuambukiza
Kwa kuwa tunawapenda watu, hatungependa kuwaambukiza
magonjwa. Tunaepuka kufanya hivyo ikiwa tuna ugonjwa unaoa-
mbukiza au tuna sababu za kuamini kwamba huenda tumea-
mbukizwa. Tunafanya hivyo ili kutii amri hii ya Biblia: “La-
zima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
—Waroma 13:8-10.
Fuatilia Usomaji Wako wa Biblia

MAANDIKO YA MAANDIKO YA
KIEBRANIA NA KIARAMU KIGIRIKI YA KIKRISTO

Uumbaji na historia ya Simulizi la Ayubu Maisha na huduma ya Yesu


mapema ya wanadamu
Ayubu 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 Mathayo 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13
Mwanzo 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26
14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 27 28 Marko 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11
27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 12 13 14 15 16 Luka 1 2 3 4 5 6 7 8 9
39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22
Kutoka 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 23 24 Yohana 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11
14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 Nyimbo na hekima 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21
27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 inayotumika
40 Mambo ya Walawi 1 2 3 4 5 6 7 8 Zaburi 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13
9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 Ukuzi wa kutaniko la Kikristo
14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26
23 24 25 26 27 Hesabu 1 2 3 4 5 6 7 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 Matendo 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13
8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28
22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62
35 36 Kumbukumbu la Torati 1 2 3 4 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73
5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 84 85 Barua za mtume Paulo
20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 Waroma 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12
33 34 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 13 14 15 16 1 Wakorintho 1 2 3 4 5 6
108 109 110 111 112 113 114 115 116 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 2 Wakori-
117 118 119 120 121 122 123 124 125 126 ntho 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13
Kuanza maisha katika
127 128 129 130 131 132 133 134 135 Wagalatia 1 2 3 4 5 6 Waefeso 1 2 3
Nchi ya Ahadi
136 137 138 139 140 141 142 143 144 145 4 5 6 Wafilipi 1 2 3 4 Wakolosai 1 2
Yoshua 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 146 147 148 149 150 Methali 1 2 3 4 5 3 4 1 Wathesalonike 1 2 3 4 5 2 Wa-
14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 Waa- 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 thesalonike 1 2 3 1 Timotheo 1 2 3
muzi 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 4 5 6 2 Timotheo 1 2 3 4 Tito 1 2 3
14 15 16 17 18 19 20 21 Ruthu 1 2 3 4 Mhubiri 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 Filemoni 1 Waebrania 1 2 3 4 5 6 7 8
Wimbo wa Sulemani 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13
Wafalme wa kale wa Israeli
Maandishi ya unabii Maandishi ya mitume na
1 Samweli 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12
13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 Isaya 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 wanafunzi wengine
25 26 27 28 29 30 31 2 Samweli 1 2 3 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 Yakobo 1 2 3 4 5 1 Petro 1 2 3 4
4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 5 2 Petro 1 2 3 1 Yohana 1 2 3 4 5
19 20 21 22 23 24 1 Wafalme 1 2 3 4 5 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 2 Yohana 1 3 Yohana 1 Yuda 1 Ufu-
6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 nuo 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14
21 22 2 Wafalme 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Yeremia 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 15 16 17 18 19 20 21 22
11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26
24 25 1 Mambo ya Nyakati 1 2 3 4 5 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39
6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52
21 22 23 24 25 26 27 28 29 2 Mambo Maombolezo 1 2 3 4 5 Ezekieli 1 2 3
ya Nyakati 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18
13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31
26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44
45 46 47 48 Danieli 1 2 3 4 5 6 7 8
9 10 11 12 Hosea 1 2 3 4 5 6 7 8 9
Kurudi kutoka uhamishoni 10 11 12 13 14 Yoeli 1 2 3 Amosi 1 2 Unaposoma Biblia, tia alama
3 4 5 6 7 8 9 Obadia 1 Yona 1 2 3 4 kila sura baada ya kuikamilisha.
Ezra 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Nehemia 1
2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 Esta 1 2 3 Mika 1 2 3 4 5 6 7 Nahumu 1 2 3
4 5 6 7 8 9 10 Habakuki 1 2 3 Sefania 1 2 3
Hagai 1 2 Zekaria 1 2 3 4 5 6 7 8 9
10 11 12 13 14 Malaki 1 2 3 4
s
JIFUNZE
MENGI ZAIDI

210615
lff-SW

Das könnte Ihnen auch gefallen